CHADEMA yaicharaza CCM Bumbuli, Tanga

CHADEMA yaicharaza CCM Bumbuli, Tanga

Hongereni sana wakuu. Kuna siku kitaeleweka nchi nzima tu!! Ni nani alikua Amerika itatawaliwa na Afro-American?
 
CHADEMA wanafanya makosa kuingilia ngome ya CUF
 
hongereni sana.
jipangeni vizuri majimbo ya Tanga mjini, Lushoto mjini, Korogwe, na Mlalo mnaweza kuyapata 2015.
 
BAADA ya hila na mbinu haramu kadhaa kuzuia uchaguzi huru na haki, kuminya demokrasia ya sanduku la kura kuchukua mkondo wake, ikiwemo Mtendaji wa Kijiji cha Kwekitui kuharibu uchaguzi kwa kukimbia na sanduku la kura wiki iliyopita, CHADEMA imeibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji cha kijiji hicho, kilichoko Jimbo la Bumbuli, wilayani Lushoto, Mkoa wa Tanga, kwa kura 196 dhidi ya CCM waliopata kura kura 189.

Uchaguzi huo wa marudio ulifanyika leo, Jumapili, Aprili 7, 2013.

Hongereni CDM kwani mmethubutu. Vyama vingi vya upinzani mara nyingi huambulia 0 katika chaguzi za marudi lkn kwa CDM upepo unawaendea vyema. Mnakubalika kwa watanzania wengi sasa. Take care
 
Ndio tatizo lenu. Mkipongezwa kosa, msipopongezwa kosa. Lami ikijengwa kosa, isipojengwa kosa. Mshahara ukiongezwa kosa, usipoongezwa kosa. Washutumiwa wakikamatwa kosa wasipokamatwa kosa. Rais akiongea kosa, asipoongea kosa.

Ili mradi tu mlalamike...

Lakini watu kama nyinyi kwenye jamii hamkosekani, TUMESHAWAZOEA...

Like like like like!!!!!!!!
 
Wame hack

Kwanini nisiwapongeze watu waliofanya jitihada mpaka wameshinda?

Wanastahili pongezi. Hakuna mtu aliye hack.

Nadhani falsafa yangu wengi wenu hamjaielewa ndio maana mnapata shida kutafsiri ninayoandika...
 
CDM imepenya mpaka kwa kijana wa Digital????
 
si wanasema chadema haijaingia vijijini?na pia wanasema chedema ni ya moshi na arusha?!
 
CHADEMA wanafanya makosa kuingilia ngome ya CUF

Du!

Bora wamepata wa kuwasemea. Maana ni kama vile kabaki Prof. Lipumba peke yake. Vipi ile mliyokopi na kupaste, wakaanzia Arusha iliishia wapi vile. Au jamaa wale wa Lumbumba walihamishia mawazo kwenye mkakati mwingine, wa kupandikiza mamluki BAVICHA na kutengeneza movies.

Mkuu Jabulani, ni ama uko kule au hapa, hakuna option ya tatu kwa siasa za nchi hii tunapoelekea kung'oa mzizi wa fitna.
 
Bado moto unaendelea kuwaka! Naamini ccm wataamini kuwa muda sio rafiki tena watakapo ona Magogoni panapakwa rangi kwa ajili ya kumkaribisha mteule mpya!
 
Pole ccm ndiyo maisha kuna kupata na kukosa, yaelekea mtaikosa ikulu pia, ni hatua kwa hatua
 
Back
Top Bottom