MALUNGU
JF-Expert Member
- Jun 2, 2011
- 250
- 97
Mkuu Molemo, kwa Kawe mtakuwa mmefanya vema, ila kwenye kete ya urais kazi bado mnayo!. Kwanza nilizungumza naye (off the record), hivyo msimamo wake binafsi naujua!. Msimamo binafsi ni tofauti na matakwa ya Chama!.
Kwa political dynamics za 2015, chances yoyote ya mgombea huyo kushinda, determinant ni mgombea wa CCM, hivyo endeleeni kusali, CCM isimamishe weak candidate, ikisimamisha strong candidate, you are dead!.
Uchaguzi wa 2015 chini ya Katiba Mpya, mshindi wa urais anapatikana sio tuu kwa simple majority, bali kwa quota system yaanini lazima ushinde kwa theluthi moja ya kura kutoka pande zote za muungano!. Kwa mgombea huyo, sioni jinsi yoyote ya Chadema kuvuna theluthi moja ya kura za urais kutoka Zanzibar!. Hivyo mtaongoza bara, kwa kukosa Zanzibar, CCM mwenye theluthi kote ndio atatangazwa mshindi!.
Kuna uwezekano mkubwa mgombea wa CCM kuwa ni Mkatoliki, na Dr. ni Mkatoliki, mtagawana kura za bara ila Zanzibar CCM ndio watavuna!. Mkimpitisha ZZK, CUF haitasimamisha mgombea urais kufuatia ukaribu wa ZZK na Jussa, hivyo kura zote za bara za wale jamaa zetu, mtavuna na kura za Zanzibar pia mtavuna na mtatangazwa washindi!.
Kama mtasimamisa mgombea ambaye nyinyi Chadema ndio mnamkubali sana, tegemeeni kuchaguliwa na wanachadema tuu lakini mkimsimamisha mgombea anayekubalika zaidi kwa wapiga kura wa 2015 ambao 80% ni vijana, then the one and only anaweza kuwapatia ushindi mnene na mnono, ni ZZK pekee!.
The choice is yours, sisi wengine kazi ni kusema tuu!.
Pasco.
Pasco wananchi gani unawazungumzia wanaompenda ZK? Vijana wa wapi? hata hapa JF huoni kuwa haugwi mkono na watu wengi? Hizi siasa watu wanazijua kuwa mnatka mgombea weak ili mafisadi wawe salama. Mkuu kama CDM wanataka kampeni zao ziwe ngumu wajaribu kufuat ushauri wako huu. Angalia kura za maoni zilizoendeshwa hapa JF kati ya DR na ZK ilikuwaje? Je hawa waliopiga hizo kura ni sehemu ya wapiga kura wa Tanzania? Kama ni sehemu ya wapiga kura utafiti wako unaufanyia wapi? Jambo lingine linalonipa wasiwasi juu ya mchango wako huu ni wewe kukiri kuwa bado upo kwenye Payrol ya mheshimiwa.