hippocratessocrates
JF-Expert Member
- Jul 1, 2012
- 3,598
- 1,539
Mkuu HAMY- D, heshima,
Naomba nikukumbushe haya;
1. Uandishi na Matumizi ya Lugha:
Kiukweli nilipata shida sana kufika mwisho kutoka na na makosa ya kisarufi mfano, hanasa( badala ya anasa), Hichi(hiki), Hustaarabu(Ustaarabu)..nk..angalau uwe unapitia tena(proof read kabla ya kuandika hoja) lakini nadhani shida ni matumizi ya lugha yetu.
2. Katika kusoma HOJA yako, UMEJICHANGANYA MWENYEWE katika Aya ya kwanza na ya tatu, kusema CHADEMA wanataka kutwaa dola na pia wanatafuta umaarufu tu...tukueleweje?
3. Katika Aya ya nne, umeuliza "CHADEMA wanakusanya pesa za walalahoi ikiwa wanapata ruzuku, na "HAMJUI" pesa hizo za WALIPA KODI zinakwenda wapi" ... sasa ingawa si mwanchama wa CHADEMA naomba nikuulize
- Umesema/Kuonyesha ufuasi wako wa CCM, sasa pesa hizo za CHADEMA zinakuhusu nini wewe?
- Unaposema "HATUJUI" zinapokwenda..ni wewe na nani?
- Uliuliza kabla ya ku-post hapa?
-Unajua kazi ya pesa za ruzuku ni ipi?Je inatosha pesa yenyewe?
-Je chama cha CCM huwa hawakusanyi/kuchangia mfuko wa chama?..kumbuka Mlimani City, pale Dodoma n.k
- Pesa hizo huwa wanfanyia nini?
3. Unaposema kila mfanyabiashara mkubwa ni "MNYONYAJI" una maana gani? ..kama UNA UHAKIKA, hebu lete orodha ya majina ya "WANYONYAJI" kutoka CCM, tufanye ulinganifu.
4. Unaposema, "kwa niaba ya wengi unaamua kutujibia" kuwa viongozi wawili uliowataja wa hicho chama yaani (CHADEMA)..Nani amekupa RUHUSA hiyo?
- Kwa hoja yako ya elimu( zaidi ya nusu ya wabunge wa TZ hawana shahada, JE bunge livunjwe?..
- Je, bunge linaundwa na wanachama wangapi wa CCM?
- Je, wenye "elimu hii kubwa" wamelifanyia nini Taifa?
Hebu mkuu, niondolee dukuduku kwa kujibu maswali haya KWA UMAKINI na kisha tuendee.
Naomba nikukumbushe haya;
1. Uandishi na Matumizi ya Lugha:
Kiukweli nilipata shida sana kufika mwisho kutoka na na makosa ya kisarufi mfano, hanasa( badala ya anasa), Hichi(hiki), Hustaarabu(Ustaarabu)..nk..angalau uwe unapitia tena(proof read kabla ya kuandika hoja) lakini nadhani shida ni matumizi ya lugha yetu.
2. Katika kusoma HOJA yako, UMEJICHANGANYA MWENYEWE katika Aya ya kwanza na ya tatu, kusema CHADEMA wanataka kutwaa dola na pia wanatafuta umaarufu tu...tukueleweje?
3. Katika Aya ya nne, umeuliza "CHADEMA wanakusanya pesa za walalahoi ikiwa wanapata ruzuku, na "HAMJUI" pesa hizo za WALIPA KODI zinakwenda wapi" ... sasa ingawa si mwanchama wa CHADEMA naomba nikuulize
- Umesema/Kuonyesha ufuasi wako wa CCM, sasa pesa hizo za CHADEMA zinakuhusu nini wewe?
- Unaposema "HATUJUI" zinapokwenda..ni wewe na nani?
- Uliuliza kabla ya ku-post hapa?
-Unajua kazi ya pesa za ruzuku ni ipi?Je inatosha pesa yenyewe?
-Je chama cha CCM huwa hawakusanyi/kuchangia mfuko wa chama?..kumbuka Mlimani City, pale Dodoma n.k
- Pesa hizo huwa wanfanyia nini?
3. Unaposema kila mfanyabiashara mkubwa ni "MNYONYAJI" una maana gani? ..kama UNA UHAKIKA, hebu lete orodha ya majina ya "WANYONYAJI" kutoka CCM, tufanye ulinganifu.
4. Unaposema, "kwa niaba ya wengi unaamua kutujibia" kuwa viongozi wawili uliowataja wa hicho chama yaani (CHADEMA)..Nani amekupa RUHUSA hiyo?
- Kwa hoja yako ya elimu( zaidi ya nusu ya wabunge wa TZ hawana shahada, JE bunge livunjwe?..
- Je, bunge linaundwa na wanachama wangapi wa CCM?
- Je, wenye "elimu hii kubwa" wamelifanyia nini Taifa?
Hebu mkuu, niondolee dukuduku kwa kujibu maswali haya KWA UMAKINI na kisha tuendee.