Chanzo cha Ugomvi wa Marekani Vs Venezuela

Chanzo cha Ugomvi wa Marekani Vs Venezuela

Mhaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2023
Posts
2,563
Reaction score
7,321
Hiko hivi Sababu kuu nyuma ya ugomvi wa U.S. na Venezuela ni Mafuta.

Venezuela ina akiba kubwa ya mafuta duniani. Malighafi hii ni nyingi sana kwa uzalishaji wa bidhaa za wese (hasa kwa ukanda wa Americas). Kwa nini hili wese linaleta shida: Kwanza mafuta = economic power, Mafuta = geopolitical leverage, ukiwa na Mafuta yasiyokuwa ndani ya nguvu ya Mmarekani = na strategic threat (Tishio) kwa nchi kama Marekani.

Historia hiko hivi: Venezuela ilikuwa ndio supplier wa wese (Mafuta) kwa Marekani kwa miongo mingi, Bwana Hugo Chávez (1999) alivyoingia madarakani, Venezuela ikabadili sheria ya Mafuta kuifanya iwe chini ya usimamizi na udhibiti wa Serikali au Taifa na ushawishi wa kibiashara wa Marekani kwenye Mafuta hayo ukachinjiwa baharini, yani wakasitisha ushirikiano wa kibiashara. Makampuni ya Marekani yakakosa udhibiti wa mafuta → Washington ikapoteza nguvu ya kutamba na kudhibiti soko la mafuta duniani na ikapunguza ushawishi wa kimkakati kwenye kufanya biashara hiyo.

Mafuta sio kichwa cha habari, Mafuta ndio kiini cha Habari yenyewe.

Tukija kwenye Itikadi: Mfumo wa Kiujamaa Vs Mfumo wa Ubepari Huru wa Kimarekani. Hapa namzungumzia Socialism Vs Liberal Capitalism.

Kwa uwazi kabisa Venezuela ilikataa mfumo wa Ubepari wa Mmarekani, ikaanza kusisitiza kuhusu ujamaa wenye kuukataa ubeberu. Ikaanza kufuata na kuambatana na misingi ya kijamaa ya nchi kama Cuba, Russia, China, na Iran

Tukija kwenye Mtazamo wa Marekani: Nchi ya Kijamaa kwenye Ukanda wa Ncni cha Magharibi (Western Hemisphere) = Ni Mfano mbaya kwa nchi za bara la Amerika na jambo lisolopaswa kuwepo katika ukanda huo. Hususani na zaidi nchi iwe inajaribu kutunisha kifua au kuitishia Marekani waziwazi.

Jambo linaloiwazisha Marekani: “Ni kama Venezuela itaweza kumudu na kutoboa chini ya falsafa za kiujamaa licha ya nchi hiyo kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na Mmarekani, basi uenda na Nchi nyingine zikafuata na kuanza kukaidi Maagizo ya Marekani”

Marekani anaogopa sana nchi nyingine za ukanda huo zisijekufuata jeuri ya Venezuela, na Jeuri kwa nchi za ukanda huo ni Jambo lisilokubalika katika Dhana ya Sera za Kigeni kwa Nchi ya Marekani. Marekani uwa apendi kukaribisha maadui katika maeneo yake ya kujidai. Akiwa katika maeneo yake ya kujidai Lazima nyote mfuate sera zake.

Marekani akaja na Dhana ya Kubadilisha Utawala (Mpango wa Uendeshaji) hili kuondoa utawala wa serikali ya Venezuela: Marekani ikidai Rais Maduro sio Rais aliyetakiwa kuwepo Madarakani (illegitimate President), yupo kimakosa. Marekani ikidai uchaguzi mkuu wa kumchagua Maduro ulikuwa na udanganyifu na wizi wa kura. Marekani ikadai kuna ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Venezuela. Marekani ikadai Rushwa imekithiri katika serikali ya Venezuela. Marekani ikadai Venezuela Inahusika na usambazaji wa madawa ya kulevya.

Ni dhahiri kuwa baadhi ya madai haya ni ya kweli, lakini Madai mengine yamekuzwa kisiasa tu. Jambo kuu hapa ni kuwa Marekani lengo lake sio Venezuela kufanya mabadiliko ya kisheria (Reform) bali lengo la Marekani inataka kuondoa Uongozi wote wa serikali ya Venezuela hili Biashara za awali ziendelee kama ilivyokuwa Mwanzo.

Ushahidi wa kwanza juu la lengo la Marekani ni: Kwanza Marekani inamtambua mgombea upinzani Bwana Juan Guaidó kama ndio Rais wa Venezuela. Vikwazo vimewekwa hili Kuidhoofisha Venezuela kiuchumi hili wairambe miguu ya Marekani na vikwazo hivyo sio kwa ajili ya kuwaadhibu viongozi wanaohusika. Kingine ni kauli za wazi za Marekani wakitaka Maduro aachie ngazi kwa hiari. Hii ni kama mbinu ya kutaka kuikomoa serikali na si utatuzi wa kidiplomasia uliozoeleka.

Vikwazo vya Kiuchumi → Uchumi Kuporomoka → Msukumo Mkali Wa Kisiasa

Vikwazo vya kiuchumi havikuwekwa kwa bahati mbaya— Ni imetumika kama Silaha za kiuchumi.

Madhara yake: Kuzuiwa kwa Usafirishaji wa Mafuta, Kuzuiwa kwa huduma za kibenki, Sarafu kuporomoka, kukosekana kwa Dawa muhimu na Chakula

“Vikwazo vya uchumi vinalenga Mamlaka au Utawala, na si watu au Raia”

Uhalisia: > Raia ndio uathirika na madhara karibu yote ya Vikwazo hivyo

Matokeo: Watu wataandamana kupinga Kodi kali za serikali, watu wanaandamana kwa ugumu wa maisha, wanajeshi wataasi au wanajeshi wataamia upande mwingine hili kupinga serikali kwa kushindwa kuongoza nchi vizuri, Serikali itayumba na miimili kuporomoka

Lakini kwa Venezuela hayo yote hayakutokea, na kushindwa kuanguka kwa utawala wa Venezuela ndiko kulikochochea ugomvi zaidi na Mmarekani. Mmarekani hesabu zake zilikataa, na serikali ya Venezuela ikazidi kuwa imara licha ya Vikwazo vyote ilivyowekewa. Mmarekani nae ndio akazidi kusala kama Nyati aliyekoswa na risasi.


Jiografia ya Kisiasa: Venezuela amechagua “Marafiki Wabaya” kwa lugha nyingine amechagua marafiki ambao ni maadui wa moja kwa moja wa Marekani.

Venezuela Imeimarisha mshikamano na:

🇷🇺 Urusi (Kimajeshi, kwenye biashara ya mafuta, kidiplomasia)

🇨🇳 China (Kwenye Mikopo, kwenye Miundombinu)

🇮🇷 Iran (Ushirikiano wa Matumizi ya Nishati, Kwenye kukataa shinikizo la Vikwazo vya Uchumi)

🇨🇺 Cuba (Ulinzi na Ujasusi)

Kutoka kwenye darubini za Washington: Huu Mshikamano wa Venezuela na hizi nchi ni kama maadui zake wanacheza kabisa kwenye eneo la Sebuleni la Marekani.
Nchi hizi kuingilia ugomvi huu inatafsiriwa kama uvunjifu wa “Sheria na Sera za Monroe” ambazo zinasema “Jaribio lolote la nguvu za Ulaya kudhibiti au kuathiri kisiasa taifa lolote la bara ya Amerika lingechukuliwa na Marekani kama kitendo cha uhasama dhidi yake.”

Oyaa, Hii ni tabia ya kawaida ya ushindani kati ya nchi zenye nguvu kubwa. Kila mtu kujaribu kuingilia masuala ya nchi zingine za adui yake hili kuonesha mwamba. Mnakumbuka pia ile vita ya Ukrein na Urusi, baada ya Mmarekani kuingilia sera za Urusi na kupeleka jeshi la NATO katika maeneo ya kujidai ya urusi.


Issue nyingine inayodaiwa kwenye ugomvi huu ni Issue ya Usafirishaji wa madawa ya kulevya na suala la Usalama kwa ujumla.

Marekani inaishitumu Venezuela kuwa: Inafadhili Magenge ya wauza madawa ya kulevya na inahusika na Usafirishaji wa dawa hizo, pia vile vile Venezuela inafadhili Mitandao ya waharifu wa makosa mbalimbali. Kingine ni Venezuela inafadhili Wanajeshi au wanamgambo wala rushwa wanaohusika na Usafirishaji wa silaha na kadharika.

Baadhi ya tuhuma ni za kweli — lakini tuwe wawazi, Usafirishaji wa madawa ya kulevya ni japo lililopo katika ukanda wote wa Amerika ya Kilatini (Latin America) huko Amerika Kusini. Na si nchi ya Venezuela pekee, lakini nchi nyingine za ukanda huo mfano Mexico hazipati shuruba kali kama namna Venezuela anavyopelekewa moto kwa issue ya madawa ya kulevya.

Kwa hiyo ni nini kiini cha sababu ya ugomvi huo?

Katika sentensi moja ni kuwa:

Venezuela inasisitiza na kukazia kwamba itathibiti mafuta yake, siasa zake, na ushirikiano wake nje ya ushawishi wa Marekani — na Marekani inakataa kukubali hilo.

Hizi story nyinginezo ni mbwembwe tu za kisiasa ila ukweli, Marekani ni king'ang'anizi, ni kama mtu anayelazimisha mahusiano kwa nguvu sehemu hasiyopendwa.


⚠️ Ukweli mchungu (No Sugar-Coating)

Marekani ni nchi isiyotaka kuvumilia upinzani wa aina yoyote iwe wa kimkakati au lah katika ukanda huo wa Amerika ya Kusini au Kaskazini. Mpinzani yoyote atakayepinga sera za Marekani katika ukanda wa Amerika basi uchukuliwa kama adui moja kwa moja.

Vikwazo na shinikizo vinalenga kuvunja upinzani dhidi ya Marekani, na si kuingia katika mazungumzo.


Mkakati endelevu ni kuwa Ugomvi hautaisha mpaka: Venezuela ibadilishe uongozi au Vipaumbele vya Marekani vifanyiwe kazi au kuwe na mabadiliko makubwa ya utawala wa kimataifa yani atokee mbabe mwingine atakayeweza kumnyamazisha Marekani.
 
Yashamalizana na waarabu sasa makafir yanauana yenyewe kwa yenyewe.

Napo yakimalizana yatarud huku kwa tumbiri watu watutawale tena tukalime kama trekta
 
Hiko hivi Sababu kuu nyuma ya ugomvi wa U.S. na Venezuela ni Mafuta.

Venezuela ina akiba kubwa ya mafuta duniani. Malighafi hii ni nyingi sana kwa uzalishaji wa bidhaa za wese (hasa kwa ukanda wa Americas). Kwa nini hili wese linaleta shida: Kwanza mafuta = economic power, Mafuta = geopolitical leverage, ukiwa na Mafuta yasiyokuwa ndani ni = na strategic threat hasa kwa nchi kama Marekani.

Historia hiko hivi: Venezuela ilikuwa ndio supplier wa wese (Mafuta) kwa Marekani kwa miongo mingi, Bwana Hugo Chávez (1999) alivyoingia madarakani, Venezuela ikabadili sheria ya Mafuta kuifanya iwe chini ya usimamizi wa Serikali au Taifa na ushawishi wa kibiashara wa Marekani kwenye Mafuta hayo ukachinjiwa baharini, yani wakasitisha ushirikiano wa kibiashara. Makampuni ya Marekani yakakosa udhibiti wa mafuta companies → Washington ikapoteza nguvu ya kutamba na kudhibiti soko la mafuta duniani na ikapunguza ushawishi wa kimkakati kwenye kufanya biashara hiyo.

Mafuta sio kichwa cha habari, Mafuta ndio kiini cha Habari yenyewe.

Tukija kwenye Itikadi: Mfumo wa Kiujamaa Vs Mfumo wa Ubepari Huru wa Kimarekani. Hapa namzungumzia Socialism Vs Liberal Capitalism.

Kwa uwazi kabisa Venezuela ilikataa mfumo wa Ubepari wa Mmarekani, ikaanza kusisitiza kuhusu ujamaa wenye kuukataa ubeberu. Ikaanza kufuata na kuambatana na misingi ya nchi kama Cuba, Russia, China, na Iran

Tukija kwenye Mtazamo wa Marekani: Nchi ya Kijamaa kwenye Ukanda wa Ncni cha Magharibi (Western Hemisphere) = Ni Mfano mbaya kwa nchi za bara la Amerika na jambo lisolopaswa kuwepo katika ukanda huo. Hususani na zaidi nchi iwe inajaribu kutunisha kifua au kuitishia Marekani waziwazi.

Jambo linaloiwazisha Marekani: “Ni kama Venezuela itaweza kumudu na kutoboa chini ya falsafa za kiujamaa licha ya nchi hiyo kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na Mmarekani, basi uenda na Nchi nyingine zikafuata na kuanza kukaidi Maagizo ya Marekani”

Marekani anaogopa sana nchi nyingine za ukanda huo zisijekufuata jeuri ya Venezuela, na Jeuri kwa nchi za ukanda huo ni Jambo lisilokubalika katika Dhana ya Sera za Kigeni kwa Nchi ya Marekani. Marekani uwa apendi kukaribisha maadui katika maeneo yake ya kujidai. Akiwa katika maeneo yake ya kujidai Lazima nyote mfuate sera zake.


Marekani akaja na Dhana ya Kubadilisha Utawala (Mpango wa Uendeshaji) hili kuondoa utawala wa serikali ya Venezuela: Marekani ikidai Rais Maduro sio Rais aliyetakiwa kuwepo Madarakani (illegitimate President), yupo kimakosa. Marekani ikidai uchaguzi mkuu wa kumchagua Maduro ulikuwa na udanganyifu na wizi wa kura. Marekani ikadai kuna ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Venezuela. Marekani ikadai Rushwa imekithiri katika serikali ya Venezuela. Marekani ikadai Venezuela Inahusika na usambazaji wa madawa ya kulevya.

Ni dhahiri kuwa baadhi ya madai haya ni ya kweli, lakini Madai mengine yamekuzwa kisiasa tu. Jambo kuu hapa ni kuwa Marekani lengo lake sio Venezuela kufanya mabadiliko ya kisheria (Reform) bali lengo la Marekani inataka kuondoa Uongozi wote wa serikali ya Venezuela hili Biashara za awali ziendelee kama ilivyokuwa Mwanzo.

Ushahidi wa kwanza juu la lengo la Marekani ni: Kwanza Marekani inamtambua mgombea upinzani Bwana Juan Guaidó kama ndio Rais wa Venezuela. Vikwazo vimewekwa hili Kuidhoofisha Venezuela kiuchumi hili wairambe miguu ya Marekani na vikwazo hivyo sio kwa ajili ya kuwaadhibu viongozi wanaohusika. Kingine ni kauli za wazi za Marekani wakitaka Maduro aachie ngazi kwa hiari. Hii ni kama mbinu ya kutaka kuikomoa serikali na si utatuzi wa kidiplomasia uliozoeleka.

Vikwazo vya Kiuchumi → Uchumi Kuporomoka → Msukumo Mkali Wa Kisiasa

Vikwazo vya kiuchumi havikuwekwa kwa bahati mbaya— Ni imetumika kama Silaha za kiuchumi.

Madhara yake: Kuzuiwa kwa Usafirishaji wa Mafuta, Kuzuiwa kwa huduma za kibenki, Sarafu kuporomoka, kukosekana kwa Dawa muhimu na Chakula



Uhalisia: > Raia ndio uathirika na madhara karibu yote ya Vikwazo hivyo

Matokeo: Watu wataandamana kupinga Kodi kali za serikali, watu wanaandamana kwa ugumu wa maisha, wanajeshi wataasi au wanajeshi wataamia upande mwingine hili kupinga serikali kwa kushindwa kuongoza nchi vizuri, Serikali itayumba na miimili kuporomoka

Lakini kwa Venezuela hayo yote hayakutokea, na kushindwa kuanguka kwa utawala wa Venezuela ndiko kulikochochea ugomvi zaidi na Mmarekani. Mmarekani hesabu zake zilikataa, na serikali ya Venezuela ikazidi kuwa imara licha ya Vikwazo vyote ilivyowekewa. Mmarekani nae ndio akazidi kusala kama Nyati aliyekoswa na risasi.


Jiografia ya Kisiasa: Venezuela amechagua “Marafiki Wabaya” kwa lugha nyingine amechagua marafiki ambao ni maadui wa moja kwa moja wa Marekani.

Venezuela Imeimarisha mshikamano na:

🇷🇺 Urusi (Kimajeshi, kwenye biashara ya mafuta, kidiplomasia)

🇨🇳 China (Kwenye Mikopo, kwenye Miundombinu)

🇮🇷 Iran (Ushirikiano wa Matumizi ya Nishati, Kwenye kukataa shinikizo la Vikwazo vya Uchumi)

🇨🇺 Cuba (Ulinzi na Ujasusi)

Kutoka kwenye darubini za Washington: Huu Mshikamano wa Venezuela na hizi nchi ni kama maadui zake wanacheza kabisa kwenye eneo la Sebuleni la Marekani.
Nchi hizi kuingilia ugomvi huu inatafsiriwa kama uvunjifu wa “Sheria na Sera za Monroe” ambazo zinasema “Jaribio lolote la nguvu za Ulaya kudhibiti au kuathiri kisiasa taifa lolote la bara ya Amerika lingechukuliwa na Marekani kama kitendo cha uhasama dhidi yake.”

Oyaa, Hii ni tabia ya kawaida ya ushindani kati ya nchi zenye nguvu kubwa. Kila mtu kujaribu kuingilia masuala ya nchi zingine za adui yake hili kuonesha mwamba. Mnakumbuka pia ile vita ya Ukrein na Urusi, baada ya Mmarekani kuingilia sera za Urusi na kupeleka jeshi la NATO katika maeneo ya kujidai ya urusi.


Issue nyingine inayodaiwa kwenye ugomvi huu ni Issue ya Usafirishaji wa madawa ya kulevya na suala la Usalama kwa ujumla.

Marekani inaishitumu Venezuela kuwa: Inafadhili Magenge ya wauza madawa ya kulevya na inahusika na Usafirishaji wa dawa hizo, pia vile vile Venezuela inafadhili Mitandao ya waharifu wa makosa mbalimbali. Kingine ni Venezuela inafadhili Wanajeshi au wanamgambo wala rushwa wanaohusika na Usafirishaji wa silaha na kadharika.

Baadhi ya tuhuma ni za kweli — lakini tuwe wawazi, Usafirishaji wa madawa ya kulevya ni japo lililopo katika ukanda wote wa Amerika ya Kilatini (Latin America) huko Amerika Kusini. Na si nchi ya Venezuela pekee, lakini nchi nyingine za ukanda huo mfano Mexico hazipati shuruba kali kama namna Venezuela anavyopelekewa moto kwa issue ya madawa ya kulevya.

Kwa hiyo ni nini kiini cha sababu ya ugomvi huo?

Katika sentensi moja ni kuwa:



Hizi story nyinginezo ni mbwembwe tu za kisiasa ila ukweli, Marekani ni king'ang'anizi, ni kama mtu anayelazimisha mahusiano kwa nguvu sehemu hasiyopendwa.


⚠️ Ukweli mchungu (No Sugar-Coating)

Marekani ni nchi isiyotaka kuvumilia upinzani wa aina yoyote iwe wa kimkakati au lah katika ukanda huo wa Amerika ya Kusini au Kaskazini. Mpinzani yoyote atakayepinga sera za Marekani katika ukanda wa Amerika basi uchukuliwa kama adui moja kwa moja.

Vikwazo na shinikizo vinalenga kuvunja upinzani dhidi ya Marekani, na si kuingia katika mazungumzo.


Mkakati endelevu ni kuwa Ugomvi hautaisha mpaka: Venezuela ibadilishe uongozi au Vipaumbele vya Marekani vifanyiwe kazi au kuwe na mabadiliko makubwa ya utawala wa kimataifa yani atokee mbabe mwingine atakayeweza kumnyamazisha Marekani.
Manufacturing tena. 🤣🤣🤣
 
Yashamalizana na waarabu sasa makafir yanauana yenyewe kwa yenyewe.

Napo yakimalizana yatarud huku kwa tumbiri watu watutawale tena tukalime kama trekta
Marekani ina Waislamu wengi tu, na wengi ndio ukimbilia huko wakidai nchi zao zinavita... sasa kwa Muktadha huo pia Waislamu ni makafiri pia kwa sababu wapo ukafirini
 
Yashamalizana na waarabu sasa makafir yanauana yenyewe kwa yenyewe.

Napo yakimalizana yatarud huku kwa tumbiri watu watutawale tena tukalime kama trekta
😂😂😂😂😂😂✨️✨️✨️✨️🤣🤣🤣🤣😂😂😂
 
Wanasema nini Madini Hadimu yaan Rare Earth Minerals
Tanzania ni nchi ya chini sana, wakitaka jambo lao hapa bongo hatuchomoi... ni kwamba tu sisi sio tishio kwao, na hatuna bidhaa ambayo inaweza kuwafanya wakinukishe
 
Mafuta ni ajenda ya Trump siyo ya Wamarekani Mkuu. Wamarekani wengi hawamuungi mkono Trump kwa hiyo issue ya kutaka kuiba mafuta ya Wanavenezuela mchana kweupee. Wanaunga mkono Maduro kuondolewa kwasababu ya ukatili wake wa kisiasa na ufisadi tu. Kwa kifupi Trump katumia madaraka yake kutimiza vision yake na wasaidizi wake wa karibu wachache siyo kutimiza vision ya Wamarekani. Hata vice president wake hayupo pamoja naye katika suala zima la foreign military interventions kama hii ya Maduro.
 
Mafuta ni ajenda ya Trump siyo ya Wamarekani Mkuu. Wamarekani wengi hawamuungi mkono Trump kwa hiyo issue ya kutaka kuiba mafuta ya Wanavenezuela mchana kweupee. Wanaunga mkono Maduro kuondolewa kwasababu ya ukatili wake wa kisiasa na ufisadi tu. Kwa kifupi Trump katumia madaraka yake kutimiza vision yake na wasaidizi wake wa karibu wachache siyo kutimiza vision ya Wamarekani. Hata vice president wake hayupo pamoja naye katika suala zima la foreign military interventions kama hii ya Maduro.
Hujui chochote

Marekani hiafanyi maamuzi kwa kuangalia wananchi wanahisia gani hasa linapokuja swala la mustakabali wa mambo ya ushawishi wa mambo ya kigeni na kueneza ubabe. Yenyewe inaangalia tu faida ya Taifa, wanataka Nchi inufahike, na ndio maana halisi ya Ubepari. Kusema kwamba maduro kukamatwa kwa manufaa ya Trump inadhihirisha wazi hujui sera za Wamarekani vizuri, Gadaffi nae walimkamata hivi hivi, same applied kwa Sadamu Husseni, same applied kwa Rais wa Panama. Gadaffi kukamatwa enzi za Obama, kwa hiyo unataka kusema kwamba wote wanaokamatwa na Marekani ni kwa sababu ya manufaa ya Rais husika. Marekani ina sera mpaka za Miaka 100 mbeleni, huyo Rais wa Venezuela mpango wa kumkamata ilikuwa ni mpango wa muda mrefu.

Pili raia wa Venezuela wanelishwa propaganda na Mmarekani hili iwe rahisi Marekani kumkamata Maduro bila vurugu, hii ni mbinu pia ilitumika kwa Magufuli wakamwita dikteta, hata Gadaffi... wanachofanya ni kukugombanisha na Raia kwa uenezi wa propaganda ili wakitaka kukuondoa iwe rahisi... hakuna cha udikteta wala ufisadi
 
Marekani, Israel(Wayahudi), Vatican,Illuminati sometime wanaharibu Dunia, yaani Hadi Umoja wa Mataifa imetiwa mfukoni na Marekani,anazivamia nchi,anachota rasilimali zao hawachukuliwi hatua yoyote...
Hio Venezuela isijekuwa kama Libya na Iraq ndio zimezid kuporomoka kiuchumi na hakuna usalama hata kama waliwatoa hao "wanaodai madikteta" hao wapya vibaraka wakurudisha demokrasia Bado wamefeli chini mwao kiuchumi na Maendeleo, chanzo ni wao U.S, tuombe yasije haya Tz viongozi wetu wasinyakuliwe hvyo ni fedheha ht km Ccm yetu/serikali baadhi Maeneo kuzingua
 
Hujui chochote

Marekani hiafanyi maamuzi kwa kuangalia wananchi wanahisia gani hasa linapokuja swala la mustakabali wa mambo ya ushawishi wa mambo ya kigeni na kueneza ubabe. Yenyewe inaangalia tu faida ya Taifa, wanataka Nchi inufahike, na ndio maana halisi ya Ubepari. Kusema kwamba maduro kukamatwa kwa manufaa ya Trump inadhihirisha wazi hujui sera za Wamarekani vizuri, Gadaffi nae walimkamata hivi hivi, same applied kwa Sadamu Husseni, same applied kwa Rais wa Panama. Gadaffi kukamatwa enzi za Obama, kwa hiyo unataka kusema kwamba wote wanaokamatwa na Marekani ni kwa sababu ya manufaa ya Rais husika. Marekani ina sera mpaka za Miaka 100 mbeleni, huyo Rais wa Venezuela mpango wa kumkamata ilikuwa ni mpango wa muda mrefu.

Pili raia wa Venezuela wanelishwa propaganda na Mmarekani hili iwe rahisi Marekani kumkamata Maduro bila vurugu, hii ni mbinu pia ilitumika kwa Magufuli wakamwita dikteta, hata Gadaffi... wanachofanya ni kukugombanisha na Raia kwa uenezi wa propaganda ili wakitaka kukuondoa iwe rahisi... hakuna cha udikteta wala ufisadi

Keep it civil. Wapi nimesema serikali ya Marekani haiwezi kufanya maamuzi kinyume na matakwa ya raia wake? Mimi nimekupa analysis yangu kwamba Trump katumia discretion aliyonayo kisheria kufanya maamuzi ambayo hayaungwi mkono na Wamarekani wengi including some of his own subordinates. That was my point. Na hapa tunazungumzia spefically about Venezuela. Waliovamia Iraq, Libya nao walikua na motivations zao and they paid a political price for their decisions. Na hizo missions zote mbili zilifeli na hivi leo wanakiri. National interest can be used as an excuse for elites to implement policies that are not in the interest of a nation at all. Unalijua hilo?
 
Back
Top Bottom