Miguel255
Member
- May 13, 2020
- 35
- 111
Sasahivi wanaotamba mjini ni wale wenye nyumba zenye visima. Yaani wakati watu wanahangaika na foleni ya madumu wao wanaoga kutwa mara mbili mpaka tatu, wanafua kila siku na wengine hadi maua wanamwagilizia.
Hii hali imenikumbusha kipindi fulani nafanya kazi kwa wahindi upanga dar es salaam. Wahindi wanatabia moja inayofanana sijui kama sikuhizi wameacha, yaani mshahara unalipwa siku ya mwisho wa mwezi. Yaani kama mwezi una siku 30 basi tarehe 30 ndo unalipwa kama una siku 31 ndo hio hio unalipwa.
Ukisikia mshahara mwisho wa mwezi ni mwisho wa mwezi kweli. Sasa ile hela haikuwa inatosha hata kidogo ni vile tu mtembea bure sio sawa sawa na mkaa. Kuna zile tarehe fulani za hatari kuanzia tarehe 20 unakuta pesa uliyonayo ni ndogo vibaya mno alafu lengo ufike mwisho wa mwezi.
Bajeti inayotembezwa hapa ni kali vibaya mno, bajeti ya msosi inapunguzwa, hela ya nauli inapunguzwa, hakuna kununua vocha hakuna kununua soda yaan lengo kuu kuendelea kuwa hai sio ku'enjoy. Sasa kuna kipindi hasa hasa nikiingia shift ya usiku kutoka asubuhi nikawa natembea kwa mguu kutoka upanga mpaka kawe ili nisave buku niongezee kwenye msosi
🤣🤣🤣🤣🤣 ila maisha haya
Sasa unatembea njiani unakuta majamaa yapo bar yanakunywa bia meza imechafuka vibaya mno. Wengine wamelewa chakali hasa hasa siku za ijumaa kuamia jmosi au jmosi kuamkia jumapili.
Unabaki unajiuliza hivi mimi na hawa wote tunaishi tanzania au wenzangu wanaishi nje ya nchi huku wanakuja tu kutumia? najiuliza sipati jibu naendelea kukanyaga vumbi tu
Wakati wanaamka kusaka maji kipindi hiki cha shida ya maji, kuna watu shida ya maji wanaisikia kwenye taarifa za habari tu. Na wote manishi nchi moja pengine jiji moja na usikute hata ni majirani. Hivyo hivyo Wakati mimi natembea kusave buku nipate hela ya kula kuna watu walitapanya pesa kwenye pombe na niliona live.
Lengo la huu uzi ni kukumbusha tu hakuna hali inayodumu milele. Cha msingi usikate tamaa, ongeza bidii lakini pia muombe sana Mungu. Sisemi haya kwamba nishajipata, la hasha ila siwezi tena tembea umbali wote kisa buku.
Kwahiyo kama unapitia changamoto fulani we jiambie HILI NALO LITAPITA
Hii hali imenikumbusha kipindi fulani nafanya kazi kwa wahindi upanga dar es salaam. Wahindi wanatabia moja inayofanana sijui kama sikuhizi wameacha, yaani mshahara unalipwa siku ya mwisho wa mwezi. Yaani kama mwezi una siku 30 basi tarehe 30 ndo unalipwa kama una siku 31 ndo hio hio unalipwa.
Ukisikia mshahara mwisho wa mwezi ni mwisho wa mwezi kweli. Sasa ile hela haikuwa inatosha hata kidogo ni vile tu mtembea bure sio sawa sawa na mkaa. Kuna zile tarehe fulani za hatari kuanzia tarehe 20 unakuta pesa uliyonayo ni ndogo vibaya mno alafu lengo ufike mwisho wa mwezi.
Bajeti inayotembezwa hapa ni kali vibaya mno, bajeti ya msosi inapunguzwa, hela ya nauli inapunguzwa, hakuna kununua vocha hakuna kununua soda yaan lengo kuu kuendelea kuwa hai sio ku'enjoy. Sasa kuna kipindi hasa hasa nikiingia shift ya usiku kutoka asubuhi nikawa natembea kwa mguu kutoka upanga mpaka kawe ili nisave buku niongezee kwenye msosi
🤣🤣🤣🤣🤣 ila maisha haya
Sasa unatembea njiani unakuta majamaa yapo bar yanakunywa bia meza imechafuka vibaya mno. Wengine wamelewa chakali hasa hasa siku za ijumaa kuamia jmosi au jmosi kuamkia jumapili.
Unabaki unajiuliza hivi mimi na hawa wote tunaishi tanzania au wenzangu wanaishi nje ya nchi huku wanakuja tu kutumia? najiuliza sipati jibu naendelea kukanyaga vumbi tu
Wakati wanaamka kusaka maji kipindi hiki cha shida ya maji, kuna watu shida ya maji wanaisikia kwenye taarifa za habari tu. Na wote manishi nchi moja pengine jiji moja na usikute hata ni majirani. Hivyo hivyo Wakati mimi natembea kusave buku nipate hela ya kula kuna watu walitapanya pesa kwenye pombe na niliona live.
Lengo la huu uzi ni kukumbusha tu hakuna hali inayodumu milele. Cha msingi usikate tamaa, ongeza bidii lakini pia muombe sana Mungu. Sisemi haya kwamba nishajipata, la hasha ila siwezi tena tembea umbali wote kisa buku.
Kwahiyo kama unapitia changamoto fulani we jiambie HILI NALO LITAPITA