Give me a break. Wewe "Mhaya" unajua "Global na national interests" za Marekani? Uliona comment ya Vice President wa Marekani wa sasa iliyo leak kwenye Signal Chat App? Alipinga Trump kushambulia Iran. Huyu ni kiongozi msaidizi wa Trump. Kwenye hiyo leaked conversation aki chat na members of the national security team, alinyakwa akitoa maoni yanayopingana na msimamo wa boss wake. Maoni yake siyo maoni ya average citizen tu.
Unasema nikutajie Rais yeyote wa USA ambaye hakufanya alichofanya Trump Venezuela. Biden alimtoa rais wa nchi gani madarakani? Jimmy Carter? JFK? Weengi tu - in fact wengi wao - hawakufanya alichofanya Trump. Jifunze tofauti kati ya conspiracy theories na empirical evidence. Empirical evidence ni facts. Conspiracy theories ni maoni ambayo yanaweza kuwa yanashawishi ila bado yakawa hayana ukweli. Maoni yako ni conspiracy theory for the most part.
Nikisema wewe jamaa bado ujui kitu husikatae... bado unaamini propaganda za Mmarekani kwamba Makamu wa Urais chat zake zimevuja kwenye ukimwengu huu wa A.I na propaganda. Kwa akili zako unahisi Chat za kiongozi wa Marekani mwenye cheo icho zinavujishwa kiboya tu. Na ikitokea chats zimevuja basi jua ni moja ya Mpango wa Propaganda. Na Marekani ni bingwa wa hizo mambo, ile nchi ikikupoga Propaganda unaweza hata mwenyewe kujikataa.
Tukija kwenye swala la Rais gani wa Marekani kamngoa nani, hii issue sio kama kuamka na kupika maandazi ni mpango mkakati endapo utaenda kinyume na matakwa yap. Hii issue hapangi Rais, zinapanga Mamlaka za kijasusi... Rais analetewa file mezani yeye anatoa tu Go Ahead... wazee wanaingia kazini... na sio lazima kila uongozi mtu atolewe madarakani, inategemea kwa wakati huo wanataka nini na nani anawazengua ku-accomplish mission zao.
hebu tuiweke sawa kwa historia, nguvu, na ukweli wa kisiasa—bila drama, bila conspiracy, bila kuchanganya majina juu ya marais uliowataja
JOE BIDEN alifanya ubabe kupitia PROPAGANDA na MFUMO, SIO MAPINDUZI ya moja kwa moja
Biden hakumtoa rais yeyote maarufu madarakani moja kwa moja. Lakini chini yake, Marekani iliendeleza ubabe kwa njia hizi:
(a) Ukraine vs Russia
Biden aliiongoza NATO kuisaidia Ukraine kumdhoofisha Urusi, Aliweka sanctions kali sana dhidi ya Russia, Alidhoofisha Uchumi wa Russia na Influence ya Putin Ulaya. Huu ni ubabe wa kimkakati, si kuondoa rais
(b) China
Biden aliendeleza vita ya kiuchumi na kiteknolojia mfano Chip bans, AI restrictions, alliances Asia-Pacific lengo ikiwa Kuzuia China isiwe “boss wa dunia”
(c) Middle East
Aliendeleza ulinzi wa Israel kutuliza mataifa ya uarabuni hasa kuinyamazisha Palestina. Akaweka pressure Iran kupitia sanctions na proxy containment
3. JIMMY CARTER yeye alitumia kitu kinaitwa SOFT POWER
Jimmy Carter (1977–1981) alikuwa tofauti kidogo: Alifanya nini? Alitumia mambo ya kutetea haki kama silaha ya kisiasa
Alitumia Diplomasia, Mikataba (Camp David Accords – Israel & Egypt), Aliepuka vita kubwa
Matokeo yake Marekani ilionekana “dhaifu”, Ilipoteza heshima kimataifa.
Maamuzi yake yaligharimu Marekani pakubwa, kiasi kwamba kuna wamarekani 66 walitekwa kwenye ubalozi wa Irani na kisha waakchilia wakabaki 52 mateka. Baadae Rais huyo akatuma kikosi kikawaokoe mateka huko Iran lakini bado wamarekani 8 walifariki.
Kwa kifupi utawala wake alichukuliwa kama Utawala mbovu na dhaifu hasa kwenye falsafa za kueneza ubabe, baada ya Miaka yake 4 kuisha alivyogombea tena kwa Muhula wa Pili aliangukia pua, wamarekani wakamtema. Akaishia kutawala Muhula mmoja tu wa miaka 4, wakati Marais wengi utawala mihula 2.... Marekani ukiona unatemwa ndani ya Muhula mmmoja basi jua Taifa limeona hakuna kitu umefanya, na ndio kilichotaka kumkuta Trump baada ya kutaka kuleta mambo ya utawala wa Amani. Lakini akapigana akarudi tena na sasa anaeneza ubabe
Baada ya Jimmy Carter kushindwa kwenye uchaguzi wa Muhula Ndiyo Reagan, Reagan alikuja na mkono wa chuma, alitembeza kichapo vibaya mno kwa maadui wote wa Marekani.
4. JOHN F. KENNEDY (JFK) – UBAABE WA BARIDI (COLD WAR)
Huyu sasa alikuwa alpha male wa Cold War (vita baridi).
JFK alifanya nini kuweka dominance?
Kuna hii issue ya Cuban Missile Crisis (1962), mchiz alisimama kidete kupambana dhidi ya USSR (Urusi). Labda nikueleze kidogo. Cuban Missile Crisis ilikuwa mgogoro hatari zaidi wa Vita Baridi, ambapo dunia ilikaribia kuingia vita ya nyuklia kati ya Marekani (USA) na Soviet Union (USSR) kwa muda wa siku 13 (Oktoba 1962). 1959: Fidel Castro anapindua serikali iliyokuwa inaegemea Marekani. Marekani ilijaribu kumng’oa Castro (Bay of Pigs – 1961) → ilishindwa vibaya. Cuba ikageukia USSR (Urusi) kwa ulinzi. Marekani ilikuwa tayari imeweka makombora ya nyuklia Turkey & Italy, karibu na USSR (Urusi). USSR ikaamua kuweka makombora Cuba, umbali wa km ~150 tu kutoka Florida. Hii ilikuwa provocation ya kiwango cha juu. Oktoba 1962: U-2 spy planes (ndege za kishushushu) za Marekani zapiga picha makombora ya nyuklia Cuba. JFK apata taarifa → mgogoro ukaanza rasmi. JFK akajibu mashambulizi kwa kuzuia meli za Soviet kufika Cuba. Dunia itagawanywa wanajeshi walikuwa tayari kupigana vita. Ndege ya Marekani ikapigwa Cuba, majeshi ya Marekani yakataka kuanzisha mashambulizi badae JFK anakataa ushauri wa mashambulizi ya moja kwa moja. Badae wakafanya makubaliano USSR ikakubali kutoa makombora Cuba, Marekani nayo akakubali Kutoivamia Cuba na Kuondoa kwa siri makombora yake Turkey.
Badae Mwaka Mmoja akapigwa Risasi na kuuwawa, hivyo alitawala miaka 3 tu (miaka 2 na miezi 10), Lakini, ndani ya historia ya mauwaji yake, kuna mvutano mkubwa kuhusu mashirika yaliyohusika, kama CIA au mafia ndio waliomuua, lakini hakuna ushahidi wa kisheria uliothibitisha hayo.
Punguza kushupaza shingo... Marais wengi wa Marekani wanaingia wanakuta tayari kuna Agenda... Rais yeye anapewa miongozo tu na anabaki kusema ndio au hapana tusifanye