CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

Huu mchakato walengwa ni kina nani? Je, hao ambao wanatakiwa kufanya huu mchakato wanaelewa malengo hasa au basi imekuwa babaisha bwege.

With all due respect majimbo yaliyo SA yaliwekwa ili kuimarisha utawala wa kibaguzi, Je, sisi tutakuwa tunaimarisha nini. Je, Tatizo la mikoa hivi sasa ni nini ukilinganisha na majimbo? Sifikirii hivi sasa ni wakati muafaka wa mchakato huu ukizingatia kwamba WTZ wengi hawashiriki kwa njia moja ama nyingine kutokana na kutokuwa na uhakika wa mafanikio ya sera hii ya majimbo.

Nafikiri CHADEMA wangeweka nguvu kubwa kuwaelimisha WTZ jinsi wanavyodhulumiwa nguvu zao rasilimali zao na MAFISADI wa CCM na kufanya regime change kama tulivyoona inavyoendelea sehemu nyingine duniani.
 
Mwafrika wa Kike,
Tafadhali dada yangu tafadhali.. muhimu kwanza ufahamu nini lengo la majimbo kisha kwa mtazamo huo huo ni muhimu kuelewa kile tulichokuwa nacho leo...

Kwanza ni lazima ufahamu kwamba majimbo na serikali zake huweka mipaka kwa sababu kila jimbo linataka ku control revenue na matumizi yake ikiwa ni pamoja na rasilimali zake..
Just think around that kisha jenga hoja inayopingana na mfumo uliopo..
Unaposema wananchi wa Buhemba wameachiwa nini zaidi ya mashimio haitokani na mfumo huu uliopo isipokuwa unatokana na watu kama kina Rostam ambao hata kama ungeweka majimbo wangekuwa viongozi wa majimbo hayo hayo na pengine angekuwa na power zaidi ya hii aliyokuwa nayo Kitaifa as to say A Premier.
Kwa hiyo Tatizo mnaloliona sasa hivi linatokana na baadhi ya watu ambao wamejengewa msingi bora wa kuiba na CCM kikatiba..ndio maana unaona watu kama Obama anaahidi changes jinsi Washington inavyofanya kazi zake na watu wanamwelewalakini akija na mpango wa kugawa nchi ama hata kuunganisha nchi hali tatizo kubwa hapa hali zao kimaisha.
Hivyo, itakuwa kazi kubwa kwa wananchi Wadanganyika kuweza ku connect dots kati ya majimbo na Uchumi ktk muda mfupi hivi, tena basi kwa bahati mbaya majimbo maskini ndiyo yenye watu wengi zaidi ikiwa ni Pamoja na dar es Salaam yenyewe.
Hivyo swala sio mfumo wa kitaifa kwa sababu nimeshasema kama nyiw Chadema mngekuwa madarakani kuna uwezekano mkubwa sehemu hiyo isingeachwa mashimo, pengine fungu lote la Loyalty lingekwenda kwao na serikali kuu ikaambulia hisa na kodi nyinginezo ambazo mngeweza kujenga barabara na madaraja ya kwenda hadi Kusini huko Ruvuma...
Tatizo letu kubwa sisi KIUCHUMI ni utawala uliopo. sasa basi bila kupoteza Muda nambie ni kitu gani ndani ya mfumo huu kinachochelewesha maendeleo ya sehemu nyingine maanake mtandao upo, fedha zinaweza toka BoT kwenda Buhemba siku moja hata kama bajeti imepangwa na Chadema...Kweli una imani Chadema wangeshindwa kuongoza chini ya mfumo huu uliopo?

Halafu kwa jinsi mnavyoizungumzia issue hii ni kama vile haya majimbo yatakuwa na full control ya uchumi wa sehemu zake bila kuzingatia kwamba kuna miradi mikubwa inayohusu Miundombinu, jimbo moja haliwezi kuimudu hata kama pato lao ni kubwa kiasi gani. Inahitajika credit ya Taifa kuvuta fedha za kujenga miundombinu kwa hiyo ni lazima kutakuwa na fungu kubwa likienda serikali kuu toka majimbo haya kuchangia huduma za kitaifa.
Kisha sielewi mpango wa ukusanyaji kodi utakuwa vipi ikiwa watu wanafanyiwa transfer kila siku toka Kaskazini kwenda Kusini, Mashariki na Magharibi hawa watu kodi zao zitawekwa ktk utaratibu gani wa majimbo yenye kujitawala kiuchumi?..
Kuna mambo mengi jamani hamjayaangalia kabisa kwa sababu huko South Afrika kwenyewe kuna majimbo yanatisha.. ni pori na duni kuliko hata Singida watu bado wanavaa ngozi za chui. Kenya ndio usiseme kabisa nenda kule juu mpakani na Sudan ama Somalia kunatisha.. yaani sioni kabisa huu mgawanyo wa umaskini unahitajika kwa sababu gani sasa hivi wakati ni muda wa kujitangaza kutafuta ushindi mwaka 2010. Guys hii ni agenda sifuli na tuiache ibakie hivyo hadi siku tutakapo fikia wakati wake sii leo wala kesho.. It stinks!.. ktk uchaguzi huu.
 
huo "utaifa" unaouengelea hapa umetusaidia nini so far? Wakazi wa Buhemba ambao wameachiwa mashimo kwenye migodi ya dhahabu iliyokombwa kifisadi na ccm wamefaidika nini na huo utaifa?

Hii nguvu ya pesa na dola ya serikali kuu ndio imetuletea umasikini huu wa kutisha na haijasaidia chochote kile zaidi ya kuwatajilisha kina Rostam, Manji na Mkapa.

Kama huoni umuhimu wa utaifa, you seriously need some help!
Hii sera ya majimbo ni mojawapo ya vitu vitakavyokifanya chama cha CHADEMA kizeekee kwenye upinzani.
 
Kama huoni umuhimu wa utaifa, you seriously need some help!
Hii sera ya majimbo ni mojawapo ya vitu vitakavyokifanya chama cha CHADEMA kizeekee kwenye upinzani.

mafisadi kama wewe mnadhani kuwa mtaongoza milele. Hii issue ya majimbo ni suluhisho la wizi unaofanywa na ccm kwa kuchukua pesa zote na kuziweka serikali kuu ili wazihamishie kwenye accounts za nje.

Utaifa gani wewe unaongelea hapa?
 
the fact that you are able to lable someone you dont know FISADI tells it all about your personality. You dont need any majimbo kama lengo ni kudhibiti mapato na matumizi.
Na kama unadhani ukitumia lugha kali utasitisha au kunyamazisha mawazo tofauti, then you are more than just wrong.
 
the fact that you are able to lable someone you dont know FISADI tells it all about your personality. You dont need any majimbo kama lengo ni kudhibiti mapato na matumizi.
Na kama unadhani ukitumia lugha kali utasitisha au kunyamazisha mawazo tofauti, then you are more than just wrong.

wewe ni fisadi tu na nitakuita kila mara nikikuona hapa maana watetezi wa mafisadi ni mafisadi tu
 
kwa hiyo kuchallenge sera ya majimbo ni kutetea mafisadi.sasa kama mnadhani sera hii haipaswi kuwa challenged kwa nini mnaileta kwenye forum?
 
kwa hiyo kuchallenge sera ya majimbo ni kutetea mafisadi.sasa kama mnadhani sera hii haipaswi kuwa challenged kwa nini mnaileta kwenye forum?

wewe ni fisadi tu na umetetea mafisadi hapa. Hujatoa challenge yoyote ya majimbo zaidi ya kulilia wizi na ufisadi wa mafisadi wa ccm kwa kutetea the status quo.

Kuna challenges kama za kina Mkandara na wengine hapa zinakubalika ila hizi zako za kifisadi ni ufisadi uliokithiri.
 
Hii sera msingi wake wa kifalsafa ni nini hasa? By the way, hii ni sera au ni mkakati wa kutekeleza sera? I am confused na ninahisi wananchi wa Kantalamba itakuwa zaidi!!

Binti Maria,
hii ni sera ambayo tangu imeanza kujadiliwa kwenye hii forum imewezekana kugundulika kuwa hakuna mkakati wowote wa kuitekeleza na sababu ya kutokuwepo kwa mkakati ni kwamba sera yenyewe haitekelezeki.
Viongozi wanakuja kutoa makala na hawataki kujibu maswali ya msingi,hii ni ishara ya nini? wanategemea kwenda kwa watu ambao hawatawauliza maswali magumu juu ya utekelezaji wa sera!!!
 
Mgaya,
Ndugu yangu acha kumtukana mtoa hoja.. jaribu kufikiria kwa faida ya wananchi... acha unazi mkuu.
Sasa wewe nambie, umeweka majimbo na CCM kachukua Utawala wa Majimbo na serikali kuu , haya majimbo yatamzuia kitu gani kuendelea kuchukua fedha hizo. Kisha hata mkijenga majimbo hiyo migodi ambayo mikataba imekwisha wekwa watapata kitu gani toka hiyo asilimia 1.1 ya ruzuku..Mnafikiria Majimbo as if uchaguzi ujao mmesha uchukua tayari jamani vipi nyie?

Nambie ni kitu gani ndani ya Majimbo kitabadilisha fedha hizi za taifa kutokwenda Hazina ama BoT na kwenda Buhemba moja kwa moja...Kisha hizo dhabhabu zitapellekwa nje kupitia wapi..
Je, Jimbo la Mashariki likitaka ushuru kwa kila Ounce ya dhahabu inayopita kusafirishwa na kila Kifaa kinachoingia mtasema nini maanake mnachotaka ni kila mtu abebe mzigo wake.. Hiyo dhahabu kama haina faida na Jimbo la Mashariki kwa nini wakubali kuingia utumwa wa babdarini hali haina manufaa kwao wala serikali kuu..

Mkuu kama alivyosema Zitto na J.J Mnyika hii ni agenda sifuri kwa hiyo usiubebeshe uzito zaidi ya kile kilicholetwa hapa. Ni lazima kuwepo mfumo mzito wa Kiuchumi Kitaifa na unahitaji muda mrefu kuandaa na kutazam kila pembe isije tokea kama tulivyofanya wakati wa Madaraka mikoani.. Mahindi ya Iringa yalikuwa yakizuiliwa kuingia Morogoro kuja Dar. Katika kila Mpaka wa mkoa kulikuwa na gate kali kuangalia kile kinachosafirishwa.. bahati mbaya ilikuwa wakati wa njaa kali na kuna sehemu mazao yaliozea shambani kwa sababu serikali ya mkoa hawakuwa na fedha za kujenga barabara nzuri, maghala na magari ya usafiri.
Hivyo sidhani kama mliweza kutazam kwa nini tulishindwa ktk mfumo wa madaraka mikoani kabla hamjaingia swal hili la Majimbo. tena basi binafsi nadhani itakuwa rahisi zaidi kama mkifikiria upya serikali za mikoa na mkatafuta makosa yaliyotendeka wakati ule kuyarekebisha.
Swala sii kuwa na viongozi karibu na wananchi?... Basi Mikoa hii tuliyokuwa nayo iwe ndio majimbo wachaguliwe hao Magavana kwa kura kuwaondoa hao Ma RC wawakilishi wa rais kisha tuone maendeleo yake...Kwa namna yoyote ile myttakavyo majimbo yaundwe bado mikoa itabakia kuwepo kwa jina tofauti tu Mwanza itabakia kuwa Mwanza na Bukoba Bukoba..kinachoongezeka hapa ni Kiungo kingine tu ambacho sioni umuhimu wake hata kidogo.
 
Mgaya,
Ndugu yangu acha kumtukana mtoa hoja.. jaribu kufikiria kwa faida ya wananchi... acha unazi mkuu.
Sasa wewe nambie, umeweka majimbo na CCM kachukua Utawala wa Majimbo na serikali kuu , hya majimbo yatamzuia kitu gani kuendelea kuchukua fedha hizo. Kisha hata mkijenga majimbo hiyo migodi ambayo mikataba imekwisha wekwa watapata kitu gani toka hiyo asilimia 1.1 ya ruzuku..
Nambie ni kitu gani ndani ya Majimbo kitabadilisha fedha hizi za taifa kutokwenda Hazina ama BoT na kwenda Buhemba moja kwa moja...Kisha hizo dhabhabu zitapellekwa nje kupitia wapi..
Je, Jimbo la Mashariki likitaka ushuru kwa kila Ounce ya dhahabu inayopita kusafirishwa na kila Kifaa kinachoingia mtasema nini maanake mnachotaka ni kila mtu abebe mzigo wake.. Hiyo dhahabu kama haina faida na Jimbo la Mashariki kwa nini wakubali kuingia utumwa wa babdarini hali haina manufaa kwao wala serikali kuu..

Mkuu kama alivyosema Zitto na J.J Mnyika hii ni agenda hewa ni lazima kuwepo mfumo mzito wa Kiuchumi Kitaifa na unahitaji muda mrefu kuandaa na kutazam kila pembe isije tokea kama tulivyofanya wakati wa Madaraka mikoani.. Mahindi ya Iringa yalikuwa yakizuiliwa kuingia Morogoro kuja Dar. Kila mkapa wa mkoa kulikuwa na gate kali kuangalia kile kinachosafirishwa.. bahati mbaya ilikuwa wakati wa njaa kali na kuna sehemu mazao yaliozea shambani kwa sababu serikali ya mkoa hawakuwa na fedha za kujenga barabara nzuri, maghala na magari ya usafiri.
Hivyo sidhani kama mliweza kutazam kwa nini tulishindwa ktk mfumo wa madaraka mikoani kabla hamjaingia swal hili la Majimbo. tena basi binafsi nadhani itakuwa rahisi zaidi kama mkifikiria upya serikali za mikoa na mkatafuta makosa yaliyotendeka wakati ule kuyarekebisha.
Swala sii kuwa na viongozi karibu na wananchi basi Mikoa hii tuliyokuwa nayo iwe ndio majimbo wachaguliwe Magavana kwa kura kuwaondoa hao Ma RC kisha tuone maendeleo yake...Kwa namna yoyote ile myttakavyo majimbo yaundwe bado mikoa itabakia kuwepo kwa jina tofauti tu Mwanza itabakia kuwa Mwanza na Bukoba Bukoba..kinachoongezeka hapa ni Kiungo kingine tu ambacho sioni umuhimu wake hata kidogo.

Labda nikuulize wewe swali,

Una suluhisho gani na suala la kubakiza sehemu kubwa ya mapato kwa wananchi kuliko kuzipeleka serikali kuu ambako zinaliwa na kina Mgonja?
 
Swali lingine la haraka,

kama nchi zilizoendelea zote zina mfumo wenye kuzipa nguvu kubwa serikali za mitaa, kwa nini Tanzania isifanye hivyo?
 
Kwanza,
Kinachopeleka fedha kwa wananchi ni sera na mrengo wa chama, sio mfumo wa Kitaifa Kiutawala ndio maana kuna uchaguzi.. Mfumo wa kiutawala huwa upo siku zote kinachotakiwa ni mbinu ya kila chama kuwahakikishia wananchi kuwa sisi kwa sera zetu tutafikisha fedha hizo kwa kufuata mkondo uliopo. Kama hakuna mkondo sijui utauza sera yako vipi!.
Kwa hiyo haipotoshi kitu fedha kwenda serikali kuu ama ndogo ya Majimbo muhimu ni kuhakikisha fedha hizo zinafika kwa walengwa. Na hakika kuwepo kwa serikali za mitaa ndio sababu kubwa hata CCM leo wanazo hizo serekali za Mitaa sio majimbo. Nchi unazozitaja zingekuwa na serikali za mitaa hata kama wasingekuwa na Majimbo kwa sababu majimbo yao yaliunganishwa kuunda nguvu ya kiutawala.. Major threat ya Marekani ilikuwa Ukubwa wa nchi, sawa na nchi zote za Ulaya ambazo ukubwa wa nchi ndio uliunda taifa lenye nguvu.. Ndio maana kina Hitler walijaribu kushika dunia nzima, Japan kuvamia China na kadhalika.. Kwa hiyo hayo majimbo hayakupatikana kwa sababu za kiuchumi hata kidogo.. Hawa wazungu walipokuja kwetu walikuja kutugawa mafungu lakini kwao waliunganisha nchi na kuziita majimbo kuunda kitu kimoja kikubwa...Kwa mfano Muungano wetu na Zanzibar ndio ulitakiwa kuwekwa ktk majimbo mawili Tangannyika na Zanzibar..
Nadhani nimekujibu maswali yako yote kwa wakati mmoja...Naomba nijibu yangu pia.
 
Hamuna huruma nyinyi watu kumusubiri mwenzenu apewe heshima za mwisho
 
Mkandara,

Kama Watanzania hawatakuwa na nia, utashi na shauku ya kuwa na mabadiliko na kutaka uadilifu na uwajibikaji, hata ukileta na kuunda Temi na falme ndogo ndogo, bado matatizo yatakuwa pale pale.

Jukumu la kwanza kwa Mwananchi kudai haki zake na hata kuhoji pato lake kutokana na jasho lake ni kwa mwakilishi wake katika Serikali, Mbunge.

Je ni jamii, wilaya ngapi ambazo zimedai kwa nguvu kutoka kwa Wabunge wao mgao wa mapato au kuhoji ni kwa nini hawana barabara, maji safi, umeme, shule, hospitali au vyuo?

Ikiwa chaguzi zetu ni kila miaka mitano na mgombea ambaye hutwaa Ubunge hutoa ahadi, je ni lini wananchi wamemshupalia Mbunge wao kudai ahadi zitimizwe? Kuna wengine watadai kisa cha Makwetta, Mzindakaya au Kimitti kuendelea kuwa Wabunge mithili ya kuwa Wabunge wa maisha na kudumu ni kutokana na wananchi kuwa masikini na kukubali kuhongwa.

Sasa swali linakuja, katika miaka 13 ya mfumo mpya wa vyama pamoja na Utamu wa CCM, vyama vya upinzani vimefanya kazi gani kwa umoja kuvunja dhana mbovu ya wananchi kuridhika na Tisheti, Khanga na Ubwabwa na kuendelea kuchagua wawakilishi wabovu?

Narudia tena matatizo makuu yanayosababisha kukwama na kuzorota kwa maendeleo ya Tanzania si mfumo wa utendaji bali ni Udhaifu mkubwa wa Uongozi na Unyonge wa Mtanzania kudai kwa nguvu haki yake bila woga au kuonea aibu.

Kama matatizo haya mawili hayatasawazishwa, kamwe hatutakuwa na uwezo wa kuwa na Maendeleo muafaka kwa Wananchi wa Taifa letu.

La mwisho, sisi tumepata fursa kubwa sana kushiriki katika mchakato wa kulijenga Taifa letu upya. Safari hii inaambatana na kutaka Uadilifu, Uwajibikaji, Ufanisi,Juhudi, Maarifa, Mipango Bora, Haki, Utu, Unyenyekevu Umakini na Uungwana. Haya matakwa si kwa ajili ya viongozi na wanasiasa pekee, ni jukumu letu sote kama kweli tuna nia ya kujenga Taifa imara, lenye uwezo wa kujitegemea na kuushinda Umasikini, Ujinga na Maradhi.

Wengi wetu hapa tuko kwenye safari moja ingawa vipawa, uwezo, maoni na mawazo yetu yanatofautiana. Hilo ni jambo la kawaida kwa jamii.

Kinachosikitisha nami nitakuwa wa kwanza kukiri, ni kule kuwa na unazi wa kuona tusipokubaliana hoja, basi wewe hufai au si mwenzetu. Kukashifiana kuwa fulani ni Fisadi kwa kuwa kahoji mantiki ya jambo, au kuambiwa kuwa ni Kibaraka wa Kikwete au CCM , tumelewa ujamaa, out of touch, mabepari uchwara na kadhalika si sahihi.

Kuna baadhi yetu ambao tunaamini Upinzani ukijengwa vizuri na kwa makini, basi CCM watajifunza na hata kujirekebisha. Kuna wengine wetu tunaamini kuwa CCM ni mama lao na hakuna mwingine kama CCM.

Sasa tukae meza moja hapa ndani katika Jamii na tufundishane pamoja na tofauti zetu za kiitikadi na falsafa kwa kuheshimiana na nia madhubuti ya kusikilizana.

Nawapa Zitto, Mnyika na Kitila ambao wako Chadema jikoni pongezi kwa unyenyekevu wao na busara za kusikiliza kauli zetu na kuzichukua kwa moyo mkunjufu na si kubeza kuwa tunaohoji hatujui tunalolizungumza.

Nawatakia Chadema kila la heri katika safari yao. Mlango wangu wote Zitto, Mnyika na Kitila mnaujua uko wazi. Tuendelee na majadiliano kama tulivyoanza kule kwenye focus 2010 na Chadema must reform.
 
Maswali mazuri sana mwanakijiji

http://www.info.gov.za/documents/constitution/index.htm.

Kimsingi majimbo yetu kutokana na historia ya nchi yetu yapasa kufuata mfumo wa Afrika Kusini. Afrika Kusini ni Unitary Republic (sio federal aina ya Canada au US au Germany) Lakini ina majimbo yanayojiendesha.

Hii ni rasimu, tunaomba maoni yenu. Mtaona kuwa kuwa makosa madogo madogo kama nafasi ya Zanzibar na hata mkoa wa Ruvuma kusahaulika. Ni rasimu sifuri ili kupata maoni ya watanzania.

Suala hili linahitaji katiba mpya kabisa.

Kwani kwenye uchaguzi mkuu uliopita mlikuwa na mikakati gani wakati mnainadi sera hii ya majimbo ambayo mpaka sasa mnakiri kuwa bado ni rasimu?

Ina maana mlingoja kwanza kuingia ikulu ndio mjifunze jinsi mtakavyoweza kuifanya sera hii iwe kamili!!!
 
Back
Top Bottom