CHADEMA yapongezwa kwa kujenga msikiti

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Taasisi ya Amani ya Kiislam (IFP) imekipongeza chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kwa kujenga msikiti katika kijiji cha Nshara mkoani Kilimanjaro, msikiti ambao umejengwa kutokana na michango ya wabunge wa chama hicho.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo Sheikh Sadik Godigodi amesema kitendo kilichofanywa na chama hicho kinafaa kuungwa mkono vyama na watu wengine kwani wameisaidia jamii. Sheikh Godigodi amesema wabunge wa chama hicho walichanga zaidi ya shilingi milioni 30 kiwango ambacho ni zaidi ya sh milioni 16 zilizokuwa zikihitajika.

Pia Sheikh Godigodi aliitaka serikali kutokupuuza maoni yaliyowasilishwa Ikulu na Chadema kuhusiana na mchakato wa katiba mpya kwani Chadema ni chama kikuu cha upinzani nchini na kinachopendwa na watanzania wengi.

SOURCE: MTANZANIA uk. 5
 
CHADEMA ni chama cha watanzania wote-wakristo, waislam, wapagani, wahindu nk!! nami nawapongeza pia!!
 
Taasisi ya Amani ya Kiislam (IFP) imekipongeza chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kwa kujenga msikiti katika kijiji cha Nshara mkoani Kilimanjaro,msikiti ambao umejengwa kutokana na michango ya wabunge wa chama hicho.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo Sheikh Sadik Godigodi amesema kitendo kilichofanywa na chama hicho kinafaa kuungwa mkono vyama na watu wengine kwani wameisaidia jamii.Sheikh Godigodi amesema wabunge wa chama hicho walichanga zaidi ya shilingi milioni 30 kiwango ambacho ni zaidi ya sh milioni 16 zilizokuwa zikihitajika.
Pia Sheikh Godigodi aliitaka serikali kutokupuuza maoni yaliyowasilishwa ikulu na Chadema kuhusiana na mchakato wa katiba mpya kwani Chadema ni chama kikuu cha upinzani nchini na kinachopendwa na watanzania wengi.

SOURCE: MTANZANIA uk. 5

Hawa jamaa wanaongoza kwa taasisi Tanzania.
 
hahahahha. posho za wabunge hizo.ok any way Chadema kama kweli huo si unafiki watueleze kwanini wanaungana na makanisa kupinga OIC na mahakama ya kadhi? huku makanisa yakinufaika na vertican?

Si vibaya kumuombea mtu mabaya,ila mara mia ungekufa wewe abaki mchawi wa JK Sheik yahya
 
Q2:14. Na wanapo kutana na walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao na mashet'ani wao husema: Hakika sisi tu pamoja nanyi. Hakika sisi tunawadhihaki tu.

wewe siku zote una roho ya kiuaji tu. hufikirii amani hata kidogo. unataka kuleta ubo haramu hapa bongo?
 
hahahahha. posho za wabunge hizo.ok any way Chadema kama kweli huo si unafiki watueleze kwanini wanaungana na makanisa kupinga OIC na mahakama ya kadhi? huku makanisa yakinufaika na vertican?

Ni vibaya kumuombea mtu mabaya,ila mara mia ungekufa wewe abaki mchawi wa JK Sheik yahya
 
Q2:14. Na wanapo kutana na walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao na mashet'ani wao husema: Hakika sisi tu pamoja nanyi. Hakika sisi tunawadhihaki tu.

Maneno ya Biblia na Quran yaweza kutumika vizuri au vibaya, itategemeana na Muhusika anataka nini? kwa mfano aya/mstari huu kuuleta hapa nia yako ilikuwa ni kukidhi haja yako ambayo ni kuonyesha kupinga kila linalofanywa na CHADEMA hata kama viongozi wako wa dini wamegundua ni zuri
 
taasisi ya amani ya kiislam (ifp) imekipongeza chama cha demokrasia na maendeleo-chadema kwa kujenga msikiti katika kijiji cha nshara mkoani kilimanjaro,msikiti ambao umejengwa kutokana na michango ya wabunge wa chama hicho.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo sheikh sadik godigodi amesema kitendo kilichofanywa na chama hicho kinafaa kuungwa mkono vyama na watu wengine kwani wameisaidia jamii.sheikh godigodi amesema wabunge wa chama hicho walichanga zaidi ya shilingi milioni 30 kiwango ambacho ni zaidi ya sh milioni 16 zilizokuwa zikihitajika.
Pia sheikh godigodi aliitaka serikali kutokupuuza maoni yaliyowasilishwa ikulu na chadema kuhusiana na mchakato wa katiba mpya kwani chadema ni chama kikuu cha upinzani nchini na kinachopendwa na watanzania wengi.

Source: Mtanzania uk. 5

waislamu hawahitaji msikiti wanazo za kuwatosha! Wanachohitaji waislamu ni mikakati ya kuwanasua na umaskini, shule, hospitali, ajira, ubaguzi wa kidini, mfumo kristo tz, nk. Hivyo chadema wasijidanganye kwa kuwajengea waislamu vijisikiti ili wapate sapoti ya waislamu ktk uchaguzi wa 2015!!

Wakati wa kudanganywa na vijikofia, kanga, fedha nk. Umepitwa na wakati na waislamu wako macho na hila za vyama vya siasa bali waislamu wa tz wanajipanga imara kwa kuchagua chama madhubuti kitakacho kuja na sera safi mbele ya waislamu na ndipo waislamu watakapo ingia mkataba na hicho chama ikiwa wanataka kura ya waislamu basi wawe tayari kukubali masharti yao!!!

Kinyume chake waislamu watapokea kanga, vikofia au fedha zenu lakini kura ng,oo
 
mtanzania huandika umbea. Yale ya msingi ya waislam huyaficha. Swali kwa chadema. Kwanini wanaungana na makanisa bungeni kupinga oic?

Jana umeliponda Nipashe,Tz Daima na leo Mtanzania la Fisadi mwenzenu haya basi waambie Al nuur na lle gazeti waandike mazuri uyatakayo
 
waislamu hawahitaji msikiti wanazo za kuwatosha! Wanachohitaji waislamu ni mikakati ya kuwanasua na umaskini, shule, hospitali, ajira, ubaguzi wa kidini, mfumo kristo tz, nk. Hivyo chadema wasijidanganye kwa kuwajengea waislamu vijisikiti ili wapate sapoti ya waislamu ktk uchaguzi wa 2015!!

Wakati wa kudanganywa na vijikofia, kanga, fedha nk. Umepitwa na wakati na waislamu wako macho na hila za vyama vya siasa bali waislamu wa tz wanajipanga imara kwa kuchagua chama madhubuti kitakacho kuja na sera safi mbele ya waislamu na ndipo waislamu watakapo ingia mkataba na hicho chama ikiwa wanataka kura ya waislamu basi wawe tayari kukubali masharti yao!!!

Kinyume chake waislamu watapokea kanga, vikofia au fedha zenu lakini kura ng,oo

"Umesema CDM wasijidanganye kuwajengea Waislam Misikiti ili wapigiwe kura 2015" Swali langu kwako wewe MDINI je hivi unajua Waislamu ni % ngapi ya waTz 45 million? Acha kuropoka na kung'ang'ana na Udini utawafikisha pabaya sana
 
kweli ubinadamu kazi, ukimsapoti atakwambia unajipendekeza, ukimuacha asimame mwenyewe atakuita mbaguzi aaaaaaaarghhhhhhhhhhhhh!!!!1

halafu wengine wanajidai hawajaridhika utafikiri wao ndo wanaswali kwenye huo msikiti...
utafikiri walitoka kwenda kuwapiga tafu wenzao kujenga msikiti.............................
utafikiri walipeleka mifuuko ya saruji kuchangia ujenzi..................

wakazi wa nshara walijua wanahitaji nini, wakaomba wenye mapenzi mema wawachangie, wakachanga nyie huku mnapondaponda mnajua shida ya kuswali walokuwa wakiipata? mnajua walikuwa wakiswali kwenye mazingira gani? mbona hamkujitokeza kuwachangia hata nondo moja?
 
Taasisi ya Amani ya Kiislam (IFP) imekipongeza chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kwa kujenga msikiti katika kijiji cha Nshara mkoani Kilimanjaro,msikiti ambao umejengwa kutokana na michango ya wabunge wa chama hicho.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo Sheikh Sadik Godigodi amesema kitendo kilichofanywa na chama hicho kinafaa kuungwa mkono vyama na watu wengine kwani wameisaidia jamii.Sheikh Godigodi amesema wabunge wa chama hicho walichanga zaidi ya shilingi milioni 30 kiwango ambacho ni zaidi ya sh milioni 16 zilizokuwa zikihitajika.
Pia Sheikh Godigodi aliitaka serikali kutokupuuza maoni yaliyowasilishwa ikulu na Chadema kuhusiana na mchakato wa katiba mpya kwani Chadema ni chama kikuu cha upinzani nchini na kinachopendwa na watanzania wengi.

SOURCE: MTANZANIA uk. 5
Nafikiri hapo nilipo RED ndio ilikuwa mzizi wa makala yake na kutaka kutupa ujumbe hadhwira.

Masjid Al Chadema.

 
"umesema cdm wasijidanganye kuwajengea waislam misikiti ili wapigiwe kura 2015" swali langu kwako wewe mdini je hivi unajua waislamu ni % ngapi ya watz 45 million? Acha kuropoka na kung'ang'ana na udini utawafikisha pabaya sana

hivi mdini ndio nini? Na hiyo dini ni ipi?
 
Nimeamini kweli kuwa usijieleze kwa yeyote kwa kuwa anayekupenda hahitaji kujeleza kwako, na asiyekupenda hata kama ukijieleza namna gani hatakuamini kamwe
 
"Umesema CDM wasijidanganye kuwajengea Waislam Misikiti ili wapigiwe kura 2015" Swali langu kwako wewe MDINI je hivi unajua Waislamu ni % ngapi ya waTz 45 million? Acha kuropoka na kung'ang'ana na Udini utawafikisha pabaya sana

Kwa takwimu zisizo rasmi. Katika Tanganyika inakadiriwa waislam na wakristo ni 50% each. Na ukisema kwa Tanzania waislam wanafika 54% na wakristo ni 46%.

Kumbuka unaposema wakristo kuna wakatoliki na wengine (protestant) ambao ni 58%.

Hizo ni takwimu zisizo sahihi kwa sababu TZ bado haijawa na takwimu rasmi za watu since hakuna sensa iliyofanyika miaka 5 iliyopita.

 
Q2:14. Na wanapo kutana na walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao na mashet'ani wao husema: Hakika sisi tu pamoja nanyi. Hakika sisi tunawadhihaki tu.

Swadaka Allahu L'adhim.

Hakika umeweka kitu mujarabu kabisa. Na kwa kuwamaliza kabisa watu hao wana macho ila hawaoni, wanamasikio hawasikii, wana pua lakini hawanusi. Na siku zote hao ndio watakao pata adhabu kali sana.

Mola atuepushilie mbali na adhabu hizo na kuwa miongoni mwa wanafiki.

 
Maneno ya Biblia na Quran yaweza kutumika vizuri au vibaya, itategemeana na Muhusika anataka nini? kwa mfano aya/mstari huu kuuleta hapa nia yako ilikuwa ni kukidhi haja yako ambayo ni kuonyesha kupinga kila linalofanywa na CHADEMA hata kama viongozi wako wa dini wamegundua ni zuri

NI SAHIHI KABISA.

Kwanza kosa lake ni kukihusianisha CDM na ukristo, kitu ambacho si kweli na havina uhusiana.

Pili mwisilamu aliyefundishwa vizuri, ameamriwa kuwaheshimu na kuishi vizuri na wakristo na wayahudi, kwa kuwa quruan inawataja kuwa ni wa kwanza kupewa vitabu vya Mungu, uislamu ulifuata baadae.(SIKUMBUKI NI QURUAN NGAPI) ila najua mtatujuza

Sasa huku kupingana waisalamu wanakutoa wapi enye FF NA MS boko haramu wa Tanzania?
 
Back
Top Bottom