Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,563
- 7,321
Hiko hivi Sababu kuu nyuma ya ugomvi wa U.S. na Venezuela ni Mafuta.
Venezuela ina akiba kubwa ya mafuta duniani. Malighafi hii ni nyingi sana kwa uzalishaji wa bidhaa za wese (hasa kwa ukanda wa Americas). Kwa nini hili wese linaleta shida: Kwanza mafuta = economic power, Mafuta = geopolitical leverage, ukiwa na Mafuta yasiyokuwa ndani ya nguvu ya Mmarekani = na strategic threat (Tishio) kwa nchi kama Marekani.
Historia hiko hivi: Venezuela ilikuwa ndio supplier wa wese (Mafuta) kwa Marekani kwa miongo mingi, Bwana Hugo Chávez (1999) alivyoingia madarakani, Venezuela ikabadili sheria ya Mafuta kuifanya iwe chini ya usimamizi na udhibiti wa Serikali au Taifa na ushawishi wa kibiashara wa Marekani kwenye Mafuta hayo ukachinjiwa baharini, yani wakasitisha ushirikiano wa kibiashara. Makampuni ya Marekani yakakosa udhibiti wa mafuta → Washington ikapoteza nguvu ya kutamba na kudhibiti soko la mafuta duniani na ikapunguza ushawishi wa kimkakati kwenye kufanya biashara hiyo.
Mafuta sio kichwa cha habari, Mafuta ndio kiini cha Habari yenyewe.
Tukija kwenye Itikadi: Mfumo wa Kiujamaa Vs Mfumo wa Ubepari Huru wa Kimarekani. Hapa namzungumzia Socialism Vs Liberal Capitalism.
Kwa uwazi kabisa Venezuela ilikataa mfumo wa Ubepari wa Mmarekani, ikaanza kusisitiza kuhusu ujamaa wenye kuukataa ubeberu. Ikaanza kufuata na kuambatana na misingi ya kijamaa ya nchi kama Cuba, Russia, China, na Iran
Tukija kwenye Mtazamo wa Marekani: Nchi ya Kijamaa kwenye Ukanda wa Ncni cha Magharibi (Western Hemisphere) = Ni Mfano mbaya kwa nchi za bara la Amerika na jambo lisolopaswa kuwepo katika ukanda huo. Hususani na zaidi nchi iwe inajaribu kutunisha kifua au kuitishia Marekani waziwazi.
Jambo linaloiwazisha Marekani: “Ni kama Venezuela itaweza kumudu na kutoboa chini ya falsafa za kiujamaa licha ya nchi hiyo kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na Mmarekani, basi uenda na Nchi nyingine zikafuata na kuanza kukaidi Maagizo ya Marekani”
Marekani anaogopa sana nchi nyingine za ukanda huo zisijekufuata jeuri ya Venezuela, na Jeuri kwa nchi za ukanda huo ni Jambo lisilokubalika katika Dhana ya Sera za Kigeni kwa Nchi ya Marekani. Marekani uwa apendi kukaribisha maadui katika maeneo yake ya kujidai. Akiwa katika maeneo yake ya kujidai Lazima nyote mfuate sera zake.
Marekani akaja na Dhana ya Kubadilisha Utawala (Mpango wa Uendeshaji) hili kuondoa utawala wa serikali ya Venezuela: Marekani ikidai Rais Maduro sio Rais aliyetakiwa kuwepo Madarakani (illegitimate President), yupo kimakosa. Marekani ikidai uchaguzi mkuu wa kumchagua Maduro ulikuwa na udanganyifu na wizi wa kura. Marekani ikadai kuna ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Venezuela. Marekani ikadai Rushwa imekithiri katika serikali ya Venezuela. Marekani ikadai Venezuela Inahusika na usambazaji wa madawa ya kulevya.
Ni dhahiri kuwa baadhi ya madai haya ni ya kweli, lakini Madai mengine yamekuzwa kisiasa tu. Jambo kuu hapa ni kuwa Marekani lengo lake sio Venezuela kufanya mabadiliko ya kisheria (Reform) bali lengo la Marekani inataka kuondoa Uongozi wote wa serikali ya Venezuela hili Biashara za awali ziendelee kama ilivyokuwa Mwanzo.
Ushahidi wa kwanza juu la lengo la Marekani ni: Kwanza Marekani inamtambua mgombea upinzani Bwana Juan Guaidó kama ndio Rais wa Venezuela. Vikwazo vimewekwa hili Kuidhoofisha Venezuela kiuchumi hili wairambe miguu ya Marekani na vikwazo hivyo sio kwa ajili ya kuwaadhibu viongozi wanaohusika. Kingine ni kauli za wazi za Marekani wakitaka Maduro aachie ngazi kwa hiari. Hii ni kama mbinu ya kutaka kuikomoa serikali na si utatuzi wa kidiplomasia uliozoeleka.
Vikwazo vya Kiuchumi → Uchumi Kuporomoka → Msukumo Mkali Wa Kisiasa
Vikwazo vya kiuchumi havikuwekwa kwa bahati mbaya— Ni imetumika kama Silaha za kiuchumi.
Madhara yake: Kuzuiwa kwa Usafirishaji wa Mafuta, Kuzuiwa kwa huduma za kibenki, Sarafu kuporomoka, kukosekana kwa Dawa muhimu na Chakula
Uhalisia: > Raia ndio uathirika na madhara karibu yote ya Vikwazo hivyo
Matokeo: Watu wataandamana kupinga Kodi kali za serikali, watu wanaandamana kwa ugumu wa maisha, wanajeshi wataasi au wanajeshi wataamia upande mwingine hili kupinga serikali kwa kushindwa kuongoza nchi vizuri, Serikali itayumba na miimili kuporomoka
Lakini kwa Venezuela hayo yote hayakutokea, na kushindwa kuanguka kwa utawala wa Venezuela ndiko kulikochochea ugomvi zaidi na Mmarekani. Mmarekani hesabu zake zilikataa, na serikali ya Venezuela ikazidi kuwa imara licha ya Vikwazo vyote ilivyowekewa. Mmarekani nae ndio akazidi kusala kama Nyati aliyekoswa na risasi.
Jiografia ya Kisiasa: Venezuela amechagua “Marafiki Wabaya” kwa lugha nyingine amechagua marafiki ambao ni maadui wa moja kwa moja wa Marekani.
Venezuela Imeimarisha mshikamano na:
🇷🇺 Urusi (Kimajeshi, kwenye biashara ya mafuta, kidiplomasia)
🇨🇳 China (Kwenye Mikopo, kwenye Miundombinu)
🇮🇷 Iran (Ushirikiano wa Matumizi ya Nishati, Kwenye kukataa shinikizo la Vikwazo vya Uchumi)
🇨🇺 Cuba (Ulinzi na Ujasusi)
Kutoka kwenye darubini za Washington: Huu Mshikamano wa Venezuela na hizi nchi ni kama maadui zake wanacheza kabisa kwenye eneo la Sebuleni la Marekani.
Nchi hizi kuingilia ugomvi huu inatafsiriwa kama uvunjifu wa “Sheria na Sera za Monroe” ambazo zinasema “Jaribio lolote la nguvu za Ulaya kudhibiti au kuathiri kisiasa taifa lolote la bara ya Amerika lingechukuliwa na Marekani kama kitendo cha uhasama dhidi yake.”
Oyaa, Hii ni tabia ya kawaida ya ushindani kati ya nchi zenye nguvu kubwa. Kila mtu kujaribu kuingilia masuala ya nchi zingine za adui yake hili kuonesha mwamba. Mnakumbuka pia ile vita ya Ukrein na Urusi, baada ya Mmarekani kuingilia sera za Urusi na kupeleka jeshi la NATO katika maeneo ya kujidai ya urusi.
Issue nyingine inayodaiwa kwenye ugomvi huu ni Issue ya Usafirishaji wa madawa ya kulevya na suala la Usalama kwa ujumla.
Marekani inaishitumu Venezuela kuwa: Inafadhili Magenge ya wauza madawa ya kulevya na inahusika na Usafirishaji wa dawa hizo, pia vile vile Venezuela inafadhili Mitandao ya waharifu wa makosa mbalimbali. Kingine ni Venezuela inafadhili Wanajeshi au wanamgambo wala rushwa wanaohusika na Usafirishaji wa silaha na kadharika.
Baadhi ya tuhuma ni za kweli — lakini tuwe wawazi, Usafirishaji wa madawa ya kulevya ni japo lililopo katika ukanda wote wa Amerika ya Kilatini (Latin America) huko Amerika Kusini. Na si nchi ya Venezuela pekee, lakini nchi nyingine za ukanda huo mfano Mexico hazipati shuruba kali kama namna Venezuela anavyopelekewa moto kwa issue ya madawa ya kulevya.
Kwa hiyo ni nini kiini cha sababu ya ugomvi huo?
Katika sentensi moja ni kuwa:
Hizi story nyinginezo ni mbwembwe tu za kisiasa ila ukweli, Marekani ni king'ang'anizi, ni kama mtu anayelazimisha mahusiano kwa nguvu sehemu hasiyopendwa.
⚠️ Ukweli mchungu (No Sugar-Coating)
Marekani ni nchi isiyotaka kuvumilia upinzani wa aina yoyote iwe wa kimkakati au lah katika ukanda huo wa Amerika ya Kusini au Kaskazini. Mpinzani yoyote atakayepinga sera za Marekani katika ukanda wa Amerika basi uchukuliwa kama adui moja kwa moja.
Vikwazo na shinikizo vinalenga kuvunja upinzani dhidi ya Marekani, na si kuingia katika mazungumzo.
Mkakati endelevu ni kuwa Ugomvi hautaisha mpaka: Venezuela ibadilishe uongozi au Vipaumbele vya Marekani vifanyiwe kazi au kuwe na mabadiliko makubwa ya utawala wa kimataifa yani atokee mbabe mwingine atakayeweza kumnyamazisha Marekani.
Venezuela ina akiba kubwa ya mafuta duniani. Malighafi hii ni nyingi sana kwa uzalishaji wa bidhaa za wese (hasa kwa ukanda wa Americas). Kwa nini hili wese linaleta shida: Kwanza mafuta = economic power, Mafuta = geopolitical leverage, ukiwa na Mafuta yasiyokuwa ndani ya nguvu ya Mmarekani = na strategic threat (Tishio) kwa nchi kama Marekani.
Historia hiko hivi: Venezuela ilikuwa ndio supplier wa wese (Mafuta) kwa Marekani kwa miongo mingi, Bwana Hugo Chávez (1999) alivyoingia madarakani, Venezuela ikabadili sheria ya Mafuta kuifanya iwe chini ya usimamizi na udhibiti wa Serikali au Taifa na ushawishi wa kibiashara wa Marekani kwenye Mafuta hayo ukachinjiwa baharini, yani wakasitisha ushirikiano wa kibiashara. Makampuni ya Marekani yakakosa udhibiti wa mafuta → Washington ikapoteza nguvu ya kutamba na kudhibiti soko la mafuta duniani na ikapunguza ushawishi wa kimkakati kwenye kufanya biashara hiyo.
Mafuta sio kichwa cha habari, Mafuta ndio kiini cha Habari yenyewe.
Tukija kwenye Itikadi: Mfumo wa Kiujamaa Vs Mfumo wa Ubepari Huru wa Kimarekani. Hapa namzungumzia Socialism Vs Liberal Capitalism.
Kwa uwazi kabisa Venezuela ilikataa mfumo wa Ubepari wa Mmarekani, ikaanza kusisitiza kuhusu ujamaa wenye kuukataa ubeberu. Ikaanza kufuata na kuambatana na misingi ya kijamaa ya nchi kama Cuba, Russia, China, na Iran
Tukija kwenye Mtazamo wa Marekani: Nchi ya Kijamaa kwenye Ukanda wa Ncni cha Magharibi (Western Hemisphere) = Ni Mfano mbaya kwa nchi za bara la Amerika na jambo lisolopaswa kuwepo katika ukanda huo. Hususani na zaidi nchi iwe inajaribu kutunisha kifua au kuitishia Marekani waziwazi.
Jambo linaloiwazisha Marekani: “Ni kama Venezuela itaweza kumudu na kutoboa chini ya falsafa za kiujamaa licha ya nchi hiyo kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na Mmarekani, basi uenda na Nchi nyingine zikafuata na kuanza kukaidi Maagizo ya Marekani”
Marekani anaogopa sana nchi nyingine za ukanda huo zisijekufuata jeuri ya Venezuela, na Jeuri kwa nchi za ukanda huo ni Jambo lisilokubalika katika Dhana ya Sera za Kigeni kwa Nchi ya Marekani. Marekani uwa apendi kukaribisha maadui katika maeneo yake ya kujidai. Akiwa katika maeneo yake ya kujidai Lazima nyote mfuate sera zake.
Marekani akaja na Dhana ya Kubadilisha Utawala (Mpango wa Uendeshaji) hili kuondoa utawala wa serikali ya Venezuela: Marekani ikidai Rais Maduro sio Rais aliyetakiwa kuwepo Madarakani (illegitimate President), yupo kimakosa. Marekani ikidai uchaguzi mkuu wa kumchagua Maduro ulikuwa na udanganyifu na wizi wa kura. Marekani ikadai kuna ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Venezuela. Marekani ikadai Rushwa imekithiri katika serikali ya Venezuela. Marekani ikadai Venezuela Inahusika na usambazaji wa madawa ya kulevya.
Ni dhahiri kuwa baadhi ya madai haya ni ya kweli, lakini Madai mengine yamekuzwa kisiasa tu. Jambo kuu hapa ni kuwa Marekani lengo lake sio Venezuela kufanya mabadiliko ya kisheria (Reform) bali lengo la Marekani inataka kuondoa Uongozi wote wa serikali ya Venezuela hili Biashara za awali ziendelee kama ilivyokuwa Mwanzo.
Ushahidi wa kwanza juu la lengo la Marekani ni: Kwanza Marekani inamtambua mgombea upinzani Bwana Juan Guaidó kama ndio Rais wa Venezuela. Vikwazo vimewekwa hili Kuidhoofisha Venezuela kiuchumi hili wairambe miguu ya Marekani na vikwazo hivyo sio kwa ajili ya kuwaadhibu viongozi wanaohusika. Kingine ni kauli za wazi za Marekani wakitaka Maduro aachie ngazi kwa hiari. Hii ni kama mbinu ya kutaka kuikomoa serikali na si utatuzi wa kidiplomasia uliozoeleka.
Vikwazo vya Kiuchumi → Uchumi Kuporomoka → Msukumo Mkali Wa Kisiasa
Vikwazo vya kiuchumi havikuwekwa kwa bahati mbaya— Ni imetumika kama Silaha za kiuchumi.
Madhara yake: Kuzuiwa kwa Usafirishaji wa Mafuta, Kuzuiwa kwa huduma za kibenki, Sarafu kuporomoka, kukosekana kwa Dawa muhimu na Chakula
“Vikwazo vya uchumi vinalenga Mamlaka au Utawala, na si watu au Raia”
Uhalisia: > Raia ndio uathirika na madhara karibu yote ya Vikwazo hivyo
Matokeo: Watu wataandamana kupinga Kodi kali za serikali, watu wanaandamana kwa ugumu wa maisha, wanajeshi wataasi au wanajeshi wataamia upande mwingine hili kupinga serikali kwa kushindwa kuongoza nchi vizuri, Serikali itayumba na miimili kuporomoka
Lakini kwa Venezuela hayo yote hayakutokea, na kushindwa kuanguka kwa utawala wa Venezuela ndiko kulikochochea ugomvi zaidi na Mmarekani. Mmarekani hesabu zake zilikataa, na serikali ya Venezuela ikazidi kuwa imara licha ya Vikwazo vyote ilivyowekewa. Mmarekani nae ndio akazidi kusala kama Nyati aliyekoswa na risasi.
Jiografia ya Kisiasa: Venezuela amechagua “Marafiki Wabaya” kwa lugha nyingine amechagua marafiki ambao ni maadui wa moja kwa moja wa Marekani.
Venezuela Imeimarisha mshikamano na:
🇷🇺 Urusi (Kimajeshi, kwenye biashara ya mafuta, kidiplomasia)
🇨🇳 China (Kwenye Mikopo, kwenye Miundombinu)
🇮🇷 Iran (Ushirikiano wa Matumizi ya Nishati, Kwenye kukataa shinikizo la Vikwazo vya Uchumi)
🇨🇺 Cuba (Ulinzi na Ujasusi)
Kutoka kwenye darubini za Washington: Huu Mshikamano wa Venezuela na hizi nchi ni kama maadui zake wanacheza kabisa kwenye eneo la Sebuleni la Marekani.
Nchi hizi kuingilia ugomvi huu inatafsiriwa kama uvunjifu wa “Sheria na Sera za Monroe” ambazo zinasema “Jaribio lolote la nguvu za Ulaya kudhibiti au kuathiri kisiasa taifa lolote la bara ya Amerika lingechukuliwa na Marekani kama kitendo cha uhasama dhidi yake.”
Oyaa, Hii ni tabia ya kawaida ya ushindani kati ya nchi zenye nguvu kubwa. Kila mtu kujaribu kuingilia masuala ya nchi zingine za adui yake hili kuonesha mwamba. Mnakumbuka pia ile vita ya Ukrein na Urusi, baada ya Mmarekani kuingilia sera za Urusi na kupeleka jeshi la NATO katika maeneo ya kujidai ya urusi.
Issue nyingine inayodaiwa kwenye ugomvi huu ni Issue ya Usafirishaji wa madawa ya kulevya na suala la Usalama kwa ujumla.
Marekani inaishitumu Venezuela kuwa: Inafadhili Magenge ya wauza madawa ya kulevya na inahusika na Usafirishaji wa dawa hizo, pia vile vile Venezuela inafadhili Mitandao ya waharifu wa makosa mbalimbali. Kingine ni Venezuela inafadhili Wanajeshi au wanamgambo wala rushwa wanaohusika na Usafirishaji wa silaha na kadharika.
Baadhi ya tuhuma ni za kweli — lakini tuwe wawazi, Usafirishaji wa madawa ya kulevya ni japo lililopo katika ukanda wote wa Amerika ya Kilatini (Latin America) huko Amerika Kusini. Na si nchi ya Venezuela pekee, lakini nchi nyingine za ukanda huo mfano Mexico hazipati shuruba kali kama namna Venezuela anavyopelekewa moto kwa issue ya madawa ya kulevya.
Kwa hiyo ni nini kiini cha sababu ya ugomvi huo?
Katika sentensi moja ni kuwa:
Venezuela inasisitiza na kukazia kwamba itathibiti mafuta yake, siasa zake, na ushirikiano wake nje ya ushawishi wa Marekani — na Marekani inakataa kukubali hilo.
Hizi story nyinginezo ni mbwembwe tu za kisiasa ila ukweli, Marekani ni king'ang'anizi, ni kama mtu anayelazimisha mahusiano kwa nguvu sehemu hasiyopendwa.
⚠️ Ukweli mchungu (No Sugar-Coating)
Marekani ni nchi isiyotaka kuvumilia upinzani wa aina yoyote iwe wa kimkakati au lah katika ukanda huo wa Amerika ya Kusini au Kaskazini. Mpinzani yoyote atakayepinga sera za Marekani katika ukanda wa Amerika basi uchukuliwa kama adui moja kwa moja.
Vikwazo na shinikizo vinalenga kuvunja upinzani dhidi ya Marekani, na si kuingia katika mazungumzo.
Mkakati endelevu ni kuwa Ugomvi hautaisha mpaka: Venezuela ibadilishe uongozi au Vipaumbele vya Marekani vifanyiwe kazi au kuwe na mabadiliko makubwa ya utawala wa kimataifa yani atokee mbabe mwingine atakayeweza kumnyamazisha Marekani.