Roho imeniuma yamepataje ivo vijiji vi4 tukaze butu mapambano yanaendelea ilitakiwa matokeo yawe 11CDM-MAGAMBA 0 inawezekana yani wasipumue.
hata mimi nashangaa au kwa kuwa m4c haijapita huko...
Siku hizi ana ID nyingi kweli subiri atakuja....Wapi Nape atoe kauli kuwa ni OIL CHAFU hao. Dah raha sana, yaani mtu unafungwa magoli wewe unaendelea kucheka tuu kuwa ni oil chafu, haya Nape endelea kutukana wapiga kura.
Upande wa pili wa shilingi mimi nadhani Nape anafanya makusudi kabisa kuua ccm na inawezekana ni shushushu wa CDM
Katika uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa kumi na moja,manispaa ya Shinyanga,CHADEMA,wamefanikiwa kupata viti 7 kati ya 11,na CCM,wakiambulia vinne!
Mitaa hiyo ni:-
1:Lubaga Farm
2:Mbuyuni
3:Magadula
4:Masekelo
5:Mwamala
6:Luhende
7:Chamaguha (Nyumbani kwa Mwenyekiti wa CCM,Wilaya).
CCM,imeshinda mitaa ya:-
1:Old Shinyanga
2:Bushushu
3:Lubaga
4:Bondeni(ambako,askari walifyatua mabomu ya machozi,baada ya kutokea vurugu,baada ya kutangazwa mgombea wa CCM,kushinda.)
Uchaguzi huo,uliofanyika jana,ilikuwa kujaza nafasi zilizokuwa wazi,ikiwa ni pamoja na mitaa iliyoongezwa,baada ya kugawanywa baadhi ya mitaa.
Wapi Ritz?
wa kagera wenzangu nilio wa-tag: (bakuza, bigaraone, chaimaharage, english learner, evoddy, gagnija, hagga, jaji, james chapacha, kagalala, kaitampunu, kanyagio, kibera, lonestriker, mkomamanga, mpiga zeze, mugunda, naivasha, ngeleshi, prn-kazi, qixima mqiqa, ruberts, rwamarungu, rweza, sangija, seneta,mukama talemwa,
speedy, timbilimu, tukundane, yakuza, tata)
mnapata picha na somo gani kutoka hapa?
huwa hapatikani kwenye thread kama hizi pamoja na Rejeo wakeWapi Ritz?
Very well done CHADEMA.
Hicho kiti kimoja walichochakachua msinyamaze wala kupuuza, pia kwa ccm kupata mitaa mitatu (halali) lifanyiwe kazi labda tu kama mitaa hiyo wanakaa wahalifu na wahamiaji haramu maana hizo kwa sasa ndizo ngome za ccm.