CHADEMA yalipuliwa

Rostam Azizi amemwambia kuwa asipowachafua cdm ataanza kumdai fedha zake alizompa../ndio kisa cha kuhaha huko!
Amesahau kuwa kule Mara walimpopoa mawe hadi akableed na kauli zake hizohizo hatarishi!
 
...............Nadhani anapaswa kuhurumiwa huyu mzee,huwa sijui anafanya kazi gani pale mahakamani...muacheni anazeeka vibaya..pole Mtikila..
 
Atofautishe UFISADI wa RA, EL na utajiri wa Freeman Mbowe ambaye alirithi kwa baba yake mzee Aikaeli Mbowe . Ndesamburo ni mfanya biashara ambaye ame struggle mda mrefu sana na ndio maana ana ujasiri wa kuonyesha vitega uchumi vyake waziwazi. Hoteli za keys zinajulikana siku nyingi na siyo hela ya serikali aliiba. freeman na Ndesamburo hawajawahi kuwa waajiriwa wa Serikali wala taasisi zake ni watu wlioibuka kwa kujishughulisha . RA na EL wao wameibuka kwa kupitia nafasi zao na uhusiano wao wa karibu na viongozi wa serikali hasa kwa kupewa tenda zenye inflated prices ambazo zimewapatia mamilioni ya fedha haramu za watanzania. wameinyonya nchi na wananchi na kuipunguzia nchi kipato na hivyo kuongeza umaskini wa mtanzania wa kijijini.Hawa ndio MAFISADI wenye sifa zoote za kifisadi
 
Mkuu nadhani kukikosoa chama ni swala tofauti na kukejeri maamuzi ya chama. Sasa kwa mfano unapotoa hukumu ya kwamba Mbowe ni dikteta tayari umeshatoa hukumu ambayo sidhani hilo neno linatoa mwanya mzuri wa kujadili. Halafu nadhani tatizo mnalo nyie zaidi kwa sababu mnayapata majibu hapa hapa bila kuwasubiri wazee wa chama kama inavyotokea kwa CCM maanake hakuna kiongozi wala mwanaCCM JF mwenye habari za uhakika.

Haya unataka kuona CV ya Mbowe na viongozi wa CDM kwa nini? je hujui kwamba CV ya mtu haimfanyi kuwa kiongozi bora? Uongozi wa nchi hauna CV yaani hawatengenezwi bali kiongozi bora huzaliwa. Haya yalimkuta Prime minister wa Canada Paul Martin ambaye alikuwa waziri mzuri sana wa fedha, CV kubwa na pengine Canada haijawahi kupata mtendaji kazi kama yeye lakini siku alochukua Uongozi alichemsha, hivyo hivyo Gordon Brown wa UK kashindwa pamoja na kuwa na CV kubwa.

Mimi naweza kusema Mbowe is a better Politician (Leader) kuliko viongozi wengi sana na hakika CDM imeweza kufikia mafanikio haya ilokuwa nayo kwa sababu kasimama yeye. Tungeweza tu kumhukumu vibaya kama CDM ingeshuka daraja na binafsi nina kashalka makubwa kama CDM ingekuwa hapa ikiwa Zitto angechukua Uenyekiti...Kisha zaidi ya hapo kwa kitendo cha Mbowe kumwachia Dr.Slaa agombee Urais mwaka 2010 sijui kuna mwanasiasa gani Tanzania ktk nafasi ya Mbowe angekuwali kuachia hilo..Na zaidi ya yote kuna fahari gani kubwa kuwa mwenyekiti wa chama badala ya kuwa rais wa nchi..

Yes Mbowe anaweza kuwa na matatizo na pengine hata mimi kuna maswala hua tunapingana lakini mara zote hufikia maelewano tofauti kabisa na jinsi watu wanavyomzungumza hapa. Na nimeshawahi kukutana na watu tofauti lakini maturity ya Mbowe ktk siasa hakika imenishangaza hata mimi ambaye tumekuwa sote ktk ujana (ingawa mimi mkubwa kwake) na kama ujuavyo sii rahisi mtu kumpitisha mtu kisiasa ambaye mmekuwa pamoja na unayajua madudu ya ujana wenu.

Lakini nakwambia tu kwamba CDM inamhitaji mtu kama Mbowe kulingana na siasa za Tanzania na hakika kama ni dikteta basi huo Udikteta wake ndio unatakiwa ktk mazingira yetu maadam mafanikio yanapatikana hilo ndio muhimu zaidi..

Naomba nizungumzie sehemu nilizored:-
1. Hiyo umeiona ni hukumu? Ni mangapi yamesemwa na viongozi wa Chadema majukwaani juu ya ufisadi, kwa kuwataja watu kwa majina; sio hukumu ni ktazamo wangu kama ulivyo mtazamo wa hao wanaosimama majukwaani na kuwahukumu wengine kwa ufisadi.

2. Sipingani na wewe hata kwa chembe juu ya hili, ila najaribu kuonyesha ni kwa jinsi gani JF ilivyo bias kwa maswala yaihusuyo Chadema, kama hatukubali kukosolewa hatutajenga chama. Chadem, Chadema ni chama prospective kuchukua nchi, changamoto ni lazima ikutane nazo na ijue jinsi ya kuzitatua. Tumeona CV za wengi hapa na nilikuwa najaribu kukumbushia kuwa na zetu tuziweke hapa.

3. Mbowe ana akili kiasi, baada ya kugombea 2010 na kushindwa kwa kishindo alielewa, he is not popular na ndio maana anamwogopa hata Zitto hasa linapokuja swala la watu kupiga kura.

NB: JF tuwe watu wa hoja na tusiwe bias ili tuweze kujenga chama na tuifute dhana ya JF sio ya Chadema.
 
Mchungaji huyo hana kitu.

Hata mimi siko mbali na msemaji aliyesema anaganga njaa huko mahakama kuu.

Angalia chama chake kilivyo hakina chochote cha kujivunia.

Hata hivyo bora ameamua kwenda mahakamani ukweli utajulikana. Ufisadi unaolitesa taifa anaujua lkn anaamua kula kona ili kutupa sura potofu ya ufisadi, amenoa hapo.
 
kweli hawa wangekuwa mafisadi chama cha magamba kingewaacha??? Wazee wa Magamba walitafuta kila jinsi ili kuweza kubalance wakashindwa inabidi watosane. Utakuwa vipi fisadi wakati huna funguo za benki kuu wala kalamu ya kusaini mkataba?

Tumsubiri mahakamani. Kazi ya 2015 imeanza maagizo ya CCM-NEC na wazee wa chama hayo.
 
Naomba nizungumzie sehemu nilizored:-
1. Hiyo umeiona ni hukumu? Ni mangapi yamesemwa na viongozi wa Chadema majukwaani juu ya ufisadi, kwa kuwataja watu kwa majina; sio hukumu ni ktazamo wangu kama ulivyo mtazamo wa hao wanaosimama majukwaani na kuwahukumu wengine kwa ufisadi.

2. Sipingani na wewe hata kwa chembe juu ya hili, ila najaribu kuonyesha ni kwa jinsi gani JF ilivyo bias kwa maswala yaihusuyo Chadema, kama hatukubali kukosolewa hatutajenga chama. Chadem, Chadema ni chama prospective kuchukua nchi, changamoto ni lazima ikutane nazo na ijue jinsi ya kuzitatua. Tumeona CV za wengi hapa na nilikuwa najaribu kukumbushia kuwa na zetu tuziweke hapa.

3. Mbowe ana akili kiasi, baada ya kugombea 2010 na kushindwa kwa kishindo alielewa, he is not popular na ndio maana anamwogopa hata Zitto hasa linapokuja swala la watu kupiga kura.

NB: JF tuwe watu wa hoja na tusiwe bias ili tuweze kujenga chama na tuifute dhana ya JF sio ya Chadema.
Nami nitakujibu pia kwa kufuata mtiririko wako mwenyewe.
1. Mwanzo nimesema unatoa hukumu ktk maamuzi ya Chama kwa kejeri, hivi Chadema wanaposimama majukwaani huwa wanafanya hukumu au wanawaarifu wananchi Ufisadi unaofanyika na wana ushahidi.
2. CDM hawawezi hawakatai kukosolewa isipokuwa utunzi wa nyirabu hizi ndio tunaupiga vita. Mkutano wa Chadema wanapojadili kitu na wakapingana au kutokubaliana iweje ndio iwe ni makundi na ugonvi ndani ya chama. Mlitaka wajumbe wetu wakubali kila kitu kinachowakilishwa ndio ionekane hakuna matatizo?.. Je tunavyobishana hapa JF ina maana tuna makundi na hatupendani au ndio lengo la kuwepo mjadala...Hayo ya kuona CV ni mawazo finyu na yanafanywa na watu wanaofikiria kwamba kuongoza chama kunahitaji elimu ya juu na yenye utaalam fulani..wakati sii kweli.
3. Umesema Mbowe ana akili kiasi, na hicho kiasi ndicho kinachotakiwa hasa unapoona kwamba ushindi hauwezi kupatikana ngazi ya Urais kama utaingia wewe na sii kukazania madaraka. Mbowe hawezi kumhofia Zitto ikiwa Zitto bado hajafika Umri wa kugombea urais, hivyo kwa udogo huo unamwondoa na kumfanya dhaifu na immature kuwa mwenyekiti wa chama.
 
Atofautishe UFISADI wa RA, EL na utajiri wa Freeman Mbowe ambaye alirithi kwa baba yake mzee Aikaeli Mbowe . Ndesamburo ni mfanya biashara ambaye ame struggle mda mrefu sana na ndio maana ana ujasiri wa kuonyesha vitega uchumi vyake waziwazi. Hoteli za keys zinajulikana siku nyingi na siyo hela ya serikali aliiba. freeman na Ndesamburo hawajawahi kuwa waajiriwa wa Serikali wala taasisi zake ni watu wlioibuka kwa kujishughulisha . RA na EL wao wameibuka kwa kupitia nafasi zao na uhusiano wao wa karibu na viongozi wa serikali hasa kwa kupewa tenda zenye inflated prices ambazo zimewapatia mamilioni ya fedha haramu za watanzania. wameinyonya nchi na wananchi na kuipunguzia nchi kipato na hivyo kuongeza umaskini wa mtanzania wa kijijini.Hawa ndio MAFISADI wenye sifa zoote za kifisadi

Kumbukumbu zilizoko BOT; Freeman aliwahi kuwafanya kazi wakati baba mkwe wake akiwa Gavana
:israel:
 
Ahahaha!! leo ndio nimejua kumbe Pro-Chadema-JF wengi ni pumba, huyo Mtikila mmemsifia sana tena mmechukuwa maneno yake kama Reference kawambia Ridhiwan Kikwete Tajiri mkubwa tena mmechangia hiyo thread kwa kasi ya ajabu, saizi anawafahamisha ubaya wa Chadema mnakataa, Hongera Mtikila kwa kutujuza ukweli sisi wengine tulikuwa atujui

Hizi zote siasa tu ndugu zangu. Ilishasemwa siasa ni mchezo mchafu. Put that behind your mind when you try to evaluate politicians' statements. Tufocus kwenye mambo ya maana kama wana JF.
 
Nataka kumuamini Mtikila, uzoefu unaonyesha kuwa Mtikila hajawahi kushindwa kesi ya madai yeyote aliyofungua na daima tunajengewa dhana kuwa huyu ni mwehu tusimsikilize ila huwa anajua nini cha kufanya daima, kwangu mimi huyu ni mpinzani wa kweli Tanzania aliyekosa wafuasi wa kweli hana historia ya kuwa mwanachama wa TANU au CCM yeye na Marando, mpaka kesho ana ililia Tanganyika yetu na daima anapeperusha bendera ya Tanganyika.

Kwa ajili ya kupigania maslahi ya taifa hili ameshawahi kupewa kesi ya uhaini
 
Amesahau kuwa alitumiwa na ccm kutaka kuvuruga uchaguzi Tarime akaamburia kipigo?
Mla rushwa mkubwa ameishapewa tena fungu na ccm kuongea hovyo zidi ya cmd
 
SISI WENGINE TUSIO WAFUASI WA VYAMA VYA SIASA MNATUCHANGANYA SANA,,,JUENI KWAMBA MILUZI MINGI INAMPOTEZA MBWA.
CDM KWANINI MNAKUA HAMPENDI KUKOSOLEWA TENA MTU KAAMUA KWENDA MAHAKAMANI ILI HAKI IPATIKANE,MBICHI NA MBIVU ZIJULIKANE?
LIPI AFADHALI SASA MTU KUONGEA BLABLA TU MAJUKWAANI BILA EVIDENCE NA MNAMSHANGILIA NA YULE ANAYEKWENDA MAHAKAMANI?
SI KWELI KWAMBA VIONGOZI WOTE WA CDM NI MAKINI/WAADILIFU.:israel::israel:
 
ahahaha!! Leo ndio nimejua kumbe pro-chadema-jf wengi ni pumba, huyo mtikila mmemsifia sana tena mmechukuwa maneno yake kama reference kawambia ridhiwan kikwete tajiri mkubwa tena mmechangia hiyo thread kwa kasi ya ajabu, saizi anawafahamisha ubaya wa chadema mnakataa, hongera mtikila kwa kutujuza ukweli sisi wengine tulikuwa atujui

ukianza chekea kumbuka ipo siku utalia! Majuzi mtikila mzuri, leo mtikila anatumiwa na mafisadi
 
Back
Top Bottom