Chaguzi zilizowahi kutenguliwa, Chadema hamjaonewa

Majasho

JF-Expert Member
Aug 4, 2009
413
220
Mwaka 1996 aliyekuwa mbunge wa Temeke, Ramadhani Ali Kihiyo alivuliwa ubunge baada ya Mahakama kumtia hatiani kwa kosa la kughushi cheti na nafasi yake ilichukuliwa na Augustine Mrema, wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Chama cha NCCR- Mageuzi.

Vivyo hivyo Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba ilitengua ubunge wa aliyekuwa mbunge wa Biharamulo Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Tanzania Labour (TLP), Phares Kabuye.

Kabuye aliyefariki dunia kwa ajali ya gari akiwa njiani kuelekea jijini Dar es Salaam, alivuliwa ubunge baada ya mahakama kuthibitisha kuwa katika mchakato wa uchaguzi mwaka 2005, alimdhalilisha mgombea mwenzake, Anatoly Choya.

Desemba 28, 2007 Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, kupitia kwa Jaji Josephat Mchome ilitengua matokeo ya aliyekuwa mbunge wa Mwibara Charles Kajege kutokana na kutiwa hatia kwa rushwa.

Kesi ya kupinga matokeo ya hayo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo kupitia TLP, Mtamwega Mgaywa, (TLP) aliyeshindwa katika Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Hata hivyo, Septemba 25, 2009, Mahakama ya Rufaa chini ya majaji watatu, wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania wakati huo, Agustino Ramadhani, January Msofe na Jaji Mbaruku, walimrejeshea Kajege ubunge kutokana na rufaa aliyokata dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu.
 
Kesi ya Kabuye dhidi ya Choya inaweza kufanana fanana na ya Lema ... alimdhalilisha mgombea mwenzake!

Kabuye alikata rufaa mahakama kuu ya rufaa, very unfortunately hadi anafariki mahakama kuu ya rufaa ilikuwa hajatolea hukumu shauri lake, Hivyo we will never know the TRUTH.
 
Unaona sasa! unamrejeshea ubunge mtu sept 2009 miezi 10 kabla ya uchaguzi mkuu 2010! hizi bangi hizi! hakuna haja ya rufaaa! twende kwenye uchaguzi Lema kafungiwa tunamtaka Dr. Slaa! hakuna njia tena ya dr. kuendelea kukataa
 
Desemba 28, 2007 Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, kupitia kwa Jaji Josephat Mchome ilitengua matokeo ya aliyekuwa mbunge wa Mwibara Charles Kajege kutokana na kutiwa hatia kwa rushwa.

Kesi ya kupinga matokeo ya hayo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo kupitia TLP, Mtamwega Mgaywa, (TLP) aliyeshindwa katika Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Hata hivyo, Septemba 25, 2009, Mahakama ya Rufaa chini ya majaji watatu, wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania wakati huo, Agustino Ramadhani, January Msofe na Jaji Mbaruku, walimrejeshea Kajege ubunge kutokana na rufaa aliyokata dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu.


JUSTICE DELAYED IS JUSTICE DENIED. Ninafikiri hii ndiyo wanajaribu kucheza nayo CCM kwa suala la Arusha.CCM sala zao zote ni kwamba CDM wakate RUFAA.

Angalia hiyo kesi Kajege hapo juu. Uchaguzi ulifanyika mwaka 2005.

Miaka miwili baadaye 2007 Mahakama ikatengue ubunge wa Kajege (kama ilivyofanya Arusha 2010-2012)

Kajege akakata rufaa mahakama kuu ya rufaa, miaka 4 baadaye 2009 ikamrudishia ubunge wake.

Ninashawishika kuamini kwamba kama Lema ataka rufaa, hukumu yake itakuwa 2014 mwaka mmoja kabla ya uchaguzi wa 2015.

Concern yangu KUBWA mimi ni hiyo HUKUMU FAKE ya Judge Rwakibalila kuendelea kuwemo kwenye kumbukumbu za mahakama kama CDM wataamua kuingia kwenye uchaguzi.

Sijui wana sheria nini kifanyike kurekebisha hii situation. Inavyonekana watu wengi, Sorry I'm not a mouth speaker of watu wengi, lakini watu wengi wanaamini HAKI HAIKUTENDEKI ktk hukumu na hii ni hatari kwa mustakabari wa TAIFA LETU.
 
tundu lisu alitoa jasho bungeni kutetea uhuru wa mahakama lakini inavyoonekana wanasheria wanatumiwa kama walimu tu!wanasimamia maslahi ya ccm.
 
Njia mojawapo kubwa ya kuondoa udahalimu wa CCM na serikali yake ni kuwa na katiba mpya itakayoweka utaratibu mpya wa kuwa na vyombo huru vya maamuzi ambavyo haviwezi kuingiliwa kwa namna yoyote kwa self-interests. Wenzetu Kenya wameenda mabli kidogo katika hili. Je katika hali hii ya mlolongo wa chaguzi ndogo ni lini watanzania watapata muda kuzungumzia katiba yao? Isije ikawa ni mbinu ya CCM ya kutupeleka 2015 bila katiba! Chonde chonde CCM...msikaribishe maafa!
 
tundu lisu alitoa jasho bungeni kutetea uhuru wa mahakama lakini inavyoonekana wanasheria wanatumiwa kama walimu tu!wanasimamia maslahi ya ccm.

Walimu hawatumiwi mkuu, we hujaona kazi ya walimu hadi sasa? We unadhani vuguvugu la mabadiliko lilipo nani amepanda hiyo mbegu kwa vijana wetu kabla ya wanasiasa wa upinzani? Bila shaka ni waalimu ndiyo maana hata watoto wa primary leo ni People's Power. Hivyo kuwafananisha walimu na mahakimu unawakosea sana.
 
Avoidance of election on election position or illegal practice to be removed No. 1 Elections 1995 47

108.-(1) The election of a candidate as a member shall not be
questioned save on an election petition.

(2) The proceedings of a meeting of the Electoral Conference, the
National Executive Committee, a Political Committee of the Party or the
Central Committee or any other organ of the Party which is held for the
purposes of this Act shall not be subject to review in any court, either by
way of an election petition or otherwise:
Provided that nothing in this sub-section shall apply to any non-compliance
with the provisions of subsections (2), (3), (4) or (5) of section 77
of the Constitution where any question of such non-compliance is raised
in the first instance on an election petition and not otherwise.
(3) The election of a candidate as a member shall be declared void on
any of the following grounds which are proved to the satisfaction of the
court, namely-
(a) that by reason of corrupt or illegal practices committed in circumstances
whether similar to those before enumerated or not the
majority of voters were, or may have been, prevented from election
the candidate whom they preferred;
(b) that, during the election campaign, statements were made by the
candidate, or on his behalf and with his knowledge and consent
or approval with intent to exploit tribal, racial or religious issues
or differences pertinent to the election or relating to any of the
candidates or, where the candidates are not of the same sex, with
intent to exploit such difference:
Provided that no petition may be presented on the grounds set out
in this paragraph without the consent in writing of not less than
one of the supervisory delegates appointed for the relevant election;
(c) non-compliance with the provisions of this Act relating to election,
if it appears that the election was not conducted in accordance
with the principles laid down in such provisions and that such
non-compliance affected the result of the election;
(d) that a corrupt or illegal practice was committed in connection with
the election by or with the knowledge and consent or approval of
the candidate or by or with the knowledge and consent or approval
of any of his agents; or
(e) that the candidate was at the time of his election a person not
qualified for election as a member.
 
Ndugu zangu, waalimu tunatakiwa kuwaheshimu sana. Hawa ndio chachu ya mabadiliko kwa vijana wetu( Rejea filamu ya Sarafina enzi zile za ubaguzi). Waalimu wana-sensitize watoto juu ya haki zao na umuhimu wa kuleta mabadiliko nchini. Kumbuka wadogo zetu waliopo mashuleni ndio wapiga kura wa kesho au tayari wameshafikia umri wa kupiga kura.Waalimu mwendo mdundo.!

A riot is the language of the unheard. Martin Luther King, Jr.
 
tundu lisu alitoa jasho bungeni kutetea uhuru wa mahakama lakini inavyoonekana wanasheria wanatumiwa kama walimu tu!wanasimamia maslahi ya ccm.

Tena ukome kabisa kutudhalilisha....nani anatumika kulinda maslahi ya ccm....???? tunapambana ucku na mchana kupiga kampeni mashule watoto wajiunge CHADEMA NA KADI ZA CHAMA TUNAWAGAWIA SISI WENYEWE LEO HII UNASEMA TUNALINDA MASLAHI YA CCM? Tuombe radhi tena haraka.....sana...!!!
 
Back
Top Bottom