CHADEMA yaicharaza CCM Bumbuli, Tanga

CHADEMA yaicharaza CCM Bumbuli, Tanga

Hongera Makamba, zimefika kwake wala msijali atakishughulikia hiki chama cha magaidi watanzania wakikwepe kama ukoma.
 
Tabora pia bado wamelala wanahitaji kuamshwa

Muulize Sikonge akwambie habari iliyojiri huko Sikonge mwaka jana huko Sikonge. CCM hawakuamini! Haya yanajiri sasa na mikakati ya kuifuta CDM yanasababishwa na jinsi wanavyopelekeshwa ktk kila uchaguzi mdogo.
 
BAADA ya hila na mbinu haramu kadhaa kuzuia uchaguzi huru na haki, kuminya demokrasia ya sanduku la kura kuchukua mkondo wake, ikiwemo Mtendaji wa Kijiji cha Kwekitui kuharibu uchaguzi kwa kukimbia na sanduku la kura wiki iliyopita, CHADEMA imeibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa kijiji hicho, kilichoko Jimbo la Bumbuli, wilayani Lushoto, Mkoa wa Tanga, kwa kura 196 dhidi ya CCM waliopata kura kura 189.

Uchaguzi huo wa marudio ulifanyika leo, Jumapili, Aprili 7, 2013.

Hongera za kipekee ziwafikie makamanda wa kijijini hapo, Jimbo la Bumbuli, Wilaya ya Lushoto, Mkoa wa Tanga, chini ya usimamizi wa Kanda ya Kaskazini. Ndiyo waliopigana na kupiganisha 'vita' hiyo.

Kanda ya Kaskazini kwa kweli inaendelea ku-take off vizuri ambapo uchaguzi wa marudio wa vijini na vitongoji huko Lushoto umekuwa na moja ya majaribio na wameonesha uwezo na mfano wa namna decentralization inavyoweza kufanya kazi nzuri kabisa, bila kusubiri Makao Makuu hata kwa vitu ambavyo vingeweza kufanywa na vipaji vingi vilivyoko ngazi za chini ambavyo CHADEMA ilikuwa haijawahi kuvitumia kwa kiwango kikubwa.

We hopefully look forward kwa kanda zingine kuja kwa kasi zaidi. Ushindani huleta ufanisi. Hili ni moja ya jambo la msingi sana katika dhana hii.

Ufanisi huu, hautakuwa kwenye kushinda uchaguzi pekee. Tutarajie kuona mengi to keep the fire burning.

kudos makamanda wa ardhini kwa kazi nzuri mwanzo wa ngoma ni lele ushindii huu uwe chachu katika chaguzi nyingine
 
Ndio tatizo lenu. Mkipongezwa kosa, msipopongezwa kosa. Lami ikijengwa kosa, isipojengwa kosa. Mshahara ukiongezwa kosa, usipoongezwa kosa. Washutumiwa wakikamatwa kosa wasipokamatwa kosa. Rais akiongea kosa, asipoongea kosa.

Ili mradi tu mlalamike...

Lakini watu kama nyinyi kwenye jamii hamkosekani, TUMESHAWAZOEA...

kila jambo linamwisho.
 
Pongezi za dhati sana zimuendee kamanda Mbelwa Germano na uongozi mzima wa Lushoto na Bumbuli.
Kazi yenu inaonekana muhimu ni kuzidi kupambana na hawa maccm.
 
Last edited by a moderator:



....tumechakaza na tunaendelea kuchakaza ....stay tuned...!!!
 
Sipati picha mtu mzima anatimua mbio na sanduku la kura.....hatareee, hongereni sana makamanda haikuwa kazi rahisi.:rockon:

huku anaangalia nyuma kama fisi aliyezubaa kwenye mzoga kukakucha pata picha raia wanamkurupua atakavochomoka.
 
Good Starter, Better Progress and Best Ending.
CHADEMA mmeanza vizuri, mnasonga mbele kwa kujiamini na Hakika mtamaliza vema.

Hongera sana CHADEMA!!!!
 
Dawa ya kuia kabisa kabisa CCM ni kuipiga Kotekote, Hakuna kuwapa nafasi ya kupumua, yaani
1/Mjini na vijijini.
2/Mchana na usiku.
3/Bungeni na Mahakamani.
4/Digital na Analogy.
5/Kisiasa na Kisheria.
6/Kaskazini na kusini.
7/Chaguzi ndogo na Uchaguzi mkuu.
8/Redioni na Luningani.
9/Majukwaani na Mitaani.
10/Masika na kiangazi
11/Jua na mvua.
 
Back
Top Bottom