Mtoto halali na hela
JF-Expert Member
- Aug 10, 2012
- 54,963
- 54,077
Nilijua wanatoa za mkopo tuwalipe kidogo kidogo, bt anyway hakijaharibika kitu sababu ni jitihada za kujihakikishia ushindi hyo 2015
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA Kamanda Freeman Mbowe ametangaza mkakati wa Uchaguzi mkuu wa 2015 na moja ya mkakati huo ni kumwaga pikipiki katika tarafa zote nchini kwa lengo la kuwafikia wananchi na kueneza elimu ya uraia.Pikipiki hizo zitakuwa na vipaza sauti maalumu ambazo zitawasaidia viongozi wa chama hicho kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Mbowe aliyasema hayo mjini Hanang jana wakati akiwa anazungumza na viongozi wa chama na wadau wakuu wa CDM mjini hapa.
Mbowe alisema wameanza mkakati wa kuhakikisha chama kinawafikia wananchi kila mahali.Kiongozi huyo machachari amesema lengo kubwa ni kutaka kusikiliza matatizo ya wananchi na hata kule ambako kuna shida ya usafiri basi kwa pikipiki chama kitafika.
Mbowe alisema upatikanaji wa pikipiki hizo unatokana na Ruzuku ya chama pamoja na ufadhili kutoka kwa wanachama na marafiki wa chama chake walioko nje ya nchi.Huku mikakati yote hii ikiwa inasimamiwa na yeye mwenyewe chini ya uratibu wa Katibu mkuu wa chama hicho Dr Wilbroad Slaa.
Source:Mwananchi Jumatatu
safi sana, ila nilitaka kujua operation sangara imeishia wapi? make tuliambiwa kipindi fulani ilisimamishwa kupisha ile tume ya wakina Nchimbi, na baada ya hapo ingeendelea lakini hadi leo kimya, vipi kulikoni?
Wazo jema!!!
Nashauri mgawanyo ulenge Jographia ya Maeneo husika. Kuna Tarafa nyingine ni kubwa sawa na Wilaya kiasi kwamba pikipiki moja nisawa na hakuna kwani itakuwa vigumu kuwafikia walengwa. Kata zingine Pia tuongoze nguvu hiyo katika MAENEO MKAKATI ambayo twaweza kumiliki majimbo yote yawe ni ngome za kuiteka nchi nzima.
Mfano; Jimbo/Kanda la Magharibi - Mwanza na Shinyanga.
Jimbo/Kanda la Nyanda za Juu Kusini - Mbeya.
Jimbo/Kanda la Kaskazini - Arusha na Kilimanjaro.
Jimbo/Kanda la Pwani/Mashariki - Dar es Salaam.
Jimbo/Kanda la Kati - Singida.
Jimbo/Kanda la Magharibi - Kigoma.
Jimbo/Kanda la Kusini - Mtwara.
Kwa Pemba na Ungija - Waungwana ongezeni.
Ngazi ya jimbo kuwe na Kurugenzi zenye kusimamia shughuli zote za chama ktk Chaguzi na Uenezaji wa Chama.
Nawasilisha!
VIVA CHADEMA. Tunazisubiri na huku Iramba mashariki hasa maeneo ya Kirumi, Mkalama, Nkinto, Mwangeza, etc.
Mkuu wangu Papa D
Onyesha kidogo walau hekima yako kwenye mijadala ya msingi.Usipende sana kuonyesha upeo wako utakaosababisha kudharauliwa na mtoto wa chekechea.
Vyovyote uonavyo mkuu wangu.
Mimi nilijua hizo pikipiki ni kwa ajili ya kuwasaidia wakina mama wajawazito na wagonjwa maeneo husika, kumbe kwa ajili ya viongozi wa chadema kufika huko na kuwapa watu elimu ya uraia,lengo likiwa ni kuikataa CCM na kuchagua Chadema 2015.Helicopter vipi haziwezi kufika huko.Kweli ndugu zangu mpo katika Strategic Dialema ya hali ya juu.Mzee Sabodo umri umekwenda sana yule,Shauri zenu.Tumieni rasilimali kidogo mlizonazo kwa kutatua kero za wananchi lazima watawachagua tu,lakini siyo kwa namna hii ya kuzunguka kama Kikwete(Vasco da Gama)