CHADEMA yalaani ubaguzi wa CCM Zanzibar

CHADEMA yalaani ubaguzi wa CCM Zanzibar

Kweli kabisa mkuu... hiyo kauli ni mbaya sana kwakweli...binafsi imenistua sana.... wamelewa sifa na madaraka hawa ccm, washajigeuza Mungu ....wamesahau kuwa kinachowafanya wafanye dharau zote hizo ni upole wa wananchi... ila wakae wakijua kuwa hakuna marefu yasiyokuwa na ncha...wasiwalazimishe wanachi kufika mahali na kusema sasa basi inatosha
Yote ni kwa sababu wana dola na jeshi LA police kamwe halita wagusa.
 
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

CCM WAMEDHIHIRISHA FIKRA ZA KIKABURU

Katika hali isiyokuwa ya kawaida ambayo kwa namna yoyote haiwezi isingeachwa imee katika fikra za watu achilia mbali kuachiwa itembezwe hadharani, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia katika mojawapo ya mabango yaliyobebwa na wanachama wake kuiadhimisha Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, imedhihirisha kuwa inakumbatia fikra hatari za kikaburu.

Kupitia bango hilo ambalo kwa namna lilivyotengenezwa na lilivyobebwa ni vigumu kuamini kuwa liliibuka ghafla kama vile kitambaa cha mfukoni, mwanachama wa CCM akiwa amesindikizwa na wenzake, waliopita mlangoni mwa Uwanja wa Amani bila kuzuiliwa, kukemewa wala kubugudhiwa, ujumbe hatari wa kibaguzi umeandikwa 'MACHOTARA HIZBU ZANZIBAR NI NCHI YA WAAFRIKA'. Hizi ni fikra za kikaburu. Ni ishara ya mbegu za kibaguzi zilizokomaa na sasa zinachipua.

Kwa wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa nchini na kipekee katika muktadha huu, siasa za Zanzibar wataelewa kuwa kauli iliyotolewa katika bango hilo, si ya bahati mbaya. Ni matokeo ya siasa za chuki zinazopaliliwa, kusimamiwa, kuratibiwa na hata kunyamaziwa na uongozi wa juu kabisa wa CCM.

Tutatoa mfano. Moja ya maskani maarufu za masuala ya kisiasa Visiwani Zanzibar inayomilikiwa na CCM iitwayo Kisonge imekuwa na kawaida ya kuandika lugha hatari zinazoashiria ubaguzi ulio wazi kabisa ulio na maudhui sawa sawa na huu uliotolewa leo kwenye Sikukuu ya Mapinduzi.

Mojawapo ya kauli ambazo ziliandikwa katika ubao ulioko katika maskani hiyo hivi karibuni wakati wa joto la Uchaguzi Mkuu uliopita, iliandikwa hivi "Katiba ni ya Unguja na nyinyi Wapemba mwende mkatengeze yenu Pemba."

Lugha hiyo na nyingine za namna hiyo kama ilivyotokea leo, zimekuwa zikitolewa mbele ya viongozi wa CCM au wanaziona lakini kwa sababu wanazozijua wao, pengine zinawasaidia katika kufikia malengo ya siasa hatarishi zinazokiuka misingi yote ya demokrasia, zimekuwa zikifumbiwa macho na kuzidi kumea vichwani mwa wanachama wao na kuleta mpasuko wa ubaguzi wa itikadi za kisiasa, rangi, kanda, kabila na hata dini, si Zanzibar pekee bali nchi nzima.

Kilichotokea leo Zanzibar, ni mwendelezo usiokuwa wa bahati mbaya bali maelekezo ya kimkakati ya kueneza propaganda za chuki miongoni mwa Watanzania ambayo ndiyo imebakia kuwa silaha pekee ya kuibeba CCM ikiwa ni dalili ya wazi ya chama kilichofilisika sera, kuacha misingi yake, kuishiwa ushawishi wa hoja na kukosa uhalali wa kisiasa hivyo kujihalalisha kwa ubaguzi kama huo.

Ni mwendelezo wa kauli za viongozi wakuu wa chama hicho ambazo hutolewa hadharani kwenye majukwaa ya siasa, wakiwabagua wanachama, wapenzi, wafuasi wa vyama vingine kuwa ni wa dini fulani, kanda fulani au kabila fulani. Wakijua kabisa hakuna kikundi chochote cha kisiasa chenye sifa hizo kwa sababu ni kinyume cha sheria na misingi ya taifa letu.

Ni mwendelezo wa kauli iliyowahi kutolewa na viongozi wa chama hicho dhidi ya viongozi wenzao na wala viongozi wakuu wa CCM hawakuthubutu hata kukaripia, tena yakiwa maazimio rasmi ya kikao kwamba "Rais wa Tanzania hawezi kutoka Kaskazini".

Kauli hiyo iliyotolewa baada ya kikao ilikuwa kauli ya kikaburu sawa sawa kabisa na ile iliyotolewa leo huko Zanzibar.

Mwalimu Nyerere, Baba wa Taifa aliwahi kusema ukaburu si rangi, ni fikra.

CHADEMA tunalaani na kupinga kwa nguvu zote mipango, mikakati, tabia na chembechembe za ubaguzi wa aina yoyote, ukiwemo huu wa kisiasa ambao sasa unaanza kusakafiwa kwa ubaguzi wa rangi kwa sababu tunaamini wanaobeba agenda hii hawataishia hapo bali watazidi kutugawa Watanzania pia kwa ubaguzi wa ukanda, ukabila na udini kama ambavyo wamekuwa wakijaribu kuchochea.

CHADEMA kwa kusimamia misingi yake na kuzingatia kikamilifu misingi ya taifa letu hasa haki, uadilifu, utu, umoja na uzalendo, haiko tayari kuona taifa likifikishwa huko na kuhatarisha maisha ya jamii nzima ya Watanzania kwa sababu ya maslahi ya kikundi cha watu wachache.

Tunamkumbusha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Ernest Mangu kuwa kauli za namna hii ambazo zimekuwa zikipaliliwa na viongozi wa CCM na wengine wakitumia nafasi za kiserikali kuchochea ubaguzi ambao ni hatari kwa amani ya nchi na usalama wa raia na mali zao, ni ushahidi wa wazi kwa ajili ya hatua za kisheria badala ya jeshi hilo kujikita katika kubambikia wanachama, wafuasi na wapenzi wa vyama vya upinzani, hususan UKAWA tuhuma na kesi zisizokuwa msingi wowote kwa maslahi tu ya kisiasa kuisaidia CCM.

Wakati tukimtaka Rais John Magufuli kutimiza kwa vitendo kauli yake ya kwamba Serikali yake haitawabagua watu kwa misingi ya kisiasa (huku Waziri Mkuu wake akitoa maagizo kinyume kabisa na kauli hiyo) tunakitaka CCM, kupitia kwa Mwenyekiti wake, Jakaya Kikwete kama hakiko nyuma ya agenda hizo za kibaguzi na fikra hizo za kikaburu, kichukue hatua za haraka mara moja kuwawajibisha viongozi wake waliosimamia na kuachia jambo lililotokea leo huko Zanzibar.


Imetolewa leo Jumanne, Januari 12, 2016 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Habari
CHADEMA

Ila ALILOLIFANYA Lowassa Kwenda Kuomba KUUNGWA MKONO NA KANISA LA KILUTHERI Ni Jambo La Kheri Kwenu CHADEMA Na Mmelibariki? Na Mlivyo WAPUUZI Najua Hili Bango Litawafanya Sasa Muungane Na Muweze Kupata Coverage Ktk Media Zetu Kwani MLISHAPOTEA Ktk Ramani. Siasa Zenu CHADEMA Ni Za KITOTO Na Ndiyo Maana Sasa MNADHARAULIKA Na Hata WALIOKUWA WAKIWASAPOTI. Acheni Kudandia Treni Kwa Mbele Na Tumieni Muda Huu KUJIJENGA ZAIDI KISIASA ILI ANGALAU MWAKA 2020 ACT Wasije Wakawapiga Bao Kwani Naona Kabisa CHADEMA Kinakwenda Alijojo. Mnadai CCM Tuna UBAGUZI Nani Asiyejua Kuwa CHADEMA Kama Siyo Mwana Kaskazini Kilimanjaro na Arusha Kupata UONGOZI WA JUU KABISA Ni Ndoto? Kwenu Nyie CHADEMA Mnatafsiri Vipi Ubaguzi? Nikimalizia Kwa Huyu Huyu Tumaini Makene Ambae Leo ANAJIFANYA Kuisema CCM Kwa UBAGUZI Wakati Yeye Yeye Pia AMESAHAU WAKATI WA KAMPENI ALIVYOKUWA AKIVIBAGUA Baadhi Ya Vyombo Vya Habari Kwa KUDANGANYA Na CHUKI Zake BINAFSI Hali Iliyopelekea Hadi AKAJIJENGEA UADUI Mkubwa Mpaka Leo Na Wana Habari. Huyo Tumaini Makene Na CHADEMA Yake WAKAWADANGANYE Wengine Na Siyo Sisi TUNAOWAJUA KINDAKINDAKI. Jipangeni Kwa Mwaka 2035 Kwani Mwaka 2025 Akimaliza Tu Rais Dr. Magufuli Nchi Tunamkabidhi Waziri Mkuu FUNDI au MTAALAM au JEMBE Majaliwa Kassim Majaliwa. Na Kuna Tetetsi Mr. Naumwa Muhimbili Anataka Kurejea CCM Kwani Huko Kwenu Anaona MNAZINGUA Tu.
 
hao machotara hisbu si ndio walikua vibaraka wa usaltani wakitambulika kushiriki kuwabagua na kuwadhulumu waafrika. bila shaka bango lilikua linakumbusha tu waliofanyiwa waafrika. waafrika siku zote ni victim wa ubaguzi hata leo kwenye nchi huru za kiafrika mbari zingine hazikati tamaa kujaribu kuwabagua waafrika.
Zama za ubaguzi zilikuwepo na sio zanzibar tu wakoloni tabia zao zilikua zinafanana hata wajerumani navwaengereza walikua hivo hivo ila mambo haya yalipigwa vita dunia nzima na mabadiliko yamepatikana ila wewe akili yako inarudi kama hao wakoloni wazamani .mganda wako wa akili ni mkubwa sana
 
UOTE="Ghosryder, post: 15079798, member: 233784"]Aaagh! chadema kwenu tayari mmepata kiki!hivi huwa hamna mipango ya kimaendeleo zaidi.ya kukaa mkivizia vimambo vidogo na kuvikuuuuza! mnaboa bana! Hela za bosi wenu zilizokwenda nje hamjafuatilia![/QUOTE]
Mkuu ndo siasa, yaan hapo tayari chadema inarudi, of course hiyo agenda inalipa sana kwa ukawa kusimama hasa ukizingatia akili za watanzania za kushikiwa hizi
 
2000 - CUF ni chama cha Waislamu,

2005 - CHADEMA ni chama cha Wachagga,

2010 - CHADEMA ni chama cha Kaskazini (Arusha, Knjaro, Mara),

2015 - Rais wa Nchi hii hawezi kutoka Kaskazini,

2016 - Zanzibar sio nchi ya Mahizbu Wala Machotara...

Dhambi ya Ubaguzi ni sawa na kula nyama ya mtu. Shame on u CCM.!!
 
Ila ALILOLIFANYA Lowassa Kwenda Kuomba KUUNGWA MKONO NA KANISA LA KILUTHERI Ni Jambo La Kheri Kwenu CHADEMA Na Mmelibariki? Na Mlivyo WAPUUZI Najua Hili Bango Litawafanya Sasa Muungane Na Muweze Kupata Coverage Ktk Media Zetu Kwani MLISHAPOTEA Ktk Ramani. Siasa Zenu CHADEMA Ni Za KITOTO Na Ndiyo Maana Sasa MNADHARAULIKA Na Hata WALIOKUWA WAKIWASAPOTI. Acheni Kudandia Treni Kwa Mbele Na Tumieni Muda Huu KUJIJENGA ZAIDI KISIASA ILI ANGALAU MWAKA 2020 ACT Wasije Wakawapiga Bao Kwani Naona Kabisa CHADEMA Kinakwenda Alijojo. Mnadai CCM Tuna UBAGUZI Nani Asiyejua Kuwa CHADEMA Kama Siyo Mwana Kaskazini Kilimanjaro na Arusha Kupata UONGOZI WA JUU KABISA Ni Ndoto? Kwenu Nyie CHADEMA Mnatafsiri Vipi Ubaguzi? Nikimalizia Kwa Huyu Huyu Tumaini Makene Ambae Leo ANAJIFANYA Kuisema CCM Kwa UBAGUZI Wakati Yeye Yeye Pia AMESAHAU WAKATI WA KAMPENI ALIVYOKUWA AKIVIBAGUA Baadhi Ya Vyombo Vya Habari Kwa KUDANGANYA Na CHUKI Zake BINAFSI Hali Iliyopelekea Hadi AKAJIJENGEA UADUI Mkubwa Mpaka Leo Na Wana Habari. Huyo Tumaini Makene Na CHADEMA Yake WAKAWADANGANYE Wengine Na Siyo Sisi TUNAOWAJUA KINDAKINDAKI. Jipangeni Kwa Mwaka 2035 Kwani Mwaka 2025 Akimaliza Tu Rais Dr. Magufuli Nchi Tunamkabidhi Waziri Mkuu FUNDI au MTAALAM au JEMBE Majaliwa Kassim Majaliwa. Na Kuna Tetetsi Mr. Naumwa Muhimbili Anataka Kurejea CCM Kwani Huko Kwenu Anaona MNAZINGUA Tu.
Osiombe maradhi ya kukosa akili ni shidaa
 
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

CCM WAMEDHIHIRISHA FIKRA ZA KIKABURU

Katika hali isiyokuwa ya kawaida ambayo kwa namna yoyote haiwezi isingeachwa imee katika fikra za watu achilia mbali kuachiwa itembezwe hadharani, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia katika mojawapo ya mabango yaliyobebwa na wanachama wake kuiadhimisha Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, imedhihirisha kuwa inakumbatia fikra hatari za kikaburu.

Kupitia bango hilo ambalo kwa namna lilivyotengenezwa na lilivyobebwa ni vigumu kuamini kuwa liliibuka ghafla kama vile kitambaa cha mfukoni, mwanachama wa CCM akiwa amesindikizwa na wenzake, waliopita mlangoni mwa Uwanja wa Amani bila kuzuiliwa, kukemewa wala kubugudhiwa, ujumbe hatari wa kibaguzi umeandikwa 'MACHOTARA HIZBU ZANZIBAR NI NCHI YA WAAFRIKA'. Hizi ni fikra za kikaburu. Ni ishara ya mbegu za kibaguzi zilizokomaa na sasa zinachipua.

Kwa wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa nchini na kipekee katika muktadha huu, siasa za Zanzibar wataelewa kuwa kauli iliyotolewa katika bango hilo, si ya bahati mbaya. Ni matokeo ya siasa za chuki zinazopaliliwa, kusimamiwa, kuratibiwa na hata kunyamaziwa na uongozi wa juu kabisa wa CCM.

Tutatoa mfano. Moja ya maskani maarufu za masuala ya kisiasa Visiwani Zanzibar inayomilikiwa na CCM iitwayo Kisonge imekuwa na kawaida ya kuandika lugha hatari zinazoashiria ubaguzi ulio wazi kabisa ulio na maudhui sawa sawa na huu uliotolewa leo kwenye Sikukuu ya Mapinduzi.

Mojawapo ya kauli ambazo ziliandikwa katika ubao ulioko katika maskani hiyo hivi karibuni wakati wa joto la Uchaguzi Mkuu uliopita, iliandikwa hivi "Katiba ni ya Unguja na nyinyi Wapemba mwende mkatengeze yenu Pemba."

Lugha hiyo na nyingine za namna hiyo kama ilivyotokea leo, zimekuwa zikitolewa mbele ya viongozi wa CCM au wanaziona lakini kwa sababu wanazozijua wao, pengine zinawasaidia katika kufikia malengo ya siasa hatarishi zinazokiuka misingi yote ya demokrasia, zimekuwa zikifumbiwa macho na kuzidi kumea vichwani mwa wanachama wao na kuleta mpasuko wa ubaguzi wa itikadi za kisiasa, rangi, kanda, kabila na hata dini, si Zanzibar pekee bali nchi nzima.

Kilichotokea leo Zanzibar, ni mwendelezo usiokuwa wa bahati mbaya bali maelekezo ya kimkakati ya kueneza propaganda za chuki miongoni mwa Watanzania ambayo ndiyo imebakia kuwa silaha pekee ya kuibeba CCM ikiwa ni dalili ya wazi ya chama kilichofilisika sera, kuacha misingi yake, kuishiwa ushawishi wa hoja na kukosa uhalali wa kisiasa hivyo kujihalalisha kwa ubaguzi kama huo.

Ni mwendelezo wa kauli za viongozi wakuu wa chama hicho ambazo hutolewa hadharani kwenye majukwaa ya siasa, wakiwabagua wanachama, wapenzi, wafuasi wa vyama vingine kuwa ni wa dini fulani, kanda fulani au kabila fulani. Wakijua kabisa hakuna kikundi chochote cha kisiasa chenye sifa hizo kwa sababu ni kinyume cha sheria na misingi ya taifa letu.

Ni mwendelezo wa kauli iliyowahi kutolewa na viongozi wa chama hicho dhidi ya viongozi wenzao na wala viongozi wakuu wa CCM hawakuthubutu hata kukaripia, tena yakiwa maazimio rasmi ya kikao kwamba "Rais wa Tanzania hawezi kutoka Kaskazini".

Kauli hiyo iliyotolewa baada ya kikao ilikuwa kauli ya kikaburu sawa sawa kabisa na ile iliyotolewa leo huko Zanzibar.

Mwalimu Nyerere, Baba wa Taifa aliwahi kusema ukaburu si rangi, ni fikra.

CHADEMA tunalaani na kupinga kwa nguvu zote mipango, mikakati, tabia na chembechembe za ubaguzi wa aina yoyote, ukiwemo huu wa kisiasa ambao sasa unaanza kusakafiwa kwa ubaguzi wa rangi kwa sababu tunaamini wanaobeba agenda hii hawataishia hapo bali watazidi kutugawa Watanzania pia kwa ubaguzi wa ukanda, ukabila na udini kama ambavyo wamekuwa wakijaribu kuchochea.

CHADEMA kwa kusimamia misingi yake na kuzingatia kikamilifu misingi ya taifa letu hasa haki, uadilifu, utu, umoja na uzalendo, haiko tayari kuona taifa likifikishwa huko na kuhatarisha maisha ya jamii nzima ya Watanzania kwa sababu ya maslahi ya kikundi cha watu wachache.

Tunamkumbusha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Ernest Mangu kuwa kauli za namna hii ambazo zimekuwa zikipaliliwa na viongozi wa CCM na wengine wakitumia nafasi za kiserikali kuchochea ubaguzi ambao ni hatari kwa amani ya nchi na usalama wa raia na mali zao, ni ushahidi wa wazi kwa ajili ya hatua za kisheria badala ya jeshi hilo kujikita katika kubambikia wanachama, wafuasi na wapenzi wa vyama vya upinzani, hususan UKAWA tuhuma na kesi zisizokuwa msingi wowote kwa maslahi tu ya kisiasa kuisaidia CCM.

Wakati tukimtaka Rais John Magufuli kutimiza kwa vitendo kauli yake ya kwamba Serikali yake haitawabagua watu kwa misingi ya kisiasa (huku Waziri Mkuu wake akitoa maagizo kinyume kabisa na kauli hiyo) tunakitaka CCM, kupitia kwa Mwenyekiti wake, Jakaya Kikwete kama hakiko nyuma ya agenda hizo za kibaguzi na fikra hizo za kikaburu, kichukue hatua za haraka mara moja kuwawajibisha viongozi wake waliosimamia na kuachia jambo lililotokea leo huko Zanzibar.


Imetolewa leo Jumanne, Januari 12, 2016 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Habari
CHADEMA
MATAMKO NA MAANDAMANO. Ndo maana siasa inawashinda.
 
Weka ushahidi, nyumbu
Ushahidi ni taarifa ya CHADEMA kwa vyombo vya habari iliyowekwa humu jamvini. Mwenye asili na moyo wa ubaguzi ni yule anayeshikilia hilo jambo kindakindaki, kama taarifa hiyo inavyojielekeza. Ukweli bado CUF, hasa Seif, kuna harufu ya ubaguzi kurudisha Zanzibar kwenye Usultani. Hili likemewe mapema na Wazanzibari wamelitambua hili hadi kuliweka wazi hadharani. Lisifumbiwe macho, kumezewa au kukemewa ati ni ubaguzi.

TAMBUA CHAMBUA CHUNGUZA FANYA MAAMUZI CHUKUA HATUA
 
Ila ALILOLIFANYA Lowassa Kwenda Kuomba KUUNGWA MKONO NA KANISA LA KILUTHERI Ni Jambo La Kheri Kwenu CHADEMA Na Mmelibariki? Na Mlivyo WAPUUZI Najua Hili Bango Litawafanya Sasa Muungane Na Muweze Kupata Coverage Ktk Media Zetu Kwani MLISHAPOTEA Ktk Ramani. Siasa Zenu CHADEMA Ni Za KITOTO Na Ndiyo Maana Sasa MNADHARAULIKA Na Hata WALIOKUWA WAKIWASAPOTI. Acheni Kudandia Treni Kwa Mbele Na Tumieni Muda Huu KUJIJENGA ZAIDI KISIASA ILI ANGALAU MWAKA 2020 ACT Wasije Wakawapiga Bao Kwani Naona Kabisa CHADEMA Kinakwenda Alijojo. Mnadai CCM Tuna UBAGUZI Nani Asiyejua Kuwa CHADEMA Kama Siyo Mwana Kaskazini Kilimanjaro na Arusha Kupata UONGOZI WA JUU KABISA Ni Ndoto? Kwenu Nyie CHADEMA Mnatafsiri Vipi Ubaguzi? Nikimalizia Kwa Huyu Huyu Tumaini Makene Ambae Leo ANAJIFANYA Kuisema CCM Kwa UBAGUZI Wakati Yeye Yeye Pia AMESAHAU WAKATI WA KAMPENI ALIVYOKUWA AKIVIBAGUA Baadhi Ya Vyombo Vya Habari Kwa KUDANGANYA Na CHUKI Zake BINAFSI Hali Iliyopelekea Hadi AKAJIJENGEA UADUI Mkubwa Mpaka Leo Na Wana Habari. Huyo Tumaini Makene Na CHADEMA Yake WAKAWADANGANYE Wengine Na Siyo Sisi TUNAOWAJUA KINDAKINDAKI. Jipangeni Kwa Mwaka 2035 Kwani Mwaka 2025 Akimaliza Tu Rais Dr. Magufuli Nchi Tunamkabidhi Waziri Mkuu FUNDI au MTAALAM au JEMBE Majaliwa Kassim Majaliwa. Na Kuna Tetetsi Mr. Naumwa Muhimbili Anataka Kurejea CCM Kwani Huko Kwenu Anaona MNAZINGUA Tu.
Kwa Chedema, ukimwomba Mungu wa walutheri hakuna neno ha ha ha
 
Inamaana na huyu waziri wa magufuli abdalla posi mwisho chumbe?
 
Ccm wanataka kufanya hii nchi iwe ya kwao peke yao, leo mmeonyesha ni jinsi gani mlivyo wabaguzi, wakabila, na wadini halafu mko mstari wa mbele kusema Chadema ni wakabila, ujinga wenu wa kutofikiri umewaacha uchi leo
 
Mkuu hii dhambi itawatafuna hadi milele mpka hapa walipo fikia imagine unaweze kumbagua ndugu yako au mtoto wako Wa kumzaa na huku ikijitapa kwa majirani tunazidi kurahani
 
Dah after a long long silence at last chadema has got something to say in public #hapakazitu era is not a joke
 
Ila ALILOLIFANYA Lowassa Kwenda Kuomba KUUNGWA MKONO NA KANISA LA KILUTHERI Ni Jambo La Kheri Kwenu CHADEMA Na Mmelibariki? Na Mlivyo WAPUUZI Najua Hili Bango Litawafanya Sasa Muungane Na Muweze Kupata Coverage Ktk Media Zetu Kwani MLISHAPOTEA Ktk Ramani. Siasa Zenu CHADEMA Ni Za KITOTO Na Ndiyo Maana Sasa MNADHARAULIKA Na Hata WALIOKUWA WAKIWASAPOTI. Acheni Kudandia Treni Kwa Mbele Na Tumieni Muda Huu KUJIJENGA ZAIDI KISIASA ILI ANGALAU MWAKA 2020 ACT Wasije Wakawapiga Bao Kwani Naona Kabisa CHADEMA Kinakwenda Alijojo. Mnadai CCM Tuna UBAGUZI Nani Asiyejua Kuwa CHADEMA Kama Siyo Mwana Kaskazini Kilimanjaro na Arusha Kupata UONGOZI WA JUU KABISA Ni Ndoto? Kwenu Nyie CHADEMA Mnatafsiri Vipi Ubaguzi? Nikimalizia Kwa Huyu Huyu Tumaini Makene Ambae Leo ANAJIFANYA Kuisema CCM Kwa UBAGUZI Wakati Yeye Yeye Pia AMESAHAU WAKATI WA KAMPENI ALIVYOKUWA AKIVIBAGUA Baadhi Ya Vyombo Vya Habari Kwa KUDANGANYA Na CHUKI Zake BINAFSI Hali Iliyopelekea Hadi AKAJIJENGEA UADUI Mkubwa Mpaka Leo Na Wana Habari. Huyo Tumaini Makene Na CHADEMA Yake WAKAWADANGANYE Wengine Na Siyo Sisi TUNAOWAJUA KINDAKINDAKI. Jipangeni Kwa Mwaka 2035 Kwani Mwaka 2025 Akimaliza Tu Rais Dr. Magufuli Nchi Tunamkabidhi Waziri Mkuu FUNDI au MTAALAM au JEMBE Majaliwa Kassim Majaliwa. Na Kuna Tetetsi Mr. Naumwa Muhimbili Anataka Kurejea CCM Kwani Huko Kwenu Anaona MNAZINGUA Tu.
Isitoshe huyu ni mwanachama tu wa kawaida kaibuka huko na bango lake basi jamaa wameshupaa utafikiri ni msimamo wa chama. Isitoshe CCM wameonyesha uungwana na ukomavu wa hali ya juu kwa kulikana hilo bango mara moja. Pengine vyama sasa inabidi viwe vinakagua mabango yote ya wafuasi wao kabla ya maandamano ili ikitokea mtu aliyevaa nguo za chama akatokelezea na bango lenye ujumbe tatanishi basi ananyang'anywa. Yote haya ni matokeo ya chama kupoteza mwelekeo na kubakiza kudandia dandia matukio ambayo hayana kichwa wala miguu. Baada ya ile ajenda ya ufisadi iliyowapa umaarufu mkubwa kuota mbawa sasa chama kipo kipo tu kinaenda kama boya katika bahari kuu iliyochafuka.

Makene mkimya kweli na wakati wa uchaguzi watu walipiga makelele kuhusu kitengo cha habari cha CHADEMA leo eti ndo anakurupuka kutoa msimamo wa chama katika jambo ambalo kimsingi halina uzito wo wote hasa ukizingatia kuwa ni bango la mwanachama wa kawaida tu katika maandamano. Maajabu ya karne aisee
 
Back
Top Bottom