Chakula bora cha Nguruwe wa kisasa

Chakula bora cha Nguruwe wa kisasa

Tunauza koudjis ya nguruwe kilo 50, ni concentrates yenye virutubisho muhimu kwa nguruwe. Tuna koudjis concentrates ya 20/15 kwa ajili ya wenye mimba, kupata joto, na wanaonyonyesha. Pia tuna koudjis concentrates ya 30/25 kwa ajili ya wanaokuwa, na ukuzaji wa nguruwe.

Formula ni rahisi kabisa karibu,

Hapo chakula chako ukichanganya na koudjis inabidi uchukue kg 25 za koudjis plus kg 75 za mahindi au pumba ya mahindi... Una mix vzr upate kg 100 then unalisha nguruwe ni rahisi sana.

Wateja wote wanaotumia koudjis concentrates pig, wana matokeo mazuri juu ya chakula chetu.
Ngoja tuone
 
Unahangaika bule kitu Mungu akishasema haramu basi ujue ni haramu tu

Kwani usizitimie hizo nguvu kufuga Ng'ombe?
Kuliko hivyo unavyohangaika kufuga binadamu wenzake wa zamani waliolaniwa
Wewe acha jamaa aenjoy kufuga mdudu.
 
Taratibu kwanza hivi concetrate ni nn kwanza maana hapa naona kuna shida mahali hakuna sehemu au ingredients inaitwa ilo jina sema makanjanja wameshawadanganya wafugaji wengi lengo wajipatie pesa kwa udanganyifu
Sio kwamba hiyo shida mahali utakuwa nayo wewe Mkuu?

Concentrate imekuwepo kwa miaka mingi na asilimia kubwa wafugaji wanaijua labda wewe tu ndio huijui

Anyway, kwa Tafsiri nyepesi kabisa concentrate ni Aina ya chakula ambacho kinakuwa na virutubisho vingi na kina uhaba wa carbohydrates na fibers

Concentrate huchanganywa kwenye chakula kingine ili kukiboresha, unakuta concentrate ina 50kg na unachanganya kwenye 150kg ya chakula cha kawaida (hasa pumba)
 
Sio kwamba hiyo shida mahali utakuwa nayo wewe Mkuu?

Concentrate imekuwepo kwa miaka mingi na asilimia kubwa wafugaji wanaijua labda wewe tu ndio huijui

Anyway, kwa Tafsiri nyepesi kabisa concentrate ni Aina ya chakula ambacho kinakuwa na virutubisho vingi na kina uhaba wa carbohydrates na fibers

Concentrate huchanganywa kwenye chakula kingine ili kukiboresha, unakuta concentrate ina 50kg na unachanganya kwenye 150kg ya chakula cha kawaida (hasa pumba)
Teheeeee ngoja nicheke na niishie hapa Mr animal feed nutritionists
 
Unahangaika bule kitu Mungu akishasema haramu basi ujue ni haramu tu

Kwani usizitimie hizo nguvu kufuga Ng'ombe?
Kuliko hivyo unavyohangaika kufuga binadamu wenzake wa zamani waliolaniwa
Hee.. ndio maana majini yanakimbia yakiona nguruwe
 
Mkuu labda ungekuwa specific kuwa hasara unapataje, kwa sababu kwa kuangalia hapo me sioni unpataje hasara labda udadavue hizo materials unanunua kwa kiasi Gani na hiyo 1tan wanakula nguruwe wangapi kwa siku ngapi
Hii walinielekeza ni majani yanaitwa LUKINA. sijajua wengine mnaitaje
 
Natumi
Mkuu labda ungekuwa specific kuwa hasara unapataje, kwa sababu kwa kuangalia hapo me sioni unpataje hasara labda udadavue hizo materials unanunua kwa kiasi Gani na hiyo 1tan wanakula nguruwe wangapi kwa siku ngapi
a 250k na wanakula kila mmoja 3-4kg kwa siku maana yake mwezi hauishi
 
Ndi
Hutopata matokeo kwa uchanganyaji huu!
Msome nguruwe na umjue vizuri mahitaji yake + soma malighafi moja moja ina undwa na nn na nini kisha rudi kwenye hesabu kupata folmula. Ila ukiona SI njia nyepesi kubali kutoboka mfuko ULIPIE formula kutoka kwa wadau/ tafuta mfugaji mzoefu atakae kubali kukuelekeza bure( sina uhakika na hili) la sivyo ukubali kununua vyakula( concentrate) na kufuata maelekezo ya mzalishaji.
o maana nikahitaji msaada mwanajamii
 
Acha ukafiri we jamaa ujue ww unaheshimika humu jf
Ukafiri gani mwamba wakati tunaona kabisa! Pembe la ng'ombe halifichiki mkuu. Wakati wa mfungo mauzo ya kitimoto huwa yanashuka mno lakini tukifungua tu hayooo!
 
Ukafiri gani mwamba wakati tunaona kabisa! Pembe la ng'ombe halifichiki mkuu. Wakati wa mfungo mauzo ya kitimoto huwa yanashuka mno lakini tukifungua tu hayooo!
Mkuu weww ni icon kwa watu humu
Sasa unavosifia nguruwe unaleta picha gani kwa jamii ya jf humu mkuu wangu.. ebu kuwa na staha ...

Jaribu hata kuheshimu vijana ambao tunakuangalia wewe kama kiongozi wetu.

Sijategemea kama utakua miongoni mwao mkuu.
Mbona unataka nikushushe vyeo mkuu wangu...
 
Mimi natumia gharama kubwa kupata mchanganyo kwaajiri ya nguruwe ambao ni:-
Pumba mahindi 700kg
Concentrate 50kg
Mashudu 200kg
OlaQuindox 500mg
Bokhash 10kg
Dcp 10pkt
Pig booster 10pkt
Toxic binder 1kg
Jumla tani 1 ya chakula.
Napata matokeo lakini faida inakuja ndogo sana.
Je wanajamii kunamwenye mchanganyo mzuri na wenye gharama nafuu.
Nguruwe asipewe Chakula Bora mana ni haramu, na mla nguruwe sawa na mtu anae bet zambi zake.
 
Mkuu weww ni icon kwa watu humu
Sasa unavosifia nguruwe unaleta picha gani kwa jamii ya jf humu mkuu wangu.. ebu kuwa na staha ...

Jaribu hata kuheshimu vijana ambao tunakuangalia wewe kama kiongozi wetu.

Sijategemea kama utakua miongoni mwao mkuu.
Mbona unataka nikushushe vyeo mkuu wangu...
Sema hatujuani, ningekualika ukutane na kitu ya moto iliyochanganywa na ka mchicha kidogo! Wewe nishushe tu hivyo vyeo lakini kuacha kitimoto siwezi!
 
Natumi

a 250k na wanakula kila mmoja 3-4kg kwa siku maana yake mwezi hauishi
Sawa Mkuu, jaribu kuangalia kiasi unachowapa labda unaweza ukawa una overfeed, kwa sababu nguruwe waga haridhiki ata umpe kilo 10 anaweza akamaliza

Unatakiwa ukumbuke kuwa wewe ndio mwenye jukumu la kumpangia kiasi cha kula mnyama wako na sio yeye akupangie kiasi cha kumpa

Nguruwe anapewa chakula kulingana na uzito wake, hivo jitahidi ujue uzito wao ili uwe unawapa kiasi kinachotakiwa, kwa sababu kama nguruwe wa kupewa 2.5kg we ukampa 3.5kg hapo ni Hasara na mbaya zaidi wakiwa wengi
 
Tunauza koudjis ya nguruwe kilo 50, ni concentrates yenye virutubisho muhimu kwa nguruwe. Tuna koudjis concentrates ya 20/15 kwa ajili ya wenye mimba, kupata joto, na wanaonyonyesha. Pia tuna koudjis concentrates ya 30/25 kwa ajili ya wanaokuwa, na ukuzaji wa nguruwe.

Formula ni rahisi kabisa karibu,

Hapo chakula chako ukichanganya na koudjis inabidi uchukue kg 25 za koudjis plus kg 75 za mahindi au pumba ya mahindi... Una mix vzr upate kg 100 then unalisha nguruwe ni rahisi sana.

Wateja wote wanaotumia koudjis concentrates pig, wana matokeo mazuri juu ya chakula chetu.
Mkuu umetangaza biashara yako ikiwa nusu sasa sijui wateja utatupata vipi

Tumejua mnauza koudjis concentrate ila hatujui bei,hatujui mnapatikana wapi,hatujui mawasiliano yenu

Nadhani ungekamilisha taarifa za msingi ili wafugaji tuone kama inawezekana kufanya kazi pamoja
 
Teheeeee ngoja nicheke na niishie hapa Mr animal feed nutritionists
Mkuu mimi ni mfugaji tu na sio mtaalamu wa chakula, na maana niliyotoa ni kwa mujibu wa watu wanaotuuzia hizo concentrate ndio wanatuambia hivo

Kwahiyo kama nimekosea karibu unisahihishe, inawezeana kwa namna moja au ingine tunadanganywa na Hawa wauzaji, kwahiyo kuliko kuishia kucheka ni bora ukatusaidia kutupa ukweli juu ya hizi concentrate
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom