Matatizo yanayotukumba kwa sasa, ombwe la kiuongozi tulilo nalo kwa sasa chanzo ni mwalimu Nyerere, ni mwalimu huyo huyo aliona katiba yetu ni mbovu lakini hakufanya chochote kuibadilisha aliishia kusema tu.
Mwalimu Nyerere alikuwa nafasi ya kuifanyia mabadiliko katiba yetu ili hata siku tukipata kiongozi asiwe mungu mtu, kitendo cha kuiacha katiba mbovu ametuachia matatizo makubwa, yale aliyoyanena yanatokea kwa sasa.
Ni katiba imetufikisha hapa rais anapewa madaraka makubwa mno, yeye huyo huyo anaweza kufanya kazi ya mahakama, kazi ya bunge na serikali, rais anateua kila nafasi kubwa tena ana uwezo wa kuteua mtu yeyote bila kuhojiwa na yeyote, hebu fikiria rais anateua mwenyekiti wa tume ya uchaguzi,wakurugenzi wa tume, na hata wakurugenzi wa majiji,manispaa,miji,na wilaya, ambao wanasimamia uchaguzi.
Imefika mahali rais amekuwa mungu mtu, hakosolewi kwa lolote, hasemwi kwa lolote akisema hapingwi kwa lolote, ukifanya hivyo wanasema umemtukana na unakamatwa kwa uchochezi, tumekuwa taifa la kusifia na kupongeza hata kama huoni chochote kinachofanyika, sababu kubwa ni katiba iliyompa madaraka makubwa.
Kitendo cha mwalimu Nyerere kuliona hili na akakaa kimya alitusaliti watanzania na kutuacha kwenye matatizo makubwa, ni sawa baba kumuona nyoka mkubwa ameingia chumbani kwa watoto wako baadala ya kumtoa unaishi kusema ipo siku huyo nyoka atawang'ata.
Mwalimu Nyerere alikuwa nafasi ya kuifanyia mabadiliko katiba yetu ili hata siku tukipata kiongozi asiwe mungu mtu, kitendo cha kuiacha katiba mbovu ametuachia matatizo makubwa, yale aliyoyanena yanatokea kwa sasa.
Ni katiba imetufikisha hapa rais anapewa madaraka makubwa mno, yeye huyo huyo anaweza kufanya kazi ya mahakama, kazi ya bunge na serikali, rais anateua kila nafasi kubwa tena ana uwezo wa kuteua mtu yeyote bila kuhojiwa na yeyote, hebu fikiria rais anateua mwenyekiti wa tume ya uchaguzi,wakurugenzi wa tume, na hata wakurugenzi wa majiji,manispaa,miji,na wilaya, ambao wanasimamia uchaguzi.
Imefika mahali rais amekuwa mungu mtu, hakosolewi kwa lolote, hasemwi kwa lolote akisema hapingwi kwa lolote, ukifanya hivyo wanasema umemtukana na unakamatwa kwa uchochezi, tumekuwa taifa la kusifia na kupongeza hata kama huoni chochote kinachofanyika, sababu kubwa ni katiba iliyompa madaraka makubwa.
Kitendo cha mwalimu Nyerere kuliona hili na akakaa kimya alitusaliti watanzania na kutuacha kwenye matatizo makubwa, ni sawa baba kumuona nyoka mkubwa ameingia chumbani kwa watoto wako baadala ya kumtoa unaishi kusema ipo siku huyo nyoka atawang'ata.