CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

Kwa hiyo swala sio Majimbo yenywe isipokuwa who do you answer to.. kwa hiyo kwa nini isiwe kila mikataba iwekwe who to answer to badala ya kwenda kwa rais kwani tatizo hapa ni madaraka ya RAIS sio ukubwa wa nchi..
Kisha ikiwa ubadhilifu unatokana na rais kwa nini tunamchagua rais asiyeweza kuongoza nchi yenye watu millioni 40 tu ukubwa wa nchi sawa na state moja ya Marekani ama serikali nyinginezo. za Africa!
 
Huyu BISKUTI kama anaharibu hii mada basi then hata haja ya kuchangia sina!
 
BP Biscuit mane,
Mkuu hata sikuelewi unakojaribu kwenda, samahani sana nipo kizani kabisa! ebu nieleze kwa kina unachojaribu kuzungumza ktk hoja hii ya Majimbo.
 
Kwa hiyo swala sio Majimbo yenywe isipokuwa who do you answer to.. kwa hiyo kwa nini isiwe kila mikataba iwekwe who to answer to badala ya kwenda kwa rais kwani tatizo hapa ni madaraka ya RAIS sio ukubwa wa nchi..
Kisha ikiwa ubadhilifu unatokana na rais kwa nini tunamchagua rais asiyeweza kuongoza nchi yenye watu millioni 40 tu ukubwa wa nchi sawa na state moja ya Marekani ama serikali nyinginezo. za Africa!

Na ndio hapo ni kwasababu yuko under a bad sytem!
Badala ya kupata msaada yeye analimbikiziwa kilakitu!
 
Hivi we BISKUTI mbona hauwi straight?
Unazunguka zunguka nini hapa?
Ama unataka biskuti iliwe?
Sema unachotaka kusema na si ulete kizunguzungu hapa!

Unajua siyo kosa lako jmushi1, kwani inaonekana kama mtu haja-drop buzz-words kama CCM, fisadi, Zitto, CHADEMA na kadhalika kwenye postings zake basi kwako binafsi mtu huyo hajazungumza lolote la maana.
 
Unajua siyo kosa lako jmushi1, kwani inaonekana kama mtu haja-drop buzz-words kama CCM, fisadi, Zitto, CHADEMA na kadhalika kwenye postings zake basi kwako binafsi mtu huyo hajazungumza lolote la maana.

Wewe mwaga pointi acha kuzungukazunguka!
Kwani wapi kina Mtanzania wametaja anything you've just mentioned above?
Kwani hatujui CCM wana imply kuwa hii sera italeta ukabila?
Si ni sawa na Obama anavyoambiwa ataleta uislam marekani?
What a shallow thinking!
Weka data na si politics of fear!
 
BP Biscuit mane,
Mkuu hata sikuelewi unakojaribu kwenda, samahani sana nipo kizani kabisa! ebu nieleze kwa kina unachojaribu kuzungumza ktk hoja hii ya Majimbo.

Kwa kifupi ninachojaribu ku-argue hapa ni kwamba sera ya majimbo ielekezwe kwenye kufua (kwa maana ya ku-harness) nguvu mwanana ya ukabila kwa manufaa ya maendeleo ya Wananchi waishio kwenye majimbo hayo. Na ukabila, kama tunavyofahamu ni natural instinct na jadi ya binadamu wote popote duniani kama vilivyo dhana za nuclear family, extended family na kinship (au ukoo). Hata Ulaya utaona mataifa karibia yote kwa ujumla yamegawanyika kutokana na vigezo vya lugha na ukabila.
 
Mkuu wale viongozi wa Majimbo wqatashindwa nini kujilimbikiza mali wao?.. unajua mkuu kama ungeweza kunijibu direct swali langu la KUTOWAJIBIKA nadhani tungekuwa hatuzunguki mbuyu huu.
Ni kitu gani kitakacho wahakikishia wananchi kwamba hapatakuwepo na miungu wadogo ktk Majimbo?.. hawa marais wadogo wenye tamaa ya kujilimbikiza mali lakini hawajapata mwanya huo.
kuwa aswerable to the people ni neno tu ambalo hata leo tunaambiwa lipo ktk katiba ya nchi lakini halitekelezwi. Je, hayo majimbo yatabadilisha vipi kitabia hiki cha kujilimbikiza mali.. kuiba mbegu zetu, kwani mtoto wa nyoka ni myoka!
 
Kwa kifupi ninachojaribu ku-argue hapa ni kwamba sera ya majimbo ielekezwe kwenye kufua (kwa maana ya ku-exploit) nguvu mwanana ya ukabila kwa manufaa ya maendeleo ya Wananchi waishio kwenye majimbo hayo. Na ukabila, kama tunavyofahamu ni natural instinct na jadi ya binadamu wote popote duniani kama viliyo dhana za nuclear family, extended family na clanship (au ukoo). Hata Ulaya utaona mataifa karibia yote kwa ujumla yamegawanyika kutokana na vigezo vya lugha na ukabila.

We kweli BISKUTI!

Haya kati ya haya majimbo nataka utaje kama ni kabila moja tu lenye kuwa kwenye jimbo moja!

a) Jimbo la Kaskazini litaundwa na Mikoa ya Arusha, Manyara na
Kilimanjaro.:Humu kuna wachagga,wamasai,wameru etc etc! Tena kuna wahamiaji wengi tu ambao si makabila hayo! The same applies to letters b-h

b) Jimbo la Kusini litaundwa kwa kuunganisha mikoa ya Lindi na Mtwara.
c) Jimbo la Ziwa litaundwa kwa kuunganisha mikoa ya Kagera, Mwanza, Shinyanga na Mara.
d) Jimbo la Mashariki – mkoa wa Tanga na visiwa vyake.
e) Jimbo la Pwani -litaundwa kwa kuunganisha Mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar- es-salaam.
f) Jimbo la Kati litaundwa na Mikoa ya Dodoma na Singida.
g) Jimbo la Magharibi litaundwa na mikoa ya Tabora, Rukwa na Kigoma.
h) Jimbo la Nyanda za Juu Kusini litaundwa kwa kuunganisha Mikoa ya Iringa na Mbeya

NADHANI UNAWEZA KUANGALIA KAMA KUNA JIMBO HAPO JUU LENYE "KABILA MOJA"
 
Jmushi1,
Mkuu nitarukia tena swali hili pamoja na kwamba yale yaliyotangulia halikupata ufumbuzi
Hivi mapato ya tuseme mgodi wa dhahabu Shinyanga utawasaidia vipi wakazi wa Bukoba chini ya Majimbo ikiwa leo wananchi wa Shinyanga wanalalamika mali zao kuchukuliwa na serikali kuu. Kisha hao Shinyanga watakuwa na upendo gani tofauti kuona kwamba utajiri wao unapelekwa Bukoba hali Bukoba hawana kitu zaidi ya ndizi na kahawa siyokuwa na soko nje. Msukuma wa Shinyanga hali ndizi wala hana mahusiano ya kutaka chochote toka Bukoba utamwambia kitu gani ikiwa shinyanga itarudi nyuma kimaendeleo. hayo Makao makuu ya Jimbo sijui yatakuwa Mwanza. Je, hiyo Mwanza ikijengwa kwa chumi za mikoa mingine mtawaeleza nini wananchi wa sehemu zinazozalisha ujenzi wa makao makuu hayo..
 
Mkuu wale viongozi wa Majimbo wqatashindwa nini kujilimbikiza mali wao?.. unajua mkuu kama ungeweza kunijibu direct swali langu la KUTOWAJIBIKA nadhani tungekuwa hatuzunguki mbuyu huu.
Ni kitu gani kitakacho wahakikishia wananchi kwamba hapatakuwepo na miungu wadogo ktk Majimbo?.. hawa marais wadogo wenye tamaa ya kujilimbikiza mali lakini hawajapata mwanya huo.
kuwa aswerable to the people ni neno tu ambalo hata leo tunaambiwa lipo ktk katiba ya nchi lakini halitekelezwi. Je, hayo majimbo yatabadilisha vipi kitabia hiki cha kujilimbikiza mali.. kuiba mbegu zetu, kwani mtoto wa nyoka ni myoka!

Mkuu ukiangalia hapo chini kwenye highlight utaona kuwa wananchi watakuwa wanawakilishwa kwa urahisi zaidi na kuwa karibu zaidi na utawala wa juu!
Masuala yote yatakayojadiliwa kwenye serikali za majimbo ambazo zina incorporate serikali za mitaa!
Kwa hiyo hapo utaona kuwa kila mtu anamwangalia mwenzake kwa karibu sana na hivyo hakuna loop holes zinazosababishwa na madaraka ya kupita kiasi kutoka kwa individuals!


b) “Tutabadili mfumo wa sasa wa utawala na kuanzisha mfumo mpya wa utawala utakaokuwa na muundo mpya wa serikali kuu na serikali za majimbo. Serikali za mitaa zitakuwa sehemu ya serikali za majimbo’’.
 
Connection kati ya serikali za mitaa na serikali kuu zinakuwa enhanced na serikali ya majimbo kupitia vikao vyenye kuhusu maendeleo ya wananchi.
Kutakuwa na close and smooth communication and decision making btn those chain of commands.
Sasa the current process ni utitiri mwingi tu wa loop holes!
 
Serikali za mitaa hizi current migawanyo yake:

3) Serikali za mitaa zimegawanyika katika ngazi kuu tano;

I. Halmashauri za wilaya/manispaa/jiji.
II. Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya/Mji/Manispaa/Jiji.
III. Wakuu wa Idara katika Halmashauri. Idara hizi ni kama idara za mipango, kilimo, elimu, maji, maliasili, maendeleo ya jamii n.k).
IV. Ofisi ya Kata – hii huwa chini ya Katibu Kata na Kamati ya Maendeleo ya Kata.
V. Serikali ya Kijiji/Mtaa – hii huundwa pia na Ofisa mtendaji wa Kijiji na Halmashauri ya Kijiji.
 
Mwingiliano wa serikali kuu na za mitaa hizi hapa chini pamoja na majukumu ya serkali za mitaa!

4) Serikali kuu na serikali za mitaa zina mahusiano na maingiliano makubwa katika utekelezaji wa majukumu yake. Kazi na majukumu ya serikali za mitaa zimeainishwa kwenye sheria ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982. Kwa mfano, sehemu ya 111 na 118 ya sheria za Mamlaka za Mijini (Urban Authorities) zimeainisha huduma zinazotolewa na serikali za mitaa kama ifuatavyo.

a) Huduma zinazotolewa na serikali za mitaa kwa usimamizi wa serikali kuu. Huduma hizi ni elimu ya msingi, huduma za afya, maendeleo ya kilimo na mifugo, maji, na ujenzi na ukarabati wa barabara.

b) Huduma zinazotolewa na kusimamiwa na serikali za mitaa yenyewe. Huduma hizi ni ukusanyaji wa taka, usafi wa mazingira, maegesho ya magari na vifaa vinginevyo, masoko na nyinginezo
.

Hapo juu umeona mwingiliano wa serikali za mitaa na serikali kuu pamoja na majukumu hayo under current system!
Swali hapa ni kwanini hakuna ufanisi kwenye hizo huduma ambazo sasa ziko chini ya serikali za mitaa?
Huduma kama elimu,kilimo,mifugo,maji etc etc..Hizi huduma kwako wewe zinaridhisha?
Na kama sivyo je tufanye nini?
 
Na dawa ya hayo yote hapo juu inapokuja kwenye ufanisi na ujenzi wa Taifa lenye nguvu na maendeleo ya kweli the...

1. Dira.
“Kuwa na taifa linaloendelea kwa haraka na kwa usawa, lenye haki, umoja na mshikamano wa kweli”

2. Dhumuni Kuu.
“Kujenga mfumo na muundo wa utawala unaotoa nguvu na mamlaka zaidi kwa umma katika kujiongoza na kutumia raslimali zao kwa usawa kujiletea maendeleo”.

3. Malengo Mahsusi.
(1) Kupunguza ukubwa wa serikali kuu kimuundo na kimajukumu pamoja na gharama zake za uendeshaji na kuachia raslimali nyingi kutumika moja kwa moja kwa maendeleo ya wananchi.

(2) Kurahisisha uongozi wa nchi kwa kuiunganisha mikoa kuwa majimbo ambayo viongozi wake watapatikana na kuongoza kwa ridhaa ya wananchi.

(3) Kupunguza urasimu wa kufikia maamuzi na kuongeza ufanisi na usimamizi wa karibu zaidi katika utoaji huduma kwa jamii chini ya tawala za majimbo.

(4) Kuondoa matabaka kwa kuweka mgawanyo mzuri na matumizi mazuri ya raslimali kati ya eneo moja la nchi na lingine.

(5) Kuimarisha mfumo na muundo wa Serikali za Mitaa kwa kuingiza ngazi ya Mkoa katika muundo huu.

(6) Kuondoa migongano ya kiutendaji kati ya Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa pande zote kufanya kazi katika eneo moja la kijiografia na katika jamii ile ile moja.

(7) Kuanzisha vyombo vya uwakilishi wa wananchi ndani ya utawala wa majimbo na kuboresha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Muundo Mpya wa Serikali za Mitaa huu:

Serikali za mitaa zitakuwa sehemu ya serikali za majimbo na zitawasiliana na serikali kuu kupitia uongozi wa jimbo. Muundo mpya wa serikali za mitaa utahusisha ngazi zifuatazo;

a) Halmashauri za wilaya/Miji.
b) Wakuu wa Idara katika Halmashauri. Idara hizi ni kama idara za mipango, kilimo, elimu, maji, maliasili, maendeleo ya jamii n.k).
c) Ofisi ya Kata itakayokuwa chini ya Katibu Kata na Kamati ya Maendeleo ya Kata.
d) Serikali ya Kijiji/Mtaa itakayoundwa pia na Ofisa mtendaji wa Kijiji na Halmashauri ya Kijiji.
 
Muundo Mpya wa Serikali za Mitaa huu:

Serikali za mitaa zitakuwa sehemu ya serikali za majimbo na zitawasiliana na serikali kuu kupitia uongozi wa jimbo. Muundo mpya wa serikali za mitaa utahusisha ngazi zifuatazo;

a) Halmashauri za wilaya/Miji.
b) Wakuu wa Idara katika Halmashauri. Idara hizi ni kama idara za mipango, kilimo, elimu, maji, maliasili, maendeleo ya jamii n.k).
c) Ofisi ya Kata itakayokuwa chini ya Katibu Kata na Kamati ya Maendeleo ya Kata.
d) Serikali ya Kijiji/Mtaa itakayoundwa pia na Ofisa mtendaji wa Kijiji na Halmashauri ya Kijiji.

Na hapo unaweza kuona ni kwa namna gani hizo idara za kilimo,maji,maliasili etc zitakavyokuwa zikipewa kipaumbele tofauti na ilivyo kwenye mfumo wa sasa!
 
[
QUOTE=Mkandara;198528]Mkuu wale viongozi wa Majimbo wqatashindwa nini kujilimbikiza mali wao?.. unajua mkuu kama ungeweza kunijibu direct swali langu la KUTOWAJIBIKA nadhani tungekuwa hatuzunguki mbuyu huu.
Ni kitu gani kitakacho wahakikishia wananchi kwamba hapatakuwepo na miungu wadogo ktk Majimbo?.. hawa marais wadogo wenye tamaa ya kujilimbikiza mali lakini hawajapata mwanya huo.

MKANDALA
MIE NAELEWA WAPI UNAPATA SHIDA LAKINI UNAJUA MAJIMBO VIONGOZI WAKEHAWATAKUWA TENA UNDER CENTRAL GOVERNMENT ILA WATACHAGULIWA HUKO HUKO MAJIMBONI KAMA TUNAVYOCHAGUA WABUNGE. POST HIZI HAZITATENGEMEA RAIS TENA BALI WANANJI WENYEWE. IKITOKEA UKUFANYA VIZURI KWA KUWA ITAKUWA NA UKOMO WA MUDA WA POST HIZO, BASI UNAKAA PEMBENI. NA KILA MTU ATAJARIBU KUONA HAABISHWI KWA KUSHINDWA KUHUDUMIA WANANCHI.


kuwa aswerable to the people ni neno tu ambalo hata leo tunaambiwa lipo ktk katiba ya nchi lakini halitekelezwi. Je, hayo majimbo yatabadilisha vipi kitabia hiki cha kujilimbikiza mali.. kuiba mbegu zetu, kwani mtoto wa nyoka ni myoka!
[/QUOTE]

ALAFU MIMI SIJUI KWA NINI UNADHANI KWA KUWA CCM WAMESHINDWA KATIKA UONGOZI WAO AU KWA VILE WAMEJAZA MAFISADI KWA HIYO KILA MTU ATAKAYEWEKWA ATAKUWA FISADI. NAKUSHAURI UONDOE WAZO HILO MAANA WAPO WATU SAFI, WAKIKUTANA NA PROCEDURES SAFI. NINAAMINI HATA UKIPEWA WEWE MKANDALA KUWA KIONGOZI WA JIMBO UTAFANYA VIZURI NA HUTAKUWA FISADI AU VIPI? KWANI WEWE PIA NI FISADI? MIMI SI MTOTO WA NYOKA FISADI. NIKIWEKWA JUU YA MALI YA WATANZANIA NITAILINDA.
 
[
QUOTE=Mkandara;198536]Jmushi1,
Mkuu nitarukia tena swali hili pamoja na kwamba yale yaliyotangulia halikupata ufumbuzi
Hivi mapato ya tuseme mgodi wa dhahabu Shinyanga utawasaidia vipi wakazi wa Bukoba chini ya Majimbo ikiwa leo wananchi wa Shinyanga wanalalamika mali zao kuchukuliwa na serikali kuu. Kisha hao Shinyanga watakuwa na upendo gani tofauti kuona kwamba utajiri wao unapelekwa Bukoba hali Bukoba hawana kitu zaidi ya ndizi na kahawa siyokuwa na soko nje. Msukuma wa Shinyanga hali ndizi wala hana mahusiano ya kutaka chochote toka Bukoba utamwambia kitu gani ikiwa shinyanga itarudi nyuma kimaendeleo. hayo Makao makuu ya Jimbo sijui yatakuwa Mwanza. Je, hiyo Mwanza ikijengwa kwa chumi za mikoa mingine mtawaeleza nini wananchi wa sehemu zinazozalisha ujenzi wa makao makuu hayo..
[/QUOTE]

AJABU ILIOJE KWA TANZANIA KARIBU KILA MKOA UNA MADINI. NA KARIBU KILA MKOA UNA DHAHABU. KAMA HAIJAANZA KUCHIMBWA BASI WAKO WANAOITWA WACHIMBAJI WADOGO WANAENDELEZA HADI MAFISADI WATAKAPOTOKEA KUWANYANG'ANYA NA KUWAFUKUZA KWA KISINGIZIO CHA UWEKEZAJI. HAWA NDIO WAVUMBUZI WAKUBWA WA MIGODI YA NCHI HII
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom