CHADEMA yalipuliwa

CHADEMA yalipuliwa

Mlengo wa Kati

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2011
Posts
2,730
Reaction score
492
Mwenyekiti wa Chama cha DP,Mchungaji Christopher Mtikila amesema CHADEMA hakipaswi kuaminiwa na Watanzania kwa kuwa ni chama chenye mafisadi na Wafanyabiashara haramu.

Pia amefananisha maneno yanayotolewa na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa kuwa ni sawa na yaliyokuwa yakitolewa na mmoja wa viongozi nchini Uganda.

Mtikila aliyasema hayo jana wakati akiongea na Wandishi wa habari Ukumbi wa Traventine, Mtikila aliongeza kuwa "ni unafiki kwa Viongozi wa CHADEMA kujifanya ni wapambanaji wa Ufisadi kwa kuwa chama chao chenyewe kimejaa ufisadi wa kutisha, ninakwenda kufungua kesi Mahakama Kuu dhidi ya kuwaonyesha ni jinsi gani walivyo hatari, kesi ninayo kwenda kufungua ina husiana na utata wa kifo cha Mwanasiasa Chacha Wange nina ushahidi juu ya baadhi ya viongozi wa juu wa Chadema kuhusika na mauaji hayo"alisema Mtikila.

Aidha alisema kesi hiyo itahusisha na baadhi ya Viongozi wa Chadema kujishughulisha na biashara haramu na jambo hilo ni Ufisadi. Kutokana na hali hiyo Mtikila aliwataka wananchi kutafakari kuhusu utajiri wa kupindukia wa Viongozi wawili wa chama hicho Philemon Ndesamburo na Freeman Mbowe.

Mtikila alihoji na kubeza hatua ya CCM kujivua gamba akisema CCM ina mafisadi wengi na sio hao watatu tu. Kama kweli CCM wanataka kupambana na Ufisadi wawatimuwe mafisadi wote ambao orodha yao ni ndefu!
 
Mtikila si anatumika na pia ana hongeka kirahisi.
Siyatilii maanani maneno ya mtu mla rushwa, alihongwa na Rostam, Watanzania bado hatujasahau.
 
Huyu Mtikila ni miongoni mwa wapuuzi wengi tuu kwenye nchi yangu, kwanza yeye hatupendi kabisa sisi waislamu na ni kinyonga, sijui hapa yeye kapewa pesa na nani mbona anawatetea wagalatia tuu kuwa ndio wasafi ndani ya CCM? KWANI aliwataja Sumaye, Warioba etc mbaona hakumtaja Salim, Mwinyi etc ni mshenzi tuu wa kupuuzwa huyu hapa kuna jambo anataka kutuaminisha ili tumuone naye ni msafi,

Arudishe fedha za Muislamu mwenzetu Rostam tukajenge madrasa kwa ajili ya Allah, kwanza ndipo asikilizwe.
 
Mtikila biashara yake ni hapo mahakama kuu. kama hana kesi basi hana cha kufanya.
 
Mtikila akikusumbua kwa maneno yake mbofumbofu we mwambie "Rostam huyo anakuja" atageuka na kusema "yupo wapi!" kisha we unapita kwa ulaini. Hana hamu na Rostam ndo breki yake.
 
NIMEISHI NA MTIKILA KARIBU MIAKA 5 PALE ILALA BREWERIES MAGHOROFANI,MTIKILA NI MTU HATARI HASA ANAPOKUWA NA NJAA,ANAWEZA FANYA LOLOTE AU KUSEMA LOLOTE HAOGOPI,NI MWANASIASA HATARI KWA SABABU SIASA ZAKE NI ZA KUPIGA,YAANI ANAWEZA LETE STORY FULANI ILI MWENYE NAYO AKISIKIE AMWITE AMKATIE MKWANJA,NI MBAMBAISHAJI MBAYA SANA:disapointed::disapointed:
 
jamani ningekuwa simfahamu mtikila ningekaa nakujiuliza sana, lakini ameshazoeleka huyo kwa kujitafutia umaarufu kupitia wenzake, ningemshauri aspend more time katika kujenga chama chake kwasasa,
MTIKILA BE SERIOUS!!!!!!
 
So, mkatieni chake anyamaze la sivyo tulieni siye tupate issues
 
Naomba kukumbushwa ni kwanini alipigwa mawe kule mara baada ya chacha wange kufari...
 
Anazeeka vibaya! Sasa hao wamemwibia nani? Hawakusanyi kodi!
 
yani mtikila sio hata wakujiuliza mara mbili, anapoteza muda mwingi katika mahakama na baadhi ya kesi ambazo hazina msingi wakati angekuwa anatumia nguvu hiyo katika kukijenga chama chake ambacho mpaka sasa kinapumuli mashine, kama vipi aachane na chama awe mwanasheria maana yeye bila kwenda kisutu haoni raha kabisa
 
Naomba kukumbushwa ni kwanini alipigwa mawe kule mara baada ya chacha wange kufari...


Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila (pichani), jana alishambuliwa kwa mawe wakati akihutubia mkutano wa hadhara. Mchungaji Mtikila alishambuliwa mjini Tarime alipokuwa akiwanadi wa gombea wa chama chake wa Udiwani na Ubunge. Habari zilizopatikana kutoka huko jana jioni zilisema kua, Mchungaji Mtikila alipatwa na mkasa huo wakati akizungumzia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime (CHADEMA), marehemu Chacha Wangwe kwamba kilisababishwa na watu fulani. Kwa mujibu wa habari hizo, Mchungaji Mtikila alipata maeraha kadhaa kichwani ambapo alipelekwa katika zahanati ya Tarime na kushonwa nyuzi tatu na Dk. Philemon Hugilo. Aidha, ilielezwa kwamba, Mchungaji Mtikila alilazimika kuvalishwa shuka nyeupe kutokana na nguo zake alizokuwa amevaa, kutapakaa damu. Habari zaidi zilisema watu wanne wametiwa mbaroni kuhusiana na tukio hilo.
SOURCE: Nipashe/Mzee Wa Mshit
 
CHADEMA bana mkiambiwa watu wa aina ya akina Mtikila hawafai kuungwa mkono kisiasa ni waropokaji tu mnakuwa wabishi. Oneni sasa hivi kuna tofauti gani kati ya kauli za mtikila na za yule jamaa mwingine wa kwenye chama chenu mgombea urais 2010.
 
CHADEMA bana mkiambiwa watu wa aina ya akina Mtikila hawafai kuungwa mkono kisiasa ni waropokaji tu mnakuwa wabishi. Oneni sasa hivi kuna tofauti gani kati ya kauli za mtikila na za yule jamaa mwingine wa kwenye chama chenu mgombea urais 2010.

Hawana tofauti kabisa afadhali Mtikila anaenda na mahakamani yule mwingine ni maneno maneno!
 
Ahahaha!! leo ndio nimejua kumbe Pro-Chadema-JF wengi ni pumba, huyo Mtikila mmemsifia sana tena mmechukuwa maneno yake kama Reference kawambia Ridhiwan Kikwete Tajiri mkubwa tena mmechangia hiyo thread kwa kasi ya ajabu, saizi anawafahamisha ubaya wa Chadema mnakataa, Hongera Mtikila kwa kutujuza ukweli sisi wengine tulikuwa atujui
 
Back
Top Bottom