Mkuu Sasa kidogo kidogo unaelekea kwenye hoja.Bahati nzuri Wewe Ni mtu unayejua maana Na matumizi ya mantiki.Ni Hivi uwezo wa Mungu hauko Limited Kwa namna yoyote ile Na kitu chochote kile.Sio Wakati au mahali kunaweza ku-limit uwezo wake.Sasa suala la kuumbwa Kwa mwanadamu Na kisha kumegewa uhuru Na utashi wa kujua jema Na baya ilikuwa sahihi Kabisa.Uhuru Kwamba aweze kuamua kadri anavyoona inafaa Kwa manufaa yake Na ya wenzie.Bila Uhuru leo ina maana ungehitaji kulala muda huu ungepaswa mtu mwingine akupe idhini hiyo.Ukitaka kula kiti moto leo mtu mwingine akupe kwanza ruhusa.Utashi unakusaidia kujua kuwa Huwezi kulala barabarani pamoja na Uhuru wa kufanya hivyo maana utahatarisha uhai wako wa kimwili Na kiroho.Utashi utakuonyesha kuwa kushindwa kuwajibika Kwa labda kufanya kazi Ni kuhatarisha maslahi yako Na ya jamii inayokuzunguka pamoja na Kwamba umepewa Uhuru huo kiasilia.Kumbe Vyote Ni check and balance.Sasa ikiwa mtu amepata imani inayomuambia kuwa kumtoa mwenzake uhai wa kimwili Ni tiketi ya kwenda Mbinguni au mtu akaamua kueneza imani ya Ukiristo Kwa kukomelea watu majambia viunoni au kueneza mafundisho ya Kikiristo Kwa "kudukua" vyeti vya "Bashite" hiyo imani inakuwa inakosa uhalali Na siyo Mungu mwenyewe ambaye asili yake Ni "Check and Balance".
Kwa hiyo kusema dini zimeenezwa Kwa migogoro Na mauaji Ndio iwe concluding premises Kwamba Mungu hayupo hiyo inakuwa Fallacy. Hivi Wewe ukifeli Kwa mfano ku-solve equation fulani ina maana aliyetunga hiyo equation naye hayupo(non-existing)? Au Wewe ukishindwa kuendesha gari vizuri ukatumbukia mtoni tuhitimishe kuwa mtengeneza gari Na gari vyote havipo na havina maana? Imani Ni utaratibu wa kuhusiana Na Mungu tuliopewa.Ikiwa sisi tunavuruga utaratibu huo Na au tunashindwa ku-handle system hiyo basi hiyo haiondoi uwepo wa Mungu!
HOJA Kwamba kama Mungu angekuwepo basi tungemufahamu tu bila kufundishwa hii nayo inajibika tu. Ni Hivi Kwa kuwa uwezo wake hauna kikomo Na au hachaguliwi njia au mfumo wa kufanyia mambo yake dhidi yetu basi aliona iwe hivyo Kwamba binadamu Lazima wajulishwe Na binadamu Wenzao kuwa Yeye yupo Na ndiye muumba wa vyote ikiwemo huo uwezo wa Yeye kuchagua kuwasiliana Na binadamu kupitia binadamu Wenzao.Hivi leo Baba yako akiamua kukueleza jambo kupitia Mkeo au mama ina maana Baba anakuwa anaondoka kwenye "Ubaba"? Anakoma kuwa ndiye " recreator" wa uhai wako toka mwanzo? Au Magufuli akimtuma CS Kwa Waziri Nape kufikisha ujumbe Fulani ina maana Ukuu wa Magufuli unakoma?
Basi ndugu yangu Mungu yupo kweli.Na ukikaa ukituliza Akili, Utashi Na Uhuru wako utagundua kweli Yu Mkuu kweli kweli.Na kila alilotenda Na atendalo Ni jema sana.Shida iko kwetu.Watu wanatamani wamshike au wamwone.Hivi hoja Ni kumuona tu basi? Hivi hoja Ni kuongea naye Kwa ndimi zetu hizi kama tunavyoongea Na Makonda? Hivi hoja Ni aondoe magumu tu katika maisha yetu basi ili Ndio ionekane yupo kweli? Basi hata hayo yangefanyika bado tungeweza kusema huyo Sio Mungu wa uweza wote.Maana tungeweza kuhoji tena Mbona hawezi kupotea au kujificha? Mbona hawezi kuuumba magumu au matatizo? Tungehoji Mbona mambo mengi kinyume tu cha tuyatakayo Leo.
Je huo uwezo wa Mungu ni nani aliyeuchunguza na kujua kuwa haupo limited? na alijuaje kuwa ni unlimited?
Kusema kuwa Mungu amewapa watu uhuru wa kutenda watakavyo[free will?] nayo ni contradiction. Maana haiingi akilini kusema Mungu aliwapa watu uhuru wa kutenda jinsi watakavyo lakini walipofanya hivyo Mungu huyo huyo aliyewapa freewill aliangamiza miji yao kwa moto pamoja na mafuriko ya dunia nzima.Je ni Mungu gani huyo anayetoa uhuru wa kutenda utakavyo lakini ukifanya utakavyo anaingilia uhuru wako?[Fairly, is he a celestial dictator?]
Halafu unaposema ''kujua jema na baya'' unatumia mizani ipi kujua hili ni jema na lile ni baya? je hiyo mizani yako ni imara kuliko ya wengine? maana lililo jema kwako kwa mwingine laweza kuwa baya.Lakini pia ni nani aliyetoa mizani ya kujua jema na baya?
Hata mimi sikubaliani na wanaojitoa muhanga ili waione pepo au wale wanaoeneza imani zao kwa majungu.Lakini pia sikubaliani na watu wanaojikataza kuoa, wanaacha mabilioni ya wanawake, wanakumbwa na kashfa ya kulawiti vivulana vidogo. Hapa napo ni kufikiri irrationally, maana hii species yetu ni designed kwamba ME na KE waishi kwa pamoja, wazae watoto ili species isonge mbele na ndio maana nature imeweka argue ya unison kati ya ME na KE[Things are not always constant]. Sasa ujinga ni mtu kupata hamu ya ku procreate then anaishia kulawiti vivulana kwa sababu zisizo za msingi.
Imani ingekuwa na maana kama uhalisia, dini, pamoja na mapenzi ya Mungu vingekuwa vinapatana kwa pamoja. Yaani pawepo na mtiririko wa kimantiki kwanzia kwenye mapenzi ya Mungu, Dini pamoja na uhalisia. Siyo dini iseme kuwa Mungu hapendezwi na Homosexual lakini wakati huo huo mashoga na mamame wanazaliwa kila uchao kwenye dunia inayodhaniwa kuwa iliumbwa na Mungu.
Mimi Baba yangu akiniagiza jambo kupitia kwa watu wengine sintakuwa na shaka maana ninamfahamu Baba yangu. Lakini mtu anapokuja from nowhere na kusema Mungu[ambaye hawezi kuthibitisha kama yupo] amesema utende jambo fulani na haya mambo usiyafanye siwezi kukubaliana naye. Kwangu naona kama ni watu wachache wenye nia ya kutekeleza matakwa yao wayajuayo wenyewe. Je nitakuwa na uhakika upi kwamba huyo Mungu ndio yupo sahihi? lakini kama yupo, je uko wapi uthibitisho?
Nihitimishe kwa kusema imani isiyo na ushahidi wala maelezo yenye mantiki juu ya inachokisimamia haina tofauti na superstition. Huenda ukabeba imani lakini mwisho wa siku ukaambulia patupu na hivyo kuyafanya maisha yako hapa duniani kama hasara kwa kuliwa na kutawaliwa na imani potufu.