Challenge: Is Mbowe another future Rostam Aziz or Edward Lowassa?

Waberoya

Platinum Member
Aug 3, 2008
15,169
10,785
Kwako Kaka

JINSI GANI TUTAZUIA MAFISADI WA SASA NA WOTE WAJAO KWA ASILI YETU HII YA UBINADAMU WA KUPENDA FEDHA.

Kichwa cha habari chajieleza;

Moja ya vitu ambavyo huwa vinanichanganya nikifikiria future ya Tanzania ni jinsi gani tutakavyoepukana kuwa na viongozi walafi.Ubepari unasababisha kuwa greedy, unasababisha kuwa na tamaa ya fedha na ubepari unasababisha mtu kutokukubali kurudi nyuma na kuangalia mbele au kuzidisha mafanikio. Hii ndio ASILI ya binadamu halisi.

Rostam na Lowassa ambao jamii ya kitanzania imewapa majina lukuki kutokana na tabia zao ni mfano mzuri sana wa viongozi ambao ni walafi wa fedha kutokana na mfumo uliopo ambao hauwazuii viongozi wa aina hiyo kuwa walafi au kutumia makampuni yao kujipatia fedha za kazi za serikali.Rostam, Lowassa tatizo lao ni kutumia nafasi zao au influence zao kupata nafasi au fursa isiyo sawa, wengi wa aina hii ya Viongozi hawa hujipatia tender isivyo halali hivyo kunyima fursa sawa kwa wote. Wakati Manji na Shubash hutumia viongozi wengine, lakini ni tabia iliyokithiri kwa watanzania wengi kupata tender isivyo halali ni tabia iliyozoeleka na kwa wabishi poleni! Rostam mbali ya kuwa mwanasiasa lakini wafanyabiashara wengi wanamuhesabu ni mjasiriamali mzuri mno ambapo hata asingekuwa kwenye ulingo wa siasa bado angekuwa tajiri, wahindi wengi wana caliber hii, tukubali tu watanzania wenye caliber hii ni wachaga huku wengine wengi hawana ndoto wala utaalamu wa biashara za ndani na nje. Ni akili zetu hizi zinawafanya umoja wa wanawake Tanzania kutoa kibali kwa Manji kuwajengea jengo lile la zain ambalo hata wao walikuwa na uwezo wa kufanya hivyo! Au Lowassa kuwaamsha UVCCM na kutumia kibali chao kujenga jengo lile! These guys are nothing but really wajanja wakubwa. Na ujinga wa watanzania wengi wamekuwa wakitegemea hawa jamaa kuwaonea huruma hili hali wao wamelala! What a joke! Ndio hii inapeleka watanzania kuwalaumu akina Rostam juu ya Dowans na sio TANESCO….. asili ile ile ye kutokukubali kuwa ujinga wetu ndio mtaji wao!

Kinachonitatiza zaidi ni namna hawa viongozi huwa wazuri sana, kwa wasiojua historia sifa ya Rostam bungeni ni kubwa na ni moja ya wabunge wachache ambao huwa hawana wapinzani kwenye kujenga hoja, Rostam anaongea Aden Rage haoni ndani. Kuna mwana JF mmoja nilimtania juzi na kusema huyu RA mnamsema mtu lakini wengi wenu hamuijui historia yake bungeni , Mwaka 2001 ni RA pekee aliyepinga mabadiliko ya kumi ya katiba yanayompa mamlaka makubwa rais, 1999 ndiye aliyepinga kesi ya uhani ya CUF wale wana cuf hamsini, mwaka 1997 ndiye pekee aliyekataa miswada ya madini kupitishwa na akaonya vizazi vijavyo vitahukumu bunge hilo, Rostam huyu ndiye aliyepambana na Salmin amour aliyetaka kubadili katiba ya kumuongezea muda madarakani. Ni rostam huyu 1994 aliyezuia mifumuko ya bidhaa za zanzibar, 1999 Rostam. 2004 Rostam alizuia shilingi kwenye wizara ya uchumi na mipango iliyokuwa chini ya Kagoda. Mwenye record ya namna hii bunge hili ni ngumu kumpata, suddely huyu jamaa kawa MKIMYA TENA SANA!

What happened with this oustanding records?? …nimechoka!

Nani anayetokea Arusha asiyejua utajiri wa familia ya Lowassa , mbuzi na ng'ombe wangapi huchinjwa kila x-mass? Lowassa anatokea familia tajiri. Nani leo atapinga uwezo wa ufanyaji kazi wa Lowassa lets just be fair on this.

Siwasemi hao watu kuwasafisha nataka tupate picha kuwa kwanza tunawatengeneza mafisadi kwa itikadi zetu na tabia zetu, pili hakuna system ya kuwazuia viognozi wa namna hii kuiba kama wanafanya hivyo.

Challenge mbili ninazozitoa ni what makes once was good leader to be corrupt, and what about those who are not yet in leadership but they are doing biashara? Swali la kizushi…tukisema fulani fisadi na kumbe sio ghafla akawa fisadi kwa sababu jamii ndiyo inamwona hivyo nani wa kulaumiwa?? ..sipati picha… jamii yetu ime-lack kitu fulani umbea na tetesi zimetawala na tangible evidence na kuchukua hatua ni mlima kwetu.

Swali langu linaelekezwa kwa wajasiriamali wengine kama Mbowe, suppose leo Slaa anakuwa Rais mbowe anaweza kuwa waziri mkuu au waziri tu , je atakubali biashara zake zife?? Mahoteli yake, makampuni yake n.k atafanyaje ili haya makampuni yawe na fair competitions na makampauni mengine. At least hawa mafisadi wa sasa wanatoka familia ambazo zinaweza kujustify utajiri wao, je wale wanaotoka familia masikini, tutafanyaje kuwazuia wasipate utajiri wa haraka, kutotumia majina ya ndugu zao kwenye makampuni yatakayovuna tenders mbali mbali? Namsema mbowe kwanza nikifurahia ujasiriamali wake japo ana madeni ya NSSF n.k hilo kwa sisi wafanyabiashara ni kitu cha kawaida, lakini ghafla anakuwa Prime minister , jamani tuwe wakweli na ushabiki tuuweke pembeni hatananilii, I mean atashindwa kulipa deni tena, au kwa lugha nyingine hawezi kupiga pande dogo tu deni likalipwa au kwa sababu mshahara utakuwa umeongezeka? maana hata hawa akina RA na EL wanamishahara mikubwa tu! au standard gani tunatumia kuwa huyu ATAKUWA SAFI NA huyu atakuwa FISADI? kwa macho??

Mbowe ameonyesha ni mjasiriamali mzuri, je ni system gani au kitu gani kinachoweza kutuhakikishia kuwa HATAWEZA kuwa Rostam au Lowassa mwingine hata kama ni kiongozi mzuri?

Nahamishia swali kwako msomaji, kaa chini tafakari angalia uzuri na utamu wa fedha , wewe ni kiongozi na una makampauni yako , uwezo wa kupata kazi unao na ukapata fedha zaidi……. Unafikiri ni KITU GANI KITAKUZUIA usitake unachoona ni chema kukipata? Ndio leo mnamlaumu mkapa wakati hakuna mechanism ya kumzuia kuiba? Na akiiba hashtakiwi? Kwani nani asiyejua SONGAS ni ya Kikwete na atasemwa baada ya kuondoka madarakani! Jamani ubinadamu na dhambi ni mapacha! We are fallible creatures no one will dare to say he is smart if nothing hinders him to enjoy his/her freeness ..fikiria sasa kama kungekuwa hakuna ukimwi! Haya hupo sasa….

Je leo hii tunapowahukumu akina RA tunatumia sheria, au utaratibu tuliojiwekea au DHAMIRA NA AKILI ZA UUNGU NA UPOLE zilizowajaa wengi? Ok! Kwa jibu lako unafikiri tuna mechanism gani ya kuzuia hili lisitokee kwa wapinzani wafanyabiashara?? Usimseme Nyerere , Nyerere alikuwa tofauti na tabia zetu na ndio maana soon will be anothe saint! Nyerere failed by thinking everyone is thinking like him...we need system or something , please tell me.

Kumbukeni hulka za binadamu haziko kwenye dini,dini haiwezi kum-control mtu wala eti dhamiri…!!! I need clear and concie system ambayo itakuwepo kuwazuia wafanyabiashara ambao ni viongozi kupata tender unfairly.

Mimi mtiifu
Waberoya
 
''I have come to the conclusion that politics are too serious a matter to be left to the politicians''. Charles De Gaulle (1890 - 1970)
 
mara unamsafisha RA na EL,mara unawaponda,kwa ufupi umeanza vizuri ila umemalizia vibaya sio tu kwa kuwatetea RAnaEL BALI KWA KUWA MTU AMBAYE HUMWAMINI MTU KUWA HAWEZI KUIBA AKIKAA MADARAKANI,...
 
mara unamsafisha RA na EL,mara unawaponda,kwa ufupi umeanza vizuri ila umemalizia vibaya sio tu kwa kuwatetea RAnaEL BALI KWA KUWA MTU AMBAYE HUMWAMINI MTU KUWA HAWEZI KUIBA AKIKAA MADARAKANI,...

Thread hii haihitaji wavivu wa kufikiri, mtasema ...anawasafisha, umetumwa, craps, umepewa sh.ngapi, huna tofauti kabisa na wanasheria wa TANESCO wasiojua A wala B na wanaingizwa mknege mchana mchana, mara unamponda mara unamsafisha tatizo ni WEWE haujanielewa... HUNA HOJA KAA NJE, sitajibu vijembe sijapiga kijembe naeleza HALI HALISI TUNAYOISHI HUMU! SINA USHABIKI WA CHAMA

nasema hivi, nasema hivi, kuwa wafanyabiashara wajao watazuiliwa vipi wasiwe rostam au el, umenipata??

Kuna hoja huwa hazijibiki mpaka umekaa chini kwanza na kutafakari this is really JF mambo ya kata hapa hayapo.

Hujaelewa -uliza
imekuchoma- lia
imekufurahisha- cheka
inafundisha katekeleze

imeakuamsha usifanye shingo yako kuwa ngumu......Nchi hii ambayo kila mtu ni fisadi we need serious reformation to believe our leaders ebo!
 
Kwako Kaka

JINSI GANI TUTAZUIA MAFISADI WA SASA NA WOTE WAJAO KWA ASILI YETU HII YA UBINADAMU WA KUPENDA FEDHA.

Kichwa cha habari chajieleza;

Moja ya vitu ambavyo huwa vinanichanganya nikifikiria future ya Tanzania ni jinsi gani tutakavyoepukana kuwa na viongozi walafi.Ubepari unasababisha kuwa greedy, unasababisha kuwa na tamaa ya fedha na ubepari unasababisha mtu kutokukubali kurudi nyuma na kuangalia mbele au kuzidisha mafanikio. Hii ndio ASILI ya binadamu halisi.

Rostam na Lowassa ambao jamii ya kitanzania imewapa majina lukuki kutokana na tabia zao ni mfano mzuri sana wa viongozi ambao ni walafi wa fedha kutokana na mfumo uliopo ambao hauwazuii viongozi wa aina hiyo kuwa walafi au kutumia makampuni yao kujipatia fedha za kazi za serikali.Rostam, Lowassa tatizo lao ni kutumia nafasi zao au influence zao kupata nafasi au fursa isiyo sawa, wengi wa aina hii ya Viongozi hawa hujipatia tender isivyo halali hivyo kunyima fursa sawa kwa wote. Wakati Manji na Shubash hutumia viongozi wengine, lakini ni tabia iliyokithiri kwa watanzania wengi kupata tender isivyo halali ni tabia iliyozoeleka na kwa wabishi poleni! Rostam mbali ya kuwa mwanasiasa lakini wafanyabiashara wengi wanamuhesabu ni mjasiriamali mzuri mno ambapo hata asingekuwa kwenye ulingo wa siasa bado angekuwa tajiri, wahindi wengi wana caliber hii, tukubali tu watanzania wenye caliber hii ni wachaga huku wengine wengi hawana ndoto wala utaalamu wa biashara za ndani na nje. Ni akili zetu hizi zinawafanya umoja wa wanawake Tanzania kutoa kibali kwa Manji kuwajengea jengo lile la zain ambalo hata wao walikuwa na uwezo wa kufanya hivyo! Au Lowassa kuwaamsha UVCCM na kutumia kibali chao kujenga jengo lile! These guys are nothing but really wajanja wakubwa. Na ujinga wa watanzania wengi wamekuwa wakitegemea hawa jamaa kuwaonea huruma hili hali wao wamelala! What a joke! Ndio hii inapeleka watanzania kuwalaumu akina Rostam juu ya Dowans na sio TANESCO….. asili ile ile ye kutokukubali kuwa ujinga wetu ndio mtaji wao!

Kinachonitatiza zaidi ni namna hawa viongozi huwa wazuri sana, kwa wasiojua historia sifa ya Rostam bungeni ni kubwa na ni moja ya wabunge wachache ambao huwa hawana wapinzani kwenye kujenga hoja, Rostam anaongea Aden Rage haoni ndani. Kuna mwana JF mmoja nilimtania juzi na kusema huyu RA mnamsema mtu lakini wengi wenu hamuijui historia yake bungeni , Mwaka 2001 ni RA pekee aliyepinga mabadiliko ya kumi ya katiba yanayompa mamlaka makubwa rais, 1999 ndiye aliyepinga kesi ya uhani ya CUF wale wana cuf hamsini, mwaka 1997 ndiye pekee aliyekataa miswada ya madini kupitishwa na akaonya vizazi vijavyo vitahukumu bunge hilo, Rostam huyu ndiye aliyepambana na Salmin amour aliyetaka kubadili katiba ya kumuongezea muda madarakani. Ni rostam huyu 1994 aliyezuia mifumuko ya bidhaa za zanzibar, 1999 Rostam. 2004 Rostam alizuia shilingi kwenye wizara ya uchumi na mipango iliyokuwa chini ya Kagoda. Mwenye record ya namna hii bunge hili ni ngumu kumpata, suddely huyu jamaa kawa MKIMYA TENA SANA!

What happened with this oustanding records?? …nimechoka!

Nani anayetokea Arusha asiyejua utajiri wa familia ya Lowassa , mbuzi na ng'ombe wangapi huchinjwa kila x-mass? Lowassa anatokea familia tajiri. Nani leo atapinga uwezo wa ufanyaji kazi wa Lowassa lets just be fair on this.

Siwasemi hao watu kuwasafisha nataka tupate picha kuwa kwanza tunawatengeneza mafisadi kwa itikadi zetu na tabia zetu, pili hakuna system ya kuwazuia viognozi wa namna hii kuiba kama wanafanya hivyo.

Challenge mbili ninazozitoa ni what makes once was good leader to be corrupt, and what about those who are not yet in leadership but they are doing biashara? Swali la kizushi…tukisema fulani fisadi na kumbe sio ghafla akawa fisadi kwa sababu jamii ndiyo inamwona hivyo nani wa kulaumiwa?? ..sipati picha… jamii yetu ime-lack kitu fulani umbea na tetesi zimetawala na tangible evidence na kuchukua hatua ni mlima kwetu.

Swali langu linaelekezwa kwa wajasiriamali wengine kama Mbowe, suppose leo Slaa anakuwa Rais mbowe anaweza kuwa waziri mkuu au waziri tu , je atakubali biashara zake zife?? Mahoteli yake, makampuni yake n.k atafanyaje ili haya makampuni yawe na fair competitions na makampauni mengine. At least hawa mafisadi wa sasa wanatoka familia ambazo zinaweza kujustify utajiri wao, je wale wanaotoka familia masikini, tutafanyaje kuwazuia wasipate utajiri wa haraka, kutotumia majina ya ndugu zao kwenye makampuni yatakayovuna tenders mbali mbali? Namsema mbowe kwanza nikifurahia ujasiriamali wake japo ana madeni ya NSSF n.k hilo kwa sisi wafanyabiashara ni kitu cha kawaida, lakini ghafla anakuwa Prime minister , jamani tuwe wakweli na ushabiki tuuweke pembeni hatananilii, I mean atashindwa kulipa deni tena, au kwa lugha nyingine hawezi kupiga pande dogo tu deni likalipwa au kwa sababu mshahara utakuwa umeongezeka? maana hata hawa akina RA na EL wanamishahara mikubwa tu! au standard gani tunatumia kuwa huyu ATAKUWA SAFI NA huyu atakuwa FISADI? kwa macho??

Mbowe ameonyesha ni mjasiriamali mzuri, je ni system gani au kitu gani kinachoweza kutuhakikishia kuwa HATAWEZA kuwa Rostam au Lowassa mwingine hata kama ni kiongozi mzuri?

Nahamishia swali kwako msomaji, kaa chini tafakari angalia uzuri na utamu wa fedha , wewe ni kiongozi na una makampauni yako , uwezo wa kupata kazi unao na ukapata fedha zaidi……. Unafikiri ni KITU GANI KITAKUZUIA usitake unachoona ni chema kukipata? Ndio leo mnamlaumu mkapa wakati hakuna mechanism ya kumzuia kuiba? Na akiiba hashtakiwi? Kwani nani asiyejua SONGAS ni ya Kikwete na atasemwa baada ya kuondoka madarakani! Jamani ubinadamu na dhambi ni mapacha! We are fallible creatures no one will dare to say he is smart if nothing hinders him to enjoy his/her freeness ..fikiria sasa kama kungekuwa hakuna ukimwi! Haya hupo sasa….

Je leo hii tunapowahukumu akina RA tunatumia sheria, au utaratibu tuliojiwekea au DHAMIRA NA AKILI ZA UUNGU NA UPOLE zilizowajaa wengi? Ok! Kwa jibu lako unafikiri tuna mechanism gani ya kuzuia hili lisitokee kwa wapinzani wafanyabiashara?? Usimseme Nyerere , Nyerere alikuwa tofauti na tabia zetu na ndio maana soon will be anothe saint! Nyerere failed by thinking everyone is thinking like him...we need system or something , please tell me.

Kumbukeni hulka za binadamu haziko kwenye dini,dini haiwezi kum-control mtu wala eti dhamiri…!!! I need clear and concie system ambayo itakuwepo kuwazuia wafanyabiashara ambao ni viongozi kupata tender unfairly.

Mimi mtiifu
Waberoya

Kiasi gani umepewa kuja hapa JF kuwasafisha Mafisadi papa RA & EL? Acha unafikir hali kila Mtanzania anajua Ufisadi wa hao Pipapa:embarassed2: Tena wala usituandikie ujinga kama huu hapa JF
 
Kiasi gani umepewa kuja hapa JF kuwasafisha Mafisadi papa RA & EL? Acha unafikir hali kila Mtanzania anajua Ufisadi wa hao Pipapa:embarassed2: Tena wala usituandikie ujinga kama huu hapa JF

JF kata bwana,

Nyie ndio wale wale wafuata mkumbo, wengine tunawaza globally zaidi ( sorry kujisifu) mnabaki na hoja dhaifu sana, umetumwa umepewa fedha...........UFISADI ni tabia iliyoko kwa watanzania wengi, na tuendako hata unaowaona wasafi utakuja ku-prove ni wachafu.

acha mkumbo jibu hoja...
 
Thread hii haihitaji wavivu wa kufikiri, mtasema ...anawasafisha, umetumwa, craps, umepewa sh.ngapi, huna tofauti kabisa na wanasheria wa TANESCO wasiojua A wala B na wanaingizwa mknege mchana mchana, mara unamponda mara unamsafisha tatizo ni WEWE haujanielewa... HUNA HOJA KAA NJE, sitajibu vijembe sijapiga kijembe naeleza HALI HALISI TUNAYOISHI HUMU! SINA USHABIKI WA CHAMA

nasema hivi, nasema hivi, kuwa wafanyabiashara wajao watazuiliwa vipi wasiwe rostam au el, umenipata??

Kuna hoja huwa hazijibiki mpaka umekaa chini kwanza na kutafakari this is really JF mambo ya kata hapa hayapo.

Hujaelewa -uliza
imekuchoma- lia
imekufurahisha- cheka
inafundisha katekeleze

imeakuamsha usifanye shingo yako kuwa ngumu......Nchi hii ambayo kila mtu ni fisadi we need serious reformation to believe our leaders ebo!

kumbe unajua kuwa tunahitaji katiba mpya sasa,..ninachoappreciate ni kwamba unajua kuandika story ndefu,ur intetions were good lakini naona umeandika kitu ambacho tayari jibu ulikuwa nalo..jibu ni katiba why beating around the bush..
 
Kwanza umelinganisha fisadi na asiye fisadi (Mbowe) mwenye nafasi ya kujifunza kupitia makosa ya wenzake kama RA na EL....Mbowe kama alivyokuwa Lowassa hatoki familia maskini,baba yake Aikael hakuwa maskini.....Mbowe kuchagua kuwa CHADEMA alichagua akijua maslahi binafsi ambayo angeweza kupata akiwa CCM na kama Mwenyekiti wa CHADEMA na mfanyabiashara kuna sehemu nyingi sana angeweza kutumia influence yake kufanya ufisadi au kudhulumu....hadi sasa bado hana record hiyo......kama ipo tungefurahi kuipata...

Nafikiri system itakayoweza kuwadhibiti ni mabadiliko makubwa ya katiba,yatakayoondoa mamlaka kubwa ya rais na yatakayotengeneza mazingira ya upatikanaji wa haki kupitia independent state organs hata kwa walio viongozi kama inavyotokea leo kwa Chirac huko Ufaransa.....tukiweza ziba mianya wanayotumia kama kinga mafisadi tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana.....sheria zetu zina mianya mikubwa ya rushwa na wenye mamlaka au wenye uhusiano na wenye mamlaka wanatumia hili vibaya.....manake kama Rais ndo anateua judge na fisadi ni shemeji yake....huoni kuwa kama kuna nafasi ya ku-influence maamuzi ataitumia???

Rostam and EL ought to be responsible for their actions....haijalishi walishachangia nini bungeni au ni wachapakazi sana.....all that does not make it right.....:smash:
 
Thread hii haihitaji wavivu wa kufikiri, mtasema ...anawasafisha, umetumwa, craps, umepewa sh.ngapi, huna tofauti kabisa na wanasheria wa TANESCO wasiojua A wala B na wanaingizwa mknege mchana mchana, mara unamponda mara unamsafisha tatizo ni WEWE haujanielewa... HUNA HOJA KAA NJE, sitajibu vijembe sijapiga kijembe naeleza HALI HALISI TUNAYOISHI HUMU! SINA USHABIKI WA CHAMA

nasema hivi, nasema hivi, kuwa wafanyabiashara wajao watazuiliwa vipi wasiwe rostam au el, umenipata??

Kuna hoja huwa hazijibiki mpaka umekaa chini kwanza na kutafakari this is really JF mambo ya kata hapa hayapo.

Hujaelewa -uliza
imekuchoma- lia
imekufurahisha- cheka
inafundisha katekeleze

imeakuamsha usifanye shingo yako kuwa ngumu......Nchi hii ambayo kila mtu ni fisadi we need serious reformation to believe our leaders ebo!


Ndugu yangu,unaposema kila mtu ni fisadi unamaanisha? mimi sio fisadi....

i agree we need serious reformation.....and that should start with corrupt leaders bn held responsible for their actions....otherwise it will be hard to reform this country!
 
Waberoya,.....Kwahiyo hitimisho lako ni kuwa UFISADI HAUWEZI KUISHA TANZANIA?
 
Kiasi gani umepewa kuja hapa JF kuwasafisha Mafisadi papa RA & EL? Acha unafikir hali kila Mtanzania anajua Ufisadi wa hao Pipapa:embarassed2: Tena wala usituandikie ujinga kama huu hapa JF

ujinga upo wapi hapo?,umeshaambiwa ni challenge,unaropoka utafikiri una kaa la moto kinywani,
jenga hoja kama mtoa hoja alivyoiwakilisha
 
Waberoya,.....Kwahiyo hitimisho lako ni kuwa UFISADI HAUWEZI KUISHA TANZANIA?

Kaka sijahitimisha naomba constructive ideas what to do?

'Dick' makamu wa rais wa zamani wa marekani ana makampuni ya ujenzi na anashindania tender kama kaiwaida, na iraq amejenge sana. still their process are transparent, smooth, hakuna influence za wakubwa kama huku kwetu kwenye tender processing.

Nataka nijue how we can remedy this situation, kipi kifanyike

Kesho nikigombea ubunge nitagombea kwa tiketi ya CDM ili hali nina makapuni yangu, nikipata uwaziri nitakubali yafe?? nataka maechanism kipi kifanyike mkuu!

we can solve this at JF and JF only!
 
kumbe unajua kuwa tunahitaji katiba mpya sasa,..ninachoappreciate ni kwamba unajua kuandika story ndefu,ur intetions were good lakini naona umeandika kitu ambacho tayari jibu ulikuwa nalo..jibu ni katiba why beating around the bush..


Katiba itakayozuia watu kufanya biashara na kuziacha biashara zao pindi wanavyotaka kuwa viongozi!!???
 
Kwako Kaka

JINSI GANI TUTAZUIA MAFISADI WA SASA NA WOTE WAJAO KWA ASILI YETU HII YA UBINADAMU WA KUPENDA FEDHA.

Kichwa cha habari chajieleza;


Nahamishia swali kwako msomaji, kaa chini tafakari angalia uzuri na utamu wa fedha , wewe ni kiongozi na una makampauni yako , uwezo wa kupata kazi unao na ukapata fedha zaidi……. Unafikiri ni KITU GANI KITAKUZUIA usitake unachoona ni chema kukipata? Ndio leo mnamlaumu mkapa wakati hakuna mechanism ya kumzuia kuiba? Na akiiba hashtakiwi? Kwani nani asiyejua SONGAS ni ya Kikwete na atasemwa baada ya kuondoka madarakani! Jamani ubinadamu na dhambi ni mapacha! We are fallible creatures no one will dare to say he is smart if nothing hinders him to enjoy his/her freeness ..fikiria sasa kama kungekuwa hakuna ukimwi! Haya hupo sasa….

Mimi mtiifu
Waberoya

Huu ujumbe kwenye RED leo ndio nausikia; au unasubiri akitoka ndio tuanze kuyasikia 2016?
 
Ni rostam huyu 1994 aliyezuia mifumuko ya bidhaa za zanzibar, 1999 Rostam. 2004 Rostam alizuia shilingi kwenye wizara ya uchumi na mipango iliyokuwa chini ya Kagoda
Mkuu umemsifia RA hadi kuna sehemu umesema tu 1999 halafu RA bila kusema alifanya nini hiyo 1999.Hata hivyo it is amazing kama hiyo record uliyoiweka hapo juu ni ya kweli,je kuna namna yoyote unaweza kuprove hizo accreditions?Yani ule ujambazi wa Kagoda unampa heshima ya kuufanyaje?Ama is it a different Kagoda you're talking about?
 
Mwl.Enginner Weboroya Mke wa Mbowe ambaye ni Daktari wa binadamu na mtafiti mzuri sana amebwaga manyanga ya kikazi kwa muda ili angalie miradi mzee asonge mbele na gurudumu la kutukomboa Mbowe nadhani ni mtu ambaye anajua mmipaka yake hata kabla yakuwa kwenye madaraka ya kiserikari huyu amejitahiidi kuhakikisha mambo ya biashara yanakuwa na uongozi mwingine kabisa ndani ya familia
 
Mkuu umemsifia RA hadi kuna sehemu umesema tu 1999 halafu RA bila kusema alifanya nini hiyo 1999.Hata hivyo it is amazing kama hiyo record uliyoiweka hapo juu ni ya kweli,je kuna namna yoyote unaweza kuprove hizo accreditions?Yani ule ujambazi wa Kagoda unampa heshima ya kuufanyaje?Ama is it a different Kagoda you're talking about?

Jmushi, inakuwaje record nzuri kam anavyoripoti "Waberoya" Gazeti la Mtanzania, Rai wasiandike kuhusiana na bosi wao!!! ama kweli ukipenda chongo utaita kengeza!!!
 
Mi ninacho fikiri hapa, Tatizo ni mfumo mzima ulivyo. Kama unavyojua Serikalini yetu watu wamekaa kwa kulindana zaidi bila kujali nchi inaumia.
Ukifatilia nchi za wenzetu, utagundua siri ya mafanikio imetoka wapi, Chukua mfano wa karibu sana Kenya, kila jambo ambalo linakwenda kinyume kidogo wanachi na wanasiasa wanapiga kelele. Lkn hapa kwetu ukipiga kelele unaleta vurugu! Sio kweli Jamani lazima watu waliopo serikalini waamushe.
Tufanye nini ili kuondokana na Khali hii: Tubadilishe Chama kilichopo madarakani, ili tulete chama kingine ambacho kitakuta na mtazamo tofauti, na mtu akiiba ataonekana na sheria itachukua mkondo wake na hii ndio siri ya nchi za magharibi. Chama kikivurunda wanawekwa pembeni,ili kijifunze na wengine wanaingia kazini. Bila hivyo, watu watadumisha maslai yao milele na milele, na tutalalamika sana.
 
Back
Top Bottom