Chakula gani ulikula mara moja na kwa mara ya kwanza hadi leo hutaki tena kukila?

3.KONGORO

natamanigi sana nikiona mtu anakula kongoro anahangaika na bomba lile,huku akpga kijiko cha supu,nahisi anakula kitu kitamu sana,siku moja isiyo na jina namimi nikaitsha kongoro,wapendwa hamna siku hela yangu iliniuma kiasi kwamba nikatamani kulia kama ile siku,maana ki ukweli lile kongoro ile nimeweka mdomoni tu nilirudsha chenchi,ikabd nisingizie naumwa,nikatoka eneo lile nikabadlisha kiwanja nikarudi kwenye supu zetu za ng'ombe.
Mkuu me unakosa vitu adimu sana asee
 
Nilikoma kufuata mkumbo,nilivyoanza kunywa tu niliota vipele mwili mzima Kama nimetambaliwa na duduwasha hapo mwili unawasha sio poa,,sitaki hata kumuona huyo mdudu
Polesana alafu ni watu wengi Kuna watoto wa nduguzangu hai hata wakigusa mchuzi tu wa pweza wanawashwa balaa
 
Mambo vipi wanaJF natumai mko poa. Kwenye misosi kuna kuwa na kile chakula una hamu nacho au tu umekuta sehemu kimepikwa kwasababu hujawahi kula unaamua kula huo msosi kwa mara ya kwanza lakini chakula hicho kina kushinda kabisa hata kukupelekea kujisikia vibaya.

Mimi miaka ya nyuma nilikuwa nasikiaga kuhusu supu ya kongoro siku na mimi nikaamua nijue ikovipi hiyo supu nikaenda sehemu nzuri tu nikaulizia nikaambiwa ipo basi nikaletewa pale nikaanza kuipiga lakini kidogo tu nilikula kama vipande viwili tu vya ile nyama nikajisikia kuchefuchefu vibaya sana hata hiyo nyama kumeza haimezeki nikaacha supu karibia yote pale hadi leo hii sitaki tena kusikia kuhusu hiyo supu

Nyingine hii ilikuwa ni juisi ile ya rozela nilikuta imetengenezwa sehemu nikanywa glasi moja ilikuwa na ladha nzuri tu lakini baada ya hapo nilijisikia vibaya sana kama kizunguzungu mara kama mwili unataka ku vibrate mara jasho linatoka japo kulikuwa na feni yaani ilikuwa ni shida mpaka leo nikiiona hiyo juisi naipitia mbali kabisa. Hata juisi ya miwa ilinishinda kabisa ni bora nile muwa kama muwa

Vipi kwa upande wenu wadau ni kitu gani ulikula lakini baada ya hapo hutaki tena kukila.
Maziwa ya kuku
 
Mambo vipi wanaJF natumai mko poa. Kwenye misosi kuna kuwa na kile chakula una hamu nacho au tu umekuta sehemu kimepikwa kwasababu hujawahi kula unaamua kula huo msosi kwa mara ya kwanza lakini chakula hicho kina kushinda kabisa hata kukupelekea kujisikia vibaya.

Mimi miaka ya nyuma nilikuwa nasikiaga kuhusu supu ya kongoro siku na mimi nikaamua nijue ikovipi hiyo supu nikaenda sehemu nzuri tu nikaulizia nikaambiwa ipo basi nikaletewa pale nikaanza kuipiga lakini kidogo tu nilikula kama vipande viwili tu vya ile nyama nikajisikia kuchefuchefu vibaya sana hata hiyo nyama kumeza haimezeki nikaacha supu karibia yote pale hadi leo hii sitaki tena kusikia kuhusu hiyo supu

Nyingine hii ilikuwa ni juisi ile ya rozela nilikuta imetengenezwa sehemu nikanywa glasi moja ilikuwa na ladha nzuri tu lakini baada ya hapo nilijisikia vibaya sana kama kizunguzungu mara kama mwili unataka ku vibrate mara jasho linatoka japo kulikuwa na feni yaani ilikuwa ni shida mpaka leo nikiiona hiyo juisi naipitia mbali kabisa. Hata juisi ya miwa ilinishinda kabisa ni bora nile muwa kama muwa

Vipi kwa upande wenu wadau ni kitu gani ulikula lakini baada ya hapo hutaki tena kukila.
Nyama ya Sungura
 
Makaroni nilikula 2004 hadi Leo sijawahi kula tena.

Hayakunivutia.

Pia zule INSTANT NOODLE Hapana kwakweli hayana ladha.

Huwezi Amini nimekula biriyani mara mbili tu tangu nizaliwe na nilikipenda sana hiko Chakula.

Tatizo Niko mazingira ambayo hiki Chakula hawana stimu nacho so hakikipatikani.
 
Una tumbo la kabureta 🤣
Mkuu ikishaitwa nyama nafyeka kama kawa. Nilienda kwa wahadza nilicshindwa kula ni jongoo flani wanakaa kwenye miti iliokufa ila nshaongeza list nyani nyoka na wadudu wengine hata sijui majina yao unakula kitu mdomoni kinafanya kachu kachuu michuzi tu kama mlenda😂
 
Back
Top Bottom