CHADEMA Yazidi kung'ara

CHADEMA Yazidi kung'ara

uchambuzi ni mzuri! safi sana.....kwa alie vaa miwani ya mbao kama nape,anaweza asielewe kincho endelea....
 
Hii inatia moyo kwa wapiganaji na makamanda wote nchini
 
Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22) -kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.

Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.

Katika Uchaguzi wa Udiwani uliopita(2009) kwa Kata hizo 22,CCM ilishinda kwa asilimia 86.36% na CHADEMA ilipata asilimia 9.09% na NCCR ilipata asilimia 4.54%.
 
wamevaa miwani ya mbao mkuu Arushaone

Tatizo la CCM wanadhani wananchi wa sasa ni wale wa enzi za "zidumu fikra sahihi za m/kiti". Nape anadhani watanzania ni makondoo. Nyeusi anasema ni nyeupe!!

Their end is near!
 
Mkuu katika kuweka rekodi zangu sawa naomba kufahamishwa mambo mawili.

1. Hivi Iyela Mbeya ndiko Mtera Mwampamba alipokwenda na kuondoka bila hata kufika nyumbani kwao?
2. Hii ndiyo sehemu Mwigulu alipozindua suti yake inayofanana na ya mfalme Bokassa?

Ninakumbuka ilikuwa sehemu mojawapo iliyokuwa na kampeni huko Mbeya ila jina limenitoka. Ni hayo tu mkuu...

People's...

Mkuu ndo hapohapo na kambi ya green guard iliwekwa hapohapo!!!imbombo ngafu!!!!
 
Kamanda Molemo ahsante kwa analysisi. Sisi tunajua kiwango cha kukubalika kwa Chadema kinaongezeka huku kiwango cha kuporomoka kwa ccm kikiongezeka pia.
Lakini kwakuwa wanasaidiwa na policcm na tiss ndio sababu ya kuonekana bado wanapumua hadi wakati huu.

Mkuu Mwita Maranya ongeza juhudi kule Serengeti manake naona Manchila hali si hali bali muhali!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu katika kuweka rekodi zangu sawa naomba kufahamishwa mambo mawili.

1. Hivi Iyela Mbeya ndiko Mtera Mwampamba alipokwenda na kuondoka bila hata kufika nyumbani kwao?
2. Hii ndiyo sehemu Mwigulu alipozindua suti yake inayofanana na ya mfalme Bokassa?

Ninakumbuka ilikuwa sehemu mojawapo iliyokuwa na kampeni huko Mbeya ila jina limenitoka. Ni hayo tu mkuu...

People's...

Ni hapa hapa iyela.Ndipo walipoenda na mwigulu na kuanzisha Jeshi lao la Green Guards ambalo matokeo yake ni mabomu na risasi za Arusha.
 
Naomba kufahamu, hivi ktk hizo kata zilizofanyiwa chaguzi na matokeo kutangazwa, JE ni chama gani Kimeonekana KUONGEZA au KUPOTEZA idadi ya VITI ukilinganiSha na matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010?
 
20-4=Faida.
2+4=hasara.
huu ndio mtaala wa mulugo mpya ambao wanaufanyia majaribio ndani ya ccm ukishakubalika utumike nchi nzima.
 
Mkuu Mungi hii kata ya Bashnet nani diwani mpya wa Chadema?yule Tara aliyehamia au kuna mwingine?

Halafu unamfaham wa dongobesh anaitwa nani?

Diwani wa Bashnet ni Laurent Tara
Diwani wa Dongobesh ni Kamanda Jorojik
 
Sasa ni dhahiri CCM Imezidiwa.Matokeo ya Uchaguzi wa Kata mbalimbali uliofanyika Jumapili yamepeleka kilio kikubwa CCM.

Ni kweli pia kwamba kwa Idadi ya Kata CCM imepata kata nyingi Lakini ikizidiwa kwa jumla ya kura na Chadema.

Ikumbukwe pia kuwa idadi kubwa ya wafuasi wa Chadema ambao ni vijana bado hawajaandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura.

Ni dhahiri Chadema sasa inasambaa kama moto wa nyika na matumaini ya kukamata dola uchaguzi mkuu ujao yanazidi kuongezeka.

Yafuatayo ni matokeo ya Kata 14 tuliyoyapata mpaka sasa ambayo yanaonyesha kura za Jumla Chadema imeizidi CCM kwa kura 1859.

ISEKE-SINGIDA
CCM 791
CDM 831

NYAMPULUKANO-SENGEREMA
CCM1088
CDM 1483

DONGOBESH-MBULU
CCM 974
CDM 1558

BASHNET-BABATI
CCM 1130
CDM 2008

IYELA-MBEYA
CCM 1163
CDM 1918

IFAKARA-KILOMBERO
CCM 3723
CDM 4353

MINEPA-ULANGA
CCM 1164
CDM 1004

STESHENI-NACHINGWEA
CCM 806
CDM 353

NGANGANGE-KILOLO
CCM 600
CDM 223

GENGE-MUHEZA
CCM 347
CDM 326

TINGENI-MUHEZA
CCM 363
CDM 244

MANCHILA-SERENGETI
CCM 672
CDM 623

MASANZE-KILOSA
CCM 833
CDM 623

RUNZEWE MASHARIKI-BUKOMBE
CCM 604
CDM 570

JUMLA KUU KATA 14
CCM 14258
CDM 16117

Big up malema kwa update ur tru great thinker
 
CCM ndiyo waliopoteza zaidi, maana chadema walikuwa wanatetea kata mbili wakaongeza zingine nne. CCM walikuwa wanatetea kata 20 wakapata 16 wamepoteza nne

Mkuu Mungi, hiyo taarifa ya Nape inasema CCM wamepata kata 16 na CDM kata 6 wakati kwa habari zilizomo humu JF tangu jana zinaonyesha CCM walipata kata 15 na CDM kata 7. Naona maelezo yako yanaashiria kitu hicho hicho anachokisema Nape (kata 16 kwa kata6), ina maana hiyo ripoti ya mwenezi imekosewa au ni kweli CDM wamepata kata 6? Hebu nifafanulie hapo mkuu.

cc Mohamedi Mtoi
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom