Kuna harakati nyingi sana zinafanywa na hichi "chama cha wavaa magwandwa" katika operesheni tofauti tofauti kwa lengo la kutwaa dola.
Ingawa viongozi wa chama hiki wamekuwa wabunifu wa kutumia njia mbalimbali kama mikutano ya hadhara, maandamano yasiyo na vibali, fujo na shari, kutoheshimu mamlaka zilizopo na mbaya zaidi kutokuwa na nidhamu na ustaharabu wa wabunge wa chama hiki katika bunge letu tukufu la jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuathiri mara kwa mara shughuli za bunge kufanyika kama ilivyopangwa na kufanya heshima na thamani ya bunge kumomonyoka mbele ya jamii ndani ya nchi na hata nje ya nchi.
Yote haya wanafanya kwa lengo la kujipatia umaarufu, taifa liwatambue kuwa wao ndio tumaini la ukombozi wa taifa, liwajengee imani kuwa wao ndio watabadili hali za watanzania wa chini kabisa na kuwapa unafuu wa maisha.
Uongo wa waziwazi wa wavaa magwanda ndio huu, kujifanya wanajali kundi la walalahoi huku wao ndio vinara wa kula bata mjini, wanachukua pesa za wavuja jasho kwa kigezo cha kuchangia chama wakati wanapata ruzuku kutoka serikalini ambayo hatujui pesa hizo za walipa kodi wanafanyia nini.
Ila tunaona wananunua helikopta mpya na magari ya hanasa, hapo wananchi tunajifanya kama hatuoni matumizi mabaya ya hawa watu. Safari zisizoisha za marekani na mataifa mengine yaliyoendelea ndio desturi na tamaduni ya wavaa magwanda. Haya yote mnayafumbia macho na kujifanya HAMUONI?
Ila bado kuna kundi kubwa la watanzania wazalendo, wapenda amani, wapenda muungano na mshikamano, wameonyeshwa kuchukizwa na siasa za CHADEMA na kuomba kifutiliwe mbali ili kiepushe michafuko inayoweza kutokea kutokana na siasa yao chafu, ya uchonganishi na ya kibabe.
Wananchi wengi wameonyesha kutokuwa na imani na hiki chama cha demokrasia na maendeleo kufuatia ukosefu wa maadili wa viongozi wake. Ninawachambua kama ifuatavyo (m/kiti na katibu wa chama)
1. Mwenyekiti wa chama ni mmiliki wa kumbi za starehe kama nightclubs, bars na guest houses. Pia alikuwa DJ katika kumbi za starehe kadhaa hapa mjini.
Kuhusu elimu naomba nisiliongelee kwani ndio mwenyekiti wa chama cha siasa mwenye kiwango cha chini kabisa cha elimu hapa nchini.
Vilevile ni mfanyabiashara mkubwa wa kimataifa, kama ilivyo ada siku zote,hakuna mfanyabiashara asiyekuwa mnyonyaji. Sasa kazi kwetu watanzania kuendelea kumuwekea imani mtu kama huyu.
2. Katibu wa chama hiki amekumbwa na misukosuko mingi hivi karibuni, kuna thread humu muitafute inaeleza ufisadi ndani ya chadema ili muweze kumjua huyu mtu vizuri.
Kwa taarifa zilizonyooka kabisa ni kwamba ni mzoefu wa mechi za mchangani na mechi za kirafiki, halafu ikumbukwe alikuwa padre na tunafahamu wote, misimamo ya ma-padre wote ulimwenguni ni ipi, sasa mtu huyu anaonyesha wazi kutoweza kuvumilia na kutokuwa na msimamo thabiti wa anayoyaamini.
Hafai kupewa taifa kwani ni rahisi kwa mtu huyu kushawishika na kubadili mwelekeo mzima wa maamuzi yake, ambayo yataathiri taifa. Hapa nawakumbusha ile kauli yake ya kutomtambua mheshimiwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, yeye na magwanda mengine ya chadema.
Baada ya muda mfupi tukamsikia anataja jina la jembe letu, mkombozi wetu wa taifa, kipenzi cha walalahoi na adui wa mafisadi, his excellency the president of united republic of Tanzania dr. Jakaya.M.kikwete kwa upole, nidhamu na unyenyekevu wa hali ya juu.
Mnaweza mkapima wenyewe kuona mtu kama huyu anafaa kusimama kama rais wetu. Kwa niaba ya wengi nachukua nafasi hii kuwajibia. Jibu ni HAPANA.
Kwa hali hii ya vingozi wa chadema kutokuwa na sifa shindani na wale wa chama tawala nikimaanisha CCM, basi niitimishe kama ifuatavyo.
"CHAMA PINZANI NDILO JINA LA MILELE LA CHADEMA".
Ingawa viongozi wa chama hiki wamekuwa wabunifu wa kutumia njia mbalimbali kama mikutano ya hadhara, maandamano yasiyo na vibali, fujo na shari, kutoheshimu mamlaka zilizopo na mbaya zaidi kutokuwa na nidhamu na ustaharabu wa wabunge wa chama hiki katika bunge letu tukufu la jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuathiri mara kwa mara shughuli za bunge kufanyika kama ilivyopangwa na kufanya heshima na thamani ya bunge kumomonyoka mbele ya jamii ndani ya nchi na hata nje ya nchi.
Yote haya wanafanya kwa lengo la kujipatia umaarufu, taifa liwatambue kuwa wao ndio tumaini la ukombozi wa taifa, liwajengee imani kuwa wao ndio watabadili hali za watanzania wa chini kabisa na kuwapa unafuu wa maisha.
Uongo wa waziwazi wa wavaa magwanda ndio huu, kujifanya wanajali kundi la walalahoi huku wao ndio vinara wa kula bata mjini, wanachukua pesa za wavuja jasho kwa kigezo cha kuchangia chama wakati wanapata ruzuku kutoka serikalini ambayo hatujui pesa hizo za walipa kodi wanafanyia nini.
Ila tunaona wananunua helikopta mpya na magari ya hanasa, hapo wananchi tunajifanya kama hatuoni matumizi mabaya ya hawa watu. Safari zisizoisha za marekani na mataifa mengine yaliyoendelea ndio desturi na tamaduni ya wavaa magwanda. Haya yote mnayafumbia macho na kujifanya HAMUONI?
Ila bado kuna kundi kubwa la watanzania wazalendo, wapenda amani, wapenda muungano na mshikamano, wameonyeshwa kuchukizwa na siasa za CHADEMA na kuomba kifutiliwe mbali ili kiepushe michafuko inayoweza kutokea kutokana na siasa yao chafu, ya uchonganishi na ya kibabe.
Wananchi wengi wameonyesha kutokuwa na imani na hiki chama cha demokrasia na maendeleo kufuatia ukosefu wa maadili wa viongozi wake. Ninawachambua kama ifuatavyo (m/kiti na katibu wa chama)
1. Mwenyekiti wa chama ni mmiliki wa kumbi za starehe kama nightclubs, bars na guest houses. Pia alikuwa DJ katika kumbi za starehe kadhaa hapa mjini.
Kuhusu elimu naomba nisiliongelee kwani ndio mwenyekiti wa chama cha siasa mwenye kiwango cha chini kabisa cha elimu hapa nchini.
Vilevile ni mfanyabiashara mkubwa wa kimataifa, kama ilivyo ada siku zote,hakuna mfanyabiashara asiyekuwa mnyonyaji. Sasa kazi kwetu watanzania kuendelea kumuwekea imani mtu kama huyu.
2. Katibu wa chama hiki amekumbwa na misukosuko mingi hivi karibuni, kuna thread humu muitafute inaeleza ufisadi ndani ya chadema ili muweze kumjua huyu mtu vizuri.
Kwa taarifa zilizonyooka kabisa ni kwamba ni mzoefu wa mechi za mchangani na mechi za kirafiki, halafu ikumbukwe alikuwa padre na tunafahamu wote, misimamo ya ma-padre wote ulimwenguni ni ipi, sasa mtu huyu anaonyesha wazi kutoweza kuvumilia na kutokuwa na msimamo thabiti wa anayoyaamini.
Hafai kupewa taifa kwani ni rahisi kwa mtu huyu kushawishika na kubadili mwelekeo mzima wa maamuzi yake, ambayo yataathiri taifa. Hapa nawakumbusha ile kauli yake ya kutomtambua mheshimiwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, yeye na magwanda mengine ya chadema.
Baada ya muda mfupi tukamsikia anataja jina la jembe letu, mkombozi wetu wa taifa, kipenzi cha walalahoi na adui wa mafisadi, his excellency the president of united republic of Tanzania dr. Jakaya.M.kikwete kwa upole, nidhamu na unyenyekevu wa hali ya juu.
Mnaweza mkapima wenyewe kuona mtu kama huyu anafaa kusimama kama rais wetu. Kwa niaba ya wengi nachukua nafasi hii kuwajibia. Jibu ni HAPANA.
Kwa hali hii ya vingozi wa chadema kutokuwa na sifa shindani na wale wa chama tawala nikimaanisha CCM, basi niitimishe kama ifuatavyo.
"CHAMA PINZANI NDILO JINA LA MILELE LA CHADEMA".