CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

CHADEMA yaiiga ODM kuhusu Sera ya Majimbo

Hii imetulia sana, na kama itapata support ya kutosha huu utakuwa mwanzo mzuri kuelekea mageuzi ya kweli ya kidemokrasia Tanzania. Kila la kheri na tunaomba zoezi hilo lifanyike kwa uwazi wa hali ya juu sana kuondoa minong'ono baadae.
 
Nimepitia habari za Kenya na Tanzania kuhusu sera ya majimbo, nimegundua kwamba CHADEMA wanaiiga ODM kuhusu sera hiyo. Ushahidi wa suala hilo ni kwa kulinganisha maelezo ya kiongozi wa ODM wa Kajiado North yanayopatikana kwa kubonyeza hapa: MAJIMBO POLICY IN KENYA (FEDERALISM IN KENYA) , Dan Ochieng' Obunga na yale ya kiongozi wa CHADEMA yanayopatikana hapa: 'Sera ya majimbo' ni siri ya maisha bora kwa kila Mtanzania na hapa: 'Sera ya majimbo' ni siri ya maisha bora kwa kila Mtanzania

Vyama hivi viwili vimeigana sera zao karibu neno kwa neno. Haiwezekani maelezo ya mtu mmoja wa kona moja ya Afrika Mashariki yakafanana na mtu wa kona nyingine

Kwa mtindo, vyama hivi vinafaa kweli kuongoza nchi zao kuelekea Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki?

.....ndiyohiyo
 
Sera ya majimbo sio ngeni ndugu yangu! USA, canada..etc wanasera za majimbo!
 
Sera ya majimbo sio ngeni ndugu yangu! USA, canada..etc wanasera za majimbo!

Tatizo sio sera tu kwa ujumla. Tatizo hapa ni kuwa CHADEMA imenukuu neno kwa neno kutoka ODM. Ni copy and paste ambayo ni plagarism! Kwa hiyo hata kwenye kuongoza nchi watafanya copy and paste ndani ya jumuia ya Afrika Mashariki


......ndiyohiyo
 
Leta ushahidi halisi! kwa maswali ya haraka haraka! Kwanini unafikiri kwamba chadema wamegeza ODM na sio ODM kugeza chedema? Nikisoma taafira yako naona imeandikwa Monday, October 08, 2007, nilipoangalia mtandao nagundua Bwana mbowe aliongelea majimbo policy 2005-10-17. Mbowe defends ’majimbo’ policy

Inawezekana kabisa mtandao unanidanganya, kwahiyo wewe nipe huo ushahidi wako wa word to word, pia nipatia tarehe za maandiko hayo. Halafu ndio tufuate swala la hoja yako ya madhara ya kuigilizia!
 
Leta ushahidi halisi! kwa maswali ya haraka haraka! Kwanini unafikiri kwamba chadema wamegeza ODM na sio ODM kugeza chedema? Nikisoma taafira yako naona imeandikwa Monday, October 08, 2007, nilipoangalia mtandao nagundua Bwana mbowe aliongelea majimbo policy 2005-10-17. Mbowe defends 'majimbo' policy

Inawezekana kabisa mtandao unanidanganya, kwahiyo wewe nipe huo ushahidi wako wa word to word, pia nipatia tarehe za maandiko hayo. Halafu ndio tufuate swala la hoja yako ya madhara ya kuigilizia!

Ushahidi

Soma maelezo haya ya ODM:

MAJIMBO POLICY IN KENYA (FEDERALISM IN KENYA)

Sera ya majimbo' ni siri ya maisha bora kwa kila Mkenya
Monday, October 08, 2007
Daniel Ochieng' Obunga (Kitengela, Nairobi)
danobunga at yahoo dot com – 0725-408720

Sera hii ya majimbo ni swala nyeti sana wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka huu 2007 kwa vijembe vya majukwaani.

Hoja kuu ya kufahamu ni kwamba chimbuko la sera ya majimbo nchini ni falsafa ya ODM ya nguvu ya umma, shirikisho pia iliunga mkono sera hii.

Kwani umma ndio unapaswa kuwa na mamlaka lakini pia umma ndio unapaswa kunufaika na rasilimali za nchi.

Majimbo ni moja kati ya sera za chama cha ODM nchini Kenya ambacho kitapewa kipaumbele.

Jinsi vigogo vya chama walivyo ongea siku ya jumamosi Uhuru park Kuzindua kampeni ya Urais Mheshimiwa Raila Odinga, waligusia zera muhimu ni ya Majimbo, na mheshimiwa Wiliam Ruto Pia aliongelea hapo awali kinaganaga kwenya radio kuhusu sera ya majimbo.

Wananchi wanataka mfumo mpya wa utawala. ODM waliongelea masuala matatu, kwanza, uongozi mpya kwa maana ya wananchi kuwaondoa viongozi walioko madarakani kwa maana wameshiriki ufisadi wa nyuma, hivyo hawawezi kufanya mabadiliko yoyote ya maana.

Pili; kusafisha mfumo wa utawala kwa maana ya kupambana na rushwa na ufisadi, na tatu, kutengeneza muundo mpya wa utawala ikiwamo kuanzisha muundo wa majimbo.

Lakini kwa kuwa suala la majimbo lilipata ladha zaidi na mashambulizi mengi yanatoka kwa wapinzani wetu, wakenya wengechagua chama cha ODM ili sera hii ya majimbo lipewewe jaribio katika taifa letu pia,

Suala la sera ya majimbo ni suala la kikatiba. Chama chochote cha siasa kinauza kwa wananchi matakwa yake kama kikipewa ridhaa na wananchi.

Matakwa hayo yanaweza kutokana na misingi ya chama husika ama matakwa ya wananchi ama matakwa ya viongozi wa chama husika.

suala la kuundwa kwa majimbo ni suala la mabadiliko ya katiba hivyo kwa vyovyote vile ODM itabadilisha katiba kwa haraka sana wakati watakapochukua utawal mwacka ujao.

Maelezo yanaendelea ukibonyeza hapa: MAJIMBO POLICY IN KENYA (FEDERALISM IN KENYA) , Dan Ochieng' Obunga

Halafu Soma maelezo haya ya CHADEMA:


14 Machi 2007

'Sera ya majimbo' ni siri ya maisha bora kwa kila Mtanzania

na John Mnyika

HIVI karibuni pameanza kujitokeza tena mjadala kuhusu ‘majimbo' na masuala kadhaa yameibuliwa.


Huu ni wakati mwafaka nami nichangie hoja kadhaa katika mjadala huu muhimu.


Nikumbushe tu kwamba mjadala huu ulishika kasi sana wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 kwa vijembe vya majukwaani.


Hoja kuu ya kufahamu ni kwamba chimbuko la sera ya majimbo nchini ni falsafa ya CHADEMA ya nguvu ya umma.


Kwani umma ndio unapaswa kuwa na mamlaka lakini pia umma ndio unapaswa kunufaika na rasilimali za nchi.


Niweke pia bayana kwamba katika uchaguzi CHADEMA haikuwa na ajenda ya majimbo kama ajenda inayosimama peke yake. Ilikuwa ni sehemu ya ajenda nyingine.


Tulisema wazi kwamba tatizo la CCM ni kwamba huwa inakuja na ilani ya kuahidi kila kitu na hatimaye kutofanya chochote.


Sisi tulisema pamoja na kuwa na sera nyingi lakini tutakuwa na vipaumbele vitano tu:


Mosi, mfumo mpya wa utawala, pili; elimu, tatu, kilimo, nne, uchumi, tano, afya. Na hata katika vipaumbele hivi bado tulichagua maeneo machache mahususi.


Mathalani katika uchumi tulilenga kodi (kupunguza ukubwa wa kodi na kuhakikisha kuwa kodi zinakusanywa ipasavyo).


Ajira na rasilimali hususan madini katika mfumo mpya wa utawala.


Hapa tulikuwa na masuala matatu, kwanza, uongozi mpya kwa maana ya wananchi kuwaondoa viongozi walioko madarakani kwa maana wameshiriki ufisadi wa nyuma, hivyo hawawezi kufanya mabadiliko yoyote ya maana.


Pili; kusafisha mfumo wa utawala kwa maana ya kupambana na rushwa na ufisadi, na tatu, kutengeneza muundo mpya wa utawala ikiwamo kuanzisha muundo wa majimbo.


Lakini kwa kuwa suala la majimbo lilipata ladha zaidi na mashambulizi mengi; sera, ajenda, maana ya mfumo mpya wa utawala ikafunikwa kabisa.


Sina nia ya kujadili katika makala ya leo kwa nini hali hii ilijitokeza.


Kwa kuwa wengi wamezoea kutumia jina ‘Sera ya majimbo' nami katika mjadala huu nitatumia jina hili ili twende pamoja.


Suala la sera ya majimbo ni suala la kikatiba. Chama chochote cha siasa kinauza kwa wananchi matakwa yake kama kikipewa ridhaa na wananchi.


Matakwa hayo yanaweza kutokana na misingi ya chama husika ama matakwa ya wananchi ama matakwa ya viongozi wa chama husika.


Lakini baada ya uchaguzi zipo sera ambazo utekelezaji wake lazima urudi tena kwa wananchi kupata ridhaa ya pamoja, mathalani CCM wamejikuta suala la mahakama ya kadhi linapaswa kurudi kwa wananchi, ingawa liko katika ilani ya chama chao.


Lakini mambo mengi ya chama hutekelezwa kwa kwenda kwa wawakilishi wa wananchi yaani Bunge.


Kadhalika, suala la kuundwa kwa majimbo ni suala la mabadiliko ya katiba hivyo kwa vyovyote vile CHADEMA ingepaswa kurudi kwa wananchi.

Maelezo hayo yanaendelea ukibonyeza hapa: http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_18.html


HUONI KWAMBA MAELEZO YAO YANAFANANA? Sasa unadhani kati ya Mbowe na Raila Odinga nani ni mkongwe katika siasa? Nani ameanza kuzungumzia majimbo? ndio maana nasema CHADEMA wameiga toka ODM

.....ndiyohiyo
 
Tatizo sio sera tu kwa ujumla. Tatizo hapa ni kuwa CHADEMA imenukuu neno kwa neno kutoka ODM. Ni copy and paste ambayo ni plagarism! Kwa hiyo hata kwenye kuongoza nchi watafanya copy and paste ndani ya jumuia ya Afrika Mashariki


......ndiyohiyo

Una uhakika gani kuwa CHADEMA ndio waliocopy na sio ODM? CHADEMA ilikuwepo kabla ya ODM.

Lakini pia yakupasa kujua kuwa tunakwenda shule na kujifunza kwa wengine, hii ndiyo iliyomfanya binadamu kuweza kutoka hatua moja kwenda nyingine!

Wewe hapa ungejadili sera yenyewe kuwa inaweza kuisaidia vipi Tanzania kwenda mbele au inaweza kuirudisha vipi nyuma.

Mimi niliona kama umeleta habari mpya kumbe hakuna lolote...
 
Nimesoma makala zote mbili vizuri. Ni hakika kunakushabihana kwa sera zao na chimbuko lake. Lakini nakupinga kabisa unaposema

Vyama hivi viwili vimeigana sera zao karibu neno kwa neno
.

Makala ziko wazi kwamba waandishi hawajaigiziana karibu kila neno, ila kunabaadhi za sentensi kama nne hivi zimerandana nazo ni

"Hoja kuu ya kufahamu ni kwamba chimbuko la sera ya majimbo nchini ni falsafa ya ODM ya nguvu ya umma, shirikisho pia iliunga mkono sera hii."

"Kwani umma ndio unapaswa kuwa na mamlaka lakini pia umma ndio unapaswa kunufaika na rasilimali za nchi."

"Suala la sera ya majimbo ni suala la kikatiba. Chama chochote cha siasa kinauza kwa wananchi matakwa yake kama kikipewa ridhaa na wananchi."

Pili umekosea unaposema Chadema wemeiga ODM, kwani makala ya Bwana Mnyika imetoka 14 Machi 2007 na makala ya Daniel wa ODM imetoka October 08, 2007. Sasa hapa nani kamuiga mwenzie. Pia soma makala ya mbowe ya 2005.

Sijui mambo ya chadema kwa kina wala ya ODM, lakini taarifa unazozileta hiziko sahihi. Labda kama kunanyeti zingine kuhakiki kashifa zilete.

Kwa mtindo, vyama hivi vinafaa kweli kuongoza nchi zao kuelekea Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki?
Tatu, sidhani kama ni jambo la ajabu vyama kufuata sera zinazoshabiana - soma maandiko ya socialism pia anangalia mfumo wa demokrasi we miaka ya tisini, karibuni afrika nzima maandiko yake yanafana! Sioni cha achabu kama sera zao zitarandana, ila hoja ya msingi, je CHADEMA ilifanya utafiti wa kina, iwe imeiga sera ama imeanzisha sera, kutafakari mfumo wa majimbo utaleta faida gani!
 
Nimesoma makala zote mbili vizuri. Ni hakika kunakushabihana kwa sera zao na chimbuko lake. Lakini nakupinga kabisa unaposema

.

Makala ziko wazi kwamba waandishi hawajaigiziana karibu kila neno, ila kunabaadhi za sentensi kama nne hivi zimerandana nazo ni

"Hoja kuu ya kufahamu ni kwamba chimbuko la sera ya majimbo nchini ni falsafa ya ODM ya nguvu ya umma, shirikisho pia iliunga mkono sera hii."

"Kwani umma ndio unapaswa kuwa na mamlaka lakini pia umma ndio unapaswa kunufaika na rasilimali za nchi."

"Suala la sera ya majimbo ni suala la kikatiba. Chama chochote cha siasa kinauza kwa wananchi matakwa yake kama kikipewa ridhaa na wananchi."

Pili umekosea unaposema Chadema wemeiga ODM, kwani makala ya Bwana Mnyika imetoka 14 Machi 2007 na makala ya Daniel wa ODM imetoka October 08, 2007. Sasa hapa nani kamuiga mwenzie. Pia soma makala ya mbowe ya 2005.

Sijui mambo ya chadema kwa kina wala ya ODM, lakini taarifa unazozileta hiziko sahihi. Labda kama kunanyeti zingine kuhakiki kashifa zilete.

Kwa mtindo, vyama hivi vinafaa kweli kuongoza nchi zao kuelekea Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki?
Tatu, sidhani kama ni jambo la ajabu vyama kufuata sera zinazoshabiana - soma maandiko ya socialism pia anangalia mfumo wa demokrasi we miaka ya tisini, karibuni afrika nzima maandiko yake yanafana! Sioni cha achabu kama sera zao zitarandana, ila hoja ya msingi, je CHADEMA ilifanya utafiti wa kina, iwe imeiga sera ama imeanzisha sera, kutafakari mfumo wa majimbo utaleta faida gani!

Sio sentensi nne tu, hebu soma makala zote mbili mwanzo mpaka mwisho. Ingia kwenye hizo links nilizotoa. Maelezo yao yanafanana kwa zaidi ya sentensi 20 neno kwa neno. Inabadilika tu, kwenye ODM hao CHADEMA wameweka CHADEMA lakini maelezo mengine yanafanana kabisa kabisa. Haiwezekani vyama viwili vya nchi mbili tofauti vikafikiria sawa neno kwa neno. Lazima CHADEMA itakuwa imeiga toka kwa ODM

........ndiyohiyo
 
Sio sentensi nne tu, hebu soma makala zote mbili mwanzo mpaka mwisho. Ingia kwenye hizo links nilizotoa. Maelezo yao yanafanana kwa zaidi ya sentensi 20 neno kwa neno. Inabadilika tu, kwenye ODM hao CHADEMA wameweka CHADEMA lakini maelezo mengine yanafanana kabisa kabisa. Haiwezekani vyama viwili vya nchi mbili tofauti vikafikiria sawa neno kwa neno. Lazima CHADEMA itakuwa imeiga toka kwa ODM

Ngoja nikubaliana na wewe kwamba ni neno kwa neno. Hoja yangu ni kwamba swala lako la mwanzo kwamba CHADEMA wameiga ODM sio sahihi kufuatia ushahidi ulioufikisha hapa, hebu rudi usome ulichoandika na ushahidi wako utagundua ushahidi wako unapinga hoja yako. Kwa misingi hiyo basi, hoja yako haina mantiki.
 
Nimepitia habari za Kenya na Tanzania kuhusu sera ya majimbo, nimegundua kwamba CHADEMA wanaiiga ODM kuhusu sera hiyo. Ushahidi wa suala hilo ni kwa kulinganisha maelezo ya kiongozi wa ODM wa Kajiado North yanayopatikana kwa kubonyeza hapa: MAJIMBO POLICY IN KENYA (FEDERALISM IN KENYA) , Dan Ochieng' Obunga na yale ya kiongozi wa CHADEMA yanayopatikana hapa: 'Sera ya majimbo' ni siri ya maisha bora kwa kila Mtanzania na hapa: 'Sera ya majimbo' ni siri ya maisha bora kwa kila Mtanzania

Vyama hivi viwili vimeigana sera zao karibu neno kwa neno. Haiwezekani maelezo ya mtu mmoja wa kona moja ya Afrika Mashariki yakafanana na mtu wa kona nyingine

Kwa mtindo, vyama hivi vinafaa kweli kuongoza nchi zao kuelekea Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki?

.....ndiyohiyo

Mzeekuna mambo ya msingi umeulizwa kuwa , kwa nini unafikiri CHADEMA, WAMEDESA KWA ODM, na sio ODM wamedesa kwa CHADEMA?? sijoana jibu naona unaruka ruka, otherwise badili title!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwa umri CHADEMA ni chama cha siku nyingi kuliko ODM na kilikuwa na sera hiyo ya majimbo tangu mwanzo wake. Sasa inakuwaje CHADEMA kiwe ndicho kilinakili sera ya chama ambacho hakikuwepo? Labda mtu aliye na chuki binafsi na CHADEMA atakisingizia chama hicho mambo yasiyo kweli ili tu kujifurahisha nafsi yake.
 
What's your point? Mbona umeng'ang'ania tu kuwa ndio CHADEMA wameplagiarize bila kujibu maswali muhimu?
 
Sera ya majimbo Chadema wamekuja nayo Bcstimes toka mwaka 2003 na wakati huo tumebishana sana hadi kufikia uchaguzi wa mwaka 2005.
Hata kwa mwenye kutumia nakala hizi kufikiria zipo wazi nani kamkopi mwenzake. Maelezo ya J.J Mnyika yamechapishwa March 2007 wakati huyo Ocheing umechapishwa October 2007..Zaidi ya sii ODM wala Chadema wamedai kwamba wao ndio Wabunifu wa mfumo huu wa Utawala..
 
Hii sera ya majimbo ni empty suit, nimeshaongelea kila mara kwamba CHADEMA wanaitaji kuja na idea nyingine inayoendana na Uchumi wa Tanzania.

Until watakapo mfukuza Mbowe ndio tutaona mchakato mzima wa CHADEMA. I believe CHADEMA contains very smart individuals, but Mbowe hinder the potential within that party. Mnyika and other fellows can come up with something better than sera ya majimbo. Tatizo la sera ya majimbo ni spending, and Tanzania doesn't have enough resource to back that up. Nigeria wanafanya lakini sababu wana resources kubwa, likewise USA and Canada. Tanzania hatuna uwezo, tuta end kuwa na Big government and Big spending. I know mnaweza kusema kwamba labda kila majimbo yata utilize resource zake na kujiendesha lakini ukweli ni kwamba Tanzania economy depends on subsidy kupita kiasi.

CHADEMA wanatakiwa kukaa chini na smart THINK TANKERS wakapewa the good package ambayo haitakuwa based on political ideaology, but scientific facts. Until then Majimbo will not work in Tanzania, ni bora tuendeleee na hihi system iliyooza ya sasa ambayo JK anaamisha takataka Mwanza analeta Dar na za Dar anapeleka KIGOMA
 
ODM na CHADEMA wataweza kuungana mara Afrika Mashariki itakapokuwa taifa moja. Ni furaha kuona wanafanana kisiasa tayari, na labda hata wanachangiana mawazo.

Ni vema Mikoa ipewe UHURU wa kujiamulia mambo yao wenyewe. Kama hiyo ni "MAJIMBO" then so be it.


<FONT face="Times New Roman"><FONT size=3>Nchi yetu haiendelei kwa sababu%2
 
ODM (orange) ilianzishwa lini?
CHADEMA ilianzishwa lini?
Je CHADEMA ilipoanzishwa tayari ilikua na sera ya majimbo?
Sera hiyo ilidokumentiwa(kuwekwa kwenye maandishi) lini?
Watu wa CHADEMA wakija hapa wakatujibu maswali haya itasaidia kujua nani alimnakiri mwingine! mbali na hapo ushahidi uliotolewa mpaka sasa haujitoshelezi..!
 
Hii sera ya majimbo ni empty suit, nimeshaongelea kila mara kwamba CHADEMA wanaitaji kuja na idea nyingine inayoendana na Uchumi wa Tanzania.

Until watakapo mfukuza Mbowe ndio tutaona mchakato mzima wa CHADEMA. I believe CHADEMA contains very smart individuals, but Mbowe hinder the potential within that party. Mnyika and other fellows can come up with something better than sera ya majimbo. Tatizo la sera ya majimbo ni spending, and Tanzania doesn't have enough resource to back that up. Nigeria wanafanya lakini sababu wana resources kubwa, likewise USA and Canada. Tanzania hatuna uwezo, tuta end kuwa na Big government and Big spending. I know mnaweza kusema kwamba labda kila majimbo yata utilize resource zake na kujiendesha lakini ukweli ni kwamba Tanzania economy depends on subsidy kupita kiasi.

CHADEMA wanatakiwa kukaa chini na smart THINK TANKERS wakapewa the good package ambayo haitakuwa based on political ideaology, but scientific facts. Until then Majimbo will not work in Tanzania, ni bora tuendeleee na hihi system iliyooza ya sasa ambayo JK anaamisha takataka Mwanza analeta Dar na za Dar anapeleka KIGOMA

Mdanganyika

Mbona una hasira hivyo na Mbowe wangu jamani? Amekukosea nini? Kuhusu sera hii ya majimbo si aulizwe Profesa Baregu ambae ndio wakati wa uchaguzi alifanya mkutano na waandishi wa habari kuielezea hii sera?

Halafu unasema tatizo ni gharama. Hebu tueleze kivipi. Mi nanavyujua sera hii ya majimbo itapunguza gharama kwa kuwa:

Mfano wa kwanza;Badala ya kuwa na watu wawili kwenye mikoa na manispaa, utakuwa na mtu mmoja. Sasa kama huko DSM unakuta kuna mkuu wa mkoa wa kuteuliwa na kuna meya wa jiji wa kuchaguliwa na madiwani. Halafu huko manispaa kuna mkuu wa wilaya wa kuteuliwa, kuna mkurugenzi wa kuteuliwa halafu kuna meya wa kuchaguliwa na madiwani. Sera ya majimbo ina mmoja tu, meya wa kuchaguliwa na wananchi wenyewe

Mfano wa pili; badala ya kuwa na wizara zote kwenye serikali kuu na mawaziri hao kuwajibika kuzunguka na kufanya kazi nchi nzima. Serikali kuu inakuwa na wizara chache tu, mathalani mambo ya nje, ulinzi na nyingine chache tu. Wizara nyingine zinakuwa kwenye majimbo yake. Kwa hiyo mzunguko unapungua. Waziri akitoka DSM kwenda Mwanza na kiongozi wa pale pale Mwanza nani atatumia gharama kubwa?

Wewe unajua sasa ni mabilioni mangapi yanapotea hivi sasa kwa kila kitu kuletwa kufanyiwa hapa DSM badala ya kumalizikia kwenye mikoa yao ama maeneo yao? Kuanzia masuala ya hati za ardhi nk!. Sasa ukitaka kujua kwamba ni mzigo, ona sasa hata mahakama, TRA, Polisi wote waanza kufungua ofisi za kanda na kuzipa baadhi ya mamlaka. Sasa badala ya kuanza kuitekeleza hii sera ovyo ovyo kwanini serikali isikiri tu kwamba mfumo bora wa utawala kwa nchi kama Tanzania ni majimbo?

Asha
 
Haijalishi kwamba ni ya ODM au ya CHADEMA au ya CCM, sera ya majimbo ni jibu la maswali yote ya kiutawala. Na nasema nitaitetea sera hii kwa moyo wangu wote, kwa roho yangu yote na kwa akili zangu zote.

Viva sera ya majimbo

SM
 
Back
Top Bottom