Chakula cha mama Mdigo Ubungo Kibo

Miaka ya 2003 Arusha alikuwepo mama mmoja maarufu kama Mama bajaa maeneo ya kanisa la st Teresa karibu na hoteli ya Barcelona, alikuwa anapika mihogo siyo ya sayari hii watu wanafurika balaa inasemekana alikua anachanganya mihogo na makamasi.....mixer ile kachumbari ya maji ya mto naura
 
inasemekana alikua anachanganya mihogo na makamasi[emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064]
 
.
 

Attachments

  • 20221204_052700.jpg
    74.2 KB · Views: 28
Hizi mambo wakati mwingine ni saikolojia tu, kiasili sisi waafrika tunaamini uchawi kuliko sayansi au fact. Ukweli kuna watu wamejaaliwa kipaji cha mapishi .

Unaweza kuta hata huyo mama anaepika vzr na anapika vizuri kweli, hajiamini mpk aweke manjonjo ya kwenda kwa "mtaalamu". Nachojua wapishi wazuri wapo na nachoelewa watu wengi hupenda kula vizuri sana, kuna wanawake wanaolewa sababu ya mapishi tu. Nawajua ndugu na jamaa wanaojua kupika vzr mno akipika lazima ujing'ate ulimi. Sasa wewe mtu anakupikia maharagwe anaweka mafuta kidogo na maji kibao, kisha uende sehemu mama anakupikia haragwe nazi shatashata na chapati za kurasa unachokokaje?

Watu wengi wa pwani hususani Tanga na Dar (wazaramo) wamebarikiwa kujua kupika vizuri, ukizoea kula vyakula vinavyopikwa vzr ukila vingine utaona tu kama wala makarasi, na hili lipo hata katika migahawa mikubwa, wanakwambia ukiwa na plan ya kufungua mgahawa cha kwanza kukifanyia kazi ni chef, kwa maana chef ndy mgahawa wenyewe.
 
Kuna ushirikina mkubwa sana kwenye biashara ya chakula. Nina shuhuda zenye ithibati za kutosha sana
 
Kuna bibi pale karibu na St benard lumumba,alikuwa anatuuzia futari aisee taamu. Ana tukana huyo lakini tuuupo tuuu, miye ule mchuzi na chapati na magimbi hoi. Uji buree teena wa unga wa muhogo. Sijui km tulikuwa salama aiseee.
 
https://www.facebook.com/
View: https://www.facebook.com/share/v/M6F9pJaJY9xPuL86/?mibextid=Mk4v2M
 
Katika vitu sivipendi,kuona wingi wa watu kuhitaji kitu,ambacho kinapatikana kila sehemu . Mfano wale wanaopanga foleni Kariakoo kwa yule mama ntilie. Machale yananicheza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…