CHADEMA yaitupa kapuni Rufaa ya Zitto

CHADEMA yaitupa kapuni Rufaa ya Zitto

Wingi wa wafanyakazi ktk gazeti la Nipashe kutoka Kilimanjao haumtendei haki ZITTO,hata siku moja hautakuta kurasa za mbele habari mzuri ya ZITTO.Ukabila na Ukanda mbaya sana.
 
Chadema Chama Makini Kuwahi tokea Afrka Mashariki.

Hamna umakini hapo mnadanganyana tu,Ningeona Chadema wako makini kama wangeachana viongozi wabovu wote wanaokwamisha ukuaji wa Chama akiwemo Mbowe mwenyewe pamoja na Zitto,Wengineo ni pamoja na akina Lema.Chadema kingeundwa na uongozi mpya wenye nia ya dhati kukipeleka Chama madarakani 2015.Chadema chini ya Mbowe ikulu 2015 tutaisikia kwenye radio huku tukitoa fursa kwa chama cha mafisadi kurejea Ikulu na ndicho hasa anachokitaka huyu bwana kwasababu kwake hiyo itakuwa fursa nzuri sana ya kutengeneza fedha kutoka kwa Mfalme wa Monduli.WanaChadema mnamwiita Zitto msaliti?Subirini 2015 ifike ndio mtamjua msaliti ni nani!!??Na mpaka mtakapokuja kushtuka mtakuwa mmechelewa sana maana jamaa atakimbilia Dubai kujipoza na Uenyekiti wa Chama hatautaka tena maana alichokitaka atakuwa ameshakipata.Hii ndio sababu Mheshimiwa ameapa kutokiachia kiti maana anajua kuna biashara nzuri 2015 inakuja na yeye si unajua tena ni Mfanyabiashara?
 
Suala la Uanachama na Uongozi vilikuwa ni separate issues. Kila kimoja kilipaswa kijadiliwe kwa muktadha wake!.
Mpaka hivi sasa Zitto Kabwe ni mwanachama halali wa Chadema
Anakata rufaa kwa sababu ya Kuvuliwa uongozi wake, Then Mwingine aakuja anasema No No No, Subiri kwanza tuone kama utavuliwa uanachama au La!!- SIJAWAHI KUONA CHAMA AMBACHO KILA MTU ANAJITAFSIRIA KATIBA APENDAVYO!
Sijui Kimesera ametumia kifungu gani cha sheria/katiba ya Chama kuzuia Mchakato huru wa Rufaa

Tewteh! Alafu mjibu hoja ndiye aliye kaimu hiyo Post, sasa wewe ulitaka akose kitumbua/Ulaji huo.
 
Suala la Uanachama na Uongozi vilikuwa ni separate issues. Kila kimoja kilipaswa kijadiliwe kwa muktadha wake!.
Mpaka hivi sasa Zitto Kabwe ni mwanachama halali wa Chadema
Anakata rufaa kwa sababu ya Kuvuliwa uongozi wake, Then Mwingine aakuja anasema No No No, Subiri kwanza tuone kama utavuliwa uanachama au La!!- SIJAWAHI KUONA CHAMA AMBACHO KILA MTU ANAJITAFSIRIA KATIBA APENDAVYO!
Sijui Kimesera ametumia kifungu gani cha sheria/katiba ya Chama kuzuia Mchakato huru wa Rufaa
Anakata rufaa ya kung'ang'ania cheo cha kuteuliwa? stupidity.

Anatakiwa kusubiri hatma yake ya uanachama ndipo ajue kama kuna haja ya kukata rufaa ya vyeo vyake ama la.

Maana ya kauli ya Kimesera ni kwamba akivuliwa uanachama na rufaa yake inakufa kifo cha mende.
 
Hamna umakini hapo mnadanganyana tu,Ningeona Chadema wako makini kama wangeachana viongozi wabovu wote wanaokwamisha ukuaji wa Chama akiwemo Mbowe mwenyewe pamoja na Zitto,Wengineo ni pamoja na akina Lema.Chadema kingeundwa na uongozi mpya wenye nia ya dhati kukipeleka Chama madarakani 2015.Chadema chini ya Mbowe ikulu 2015 tutaisikia kwenye radio huku tukitoa fursa kwa chama cha mafisadi kurejea Ikulu na ndicho hasa anachokitaka huyu bwana kwasababu kwake hiyo itakuwa fursa nzuri sana ya kutengeneza fedha kutoka kwa Mfalme wa Monduli.WanaChadema mnamwiita Zitto msaliti?Subirini 2015 ifike ndio mtamjua msaliti ni nani!!??Na mpaka mtakapokuja kushtuka mtakuwa mmechelewa sana maana jamaa atakimbilia Dubai kujipoza na Uenyekiti wa Chama hatautaka tena maana alichokitaka atakuwa ameshakipata.Hii ndio sababu Mheshimiwa ameapa kutokiachia kiti maana anajua kuna biashara nzuri 2015 inakuja na yeye si unajua tena ni Mfanyabiashara?

Ndio maana nilisema wengi wunu mnataka Uongozi mpya and hope na wanachama wapya pia maana hawa wachadema wa sasa washakomaa na viroba, hawawafai nyinyi.

Ushahuri aznisheni chama chenu Kipya, wanachama wapya pia, Hakika Mtafanikiwa.
 
Ila ninachofurahia sarakasi hizi kutoka ndani ya chadema ni kwamba, Inawafungua macho watu kuona kwamba Zitto Kabwe hatakiwi na Wakubwa wa Chama, na kwamba Zitto Kabwe ni hatari kwa maslahi binafsi ya Viongozi hawa, na si hatari kwa maslahi ya Chama.
Wameamua kumuundia Zengwe, wakalisukuma Zengwe bila kufuata utaratibu halali wa kanuni za adhabu kwa viongozi, kisha wanaibaka katiba ili Rufaa yake isisikilizwe.
Hii maana yake nini?-ZIITO KABWE LAZIMA AONDOKE BY ANY MEANS NECESSARY, KIHALALI, KIHARAMU AU BOTH, THESE GUYS DON'T CARE. THEY ONLY CARE ABOUT THEMSELVES NOT EVEN THE PARTY!
 
Wingi wa wafanyakazi ktk gazeti la Nipashe kutoka Kilimanjao haumtendei haki ZITTO,hata siku moja hautakuta kurasa za mbele habari mzuri ya ZITTO.Ukabila na Ukanda mbaya sana.
Kama unataka habari nzuri za Zitto uwe unasoma magazeti ya Jamba Leo, UMMA, Habari Leo, Majira na Al-nuur
 
Hamna umakini hapo mnadanganyana tu,Ningeona Chadema wako makini kama wangeachana viongozi wabovu wote wanaokwamisha ukuaji wa Chama akiwemo Mbowe mwenyewe pamoja na Zitto,Wengineo ni pamoja na akina Lema.Chadema kingeundwa na uongozi mpya wenye nia ya dhati kukipeleka Chama madarakani 2015.Chadema chini ya Mbowe ikulu 2015 tutaisikia kwenye radio huku tukitoa fursa kwa chama cha mafisadi kurejea Ikulu na ndicho hasa anachokitaka huyu bwana kwasababu kwake hiyo itakuwa fursa nzuri sana ya kutengeneza fedha kutoka kwa Mfalme wa Monduli.WanaChadema mnamwiita Zitto msaliti?Subirini 2015 ifike ndio mtamjua msaliti ni nani!!??Na mpaka mtakapokuja kushtuka mtakuwa mmechelewa sana maana jamaa atakimbilia Dubai kujipoza na Uenyekiti wa Chama hatautaka tena maana alichokitaka atakuwa ameshakipata.Hii ndio sababu Mheshimiwa ameapa kutokiachia kiti maana anajua kuna biashara nzuri 2015 inakuja na yeye si unajua tena ni Mfanyabiashara?

hakutoshi kuushawishi umma wa tanzania
 
Maanake uamuzi wa kumfukuza ushatolewa fatwa na wahafidhina lazima wamvue uanachama ndio maana jamaa wanambwela.
 
Ila ninachofurahia sarakasi hizi kutoka ndani ya chadema ni kwamba, Inawafungua macho watu kuona kwamba Zitto Kabwe hatakiwi na Wakubwa wa Chama, na kwamba Zitto Kabwe ni hatari kwa maslahi binafsi ya Viongozi hawa, na si hatari kwa maslahi ya Chama.
Wameamua kumuundia Zengwe, wakalisukuma Zengwe bila kufuata utaratibu halali wa kanuni za adhabu kwa viongozi, kisha wanaibaka katiba ili Rufaa yake isisikilizwe.
Hii maana yake nini?-ZIITO KABWE LAZIMA AONDOKE BY ANY MEANS NECESSARY, KIHALALI, KIHARAMU AU BOTH, THESE GUYS DON'T CARE. THEY ONLY CARE ABOUT THEMSELVES NOT EVEN THE PARTY!
Ninachojua Zitto must go na baadae atakimbilia mahakamani mwisho atakuwa mbunge wa mahakama hiyo itakuwa faraja kwa chama.
 
Maombi ya rufaa ya ZITTO KABWE hayatajadiliwa hadi hatima ya uanachama wake kujulikana.

Source: NIPASHE.
Sijaelewa mantiki ya msimamo huu. Sasa kama akishinda hiyo rufaa, si hata suala la yeye kutetea uanachama wake linakosa uhalali wa kuendelea? Kwa nini wanataka wamvue uanachama (kama ikitokea hivyo) na kidha ndio wafanye maamuzi juu ya uhalali wa maamuzi ya CC? Je katika rufaa ikiamuliwa kuwa CC ilikosea itakuwaje kama uamuzi wa kunvua uanchama umeshafanyika? Si matumizi mabaya ya resources/muda na kuongeza "majeraha" na mivutano isiyo na msingi?
 
mie ni mwanachama wa dhati kabisa wa CDM - ila nakiri kuna ubaguzi tena wa wazi kabisa ndani ya chama..........kuna 'watu' ndani ya chama hata wafanye makosa gani kamwe hawawezi kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa katiba mfano lema alivyokurupuka hapa hapa jf!
ishu ya mbowe kutumia madaraka yake vibaya kama KUB (uzinzi na viti maalum tena wa ndani ya chama) chama kinavunga na kitaendelea kuvunga as if hakuna kilichotokea wakati ukweli ni kwamba mbowe kama kiongozi mkuu hakupaswa kufanya hayo coz anaharibu image ya chama, tafakari ingekuwa ishu inamuhusu zito hali ingekuwaje?!
badala yake watu wanazidisha chuki zao tu kwa zito utadhani yeye ndo alimtuma mbowe kufanya upuuzi - wanachama na viongozi CDM achene unafki, kunya anye kuku akinya bata................
 
Zitto apelekwe kwenye mahakama ICC the Heague na chama kwa kosa la usaliti na uhaini, Kwani kusaliti watu waliokuamini ni zaidi ya jinai tena ni kosa kubwa zaidi hata ya ugaidi.
 
Last edited by a moderator:
Maskini Zitto Kabwe Chadema
NA MUHIBU SAID
19th December 2013

Zitto%20Kabwe(3).jpeg

Zitto Kabwe


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakitashughulikia rufaa iliyokatwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kwa Baraza Kuu kupinga uamuzi wa Kamati Kuu (CC) wa kumvua nyadhifa zake katika chama, hadi hapo itakapopitia utetezi wake na kuamua hatima ya uanachama wake katika chama hicho.

Pia kimethibitisha kupokea utetezi dhidi ya mashitaka 11 yanayohusisha usaliti dhidi ya chama na kuwachafua viongozi wakuu kupitia waraka wa mabadiliko.

Mashtaka hayo yanamkabili Zitto, pamoja na aliyekuwa Mjumbe wa CC, Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Victor Kimesera, alisema hayo alipozungumza na NIPASHE, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana.

Kimesera, ambaye ni Katibu Mtendaji Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chadema, alisema rufaa hiyo ni kitu kidogo, hivyo haiwezi kuanza kushughulikiwa na chama katika sakata la Zitto na watuhumiwa wenzake.

"Kuna (kitu) kikubwa cha mbele yake (rufaa)," alisema Kimesera akijibu swali la NIPASHE lililotaka kujua nini kinaendelea kwenye chama baada ya Zitto kukata rufaa.
Kimesera alisema kitu kikubwa kuliko rufaa, ambacho kitaanza kushughulikiwa na chama ni maelezo ya utetezi wa Zitto na watuhumiwa wenzake.

Alisema hiyo ni kwa sababu tayari kuna hoja ya CC, ambayo inataka ijiridhishe kama Zitto na wenzake waendelee kuwa uanachama au la.

Kwa mujibu wa Kimesera, baada ya Zitto na wenzake kuwasilisha utetezi wao, CC itaitishwa na kuyapitia na kisha itatoa maamuzi juu ya uanachama wao.
"Sasa huwezi kuongea juu ya rufaa wakati hujajua uanachama wao kwanza," alisema Kimesera.

Hivyo, alisema rufaa ya Zitto itaendelea kuhifadhiwa kwenye jalada hadi hapo hatua ya kwanza ya kupitia maelezo yao ya utetezi na kuyatolea maamuzi itakapochukuliwa. "Lazima twende kwa hatua. Kwa hiyo, hiyo (rufaa) imekaa," alisema Kimesera.

Mwanasheria wa Zitto, Albert Msando, alitaja sababu mbili za mteja wake kukata rufaa kuwa ni kukiukwa kwa taratibu za kuchukua hatua za nidhamu na sababu zilizotolewa kutokuwa sahihi.

Msando alitaja kifungu cha 6.5.6 cha Kanuni ya Uendeshaji ya chama hicho, akisema utaratibu uliotakiwa kufuatwa kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kiongozi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni ni kupewa kwanza mashtaka kwa maandishi ili apate nafasi ya kujibu.

Alisema kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashtaka yake kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi.

Alitaja ibara ya 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba kwamba mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili."

Alitaja vipengele vingine ni kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika na atajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao ndani ya wiki mbili baada ya kusikilizwa.

Katika hatua nyingine, Kimesera alisema Chadema imepeleka majibu baada ya Mwigamba kupeleka barua yenye malalamiko kwa Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya uongozi wa chama hicho.

Katika malalamiko yake, Mwigamba anadai kuwa katiba ya Chadema ilivurugwa na viongozi wa chama kwa kuondoa kinyume cha taratibu maelezo ya kifungu cha katiba ya chama yaliyokuwa yakiainisha ukomo wa vipindi viwili vya uongozi.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, alithibitisha kupokea barua hiyo ya Mwigamba na kusema ofisi yake inaifanyia kazi.

Kimesera jana aliliambia NIPASHE kuwa walipeleka majibu dhidi ya malalamiko ya Mwigamba baada ya kuagizwa na msajili kufanya hivyo kabla ya Desemba 19, mwaka huu.

Katika barua yake, Mwigamba amemuomba msajili kutoa mwongozo kuhusu anachodai kuwa ni mgogoro wa kikatiba uliopo ndani ya Chadema kufuatia kipengele cha katiba kinachogusia ukomo wa uongozi kubadilishwa kinyume cha utaratibu.

Novemba 22, mwaka huu, CC iliwavua madaraka viongozi hao na kuwataka wajieleze kwa maandishi ndani ya siku 14 baada ya kudaiwa kuhujumu chama kwa kuandika waraka wa siri unaodaiwa pamoja na mambo mengine, kuwadhalilisha viongozi wakuu wa Chadema.




CHANZO: NIPASHE


 
Hamna umakini hapo mnadanganyana tu,Ningeona Chadema wako makini kama wangeachana viongozi wabovu wote wanaokwamisha ukuaji wa Chama akiwemo Mbowe mwenyewe pamoja na Zitto,Wengineo ni pamoja na akina Lema.Chadema kingeundwa na uongozi mpya wenye nia ya dhati kukipeleka Chama madarakani 2015.Chadema chini ya Mbowe ikulu 2015 tutaisikia kwenye radio huku tukitoa fursa kwa chama cha mafisadi kurejea Ikulu na ndicho hasa anachokitaka huyu bwana kwasababu kwake hiyo itakuwa fursa nzuri sana ya kutengeneza fedha kutoka kwa Mfalme wa Monduli.WanaChadema mnamwiita Zitto msaliti?Subirini 2015 ifike ndio mtamjua msaliti ni nani!!??Na mpaka mtakapokuja kushtuka mtakuwa mmechelewa sana maana jamaa atakimbilia Dubai kujipoza na Uenyekiti wa Chama hatautaka tena maana alichokitaka atakuwa ameshakipata.Hii ndio sababu Mheshimiwa ameapa kutokiachia kiti maana anajua kuna biashara nzuri 2015 inakuja na yeye si unajua tena ni Mfanyabiashara?
Nikweli tumechelewa kumfukuza msaliti

kama ulivyoshauri tunaanza kufukuza viongozi wabovu akiwemo Zitto kabla ya 2015.
 
Back
Top Bottom