Chama cha Kilaghai Tanzania...

Njaa ni kitu kibaya sana!!! Kwa hiyo hapa malipo yako ni kiasi gani kwa leo?????!!!!! Kama huridhiki kwa nini usiende mahakamani? Povu la nini hapa???!!!

mkuu unatumia kichwaa kufugia tu nywele? mjadala umeletwa jukwaani, kama una hoja ya kupinga itoe, sio haya maneno yako yasiyo na tija kwa wasomaji.

Mods, michango ya namna hii muwe mnaifuta on spot, ili heshima ya JF kuwa mahali pa Great Thinkers irudi.
 
Natamani sana mleta mada ungetuambia baada ya uchambuzi wako nini kifanyike, wananchi waisuse chadema na kurudi ccm au tuiache ccm iendelee kuuza twiga wetu nje ya nchi na kugawana rasilimali zetu?

unapaswa kujiongeza sio kila jambo utafuniwe. Inshort, amejaribu kuonesha mapungufu hayapatikani ccm tu hata vyama vingne km cdm. Pia uone kwmba cdm ni chama chenye maslahi ya watu wachache na muelekeo wake ni wakibinafsi zaidi wanapaswa kubadilika km wanahitaji dola. Lkn mpk sshv dola kwao itabaki ndoto,hawana mkakati wa kuwafikia mwananchi wameanzisha uongozi wa kanda ambao bado ni centralizatn,ccm wamedecentralize mpk kwa balozi wht do u espect?
 
Kama umethubutu kuisemea cdm yote hayo cjui ccm itakuwa mara ngapi ya hiyo maana kila baya linalofanyika ktk nchi hii linawahusu baya zaidi hii ya kutugawa kwa nisingi ya kidini na ukabila
 
Pole sana ndugu haya mambo ungeyaleta miaka ile....siyo leo too late! kama ni ulaghai basi baba yake ni yule aliyekisajiri na ndiyetunapaswa kuanza naye. Pia fuatilia hesabu za pesa ya viwanja vya michezo, packing, vyumba vya kupangisha n.k hapa kunatatizo kubwa sana kuliko hizo sadaka za M4C.Aidha unaonekana wewe ni muungwana sana tena mtetezi mzuri wa masilahi ya wananchi hebu tuungane tudai pesa zetu za EPA, Richmond, Deepgreen, meremeta, Dowans n.k n.k n.k
 
ZeMarcopolo,hakuna chama chochote cha siasa ambacho asilimia mia moja wanasema ukweli.Kiangalie CCM chenyewe ni waongo wakutupwa mpakaa rushwa wameifanya haki.Angalia CUF leo wanongelea hiki kesho wakija wanakanusha wataongelea kingine.Hakuna chama ambacho kinaukweli kwa asilimia mia.

Kwa wanachama ulivyowapanga inategemea na utafiti wako pia,lakini sidhani kama utafiti uliofanya umefanya kwa watu gani.Kuna vijana kama Mwampapa na Shonzi walikosa kitu kidogo sana hekima ,kama wangekuwa na hekima wangekuwa supported na watanzania wengi.Tatizo lingine chama chetu tawala bado hakijapokea vyama vya upinzani kama changamoto na wamepokea kama maadui ndio maana wanatumia pesa nyingi na ngonjeara nyingi ili kuvifanya vyama hivi visisongembele na kupata wanachama au kuwapa muamko watanzania kuhusu hatima ya nchi yao na elimu ya uraia.
Ukiuliza kwa nini CCM wanapamba vyama vya upinzani kwa matamko ya udini ,ukabila ,waongo wanapenda madaraka n.k ni kwa sababu wao wenyewe ndio waanzishaji wa hayo yote.Na hakuna mwanachama wa ccm asiyependa madaraka,kwani kama wasingependa madaraka sidhani kama rushwa ingekuwa kigezo.

Kwenye mada yako ungeweka vyama vyote vya siasa kuwa ni waongo na wapenda madaraka ningekuelewa zaidi,vinginevyo ninaona hauna tu mapenzi na chadema bali unamapenzi na CCM au CUF
 


Duniani kuna watu na Viatu, viatu huwa ni vingi kuliko watu maana mtu mmoja ana zaidi ya jozi moja.

Kwenye CHADEMA ungeweka CCM article yako ingeleta maana kwa Taifa.

Kwenye makundi yanayopenda CCM umesahau kundi la tatu:-

3: Ni wale wenye malengo ya kujiunga na chama ama kujipendekeza kwa "wakubwa" ili wafisadi nchi au wapate madaraka.

Kwenye mambo uliyo taja kuwa yanaiondoa CDM machoni pa watu naona ulikuwa unaisema CCM kimafumbo, mfano:-

Kwenye No. 4: Ulikuwa unamsema "First 'Red" (First Lady wa ukweli ni My wife wake wa kwanza!) anaye zunguka kukagua mikoani kwa kutumia rasilimali za nchi kama Waziri Mkuu!

No. 6: Serikali ya SSM imekuwa na Matumizi mabaya ya fedha za umma tangu mafisadi walipo shika dola!
No. 7: Hapa umemsema Kinanah na biashara yake ya ujangili wa nyara za Taifa.
No. 8: Umemsema Mkulu kwa kuteuwa wakuu wa wilaya, mikoa, wakurugenzi wa mashirika ya umma na mawaziri kwa misingi ya kujuwana kindugu, kidini, kirafiki na "kiurafiki"!
No: 11: Hapa ulikuwa unazungumzia mikataba ya madini ambayo hata wananchi kupitia wabunge wao ni marufuku kuiona, na kwa nini deni la Taifa linakuwa kwa kasi ya ajabu lakini tuna ambiwa tumepunguza utegemezi wa budget toka 44% mpaka 22%-Pesa hiyo inakopwa inakwenda wapi?

Nimekukubali mzee wa reverse!
 

Anakupotezea muda?. KWELI?
Kama angekuwa kweli kweli anakupotezea muda wako wenye gharama kubwa usingepoteza muda mwingi kuandika kwa kirefu namna hii wakati kuna issues za msingi zinahitaji sana mjadala na uchangiaji wako. Vinginevyo, kwa maandishi haya, wewe unakuwa ndiyo siyo mtunza muda mzuri.

Ni angalizo tu.
 
Mkuu wewe ndiyo umeelewa vibaya sentesi inavyobainisha, jaribu kuisoma vizuri tena, utaelewa ina maana gani.
Chris Lukosi amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya kujitoa kwake chadema ni kunyimwa tenda hii,
 
Kwakweli tupo mahala pabaya sana tanzania. Tatizo letu naamini sio vyama bali ni watendaji ndani ya vyama hadi serikalini na tuseme ukweli kutokuwajibika,ufisadi na kujipendelea ndio kunakoleta hali ya kutugawa watanzania na mwenye kuweza kuweka sawa mambo haya sio CDM bali ni chama tawala na hadi tulipofikia kinaonesha kulegalega kuliko wazi ktk kuweka mambo sawa na ndio maana wapinzani wanapata la kusema, si mpenzi wa chama chochote cha siasa ila nimeufuatilia huu uzi nimeona kila mmoja anajaribu kuchanhia kwa kulinda maslahi ya chama chake ila iko wazi tatizo ni utawala na kwa mwendo huu tunaoenda nao tutakuja kuvuruga amani yetu tena si kwa ukabila,udini wala tofauti za vyama bali ni vita baina ya masikini[wanyonge] na matajiri ambapo kila tajiri itaaminika ni fisadi. 2015 sio mbali watanzania ili mambo yaende sawa tumchague mtu makini asiye na mzaha wala utani kwenye kusimamia taifa bila kujali atakuwa mgombea binafsi,ccm,cdm,tlp,nra au nccr. Wengi wanaopiga kelele kuhusu vyama ni watu wanaojaribu kuweka sawa maslahi yao ila mioyoni mwao wanajua tulipo ni katika wakati mbaya kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa letu. Nawasilisha

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 

Na wewe kitendo cha kushabikia ccm inaonyesha jinc gani huwa unashirikisha masaburi kwenye kupambanua kuliko akili.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu hemu jitambue, kama CCM inakombatia mafisadi, wahujumu uchumi na wabadhilifu wa mali za umma, hata kama CCM na serikali haitambui utawala wa sheria, haitoi uhalali kwa CHADEMA kufanya maovu yanayofanywa na CCM, hemu mlisome chapisho la mtoa mada kwa ustadi mkubwa, wenda mkisoma tena na tena mtaelewa, maana vichwa vya binadamu havifanani katika kuelewa mambo, binafsi nimemuelewa vizuri mtoa mada, yeye anataka mumpe hoja za msingi za kwanini CHADEMA itawale? wakati madudu ya CCM yameonekana onekana CHADEMA? Sio kwa lengo baya kuufanya huu mjadala, wenda ukatoa ukungu kichwani mwa watu wanaipenda CHADEMA kama hawa WAFATA UPEPO waliojaa humu JF.
 
Chadema ni chama kinachozungumzia mipango yake ya kuendesha nchi kinadharia kwa vile hakijapata fursa ya kupewa dola. Hata hivyo kinaonyesha kukerwa na ufisadi,umasikini na ukosefu wa elimu kwa wananchi wake.
CCM kimechukua dola(sio kupewa) na hakina kifanyacho,ni kama toothless bulldog, hakina uwezo wa kung'ata zaidi ya blabla na nchi inaangamia tukishuhudia. Jee kuna faida ya kuendelea kufuga "Toothless Buldog"?
Nadhani hakuna faida hiyo hata kidogo.
Kuilalamikia CDM wakati haina dola huo ni uzandiki mkubwa,kwanza mengi yaliyoibadili nchi kwa sasa hata ikaanza kuonekana kuwa ina mwelekeo ni yale yaliyopiganiwa na Chadema kwa nguvu kubwa.
Wananchi wa sasa wameshaelewa nini Chadema inafanya,propaganda zenu kwenye mitandao hazisaidii lolote kwa CCM na hazina madhara kwa Chadema. Mbona kama chama ni cha kikanda kama msemavyo wajumbe wa vikao vya CCM hapa Mwanza wajumbe wanavalia mashati yao ya kijani ukumbini? Wanaogopa nini kuyavaa mitaani siku hizi?
Zamani ilikuwa fahari kuvaa sare ya CCM hadharani mbona sasa imekuwa aibu mtaani kwa watu wa kawaida?
Ukijiuliza hayo yote ndio utapata majibu kuwa hicho chama kwa wananchi ni kama ugonjwa wa Ukoma ambao haupendwi na watu.
 
Hivi chama chako unachokitumikia yaani CCM kimewafanyia nini watanzania kwa miaka 36?
wizi wa rasilimali,
madaraka ya kujuana
nchi maskini.
elimu duni,
ahadi hewa ambazo hazitatekelezwa kama tren za kasi kigoma dar,
meli ya kisasa ziwa tanganyika,
viwanja vya ndege vya kisasa kila mkoa,
kufuga mafisadi wa EPA, na wengineo.
kununua magari ya kifahari kama mashangingi ambayo hata Japan wanotengeneza hawayatumii,
hospitali duni..
kutuma mamluki katikia vyama vya siasa ili kuviuwa,
na madhambi negineyo mnayojua...

tukishawatoa madarakani nyie wezi wa rasilimali zetu, tukaweka chama kingine kinachofaa,
tukamweka kiongozi makini ndoto za watanzania zitatimia..
tutafaidi rasilimali zetu
tutakuwa the hub of Africa
tuna kila utajiri ambao wachache CCM ndio wanaofaidi.
HUWA NAMWONA MTU ANAESHABIKIA CCM KWA SASA LABDA SIO MSOMI AU MSOMI AMBAE HAJAELIMIKA.
HUWEZI KUWA NA AKILI TIMAMU KWA SASA UKAJIITA MWANA CCM NA UKAPITA MITAANI NA NGUO ZA KIJANI
SINA CHAMA CHA SIASA NAUNGA MKONO MAGEUZI YA KWELI
 
Mkuu [MENTION]Ommunist[/MENTION] tujuze juu ya hiyo kitu ardhi nani amewalaghai hao watu. Maana tunaambiwa ni CDM hapa.

cc Kijakazi, ZeMarcopolo, Ng'wamapalala na Kitoabu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mbona unataka kulinyima jukwaa fursa ya kujadili mambo? Yaani ulitaka ZeMarcopolo aende kuwatafuta wanachama wa CHADEMA mitaani na kuwaambia hayo? Nadhani hapa kuna wana CHADEMA ambao wanaweza kutusaidia kujibu huu "upuuzi" wa mtoa hoja.
 
Last edited by a moderator:

Uandishi wako unafanya hoja yako iwe na utapia mlo, jifunze uandishi unaovutia ili hoja yako ionekane, kama hizo barabara za Kenya.
 

Ndugu umetoa maelezo mengi ambayo sio mageni sana kwetu ebu naomba nifafanulie yafuatayo

1.Kuna kundi umesema linataka kupanda haraka kisiasa na hapo hapo umesema ni chama cha Kilaghai inakuwaje mtu atake kupanda kisiasa kwenye chama cha kilaghai ambacho kwa mtazamo wako akina mvuto wala mwelekeo?

2. Unaposema wadau wanajiuliza CDM kinataka nini hadi kipinge chama kilichoasisiwa na wapigania Uhuru? ebu tupe maelezo wakati CCM ikiongozwa na Baba wa Taifa (R.I.P) mambo yaliyokuwa yakifanyika wakati huo na sasa ni sawa? je alivyo Makongoro Nyerere na Riz 1 ni sawa? na je yanayosemwa na CDM na vyama vingine kuhusu udhaifu wa Serikali unayoipenda ni uongo? pia jiulize mbona Kenya (KANU) na zambia na baadhi ya nchi vyama vilivyoleta ukombozi wa nchi hizo havipo madarakani na vilipingwa na wananchi wakachagua vyama vingine.

3. Pia naomba utuambie kwa nini unaishambulia sana CDM? hivi haujui kuna msemo unaosema **MTI WENYE MATUNDA NDO UPOPOLEWA MAWE**
 



Mkuu punguza hasira,una hoja nzuri ila umeharibu neno mwehu na ---- first class.....sio mazuri usiwe kama wao wamezoea matusi,tujitofautishe kwa hoja na wao
 
kuna hoja zingine hazihitaji hata kujadiliwa kwa sababu mleta hoja analeta kwa malengo yake toka huko walikomtuma.
ndo maana wachangiaji wanajibu wanavyojisikia kwa sababu mada imeegemea zaidi kimasilahi zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…