Chanzo cha Mwanamke wako Kukudharau/ Kukushushia Heshima

Infinite_Kiumeni

JF-Expert Member
Jan 23, 2023
382
661
Una mwanamke sasa ni miezi kadhaa. Pengine una miaka kadhaa pamoja naye. Lakini kuna vitu anavifanya huelewi hujui ufanye nini. Hujui kama uko peke yako au la. Muda mwingi anakua na jeuri, anakudharau na kukupandishia sauti hadi unatamani umpige. Unajihisi huna uhuru tena ukiwa naye. Hutaki ata kuwa naye karibu. Mpaka unahisi anataka kukutawala yeye.

Chanzo kikuu ni kukosa mipaka.

Mipaka inaanzia kwako.
Jinsi unavyojiendesha wewe mwenyewe kama mwanaume. Hauwezi ukamfanya mtu aheshimu mipaka yako kama we mwenyewe huna/ hujui hiyo mipaka. Mipaka yako inaanza kwa kujijua wewe. Unapenda vitu gani, unataka siku yako iweje, unataka kuwa na marafiki aina gani, hutaki kumfanyia mtu kitu gani na yeye hutaki akufanyie kitu gani, nini chanzo cha amani yako, nini kinaondoa amani yako, na maswali kama hayo ndo yatakayoanza kukupa mwanga uwe na mipaka gani.

Mipaka yako ni thamani zako. Mipaka ni picha yako mbele ya jamii. Kama we unatukanwa na mkeo/ mwanamke wako/ na mwanamke yoyote. Picha yako ni mtu unayeburuzwa. Kama wanawake wakikuona wanaongea nawe kwa heshima. Picha yako ni ya mwanaume anayeheshimika.

Kama we hadi watoto wadogo wanakutania matani hadi ya nguoni. Picha yako ni mtu asiyeheshimiwa.

Mipaka pia inashushwa na we mwenyewe. Kwenye kuweka mipaka kuna kile kisauti kinakuambia “naweza nkampoteza huyu mwanamke/ atanionaje/ ataninyima kitu fulani”. Unajikuta unakausha. Unaendelea kuburuzwa lakini moyoni unaumia. Unavumilia. Kadri unavyozidi kuvumilia, ndivyo mipaka yako inavyozidi kuvamiwa.

Mwisho wa siku unajikuta huna mpaka, umeshatekwa na mwanamke. Umewekwa kiganjani. Mwanamke anakua hana wasiwasi na wewe, hakuogopi, anajua chochote anachofanya huwezi mfanya lolote. Japo anaweza kukuambia anahitaji uhuru, lakini haina maana usiweke mipaka.

Ubize, uoga, kukataliwa, au kuchukiwa kusiwe chanzo cha wewe kutokuweka mipaka. Jitahidi kuushinda woga wako. Jitahidi kuvuka mstari uliojiwekea ukiogopa kuharibu mapenzi. Mapenzi yoyote hayana maana kama ni ya kuumizana/ kurudishana nyuma. Hivyo huna sababu ya kuogopa kuchora mipaka yako. Ukisema kitu maanisha. Ukiweka mpaka maanisha.

Kuwa na msimamo. Sio umwambie mwanamke wako/ mkeo kitu alafu baadaye ubadilishe kisa umechuniwa. Au kisa umenyimwa penzi. Au kisa mwanamke ameanza kukuropokea na hutaki/ unaogopa kuzua gumzo. Huo ni ujinga na udhaifu. Wengi wanaoogopa wanawake waliofanikiwa hili ndo jambo linalowashinda. Wanajihisi wadogo mbele yao. Huwa inasikitisha mwanaume anatukanwa na mwanamke mbele ya umati, alafu anajichekesha tu.

Kama mtu hatokubali kuiheshimu mipaka yako basi hastahili muda wako. Na kama we mwenyewe huna mipaka ujue wewe ndiye uliyeruhusu kudharauliwa mana mwanamke wako ameona unamruhusu kufanya hivyo.
 
Kukosa mipaka. Hiii ni siri nzito sana
Mwanamke atakuchukulia poa kama kila akijaribu kuvunja mipaka yako na ww unamchekea au unakaa kimya.

Atazidi kukudharau na itapelekea akuchukulie poa mwishowe akuone poyoyo.
Ndio maana msimamo kwa mwauame ndio key component
Ukikosa msimamo utadharaulika siku zote
 
Muoe nyie kulia Lia nyie, nani kasema hio experience ni yako, hujawa na visa mafunzo, sijaona maelezo yenye kubainisha na kuainisha ujumbe uko vululuvululu, na mtanyooka na hizo ndoa zenu uchwara. Uishi na kupe unategemea nini.

Chama Cha kataa ndoa tuko imara na mtakuja na thread za kujifariji sana mwaka huu mtanyooka tu.
 
Kukosa mipaka. Hiii ni siri nzito sana
Mwanamke atakuchukulia poa kama kila akijaribu kuvunja mipaka yako na ww unamchekea au unakaa kimya.

Atazidi kukudharau na itapelekea akuchukulie poa mwishowe akuone poyoyo.
Ndio maana msimamo kwa mwauame ndio key component
Ukikosa msimamo utadharaulika siku zote
Kweli kabisa
 
Kila chenye mwanzo lazima kiwe na mwisho. Hali kadhalika mapenzi, huo ndiyo mwanzo wa mwisho, chukua hatua
 
Mipaka ? Au minyau??

Mkeo anatakiwa awe rafiki yako ..
Mipaka weka na wafanyakazi wenzio ofisin...
Mkeo na watoto wanapaswa kuwa marafiki zako
 
Tafuta pesa wewe.mchicha ni type za majani ya magugu shambani.
Heshima kwa mwanamke ni pesa tu mengine utanunua sijui nguvu za kiume.
 
Una mwanamke sasa ni miezi kadhaa. Pengine una miaka kadhaa pamoja naye. Lakini kuna vitu anavifanya huelewi hujui ufanye nini. Hujui kama uko peke yako au la. Muda mwingi anakua na jeuri, anakudharau na kukupandishia sauti hadi unatamani umpige. Unajihisi huna uhuru tena ukiwa naye. Hutaki ata kuwa naye karibu. Mpaka unahisi anataka kukutawala yeye.

Chanzo kikuu ni kukosa mipaka.

Mipaka inaanzia kwako.
Jinsi unavyojiendesha wewe mwenyewe kama mwanaume. Hauwezi ukamfanya mtu aheshimu mipaka yako kama we mwenyewe huna/ hujui hiyo mipaka. Mipaka yako inaanza kwa kujijua wewe. Unapenda vitu gani, unataka siku yako iweje, unataka kuwa na marafiki aina gani, hutaki kumfanyia mtu kitu gani na yeye hutaki akufanyie kitu gani, nini chanzo cha amani yako, nini kinaondoa amani yako, na maswali kama hayo ndo yatakayoanza kukupa mwanga uwe na mipaka gani.

Mipaka yako ni thamani zako. Mipaka ni picha yako mbele ya jamii. Kama we unatukanwa na mkeo/ mwanamke wako/ na mwanamke yoyote. Picha yako ni mtu unayeburuzwa. Kama wanawake wakikuona wanaongea nawe kwa heshima. Picha yako ni ya mwanaume anayeheshimika.

Kama we hadi watoto wadogo wanakutania matani hadi ya nguoni. Picha yako ni mtu asiyeheshimiwa.

Mipaka pia inashushwa na we mwenyewe. Kwenye kuweka mipaka kuna kile kisauti kinakuambia “naweza nkampoteza huyu mwanamke/ atanionaje/ ataninyima kitu fulani”. Unajikuta unakausha. Unaendelea kuburuzwa lakini moyoni unaumia. Unavumilia. Kadri unavyozidi kuvumilia, ndivyo mipaka yako inavyozidi kuvamiwa.

Mwisho wa siku unajikuta huna mpaka, umeshatekwa na mwanamke. Umewekwa kiganjani. Mwanamke anakua hana wasiwasi na wewe, hakuogopi, anajua chochote anachofanya huwezi mfanya lolote. Japo anaweza kukuambia anahitaji uhuru, lakini haina maana usiweke mipaka.

Ubize, uoga, kukataliwa, au kuchukiwa kusiwe chanzo cha wewe kutokuweka mipaka. Jitahidi kuushinda woga wako. Jitahidi kuvuka mstari uliojiwekea ukiogopa kuharibu mapenzi. Mapenzi yoyote hayana maana kama ni ya kuumizana/ kurudishana nyuma. Hivyo huna sababu ya kuogopa kuchora mipaka yako. Ukisema kitu maanisha. Ukiweka mpaka maanisha.

Kuwa na msimamo. Sio umwambie mwanamke wako/ mkeo kitu alafu baadaye ubadilishe kisa umechuniwa. Au kisa umenyimwa penzi. Au kisa mwanamke ameanza kukuropokea na hutaki/ unaogopa kuzua gumzo. Huo ni ujinga na udhaifu. Wengi wanaoogopa wanawake waliofanikiwa hili ndo jambo linalowashinda. Wanajihisi wadogo mbele yao. Huwa inasikitisha mwanaume anatukanwa na mwanamke mbele ya umati, alafu anajichekesha tu.

Kama mtu hatokubali kuiheshimu mipaka yako basi hastahili muda wako. Na kama we mwenyewe huna mipaka ujue wewe ndiye uliyeruhusu kudharauliwa mana mwanamke wako ameona unamruhusu kufanya hivyo.
.....unachosema ni kweli kabisa chamato pia tuliyonayo wanaume kushindwa kuenenda kiusahihi katika kile kinachoitwa 'being romantic or gentlemen' , dada zetu pia walio wengi hawajui nanna ya kuishi na mtu anaeonekana kumjali Kwa mambo mengi, wao wnaona huyu ni sakala tu, ndo hapo unakuta mwanaume anakaripiwa na mke wake hadi unashangaa, nadhani waafrika turudi kwenye uhalisia wamaiha yetu ya kiafrika.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom