CHADEMA Yatikisa Mwananyamala Hospitali

CHADEMA Yatikisa Mwananyamala Hospitali

Hii Chadema Family iwe ya kudumu kama m4c na ibuni strategy mbalimbali na isijikite sana mijini. Vijijini muwepo pia.Hongereni sana mliyoyafanya Mwananyamala.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo 'CHADEMA' leo katika siku ya wapendanao ''Valentine's Day'' wameiadhimisha kwa kutembelea wagonjwa katika hospitali ya Mwananyamala ambayo iko katik Halmashauri ya Manisipaa ya Kinondoni. Matembezi hayo yaliongozwa na madiwani na viongozi wa jimbo na kata na matawi na wanachama wengine wa CHADEMA.

''Siku ya leo CHADEMA tumefanya usafi; kufagia, kufyeka, kukusanya takataka, kusikiliza changamoto zinazowakabiri wagonjwa na wauguzi, pia katika kuonyesha ishara ya upendo katika siku hii tumewaletea wagonjwa vitu mbalimbali ikiwemo mikate, juice, maji, sabuni nakadhalika.'' Alikaririwa mmoja wa makanda.
DSCF3950.JPG DSCF3956.JPG DSCF3960.JPG DSCF3961.JPG DSCF3962.JPG DSCF3965.JPG DSCF3966.JPG DSCF3968.JPG DSCF3978.JPG DSCF3973.JPG DSCF3980.JPG DSCF3979.JPG
 
Taarifa za kiintelegensia hazikufika mapema kwa kamanda wa polisi?? manake angwezauia kabisa kufanya hayo waliyoyafanya leo.
 
Haya ndiyo mambo yanatakiwa kufanywa na vyama vya siasa. Kuwa karibu na wananchi hasa wakati wa matatizo ni kujihakikishia ushindi wakati wa kura. Tutegemeee nao CMM watoe misaada hospitali ya Muhimbili au Temeke kesho.
 
Pongezi sana kwa mkakati huu mzuri,suala hili liendelee mpaka sehemu nyingine mikoani.Naamini makamanda wakiamua wanaweza hivyo kanda za chama ziendeleze mkakati wa kufanya usafi,kuwaona wagonjwa na kuwatembelea wafungwa ikiwa ni pamoja na kuwafariji.
 

...Mama mmoja mwenye tatizo la miguu ameonekana akiangua kilio alipowaona Chadema Family na kupaza sauti akisema '' Mungu wangu naona kama Nyerere amefufuka''
...

...IN CHADEMA WE TRUST..
 
Hapa CHADEMA wamefanya jambo jema na la kuigwa.Kila mwenye akili na nia njema aige hili.Mungu awabariki wote waliohusika.Wote tuseme amina!


Betlehem you are now getting back to your senses! Hongera kwa kuanza kuuona mwanga.
 
Tanzania tunayoitaka itajengwa na sisi wenyewe watanzania na Tanzania tusiyoitaka inaweza kuratibiwa na sisi watanzania pia. CDM Family mmefanya kazi nzuri songeni mbele! Together we can build the Tanzania we want!


Chama cha Chadema leo kupitia mtandao wake maarufu Dar es Salaam ujulikanao kama CHADEMA FAMILY kimefanya tukio kubwa la kihistoria.

Chadema Family huku wakiwa na mavazi yao maalum wamefanya usafi katika hospitali ya mwananyamala na kutembelea wagonjwa.Pia watatoa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa.

Mmoja wa Makamanda wa Chadema Family Ally Bananga amesema lengo kubwa la tukio la leo ni kuonyesha moyo wa upendo kwa wagonjwa na wahitaji.Kamanda Bananga ameendelea kusema kwamba alama ya rangi nyekundu kwenye bendera ya Chadema ina maana nyingi ukiwemo upendo kwa masikini,wagonjwa na wahitaji.

Chadema Family wameacha gumzo hapa Mwananyamala na wagonjwa mbalimbali wameonekana wakiwakimbilia Makamanda wa Chadema Family kuwauliza namna ya kujiunga na Chadema.

Mama mmoja mwenye tatizo la miguu ameonekana akiangua kilio alipowaona Chadema Family na kupaza sauti akisema '' Mungu wangu naona kama Nyerere amefufuka''.


Chini ni mavazi ya Chadema Family:
attachment.php
 
Hayo ndio mambo ya maana yanayopaswa kufanywa na wapenda maendeleo katka nchi. Big makamanda wa CHADEMA kwan lisemwalo lipo kama halipo bas linakuja.
 
Back
Top Bottom