Mama Anauza Sufuria 5 Kubwa za Chakula Kwa Siku: Halipi 100 Serikalini!

Mama Anauza Sufuria 5 Kubwa za Chakula Kwa Siku: Halipi 100 Serikalini!

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
16,688
Reaction score
25,467
"Mama Manyema" anayefanya biashara ya Chakula kariakoo, ana siri kubwa!

1. Hana fremu wala kizimba!
2. Hajapima afya kama miongozo ya afya wala hakaguliwi.
3. Haijulikani anapopikia kwakuwa huleta chakula kwa kirikuu na toroli/guta toka Temeke Sudani!
4. Mama hatoi risiti wala hana leseni ya manispaa wala BRELA.
5. Mama hana TIN wala halipi kodi.
6. OSHA, TBS, bibi afya wanampita kama mgonjwa wa EBOLA.
7. Mama hana Risiti
#Ujanja ni kutochukua Fremu/Hakuna wa Kukidai.
 
Mama Manyema anayefanya biashara ya Chakula kariakoo, ana siri kubwa!

1. Hana fremu wala baraza.
2. Hajapima afya wala hakaguliwi.
3. Haijulikani anapopikia kwakuwa huleta chakula kwa kirikuu na toroli/guta.
4. Mama hatoi risiti wala hana leseni ya manispaa wala BRELA.
5. Mama hana TIN wala halipi kodi.
6. OSHA, TBS, bibi afya wanampita kama mgonjwa wa EBOLA.
#Ujanja ni kutochukua Fremu/Hakuna wa Kukidai.
Hivi vyakula huwa sili kwa sababu kuna wengine wanatumia mambo ya kishirikina sana ili kuvuta watu. Unaweza kutapika utumbo ukiambiwa wengine huwa wanaweka nini kwenye hiyo michuzi!
 
Watakwambia amejiari kwakuwaa eweka mazingira mazuri ya kufanyia biashara.
Mama mama mama mama
Pumbav
Umeona mbali!
Yani mtu unaenda benki kukopa, unaambiwa uje na dhamana ya nyumba, uje na TIN, uje na BArua, uje na Valuation, ukishapata una ambiwa sasa subiri miezi miwili. Ukishapata, Unaambiwa kibali , OSHA,WCF, Manispaa, Taka na mazaga mengine wacha tu ile kila mtu anataka kupima afya.
Ukifungua fremu wanataka ulinzina kila aina ya kodi, alafu. inabiidi auze ghali kufidia gharama za kodi wakati huyu mama halipi chochote.
 
Kuna nyakati ukisharasimisha tu biashara ni kama umetangaza vita, kuanzia bibi Afya mpaka halmashauri wanakuwa washirika wako wakuu wa biashara.

Hujafanya hili, hujafanya lile, huna fomu hii, huna fomu ile, mara wito. Yaani mtu asiyerasimisha hapati usumbufu kama mrasimishaji ambaye ndo mlipa kodi.
 
Ndo tabia ya wafanyabiashara wengi wa Kibongo! Akiona wateja wanahitaji huduma yake kwa wingi anawadharau mawasiliano yanakua 0
Tuna shida eneo hili, naona wanawakemea tu
 
Kuna nyakati ukisharasimisha tu biashara ni kama umetangaza vita, kuanzia bibi Afya mpaka halmashauri wanakuwa washirika wako wakuu wa biashara.

Hujafanya hili, hujafanya lile, huna fomu hii, huna fomu ile, mara wito. Yaani mtu asiyerasimisha hapati usumbufu kama mrasimishaji ambaye ndo mlipa kodi.
Kazi kweli kweli
 
Back
Top Bottom