Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,349
Katika umri wa 40+ wengi wanakua na watoto, iwe kwenye ndoa au nje ya ndoa. Ni nadra kumkuta mtu wa 40+ hana mtoto.
Katika harakati za maisha wengine wameachana na wenza wao na wengine kufiwa. Kwa kuepuka upweke wengi hutafuta mtu wa kuliwazana nae.
Mnapokutana wawili kufahamiana na kuona kama mtawezana hiki ni kipengele A cha mtihani. Kipengele B ni kukutana na watoto.
Mara nyingi watoto wa kiume hawana matatizo. Usiombe ukutane na mabinti. Kwanza watakulinganisha na mama yao au baba yao Watataka kujua unafanya kazi gani. Hapa sasa ndipo panakuja swala la U-gold digger. Wanafikiri ulimpenda baba yao au mama yao kwakua ana mali. Kumbe mwenyewe umesharidhika na maisha yako ila ni huyu baba yao au mama yao ndiye anaekuhitaji mno katika maisha yake.
Katika harakati za maisha wengine wameachana na wenza wao na wengine kufiwa. Kwa kuepuka upweke wengi hutafuta mtu wa kuliwazana nae.
Mnapokutana wawili kufahamiana na kuona kama mtawezana hiki ni kipengele A cha mtihani. Kipengele B ni kukutana na watoto.
Mara nyingi watoto wa kiume hawana matatizo. Usiombe ukutane na mabinti. Kwanza watakulinganisha na mama yao au baba yao Watataka kujua unafanya kazi gani. Hapa sasa ndipo panakuja swala la U-gold digger. Wanafikiri ulimpenda baba yao au mama yao kwakua ana mali. Kumbe mwenyewe umesharidhika na maisha yako ila ni huyu baba yao au mama yao ndiye anaekuhitaji mno katika maisha yake.