CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

Jamani CHADEMA mbona tunarudishana nyuma mimi nadhani huu utawala wa majimbo tulishapitia enzi za mkoloini na ukafeli.
Au nyinyi wenzetu emeona tusichokiona? tuoneshane

Utaratibu wa central government kubakia wenye mamlaka kwenye shughuli zote za kimaendeleo ni mzigo mkubwa ambao unapelekea loopholes zinazotumiwa so often na Mafisadi!
Hapa accountability pia itakuwepo zaidi kwasababu wananchi watakuwa na uwezo zaidi wa kuwa monitor viongozi wao kwa ukaribu kuliko ilivyowahi kuwa before!!
 
Jmushi1,
Nakubaliana na maelezo yako lakini kabla hujabadilisha kitu ni muhimu sana ufahamu source ya matatizo na sio kufanya Ubunifu wa mbinu..Nitakubaliana sana na wazo hili ikiwa limefanyiwa utafiti na kuonekana kwamba kweli tumekwama kutokana na mfumo mzima wa Utawala.
Hivi sasa kuna serikali za mitaa na hawa jamaa wanaiba kama vile hakuna kesho.. Madiwani leo hii ni watu wa kuogopwa! wote wamejaa kishenzi na wanamiliki mali za wilayani utadhani wamerithishwa. Yote haya ni ktk hali ya kudecetralize power pamoja na kwamba bado tupo ktk mfumo wa zamani..yaani sasa hivi tunaibiwa kila kona na tunashindwa..
Je, huko vijijini mwananchi anayo sauti ya kumshutumu Diwani ama mayor na wafanyakazi wake?.. HAPANA.. hivyo hivyo tukiweka majimbo bado hawahawa watu ambao ni wakuu wa halmashauri zetu za miji na kadhalika wakakuwa watawala wenyewe -Mafisadi. Wataendelea kuiba kwa sababu wanaweza jijengea ukuta vizuri zaidi na kuyaweka maswala ya majimbo kuwa ni maswala ya Taifa. Mfano mkubwa ni huu wa Richmond!.. leo hii mimi hapa Mkandara kwa sababu natoka Mwanza nisingekuwa na sauti kuzungumzia Richond kwa sababu pengine sii mkazi resident wa jimbo hilo..
Kwa hiyo tatizo hapa sio kuwepo kwa mkoa wa Dar es saalaam na matatizo yake ya Umeme yaliyozua uhaba wa maendeleo ktk mkoa huu isipokuwa ni viongozi wabaya, wezi mafisadi amabo they can stop at nothing kupata Utajiri..
Nitarudia kusema bila kuwaondoa Mafisadi hata kama tutaleta mfumo gani haiwezi kutusaidia kitu labda ndio tunaweza jenga NIGERIA ya pili Africa..
tatizo sio nchi hata kidogo na ndio maana nakubaliana na usemi wa kina Dr.Slaa kuwa Tanzania kama nchi sio maskini isipokuwa watu wake ndio maskini.. na hii inatokana na UONGOZI mbaya.
Hivyo basi ni muhimu kwanza kuondoa UFISADI tujenge sheria kali dhidi ya Ufisadi kisha hapo ndipo tunaweza pima maendeleo vizuri..

Lakini kama tutafikiria maendeleo wakati sisi wenyewe bado hatujajipanga kisawasawa sidhani kama tutafanya kitu cha maana zaidi ya kuharibu hata Muungano ambao unasubiri tu cheche za moto...
 
Utaratibu wa central government kubakia wenye mamlaka kwenye shughuli zote za kimaendeleo ni mzigo mkubwa ambao unapelekea loopholes zinazotumiwa so often na Mafisadi!
Hapa accountability pia itakuwepo zaidi kwasababu wananchi watakuwa na uwezo zaidi wa kuwa monitor viongozi wao kwa ukaribu kuliko ilivyowahi kuwa before!!
Nafahu kwamba viongozi wanamapungufu yao kwenye huu mfumo wa sasa, lakini tusisahau kwamba hata sisi wananchi tunamajuku ya kuungalia uongozi wetu unfanya nini(check and balance).kwahiyo tatizo sio mfumo tatizo ni uoga au utofamu wa wananchi wa majukumu yao, mfano hivi ni mwananchi gani emeshauliza matumi ya serikarli za mikoa au wilaya?
Therefore hata tukileta utawala huu wamajimbo kama wananchi hawatafanya kazi yao, then viongozi watakao kuwepo madarakani watatumia loop-holes zitakazo kuwepo
 
Mchelea Mwana,
Tatizo ni kuwa ukiuliza utawekwa ndani... RULE OF LAW hakuna kabisa mkubwa hakuna na ndio maana tumepata Mafisadi.
 
Ni uundwaji wa serikali za majimbo ambapo badala ya serikali kuu kuchukua mapato yote kutoka kwa wananchi..Tunahakikisha kuwa pasenti flani ya kutosha inabaki kuwasadia kwenye shughuli zao za kimaendelo na za kijamii kama vile maji hospitali nk!
Badala ya mapato hayo kwenda kwa mafisadi..Sasa yatawasaidia wananchi kwa kuwaweka karibu zaidi na viongozi wao!
Hakuna tena cha kusubiri Mkuu aseme...Bali tutakuwa na watu wa kuwashika mashati pale mambo yanapokuwa hayaendi vile wananchi wanataka!

It is all good.

This will stimulate COMPETITION among us kabla ya kukimbilia shirikisho la East Africa, hasa ukizingatia background yetu ni UJAMAA.
We still need preparation though!
 
Mchelea Mwana,
Tatizo ni kuwa ukiuliza utawekwa ndani... RULE OF LAW hakuna kabisa mkubwa hakuna na ndio maana tumepata Mafisadi.
Then unakubaliana na mimi kwamba kosa sio system ilopo sasa ila ni udictator wa Kiongozi binafsi.
Kwa maoni yangu ni kwamba hata tukibadilsha mfumo bila kumpunguzia nguvu kiongozi wa juu anaweza kuingia madarakani na huu mfumo wa majimbo na bado akawa mungu rais
 
Then unakubaliana na mimi kwamba kosa sio system ilopo sasa ila ni udictator wa Kiongozi binafsi.
Kwa maoni yangu ni kwamba hata tukibadilsha mfumo bila kumpunguzia nguvu kiongozi wa juu anaweza kuingia madarakani na huu mfumo wa majimbo na bado akawa mungu rais

Nakubaliana na wewe juu ya mamlaka kubwa kuwa juu ya mtu mmoja inaleta shida katika utekelezaji. Tanzania ya miaka ya 70 siyo hii ya sasa. Idadi ya watu imeongezeka hivyo pia majukumu yameongezeka. Polisi, PCCB, CAG nk walipaswa kuwa na nguvu za kuanzisha uchunguzi na kuchukua hatua dhidi ya waovu bila kusubiri maagizo ya Rais.

Ila huku mikoani na wilayani nadhani kuna tatizo la kuingiliana majukumu hususani kati ya Mkuu wa Mkoa na RAS, Mkuu wa wilaya na DAS. Mimi binafsi sioni ulazima wa kuwepo kwa hawa wote wawili. Tunaweza kuachana na vyeo vya Wakuu wa mikoa na Wakuu wa wilaya tukabakiwa na RAS na DAS au Tukaachana na RAS na DAS tukawa na RC na DC ila wateulewe kutokana na taalumu yao katika masuala ya utawala. siyo mfumo huu wa sasa ambao uDC na uRC unatolewa kama zawadi.
 
Jmushi1,
Nakubaliana na maelezo yako lakini kabla hujabadilisha kitu ni muhimu sana ufahamu source ya matatizo na sio kufanya Ubunifu wa mbinu..Nitakubaliana sana na wazo hili ikiwa limefanyiwa utafiti na kuonekana kwamba kweli tumekwama kutokana na mfumo mzima wa Utawala.
Hivi sasa kuna serikali za mitaa na hawa jamaa wanaiba kama vile hakuna kesho.. Madiwani leo hii ni watu wa kuogopwa! wote wamejaa kishenzi na wanamiliki mali za wilayani utadhani wamerithishwa. Yote haya ni ktk hali ya kudecetralize power pamoja na kwamba bado tupo ktk mfumo wa zamani..yaani sasa hivi tunaibiwa kila kona na tunashindwa..
Je, huko vijijini mwananchi anayo sauti ya kumshutumu Diwani ama mayor na wafanyakazi wake?.. HAPANA.. hivyo hivyo tukiweka majimbo bado hawahawa watu ambao ni wakuu wa halmashauri zetu za miji na kadhalika wakakuwa watawala wenyewe -Mafisadi. Wataendelea kuiba kwa sababu wanaweza jijengea ukuta vizuri zaidi na kuyaweka maswala ya majimbo kuwa ni maswala ya Taifa. Mfano mkubwa ni huu wa Richmond!.. leo hii mimi hapa Mkandara kwa sababu natoka Mwanza nisingekuwa na sauti kuzungumzia Richond kwa sababu pengine sii mkazi resident wa jimbo hilo..
Kwa hiyo tatizo hapa sio kuwepo kwa mkoa wa Dar es saalaam na matatizo yake ya Umeme yaliyozua uhaba wa maendeleo ktk mkoa huu isipokuwa ni viongozi wabaya, wezi mafisadi amabo they can stop at nothing kupata Utajiri..
Nitarudia kusema bila kuwaondoa Mafisadi hata kama tutaleta mfumo gani haiwezi kutusaidia kitu labda ndio tunaweza jenga NIGERIA ya pili Africa..
tatizo sio nchi hata kidogo na ndio maana nakubaliana na usemi wa kina Dr.Slaa kuwa Tanzania kama nchi sio maskini isipokuwa watu wake ndio maskini.. na hii inatokana na UONGOZI mbaya.
Hivyo basi ni muhimu kwanza kuondoa UFISADI tujenge sheria kali dhidi ya Ufisadi kisha hapo ndipo tunaweza pima maendeleo vizuri..

Lakini kama tutafikiria maendeleo wakati sisi wenyewe bado hatujajipanga kisawasawa sidhani kama tutafanya kitu cha maana zaidi ya kuharibu hata Muungano ambao unasubiri tu cheche za moto...

Mkandara nimekuelewa lakini kumbuka usemi wa "semi-autonomous"
Lazima majimbo yataendelea kuwa na sera zenye manufaa kwa taifa!
Haina maana kwamba hizi serikali za majimbo zitakuwa na madaraka ya kujiamulia mambo yenye kugusa maslahi ya Taifa!
Kumbuka sio kuwa tunagawanyika..NO Bali ni mfumo wa kiutendaji wenye kuleta ufanisi zaidi na sauti kwa myonge!
 
Sasa huu utaratibu wa kusubiri jimbo lipelekewe maendeleo eti tu kwasababu mbunge wake kawa waziri utakwisha!
Tizama mifano ya mikoa kama Rukwa mbayo imebaki nyuma na sasa eti unakumbukwa simply because waziri mkuu Pinda katokea huko!
Ama wabunge kufanya ufisadi na kuenda majimboni kwao kujijenga kwa uwezo walioupata baada ya kuukwaa uwaziri!
Ni wakati wa mabadiliko ya kweli!
 
Nafahu kwamba viongozi wanamapungufu yao kwenye huu mfumo wa sasa, lakini tusisahau kwamba hata sisi wananchi tunamajuku ya kuungalia uongozi wetu unfanya nini(check and balance).kwahiyo tatizo sio mfumo tatizo ni uoga au utofamu wa wananchi wa majukumu yao, mfano hivi ni mwananchi gani emeshauliza matumi ya serikarli za mikoa au wilaya?
Therefore hata tukileta utawala huu wamajimbo kama wananchi hawatafanya kazi yao, then viongozi watakao kuwepo madarakani watatumia loop-holes zitakazo kuwepo

Na dio maana nasapoti hii sera kwasababu sasa wananchi watakuwa wanahamasishwa kwa karibu.
Just imagine unakuwa na viongozi jimboni ambao tunauwezo wa kuwauliza maswali ambayo before ilikuwa inabidi tusubiri serikali kuu ambayo nayo kutokana na majukumu mengi haiwezi kutilia mkazo kwenye mikakati mbinu ya kimaendeleo kutokana na kubanwa na matatizo mengine!
Tusisahahu kuwa hizi sera zinaweka msisitizo kwenye maendeleo!
 
Na pia tusisahau kuwa kuna potential ya ajira kuongezeka kwa kasi ya ajabu na hivyo kupelekea maendelo kwa Taifa.
 
jmushi!, Swala la Richmond halikuwa swala la taifa hata kama lingekuwa ktk serikali ya majimbo bado ni tatizo la mkoa wa Dar es salaam.
Sasa kama hawa viongozi wanaoendesha nchi nzima ndio mafisadi kisha tugawe nchi ktk majimbo kuwapa nafasi hata mafisadi wadogo kushika madarakka ya juu ktk kila Jimbo who will be responsible ikiwa leo hii swala dogo kaa la Richmond la mkoa ambalo tunashindwa kulishughulikia Kitaifa?..
Mkuu sijasema kwamba majimbo yatakuwa na mamlaka ya maswala ya Taifa isipokuwa nachojaribu kujenga hapa hoja yangu ni sawa na kusema hivi;- Tatizo letu kubwa la kiuchumi ni Uongozi wetu wala sio wa mtu mmoja isipokuwa viongozi wote wa juu kutowajibika. Tumewaona kina Yona, Karamagi, Lowassa, na pengine naweza sema mawaziri wote walioachishwa nafasi zao za Uongozi kumetokana na utendaji wao wa kazi na sio nguvu ya rais..
katika serikali ya Majimbo kina Karamagi watakuwepo bado kitaifa na poengine kuzaa kina Karamagi wengine ktk Majimbo kwa sababu kazi inayotakiwa kufanyika ni ile ile.
Nitakubali Majimbo ikiwa kuna utafiti wa kisayansi unaodhihirisha wazi kuwa kina Lowassa na kundi zima walishindwa kazi zao kutokana na ukubwa wa nchi ama system nzima iliyopo sasa hivi..badala ya kuwapa watu hawa nafasi wapate kuwa marais wadogo wa kanda zetu kwani wapo kina Karamagi wengi tu wanasubiri nafasi kama hizi. na ndio maana nikatoa mfano wa hizi Halmashauri za miji tulizojenga sasa hivi kuwa na madaraka ktk maendeleo ya sehemu zao zimegeuka kuwa sehemu baabu kubwa za Ulaji. Kila kijana leo hii Tanzania anatafuta kupata kazi City kwa sababu kuna Ulaji mkubwa. Nenda huko wilayani, Madiwani siku hizi wanajirusha na kuonekana wenye fedha yote haya ni matokeo ya kumpa mamlaka mtoto wa Fisadi...Barabara hazijengwi hadi utakapo fika wakati wa uchaguzi, yale mabillioni ya Kikwete yameliwa vibaya sana na viongozi wadogo wa mikoa ambao kesho watakuwa na madaraka zaidi chini ya serikali ya Majimbo....
Hivyo problem sio majimbo ila ni watu wenyewe na sio kusema ati nguvu ya rais peke yake ndio tatizo bali mfumo mzima wa sheria kutoheshimu rule of law kwa sababu ya kipengele kidogo kilichoundwa na serikali ya CCM kuweka maazimio kama Azimio la Zanzibar..
Ondoeni kwanza UFISADI, jenga mfumo wa uwazi na good governance kwa sababu Utawala bora haujengwi na mipaka bali watu wenyewe...
Kwa hao wanaosema Utawala wa mtu mmoja kuwa rais wanchi nzima sielewi hata wanachojaribu kusema hapa kwa sababu zipo nchi kibao zinazoendelea mfumo huo na wamefanikiwa. Binafsi siamini kabisa kwamba Botswana ingeweza kuwa na tofauti mbili za kiuchumi kama ingekuwa na mfumo fulani wa kuigawa/ kuunganisha nchi hiyo kwa mipaka yake, kwa sababu hawa jamaa zetu viongozi wake ni wawajibikaji kwanza na wote abide by the rule of law..hakuna Mungu mtu isipokuwa hapa kwetu Tanzania ambako tumeona haya yakijijenga taratibu mbele ya macho yetu. Kesho tukiumba Miungu wengine wadogo sidhani kama itaongeza uadilifu..
Enzi za mwalimu viongozi wetu waliheshimika lakini sasa hivi viongozi wetu wanaogopwa!.. Kwa mtazamo wa haraka unaweza sema tunawaheshimu kumbe kuogopa sio kabisa kuheshimiwa...
 
jmushi!, Swala la Richmond halikuwa swala la taifa hata kama lingekuwa ktk serikali ya majimbo bado ni tatizo la mkoa wa Dar es salaam.
Sasa kama hawa viongozi wanaoendesha nchi nzima ndio mafisadi kisha tugawe nchi ktk majimbo kuwapa nafasi hata mafisadi wadogo kushika madarakka ya juu ktk kila Jimbo who will be responsible ikiwa leo hii swala dogo kaa la Richmond la mkoa ambalo tunashindwa kulishughulikia Kitaifa?..
Mkuu sijasema kwamba majimbo yatakuwa na mamlaka ya maswala ya Taifa isipokuwa nachojaribu kujenga hapa hoja yangu ni sawa na kusema hivi;- Tatizo letu kubwa la kiuchumi ni Uongozi wetu wala sio wa mtu mmoja isipokuwa viongozi wote wa juu kutowajibika. Tumewaona kina Yona, Karamagi, Lowassa, na pengine naweza sema mawaziri wote walioachishwa nafasi zao za Uongozi kumetokana na utendaji wao wa kazi na sio nguvu ya rais..
katika serikali ya Majimbo kina Karamagi watakuwepo bado kitaifa na poengine kuzaa kina Karamagi wengine ktk Majimbo kwa sababu kazi inayotakiwa kufanyika ni ile ile.
Nitakubali Majimbo ikiwa kuna utafiti wa kisayansi unaodhihirisha wazi kuwa kina Lowassa na kundi zima walishindwa kazi zao kutokana na ukubwa wa nchi ama system nzima iliyopo sasa hivi..badala ya kuwapa watu hawa nafasi wapate kuwa marais wadogo wa kanda zetu kwani wapo kina Karamagi wengi tu wanasubiri nafasi kama hizi. na ndio maana nikatoa mfano wa hizi Halmashauri za miji tulizojenga sasa hivi kuwa na madaraka ktk maendeleo ya sehemu zao zimegeuka kuwa sehemu baabu kubwa za Ulaji. Kila kijana leo hii Tanzania anatafuta kupata kazi City kwa sababu kuna Ulaji mkubwa. Nenda huko wilayani, Madiwani siku hizi wanajirusha na kuonekana wenye fedha yote haya ni matokeo ya kumpa mamlaka mtoto wa Fisadi...Barabara hazijengwi hadi utakapo fika wakati wa uchaguzi, yale mabillioni ya Kikwete yameliwa vibaya sana na viongozi wadogo wa mikoa ambao kesho watakuwa na madaraka zaidi chini ya serikali ya Majimbo....
Hivyo problem sio majimbo ila ni watu wenyewe na sio kusema ati nguvu ya rais peke yake ndio tatizo bali mfumo mzima wa sheria kutoheshimu rule of law kwa sababu ya kipengele kidogo kilichoundwa na serikali ya CCM kuweka maazimio kama Azimio la Zanzibar..
Ondoeni kwanza UFISADI, jenga mfumo wa uwazi na good governance kwa sababu Utawala bora haujengwi na mipaka bali watu wenyewe...
Kwa hao wanaosema Utawala wa mtu mmoja kuwa rais wanchi nzima sielewi hata wanachojaribu kusema hapa kwa sababu zipo nchi kibao zinazoendelea mfumo huo na wamefanikiwa. Binafsi siamini kabisa kwamba Botswana ingeweza kuwa na tofauti mbili za kiuchumi kama ingekuwa na mfumo fulani wa kuigawa/ kuunganisha nchi hiyo kwa mipaka yake, kwa sababu hawa jamaa zetu viongozi wake ni wawajibikaji kwanza na wote abide by the rule of law..hakuna Mungu mtu isipokuwa hapa kwetu Tanzania ambako tumeona haya yakijijenga taratibu mbele ya macho yetu. Kesho tukiumba Miungu wengine wadogo sidhani kama itaongeza uadilifu..
Enzi za mwalimu viongozi wetu waliheshimika lakini sasa hivi viongozi wetu wanaogopwa!.. Kwa mtazamo wa haraka unaweza sema tunawaheshimu kumbe kuogopa sio kabisa kuheshimiwa...

Sera za majimbo zinawashirikisha wananchi kikaribu zaidi kwenye issue nyeti zinazohusu maendeleo yao.
Hivi Mkandara we unaona ni haki kuwa mapato yapelekwe yote serikali kuu na halafu wao ndio wazigawe kwa jamii vile wanavyotaka?
Ugawaji wao huo wanaouita wa kitaifa umekuwa na manufaa gani?
Yani mpaka Mkapa awe Rais ndio Kibiti Lindi ijengwe?
Ama Rukwa ipate maendeleo eti baada ya kupata waziri mkuu?
Ama na sasa tumpe Zitto uraisi ili Kigoma nao wapate maendeleo zaidi?
Sera za majimbo ni sera madhubuti zenye kulenga kuwahusisha wananchi na kuwa engage kwa karibu kwenye maamuzi muhimu ya rasilimali zao rather than just the similar rhetorics we're acustomed to...The rhetorics which have proven to be failures!
 
Kama ukiweza kuniwekea bayana mapungufu ya sera za majimbo..Then weka hapa ili tujadili!
If its not perfect...We can still do something in oreder to perfect the imperfects!
Kama vile ambavyo tunavyotakiwa tufanye kwenye kuaply sera za kibepari VS zile za kisoshalisti..Cha muhimu ni kuangalia yale mazuri ya pande zote na kuyakumbatia!
Kuchanganya zile nzuri za capitalism na zile nzuri za socialism ili kuwa na perfect balance!
Kama unataka niwe specific nitakushukia data!
 
Sort of lakini with emphasis on development rather than just authorities!

Kama ni kweli kwamba sera hii ya majimbo itasababisha majimbo kuwa na political autonomy kwenye maamuzi muhimu ya maendeleo yao haswa yale yanayohusiana na uchumi na utumiaji wa maliasili zilizomo majimboni, basi kwa maoni yangu sera hii iko long-due kwa nchi yetu kwani itawezesha Wananchi ku-exploit nguvu ya ukabila kwa faida ya maendeleo yao binafsi bila ya serikali kuu kuingilia kati.
 
You can't seperate Development from Authorities in any form.

You can through chain of commands...Kumbuka kuna uwakilishi wa wananchi kwenye grassroot level ambayo ina connection fupi, smooth na efficient btn the central government and the regular citizens wakati wa implementation ya sera!Kunakuwa na smooth and substantiative chain of command ikiwa na malengo madhubuti ya kuwaanda wananchi kwa kila namna ili kuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kimaendeleo!
Kumbuka kuwa serikali kuu ina wajibu wa kuhakikisha kuwa sera za kimaendeleo zinatekelezwa kwa niaba ya wananchi kwa kupitia uwakilishi wa serikali zao za kimajimbo!
 
Kama ni kweli kwamba sera hii ya majimbo itasababisha majimbo kuwa na independent autonomy kwenye maamuzi muhimu ya maendeleo yao haswa yale yanayohusiana na uchumi na utumiaji wa maliasili zilizomo majimboni, basi kwa maoni yangu sera hii iko long-due kwa nchi yetu kwani itawezesha Wananchi ku-exploit nguvu ya ukabila kwa faida ya maendeleo yao binafsi bila ya serikali kuu kuingilia kati.

Inapokuja kwenye mamlaka ya majimbo..Sera za Taifa ni zilezile!
Majimbo yanakuwa ni uwezeshwaji wa wananchi kushiriki kikamilifu kwenye maendeleo ya Taifa lao!
 
Back
Top Bottom