CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

Kuweko na direct link kati ya viongozi wanaosaini mikataba na wananchi wa eneo husika!Wanaosaini mikataba wawe wamekubalika na wananchi na waweze kuwajibishwa na wananchi kama wana nia mbaya na rasilmali zao.
Wananchi wawe wadau asilia kwa asilimia kubwa pale inapokuja kwenye maamuzi yanayozigusa rasilimali zao na mchango wao upokelewe moja kwa moja bila spin!

Hujaeleza kuhusu hilo hapo juu!
 
Hivi Kigarama ngoja nikuulize swali moja!
Hivi wananchi wa Buzwagi walipata nafasi gani ya kummuliza Karamagi na wenzake kuhusu hiyo mikataba?
Kwani hatujui wabunge wanazimwa na hoja zao huko bungeni kwa maslahi ya chama tawala?
Wananchi wanatakiwa waonyeshwe ni kwa jinsi gani system hii itafanikisha uwajibikaji kwa wananchi!

Wala hilo hapo juu!
 
Nafikiri tunaweza kuendelea na mjadala huu.
Lakini sishani kama wakati huu ni muafaka wa kuitumia kabla hatujapata maoni ya kutosha ili kuweza kuona udhaifu wake na uzuri wake.
Pia nataka nielewe kama CHADEMA itaungana na vyama vingine...Then nini msimamo wao na ni sera gani zitakazo simamiwa kama wakipata idhini ya wananchi na kuingia madarakani kwa tiketi moja ya urais?

Wala hujaweka wazi kama unataka mjadala uendelee..Ama simply hoja ni mbaya na haifai kujadiliwa?
Kuwa specific nyie watu wa CHADEMA mnachanganya watu!!
 
Pia nataka nielewe kama CHADEMA itaungana na vyama vingine...Then nini msimamo wao na ni sera gani zitakazo simamiwa kama wakipata idhini ya wananchi na kuingia madarakani kwa tiketi moja ya urais?


hapo ndipo siasa za Afrika zinapokuwa na matatizo kwani sasa hivi tatizo la wengine wetu siyo CCM bali falsafa inayotumiwa na CCM kuendesha nchi. Kama wapinzani wataungana kwa nia ya kuiondoa CCM tuu bila ya kuwa na falsafa zinazofanana basi tumekwisha!

Hoja yangu itakuwa kama vile Musseveni alivyoungana na wenzie kumuondoa Obote, au Chiluba dhidi ya Kaunda au Kibaki dhidi ya KANU na Uhuru Kenyatta. Tunataka kuona kwanza vyama vya upinzani vilivyoshiba falsafa na siyo vinavyotumia uchovu wetu dhidi ya CCM kujijengea uhalali. Ikumbukwe kuwa hata Hitler alitumia uchovu wa Wajerumani kuingia madarakani.
 
Naona muende mkachangie kwenye ile mada ya CHADEMA kunani ili tujue whats going on kabla hatuja jump on band wagons!
 
hapo ndipo siasa za Afrika zinapokuwa na matatizo kwani sasa hivi tatizo la wengine wetu siyo CCM bali falsafa inayotumiwa na CCM kuendesha nchi. Kama wapinzani wataungana kwa nia ya kuondoa CCM tuu bila ya kuwa na falsafa zinazofanana basi tumekwisha!

Hoja yangu itakuwa kama vile Musseveni alivyungana na wenzie kumuondoa Obote au Chiluba dhidi ya Kaunda au Kibaki dhidi ya KANU na Uhuru Kenyatta. Tunataka kuona kwanza vyama vya upinzani vilivyoshiba falsafa na siyo vinavyotumia uchovu wetu dhidi ya CCM kujijengea uhalali. Ikumbukwe kuwa hata Hitler alitumia uchovu wa Wajerumani kuingia madarakani.

Hakuna atakayeruhusu hilo kwenye kizazi hiki kipya kigarama!
Mijadala ipo na itaendelea kuwepo!
Tunataka facts za kwanini system moja ni mbaya VS nyingine and how we can fix whichever suits us!
Hakuna kitu kama kumpa mtu nafasi ya udikteta kama na sisi tuna akili! na uelewa wa kutosha!
Mimi niko radhi kunadi something positive!
Il mabadiliko this time ni LAZIMA!
Nilishawahi kuanzisha thread ya kuhusu CCM kuhitaji mabadiliko!
Mabadiliko ni LAZIMA!
Cha muhimu ni mjadala uendelee ili tuyakumbatie yale mabadiliko mema!
Lakini same ol same ol?NO WAY this time around!
 
Ndugu Zitto,
Shukran mkuu, kuja kwako hapa na haswa kutupa nafasi hii sisi Wananchi kueleza yetu machache ambayo pengine yameshindikana kutazamwa ama yamepuuzwa na baadhi ya watu kwa sababu tu yanaonyesha Upinzani wa kimawazo, Hilo moja lakini maadam haya ni mapendekezo yanayotayarishwa kujenga sera kamili ni muhimu sana kama utapitia sehemu alizozungumzia Moelex na Ndugu Rev.Kishoka kwa jicho la wazi badala ya kujenga hoja ambayo inachukua dhamana ya wananchi wote kama anavyojaribu Jmushi1 akifikiria kwanza sera ya chama ktk kundi la watu fulani bila kutanguliza kutazama maswali muhimu yanayohusiana na WATU hao, MAZINGIRA, na MUDA ili upate kujenga mkakati bora wa malengo yatakayowezesha kufanikiwa kwa sera hiyo. Ni sawa na kujaribu kumfuga Simba ukamlisha mimea yenye neutrician ya hali ya juu kuliko nyama..
Kama alivyosema Moelex mkuu, Majimbo ni hoja nzito sana na wala sii rahisi kama watu wanavyofikiria kwa sababu nyingi za kimsingi...na pia nitatanguliza kusema kwamba hayo Majimbo ya South Africa hayana tofauti kubwa na Majimbo ya Canada kiutendaji zaidi ya sababu zilizotangulia kuundwa kwake, nadhani hili tuliwahi kulizungumzia...

Kwanza kabisa, mkuu inabidi watu wafahamu kwamba Majimbo yanaundwa kwa lengo moja kubwa nalo ni UHURU. Uhuru wa kuweza kutambua mipaka ya watu ktk ardhi moja ili kuboresha maisha na maendeleo ya watu hao Kiuchumi dhidi ya mfumo uliokuwepo ambao kwa namna fulani umeonyesha utengano baina ya watu wake.
Hata ule Uhuru wetu tulioupata toka kwa mkoloni ulikuwa ni Uhuru wa kiuchumi ambao hauwezi kupatikana bila kupata mwongozo ambao hujengwa na wanasiasa.Hivyo Mwalimu na waasisi wote wa mwanzo lengo kubwa la Uhuru wetu lilikuwa kutokana na hoja ya Utumwa kiuchumi kumtumikia mkoloni - nikitumia tafsiri finyu..
Kwa maana hii wazo la Uhuru ni kinyume cha Utumwa ktk nafasi ya Kiuchumi lakini sio lazima iwe utumwa hata yule anayetaka kuanza kujitegemea mwenyewe kiuchumi hudai uhuru wake na kujikata toka kwa wazazi. Hivyo neno Uhuru linakwenda sambamba na neno KUJITEGEMEA ambalo linaweka mipaka ya umilikaji mali, uhuru wa kutoa maamuzi ya mwelekeo wa afya ya mtu huyo kiuchumi..na ndio maana huundwa bunge tofauti (Legislative) kama wawakilishi halali wa kundi moja...ndoa zetu ni pamoja na kujikata lakini huunganisha mume na Mke kuwa kitu kimoja lakini muhimu ni ule uhuru wa maamuzi ya watu hawa ktk maisha yao.

Kwa hiyo basi tunapotaka kujenga Majimbo ni muhimu tufahamu kwamba tunajenga mipaka baina yetu ili kila mmoja wetu awe responsible na ujenzi wa uchumi wake na ndio sababu ya kuwepo kwa bunge hizi ambazo zitatambua kwanza mipaka yake ya ardhi ktk kupanga malengo ya kimaendeleo. Kama unakumbuka hata Uhuru wetu mwanzo ulijengewa hoja ya kuwa Uhuru wa nchi zote za Africa Mashariki lakini kutokana na sababu za kisiasa tulijikata vipande kwa dhana ya urahisi wa maendeleo ktk jumuiya yetu na tukaahidi kuboresha zaidi EAC ikiwa chini ya watawala weusi.

Ukitazama kiharaka utaona kwamba lilikuwa wazo zuri hasa watawala watakapokuwa weusi ni rahisi kwetu kuendeleza jumuiya hiyo kwa sababu sisi tulikuwa na tofauti chache sana na kutawaliwa na mzungu, kitu ambacho tuli overlook mahusiano ya UHURU na malengo ya uwezo wa kujitegemea ambao huweka mipaka baina yetu..
Matokeo yake ktk kujenga sera za maendeleo ambazo zinaheshimu mipaka hii kulitokea kutoelewana kati ya nchi zetu na matokeo yake tukavunja EAC...

Hivyo basi yapo maswala mawili muhimu hapa ambayo ni lazima tuyaangalie kwa makini sana.... Uhuru wa kujitegemea kiuchumi tofauti na Majimbo yaliyojengwa na nchi za Magharibi kuunda Umoja utakao imarisha nguvu ya National Security ya nchi tofauti na kutafuta uhuru wa kujitegemea (kujikata) kuboresha Uchumi. Ndio maana nikasema Aghalab nchi nyingi kukata majimbo katikati ya tawala uliokwisha kuwa huru ili kuimarisha ufanisi wa kazi. Hii ni process inayochukua miaka kujenga ama kubomoa yote yanatokana na factors kubwa zinazohusiana na kile kilichotangulia.
Kwa hiyo kabla sijaingia kuzungumzia WATU, MAZINGIRA na MUDA inabidi niweke pause hapa yasije kuwa maelezo marefu yanayojirudia yenyewe hali lengo hapa ni kujenga na sio kubomoa..
 
Mkoa wa RUVUMA utakuwa jimbo gani?

Asante kwa kugundua hilo, na mimi naongeza Zanzibar itakuwa jimbo gani?Halafu ni vyema CHADEMA wakasema wanatarajia uundaji wa serikali hii uchukue muda gani kukamilika?

Kwa kifupi iwapo serikali ya CHADEMA haina mpango wa kuwa ya kidikteta basi fikra zao hizi zitaishia kwenye maandishi tu.

Yaani mwandishi wa mapendekezo haya anaandika kama mtu aliyekuwa anasafiri na ngalawa akakuta kisiwa ambacho hakuna mtu anayeishi akaamua kuwaita watu wakae na waunde serikali!

kwanini nasema hivyo? je mwandishi anajua hatua zitakazotakiwa kupitiwa ili kuondoa cheo cha waziri mkuu?amejiandaa vipi na hatua hizo mpaka anaahidi kukiondoa cheo hicho kama si dikteta?
Katika hizo wizara nne ni ipi itashughulikia hospitali za rufaa?

Maswali ni mengi,ila kila atakayesoma mipango hii ya CHADEMA ataelewa vizuri ni kwa kiasi gani hawako tayari kuongoza nchi.
 
Mabadilko ya current system ni YA LAZIMA!
Sisi tuwasubiri tu hawa viongozi wetu wailete mijadala hapa na tuijadili..Tusiende nje ya hapo!
 
Asante kwa kugundua hilo, na mimi naongeza Zanzibar itakuwa jimbo gani?Halafu ni vyema CHADEMA wakasema wanatarajia uundaji wa serikali hii uchukue muda gani kukamilika?

Kwa kifupi iwapo serikali ya CHADEMA haina mpango wa kuwa ya kidikteta basi fikra zao hizi zitaishia kwenye maandishi tu.

Yaani mwandishi wa mapendekezo haya anaandika kama mtu aliyekuwa anasafiri na ngalawa akakuta kisiwa ambacho hakuna mtu anayeishi akaamua kuwaita watu wakae na waunde serikali!

kwanini nasema hivyo? je mwandishi anajua hatua zitakazotakiwa kupitiwa ili kuondoa cheo cha waziri mkuu?amejiandaa vipi na hatua hizo mpaka anaahidi kukiondoa cheo hicho kama si dikteta?
Katika hizo wizara nne ni ipi itashughulikia hospitali za rufaa?

Maswali ni mengi,ila kila atakayesoma mipango hii ya CHADEMA ataelewa vizuri ni kwa kiasi gani hawako tayari kuongoza nchi.

Nakubali pia maelezo zaidi yanahitajika hapa kuhusiana na hii hoja ya majimbo!
 
Nataka tujadili zile sehemu ambazo zitakuwa zinaleta wasiwasi wa UDIKTETA pamoja na migawanyiko ya KIKABILA kama vile wengi wanavyoonyesha ku suspect!
 
Nakubali pia maelezo zaidi yanahitajika hapa kuhusiana na hii hoja ya majimbo!

Majimbo siyo utatuzi wa kukosekana ufanisi hata kidogo,mfumo uliokuwepo sasa ni mzuri kabisa.Kinachohitajika ni true political will ya kuwezesha mfumo huo kufanya kazi.

Ili political will iwepo ni lazima viongozi waone what is at stake iwapo hawatawaridhisha waliowachagua.kwa kifupi ninachosema ni kwamba cha msingi ni kukuza usambazaji wa habari nchini na kuwapa uhuru wale wanaosambaza habari hizo-habari za kuelimisha umma.

Mfumo wa majimbo hivi sasa Tanzania tayari upo na wala sio kitu kipya.Unatumiwa na wizara ya afya na wizara ya elimu.Lakini bado tunaona ufanisi unasuasua.

Bila true political will hakuna achievement yoyote katika utawala.
 
Mfumo huu uliopo ni wa maslahi ya CCM..Kwani hatujaona jinsi walivyoigawa mikoa upya kuanzia Mkapa na sasa Kikwete?
Kwani huoni kuwa system ya sasa ndio inachochea ukabila licha ya kwamba CCM wao wanaimba lugha ya umoja?
Janja ya nyani...
 
Mi nashangaa kwa nini maswali yote ambayo nimeuliza hakuna anayetaka kujibu kuwa hiyo system wanayoitetea itayasimamia vipi maslahi ya wananchi na kuuzika UFISADI? YEYOTE MWENYE KUJA NA POINT HAPA NDIO WA KUUNGWA MKONO NA SI TIT FOR TATS!
Bado nasubiri majibu kutoka pande zote!
 
Jmushi1,
Nimeandika kitu hapo juu kukuonyesha kipengele cha kwanza ambacho ni chachu ya Majimbo..Binafsi kama raia sioni tofauti ya Utawala huu uliopo KIUCHUMI na ule wa mkoloni pamoja na kwamba lengo kubwa la sisi kudai uhuru wetu lilikuwa linahusiana sana na umilikaji wa UCHUMI wetu.
Tukatangaziwa maneno kama yako Power to the people na kadhalika lakini kweli tumeweza kuujenga uchumi ambao unamnufaisha mwananchi zaidi?..No..tumebadilisha mmliki tu wa chumi hizo toka mzungu na kuwa mtawala mwingine mweusi - Tumejenga tabaka kati yetu. Kwa muundo wa serikali hizi Mkoloni alitugawa kwa MAJIMBO (states) kutahisisha Utawala na himaya yake lakini kwetu sisi wananchi haikuwa na matokeo ya uhuru wa kiuchimi..
Leo hii Chadema kama watawala wanajenga hoja ama sera ambayo madhumuni yake ni kurahisisha Utawala lakini kama nilivyosema sijaona tofauti ya Mtawala binadamu kwa rangi zake inapofikia kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wake zaidi ya kurahisisha Utawala wenyewe. Kwa mwananchi kama mimi hii inanipa picha ya DEVIDE and RULE! ambayo haina tofauti na malengo ya mkoloni.
Ndio maana nikasema tatizo kubwa lipo ktk VIONGOZI wenyewe hata kama tutagawanyika kwa wilaya lakini kama ndani ya wilaya hizo wapo viongozi watawala badala ya vinara wa kuleta maendeleo bado tutakuwa tunajenga makoloni yanayomilikiwa na watu wachache.
Hivyo wimbo uliopo sasa hivi ni viongozi gani tuliokuwa nao, haijalishi ukubwa wa mipaka hiyo.. Nini kilicholala ndani ya mioyo yao kama kweli ni kuleta maendeleo ama nafasi ya wao kujitajirisha zaidi.. speaking from this end!..
Hivyo ni muhimu kwanza Chadema wapate kujenga mioyo ya wananchi kuwa wao ni tofauti na Mtawala aliyepo lakini hizi hoja za Majimbo ni mipaka tu inayoweza kutubomoa zaidi ya kutujenga.. hakuna kati yetu anayeweza kusema nini hatma ya majimbo kiuchumi isipokuwa uhakika wa uhuru wa kutambua mipaka baina yetu..
 
Jmushi1,
Nimeandika kitu hapo juu kukuonyesha kipengele cha kwanza ambacho ni chachu ya Majimbo..Binafsi kama raia sioni tofauti ya Utawala huu uliopo KIUCHUMI na ule wa mkoloni pamoja na kwamba lengo kubwa la sisi kudai uhuru wetu lilikuwa linahusiana sana na umilikaji wa UCHUMI wetu.
Tukatangaziwa maneno kama yako Power to the people na kadhalika lakini kweli tumeweza kuujenga uchumi ambao unamnufaisha mwananchi zaidi?..No..tumebadilisha mmliki tu wa chumi hizo toka mzungu na kuwa mtawala mwingine mweusi - Tumejenga tabaka kati yetu. Kwa muundo wa serikali hizi Mkoloni alitugawa kwa MAJIMBO (states) kutahisisha Utawala na himaya yake lakini kwetu sisi wananchi haikuwa na matokeo ya uhuru wa kiuchimi..
Leo hii Chadema kama watawala wanajenga hoja ama sera ambayo madhumuni yake ni kurahisisha Utawala lakini kama nilivyosema sijaona tofauti ya Mtawala binadamu kwa rangi zake inapofikia kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wake zaidi ya kurahisisha Utawala wenyewe. Kwa mwananchi kama mimi hii inanipa picha ya DEVIDE and RULE! ambayo haina tofauti na malengo ya mkoloni.
Ndio maana nikasema tatizo kubwa lipo ktk VIONGOZI wenyewe hata kama tutagawanyika kwa wilaya lakini kama ndani ya wilaya hizo wapo viongozi watawala badala ya vinara wa kuleta maendeleo bado tutakuwa tunajenga makoloni yanayomilikiwa na watu wachache.
Hivyo wimbo uliopo sasa hivi ni viongozi gani tuliokuwa nao, haijalishi ukubwa wa mipaka hiyo.. Nini kilicholala ndani ya mioyo yao kama kweli ni kuleta maendeleo ama nafasi ya wao kujitajirisha zaidi.. speaking from this end!..
Hivyo ni muhimu kwanza Chadema wapate kujenga mioyo ya wananchi kuwa wao ni tofauti na Mtawala aliyepo lakini hizi hoja za Majimbo ni mipaka tu inayoweza kutubomoa zaidi ya kutujenga.. hakuna kati yetu anayeweza kusema nini hatma ya majimbo kiuchumi isipokuwa uhakika wa uhuru wa kutambua mipaka baina yetu..

Mkandara mwalimu hakutaka kubadilisha sytem kwasabau alikuwa akiamni kuwa demokrasia bado ni changa na hivo kuwapa wananchi uhuru wa kujiamulia itakuwa ni hatari wakati ambapo alitaka kuzishinikiza sera zake za ujamaa!Ikabakia kwenye propaganda KUWA TUKO HURU huku tool yenyewe ya kurule na tactics zikibaki kuwa zile zile za kikoloni na zisizo na uhuru wowote kwa mwananchi!
Ni kivipi system aliyoiacha mkoloni itufae na wakati ni wazi uwa system hiyo ndiyo responsible kwa umasikini wetu uliokithiri?
Hivi unafikri mkoloni aliondoka kwa kupenda?
Nasema hivi..Bila mabadilko hakuna kitu!
Usiseme tu viongozi wazuri kama system haiwabani na hawawajibiki kwa wananchi!
Huwezi kusema kuwa hawa wachezaji ni wazuri na hawahitaji usimamizi!
Referee anaweza kuwa mzuri ama mbaya!
Hata kama wachezaji ni wazuri refarii anaweza akaharibu mchezo simply because of the system!
Mimi naitasapoti system ambayo itawapa wananchi nguvu zaid za kusimamia rasilimali zao!
 
Jmushi1,
Unatafuta jibu la swali ambalo tumekwisha kwambia toka mada hii ianze?..
Hakuna system ambayo iko 100% laa sivyo tusingekuwa na vyama vyenmye mirengo tofauti... Swala la Mafisadi nchini ni swala la KIONGOZI mkuu wa nchi ambaye kashindwa kuchukua hatua kisheria kwa sababu mhalifu hapa ni mzazi ama toto wake mwenyewe allomzaa kisiasa..
WE do understand position na uwezo wa JK hadi sasa hivi kwa hiyo tunahityaji kiongozi mwingine mwenye uwezo wa kuwawajibisha wale wote wanaohujumu nchi kwa kuweka sheria kali ambazo zitafuatiwa na utekelezaji wa sheria hizo.
JK kashindwa IKULU na kwa mara ya kwanza maneno ya Mwalimu kuwa IKULU sii kiti cha kuchezea imeanza ku sink in ktk fahamu zetu.. Tunataka kiongozi ambaye kuongoza watu millioni 40 ni ktk uwezo wake. Kuongoza Tanzania akiweka malengo mbele ya Uhuru tuliopigania toka kwa mkoloni na yeyote anayetaka kupotosha malengo hayo ni adui wa Uhuru huo...
Sasa huyu kiongozi awe Chjadema, TLP, CUF ama CCM, hili ndilo swala linalotangulia ktk uchaguzi wa mwaka 2010... na hapo ndipo kura za wananchi zitakapoweza kutambua nani anaaminika zaidi na wananchi ktk kufikia malengo haya..Chadema should concertrate on this rather than Majimbo ambayo ni lugha tofauti na PRIME concern ya wananchi. Muhimu Chadema watambue kwamba KUJENGA UCHUMI ndilo swala kubwa ktk mawazo ya wananchi wakitambua kwamba mbegu zao za kuimarisha uchumi huo zinaliwa na viongozi... Majimbo ni sera inayozungumzia zaidi KUGAWANA mavuno na pengine itaeleweka zaidi kama ni mfumo wa Kila mtu (kanda) na mzigo wake!
 
Jmushi1,
Unatafuta jibu la swali ambalo tumekwisha kwambia toka mada hii ianze?..
Hakuna system ambayo iko 100% laa sivyo tusingekuwa na vyama vyenmye mirengo tofauti... Swala la Mafisadi nchini ni swala la KIONGOZI mkuu wa nchi ambaye kashindwa kuchukua hatua kisheria kwa sababu mhalifu hapa ni mzazi ama toto wake mwenyewe allomzaa kisiasa..
WE do understand position na uwezo wa JK hadi sasa hivi kwa hiyo tunahityaji kiongozi mwingine mwenye uwezo wa kuwawajibisha wale wote wanaohujumu nchi kwa kuweka sheria kali ambazo zitafuatiwa na utekelezaji wa sheria hizo.
JK kashindwa IKULU na kwa mara ya kwanza maneno ya Mwalimu kuwa IKULU sii kiti cha kuchezea imeanza ku sink in ktk fahamu zetu.. Tunataka kiongozi ambaye kuongoza watu millioni 40 ni ktk uwezo wake. Kuongoza Tanzania akiweka malengo mbele ya Uhuru tuliopigania toka kwa mkoloni na yeyote anayetaka kupotosha malengo hayo ni adui wa Uhuru huo...
Sasa huyu kiongozi awe Chjadema, TLP, CUF ama CCM, hili ndilo swala linalotangulia ktk uchaguzi wa mwaka 2010... na hapo ndipo kura za wananchi zitakapoweza kutambua nani anaaminika zaidi na wananchi ktk kufikia malengo haya..Chadema should concertrate on this rather than Majimbo ambayo ni lugha tofauti na PRIME concern ya wananchi. Muhimu Chadema watambue kwamba KUJENGA UCHUMI ndilo swala kubwa ktk mawazo ya wananchi wakitambua kwamba mbegu zao za kuimarisha uchumi huo zinaliwa na viongozi... Majimbo ni sera inayozungumzia zaidi KUGAWANA mavuno na pengine itaeleweka zaidi kama ni mfumo wa Kila mtu (kanda) na mzigo wake!

Lakini hii system ambayo fisadi hawezi kuguswa hadi JK aamue ndiyo mnayoitetea wewe na Kishoka?
 
Kwahiyo Mkandara unakubaliana na mimi kuwa mabadiliko yanahitajika hata kama ni hayo unayodai ni ya kisheria?
 
Mkuu hata Ujamaa unasema Power toi the People! kumbuka tu imani ya itikadi zote hizi ni kumweka mwananchi mbele ya Mtawala lakini in real life inategema mtawala mwenyewe. Castro kwa waCuba anaonekana kuwa ni mtu anayewapa nguvu za maamuzi wananchi wake lakini kiuchumi nguvu hiyo ni kilema cha maendeleo yenyewe.. Hizi ni Politics tu mkuu na Chadema wanachojaribu kuuza hapa ni Politics hivyo utekelezaji wake lazima utazamwe nje ya Chadema kwani CCM pia atatakiwa kuongoza ndani ya mfumo huu huu wa Majimbo. Hivyo Majimbo sio swala la chama kimoja na kwamba kama chadema wakiondoka basi CCM wanaweza kurudisha mikoa...Think beyond.. think nje ya box mkuu.
Kisha sio swala la system mkuu kama angekuwa Dr. Slaa leo ndani ya system hii hii ama Salim,Mwakyosa pengine kungekuwa na kukamatwa kwa mafisadi hawa, sheria zipo isipokuwa ni utekelezaji wake.. kisha system sio katiba ya chama CCM isipokuwa ni katiba ya Taifa..CCM wanaweka katiba yao mbele ya ile ya kitaifa.. kama hayo maazimio ya chama.
 
Back
Top Bottom