CHADEMA Yazizima TANGA

CHADEMA Yazizima TANGA

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Tanga kimepata wanachama wapya zaidi ya 300.
Wanachama hao wamepatikana katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika wilaya za Handeni, Muheza na Korogwe uliohutubiwa na Katibu wa chama hicho Mkoa wa Tanga, Jonathan Bahweje.

Wanachama 220 wamejiunga na chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Kwengoma, Kata ya Kwamatuku, Wilaya ya Handeni na wanachama 71 ni kutoka Kibanda, wilayani Muheza.

Wanachama wengine 21 akiwamo mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Turiani, Bakari Kimea walijivua uanachama wa CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kwashemshi, Wilaya ya Korogwe.

Wakizungumza katika mikutano hiyo baada ya kujiunga na CHADEMA, walisema wameamua kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa kimeshindwa kuondoa kero zinazowakabili kwa miaka mingi.

Miongoni mwa kero hizo kwa mujibu wa wananchi hao ni unyanyaswaji unaofanywa na viongozi wa serikali za vijiji, kunyang'anywa ardhi, kero ya maji na kuvunjiwa mikataba na muwekezaji.

Source:Tanzania Daima Jumanne
Kiwanda cha uongo na uzushi, tz daima/dumuzi. Watu wa tanga wana akili timamu hawawezi kudanganyika ht siku moja
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Tanga kimepata wanachama wapya zaidi ya 300.
Wanachama hao wamepatikana katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika wilaya za Handeni, Muheza na Korogwe uliohutubiwa na Katibu wa chama hicho Mkoa wa Tanga, Jonathan Bahweje.

Wanachama 220 wamejiunga na chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Kwengoma, Kata ya Kwamatuku, Wilaya ya Handeni na wanachama 71 ni kutoka Kibanda, wilayani Muheza.

Wanachama wengine 21 akiwamo mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Turiani, Bakari Kimea walijivua uanachama wa CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kwashemshi, Wilaya ya Korogwe.

Wakizungumza katika mikutano hiyo baada ya kujiunga na CHADEMA, walisema wameamua kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa kimeshindwa kuondoa kero zinazowakabili kwa miaka mingi.

Miongoni mwa kero hizo kwa mujibu wa wananchi hao ni unyanyaswaji unaofanywa na viongozi wa serikali za vijiji, kunyang'anywa ardhi, kero ya maji na kuvunjiwa mikataba na muwekezaji.

Source:Tanzania Daima Jumanne

Hatudanganyiki ng'ooooooooooooooooo!!!!!!!!! Weka picha hapa km hujaumbuka
 
Hoja za CHADEMA siku zote hazibadiliki kuanzia mwenyekiti wao hadi wapambe wao walioko humu Jf na hata wale wanaojidanganya kuwa kero zao zitaondolewa na mtu mwingine au chama fulani badala ya kufanykazi kwa bidii kwa kutumia fursa zilizopo.

Tatizo ni kuwa chama tawala kinagandamiza wananchi badala ya kuwasaidia na kuwaelimisha. Kiongozi yeyote anapaswa awaeleweshe wananchi hali halisi na jinsi ya kupambana na kero zilizopo na aonyeshe mfano wa kweli wa kupambana na kero zenyewe.

Viva CDM kwa taarifa na nawapa viongozi wa CDM Tanga kwa kueneza sre za chama. Tuleteeni na za mikoa mingine pia na wasingojee viongozi wakuu wafike bali wapambane mpake kieleweke.
 
Tumeshazoea kuona wapambe na viongozi wa ccm wakitukana na kuwakashifu wanao wahama, ila wajue cdm hakina majungu. M4C ili kuongeza wanachama na wapiga kura kukiwezesha 2015 kushika dola
 
Watanzania kwa kuhama Hama vyama!!!!! Ni kutafuta maslahi, Leo CCM kesho Cuf keshokutwa chadema mtondogoo wanarudi CCM
 
Hawa wanachama hata kadi huwa hawalipii. Wengi ni kama mamluki.
 
Safi sana, wao wanahangaika na kubambikia raia kesi, CHADEMA inapiga kazi tu, safi sana ma kamanda kuendelea kuwavua magamba na kuvalisha gwanda...
Kubambika kesi wapiganaji na kusafisha magamba wenzao.
 
Kiwanda cha uongo na
uzushi, tz daima/dumuzi. Watu wa tanga wana akili timamu hawawezi
kudanganyika ht siku moja


je ? ni chadema walimlisha sumu Mwakyembe ni jibu kwanza hili swali ,ndo utapata jibu ni nani anamwagia watu tindi kali.
 
Back
Top Bottom