Elections 2010 Changia kesi dhidi ya Mahanga vs Mpendazoe

Nashukuru kwa kunikaribisha jamvini wana JF japokuwa sikubisha hodi.
Ni matumaini yangu kuwa kutokana na jamvi hili nchi yetu ya Tz itaweka historia ambayo vizazi vijavyo vitaithamini na kuienzi.
Tutaendeleza mapambano ndani ya jamvi na zaidi zaidi tunakoishi ili kuhakikisha kizazi chetu hiki hakipiti kabla tanzania yenye neema kupatikana.
ANY

Hakuna shida karibu sana saa nyingine mlango unakuwaga wazi tu na mgeni anachoma ndani straight karibu sana.
 
Kama huna cha kuchangia jamanai aacheni kuuma maneno kheri ukae kimya
 
Tupambane daima, tuungane, si kwa kesi ya Fred pekee bali popote ambapo unyang'au umefanyika kuiba haki na ushindi, kesi za kupinga matokeo ni lazima kufanywa na haki kupatikana

naafiki mwanangu hata ikibidi nitaua mlo mmja kitakacho patikana nichangie ukombozi!
 
Hapo umelenga. Kwa sasa anaitwa "mtaalam wa open space". Katika jimbo la Segerea, anaongoza kwa kuvamia maeneo ya wazi. Wengi mtakuwa mnajua Nyantale ...

Kumbe Nyantale ni ya kwake???!!!!!! mi sitii mguu pale tena! shwain, bure kabisa!
 
Bwana Quality na wengine ambao wanaweza kututumia mchanganuo ufuatao utatusaidi wengine tulio nje ya Tz kuweza kuwakilisha michango yetu pia.

BANK NAME:
BANK ADDRESS:
ACCOUNT NAME:
SWIFT CODE:
ACCOUNT NUMBER, ACCOUNT TYPE
ROUTING NUMBER & BRANCH NUMBER
Na kama kuna IBAN itasaidia pia japo kuwa nashaka kuwa Tz huwa hatutumii IBAN as such.
Kwa kifupi maelekezo ya kutosha kumwezesha mtu kutuma pesa moja kwa moja kwenye akaunti kutoka nje ya Tz.

Aluta continua...

pOLE IMECHUKUA MUDA SABABU NILISAFIRI KIDOGO. nDO NIMERUDI NA KUPATA INFO KUTOKA KWA MPENDAZOE MWENYEWE. SO INFO NI KAMA ZIFUATAZO:

BANK NAME: Tanzania Posta Bank
BANK ADDRESS: AZIKIWE STREET, DAR ES SALAAM

Branch: Mkwepu
ACCOUNT NAME: MPENDAZOE & FRIENDS
SWIFT CODE: TAPBTZTZ
ACCOUNT NUMBER: 010-00263962

ACCOUNT TYPE: SAVINGS
Note: Use CITI BANK or STANDARD CHARTERED BANK to send money to this account because they have a contract with TPB
 
Tuwekee wazi jinsi ya kuchangia. Wenye akili fupi bado wanaamini dhuluma inaweza kutawala ulimwengu daima. Si kweli. Mwisho wake ukweli utashinda na huyo Mahanga kama hijui mwisho wake hauko mbali

Matawi,
kuchangia, tumia njia zifuatazo:
(i) Akaunti namba 010-00263962 Benki ya posta- Mpendazoe & Friends

(ii) M-Pesa simu namba 0762 926556
(iii) Zap simu namba 0787 638575 na
(iv) Tigo pesa simu namba 0717 050335 au 0656 650334
 
Huyu Mpendazoe alimuiga Augustine Mrema, akapiga kelele bungeni, akajitoa CCM akifikiri atagombea urais Chama cha Jamii matokeo yake kajikuta anahangaika, siasa hesabu. Asingejitoa CCM leo si angeendelea kuwa mbunge, mwacheni aendelee kuumia

Maskini Mpendazoe.
 
Sasa kama mahakama zipo, na hao majaji wanateuliwa na Rais ambae mnasema hakuchaguliwa kwa haki, nashindwa hata kuwaelewa, contradictions tupu. Hamjuwi mlifanyalo mnatapa-tapa kama wafa maji.

Ushauri: kama mnaikubali mahakama basi mkubali na matokeo ya uchaguzi, msipoteze wakati. Mlikuwa na wasimamizi vituoni, hamuwaamini? Na ikiwa hata hao wasimamizi wenu hamuwa amini, ni kweli mtaweza kukubali hukumu zitazotolewa na mahakama ambayo majaji wake wanateuliwa na Rais msiemkubali? Hamueleweki.

Wacheni Jazba, nendeni bungeni mkachape kazi, jifunzeni kwa wenzenu wa CUF, walijaribu mbinu zote hizo, matokeo, kuvunjika kwa amani. Walipoamuwa kukaa chini na kusikilizana, na JMK ni msikivu, wakakubaliana yakaisha na sasa wanakula matunda ya uhuru.

Hili nalo neno.
 
Kesi imeshapangangiwa jaji wa kusikiliza kesi za gharama hope january itaanza
 
kuchangia, tumia njia zifuatazo:
(i) Akaunti namba 010-00263962 Benki ya posta- Mpendazoe & Friends
(ii) M-Pesa simu namba 0762 926556
(iii) Zap simu namba 0787 638575 na
(iv) Tigo pesa simu namba 0717 050335 au 0656 650334

Nitachangia kupita kwenye blue
 
Alipokuwa Mbunge alipata marupurupu ya kutosha je aliyapeleka wapi? Kama aliwarudishia watu wa kishapu fadhila its okay wao wangelikuwa wa kwanza kumchangia..... NASIKITIKA, TUNA MATATIZO YA MSINGI YA KUCHANGIA KAMA ELIMU NK. kwa hili mtanisamehe... kwa maana sijui kama tukishamchangia hatoenda kuanzisha CHAMA KIPYA!!:embarrassed:
 
Huyu Mpendazoe alimuiga Augustine Mrema, akapiga kelele bungeni, akajitoa CCM akifikiri atagombea urais Chama cha Jamii matokeo yake kajikuta anahangaika, siasa hesabu. Asingejitoa CCM leo si angeendelea kuwa mbunge, mwacheni aendelee kuumia

CCM alikuwa anapingwa sana kwa kauli zake dhidi ya Mkapa Bungeni, ni wazi asingepata kitu, tena kulikuwa na tetesi angetimuliwa Uanachama wa CCM katika kikao amboacho kingekutana J5, yeye akajitoa J3, nadhani alipata Inside information
 
Sasa kama mahakama zipo, na hao majaji wanateuliwa na Rais ambae mnasema hakuchaguliwa kwa haki, nashindwa hata kuwaelewa, contradictions tupu. Hamjuwi mlifanyalo mnatapa-tapa kama wafa maji.

Ushauri: kama mnaikubali mahakama basi mkubali na matokeo ya uchaguzi, msipoteze wakati. Mlikuwa na wasimamizi vituoni, hamuwaamini? Na ikiwa hata hao wasimamizi wenu hamuwa amini, ni kweli mtaweza kukubali hukumu zitazotolewa na mahakama ambayo majaji wake wanateuliwa na Rais msiemkubali? Hamueleweki.

Wacheni Jazba, nendeni bungeni mkachape kazi, jifunzeni kwa wenzenu wa CUF, walijaribu mbinu zote hizo, matokeo, kuvunjika kwa amani. Walipoamuwa kukaa chini na kusikilizana, na JMK ni msikivu, wakakubaliana yakaisha na sasa wanakula matunda ya uhuru.
Wewe Dar es Salaam, acha wachange hizo fedha. Kazi ya fedha hizo za deposit ni kuwezesha pia washitakiwa waje walipwe gharama za kesi kama anayeshitaki akishindwa kesi. Itamwuma sana huyo mtu wao kama atatakiwa kuwalipa washitakiwa baada ya kesi yake kutupiliwa mbali kama fedha ni ya kwake. Lakini kwa kuwa atakuwa amechangiwa hizo fedha wala hataona uchungu. Wanaweza kudhani wanamchangia Mpendazoe kumbe wanamchangia Mahanga! Wajinga ndiyo waliwao!
 
Hapo umelenga. Kwa sasa anaitwa "mtaalam wa open space". Katika jimbo la Segerea, anaongoza kwa kuvamia maeneo ya wazi. Wengi mtakuwa mnajua Nyantale ...

Mimi namfahamu sana Mahanga. Iko siku watu kama QUALITY na Msaki001 watajua kwamba Mahanga si fisadi wa elimu bali ni msomi, mwalimu, mtafiti na mwana taaluma mahiri. Iko siku watajua Mahanga si fisadi wa viwanja wala mvamizi wa open spaces, na kwamba huko Segerea wala hana kiwanja chochote zaidi ya hicho kiwanja anapoishi. Iko siku watu kama QUALITY na Msaki001 watajua kwamba Mahanga hafanyi biashara ya baa, na wala hizo baa za Nyantare si za kwake, na wala hamjui hata kwa sura huyo mwenye baa hizo. Iko siku watajua kwamba Mahanga si mwizi wa kura na alishinda kihalali jimbo la Segerea. Lakini iko siku watu kama QUALITY watajua kwamba hata Mpendazoe hajamtuhumu Mahanga kwenye kesi aliyofungua Mahakama Kuu! Ndiyo maana Mwenyezi Mungu anaendelea kumlinda na kumpa Baraka pamoja na chuki na wivu wa kisiasa zinazoelekezwa kwake kwa sababu tu ya ukweli, msimamo na ujasiri wake wa kupigania haki yake na yale anayoyaamini. Nimalizie kwa kuwaomba watu kama QUALITY na Msaki001 wasinunue tu uzushi na chuki za mitaani na kuzibeba wao kama za kwao bila kuzitafiti kama wajinga. MAFISADI WA USHUZI WAKUBWA NYIE!!
 
Well said bro/sisy,magazeti ya leo yamereport kuwa polisi imemsafisha mpendazoe ni baada ya kumsingizia gari la wizi.hii ina maana ilikuwa ni mbinu chafu inayotumiwa na mpinzani wake kumpunguza nguvu ila atashindwa tu na unaibu waziri ataucheua
Jamani mbona mnakuwa nincompoops! Hamtumii hata akili zenu na hata mbayuwayu anawashinda? Mnachoambiwa au kusikia ni vyema mkachanganya na akili zenu kabla ya kukurupuka! Hivi Mahanga ndiye aliyembeba Mpendazoe akamwuingiza ndani ya gari lililokuwa linatafutwa na polisi kwa tuhuma za ujambazi? Naona kwa akili zenu kuanzia sasa Mpendazoe akipata mafua tu au akijikwaa ni Mahanga atakuwa amehusika! Na hata huyo "mke" wake aliyemwacha na kutorokea Darfur bila shaka mtasema Mahanga ndiye kamtorosha! Hata hiyo nyumba yake inayopigwa mnada kwa madeni bila shaka mtasema Mahanga anahusika! By the way, baada ya nyumba yake kupigwa mnada kurudisha madeni, kwanini balance inayobaki (kama itakuwepo) asitumie kwa gharama za kesi badala ya nyie nincompoops kumchangia? Mwaka huu mtamchangia mpaka mkome! Baada ya kumchangia kwenye kesi mjiandae kumchangia kumjengea nyumba baada ya hii ya sasa kupigwa mnada!
 
Back
Top Bottom