Changamoto za mpenzi zinanikosesha raha

Changamoto za mpenzi zinanikosesha raha

Akikublock nawe mblock ili akija kuku-unblock akute block yako ili ajue inavyokera

Alafu mbona haya ya kublock huwa tunafanya sisi wa kike
Pacha ndio ujue wanaume wanavyoelekea kupungua.

Mana mwanaume na block wapi na wapi. Chaaaaa.
 
Fal* huyo achana nae, Kama vipi chukua hata pic yangu weka katika prof pic ya whatsapp, alafu Annika jinsi unavyofurahia kuwa na mwaume anayekujali....shenzy kbsa
Aisee sio kwa kutopenda ujinga kiasi hicho swahiba. Lol
 
Habari zenu?

Moja kwa moja niende kwenye mada.

Mimi ni mdada mwenye elimu yangu, kazi zangu na malengo mazuri nikipata uhai na kibali cha Muumba.Nilipata mpenzi ambaye tumedumu nae kwa mwaka sasa. Ananijua vema. Kuanzia familia mpaka kila kitu kinachonihusu. Yeye pia ninamjua sana hata familia yake ingawa hatujatambulishana. Mwenzangu simuelewi. Mwanzo alinijali kwa kidogo alichonacho.

Kabla sijapata kazi yeye alikua namba moja kujua nimekula nini au kuvaa nini.Lakini baada ya mwenzangu kuhamishia makazi yake mbali kidogo na nyumbani, amebadilika sana.Hanijali kama mwanzo.

Ugomvi kidogo ukitokea ananiblock. Hata kama hakuna la maana. Kuunblock ni mpaka ajisikie yeye. Anaweza akakaa hata mwezi alafu akanipigia simu usiku kuomba radhi na maisha yanaendelea.

Hapo atafululiza kunijali kwa siku kadhaa lakini ninapomuuliza jambo ambalo pengine amenikosea, basi anasusa na kuniblock. Kuniunblock tena ni mpaka ajisikie. Lakini ni lazima anarudi.

Wakuu mi simuelewi. Nimeshamsema tabia hii na bado nikaambulia block. Nikamtafuta kwa namba mpya na kumwambia bora tuachane. Akakubali lakini baada ya siku kadhaa akanipigia simu na kuniomba msamaha na kudai hawezi kuniacha kabisa.

Wakuu hapa nilipo nimepigwa block tena. Nimemuambia asirudi tena ingawa najua atarudi. Siwezi kubadili namba kwa ajili yake. Hivi na wengine wanapata changamoto kama mimi au? Mimi nimechoka kwa kweli.

Ananiambia nimvumilie ye ndivyo alivyo. Namwambia anapoteza muda sana, huo muda wa kuniblock tungekuwa tumefanya jambo la maana la maendeleo, wala haelewi. Na ni mtu mzima kuliko mimi. Yeye ana 28 years sasa.
Huyo ni mtu mzima miaka tuu !! Kifikra bado anaonekana ni teenage..!! Ni ngumu sana kutoka ushauri wa kimahusiano, wewe pekee ndio unajua umuhimu na hasara za huyo mtu, ni kiasi cha wewe Kuchagua jema na kuacha mabovu, maisha yakianza huta kuwa na sisi, kwahiyo jaribu kujiongeza kitu uzima, onesha utofauti wako wewe na huyo kiumbe wa kiume...!! Msimamo utakusaidia kwenye maisha yako, usiwe gari bovu..
 
Huyo atakuwa ni Moderator wa jf si bure.
Kazoea kila kosa adhabu ni block tu kama Ban.

Chunguza vizuri kazi yake utakuja kuniambia hapa.
 
Amesema mwanaume ana 28,ni mkubwa sana
Hahaaa. Huo ni ukubwa kiumri ila kiakili bado hajakomaa. Ila pacha wacha mapenzi yaitwe mapenzi mana unaweza kuta mtu anafanyiwa vitu ambavyo ukikaa unajiuliza mara tatu tatu kwa nini achangamshi akili na kuona anavyofanyiwa havifai.
 
Habari zenu?

Moja kwa moja niende kwenye mada.

Mimi ni mdada mwenye elimu yangu, kazi zangu na malengo mazuri nikipata uhai na kibali cha Muumba.Nilipata mpenzi ambaye tumedumu nae kwa mwaka sasa. Ananijua vema. Kuanzia familia mpaka kila kitu kinachonihusu. Yeye pia ninamjua sana hata familia yake ingawa hatujatambulishana. Mwenzangu simuelewi. Mwanzo alinijali kwa kidogo alichonacho.

Kabla sijapata kazi yeye alikua namba moja kujua nimekula nini au kuvaa nini.Lakini baada ya mwenzangu kuhamishia makazi yake mbali kidogo na nyumbani, amebadilika sana.Hanijali kama mwanzo.

Ugomvi kidogo ukitokea ananiblock. Hata kama hakuna la maana. Kuunblock ni mpaka ajisikie yeye. Anaweza akakaa hata mwezi alafu akanipigia simu usiku kuomba radhi na maisha yanaendelea.

Hapo atafululiza kunijali kwa siku kadhaa lakini ninapomuuliza jambo ambalo pengine amenikosea, basi anasusa na kuniblock. Kuniunblock tena ni mpaka ajisikie. Lakini ni lazima anarudi.

Wakuu mi simuelewi. Nimeshamsema tabia hii na bado nikaambulia block. Nikamtafuta kwa namba mpya na kumwambia bora tuachane. Akakubali lakini baada ya siku kadhaa akanipigia simu na kuniomba msamaha na kudai hawezi kuniacha kabisa.

Wakuu hapa nilipo nimepigwa block tena. Nimemuambia asirudi tena ingawa najua atarudi. Siwezi kubadili namba kwa ajili yake. Hivi na wengine wanapata changamoto kama mimi au? Mimi nimechoka kwa kweli.

Ananiambia nimvumilie ye ndivyo alivyo. Namwambia anapoteza muda sana, huo muda wa kuniblock tungekuwa tumefanya jambo la maana la maendeleo, wala haelewi. Na ni mtu mzima kuliko mimi. Yeye ana 28 years sasa.
Stop! Wewe ni dada au kaka? Ninatamani kurudi kwake...
 
Hahaaa. Huo ni ukubwa kiumri ila kiakili bado hajakomaa. Ila pacha wacha mapenzi yaitwe mapenzi mana unaweza kuta mtu anafanyiwa vitu ambavyo ukikaa unajiuliza mara tatu tatu kwa nini achangamshi akili na kuona anavyofanyiwa havifai.
Mapenzi upofu
Hapa watu watamshauri weee ila utakuta yupo na huyo mpenzi wanatusoma tu na comments zetu wanatucheka
 
Kwa uelewa wangu na kwa vile mimi ni mhenga, kwa ushauri mzuri tu Dada achana na huyo jamaa hana jipya bali anakupotezea muda. Pia nawe mpige block na ingekuwa vizuri u install true call upige block unknown numbers ili hata akibadili namba inakuwa rejected pia piga block hadi sms za kawaida na whatsapp ili apate akili kwanza maana huyo jamaa hajui maisha
 
Mapenzi upofu
Hapa watu watamshauri weee ila utakuta yupo na huyo mpenzi wanatusoma tu na comments zetu wanatucheka
Umeonaeee. Huwa siamini kwamba ushauri anaopewa mtu huwa anaufata huo huo bali huwa naamini huwa anajazia katika kile alichonacho akilini mwake.
 
Ingekua ni mimi ningeshafanya maamuzi magumu. Habari ya kupotezeana muda hapana aise
 
Ivi kwann utesek na mtu mmoj tu why ulizaliw nae? Si umpotezee uangalie mtindo mwingine wa maisha duh mi sjawai tesek ivo ATI mapenz labda uenda namm yatanifik ila sizan


mie mwenyewe jaman sinaga histry za namna hii ! mie huyu angeniblock kwa mara ya kwanza tu ndo ingekuwa tiket yake dadek zake !sema huyu mdada naye ana mpenda !
 
wewe dada kuwa makini sana na huyo mwanaume wako aisee !au ni kitinda mimba kwao? na kweli suala la kushare mirad bado hamjatambulishana UKOME
 
Kwa kifupi huyu mtoa mada bado anampenda huyo kaka sema changamoto hizo ulizoeleza.Endelea Ku Pima kwa mda kidogo asipobadilika angalia mbele asikupe presha.
 
Pole sana...

Akiku-block... Usihangaike sana... Nenda kwenye WhatsApp yako weka DP ya mwanaume ambayo siyo yeye...

Siku akiku-unblock na akaamua kukutumia WhatsApp anakutana na DP ya mwanaume.. Na ka-status kakisema.

Thank you God.

Wait and see...



Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom