CHADEMA yahamishiwa Ubelgiji na Mtandaoni

Mkirindi

JF-Expert Member
Mar 2, 2011
6,750
4,958
Ninapenda kwanza kutoa heshima zangu kwa Mheshimiwa Mbowe, aliyekuwa kizuizini, kwa kuonewa na bila kupewa haki yake kama sheria inavyosema.

Nikirudia mada yangu, hivi karibuni tumeona kuwa shughuli zote za hiki chama kikubwa cha upinzani zikihamishwa, kutoka mikoni mwa Ofisi zake za kisheria na mikononi mwa Viongozi wake, na kuhamishiwa kwa wale viongozi waliokimbia nchi kwa usalama wao, na pia kuweka makao makuu ya chama mitandaoni haswa kwenye kipindi cha MARIA SPACE.

Hili jambo linazungumzwa sana na limewabughudhi sana wengi wetu, kwani Chadema ni mali ya watanzania na kina manufaa kwa waliomo na wasiokuwemo, inaumiza kuona Chama kimetekwa Nyara.

Inashangaza sana kuona wale wazee muhimu na wenye busara wa CHADEMA, wamekaa kimya huku wakiona Chama kikiyumbayumba.
 
Huoni mfululizo wa kesi dhidi ya viongozi wa CDM Kwa kufanya mikutano?

CDM wanatoa taarifa Polisi,huko vibali vya mikutano havitoki na Bado wanakuja kushughulikiwa!

Acha waendelee kuwafikia wananchi Kwa namna yoyote Ile iwezekanavyo!

Unawalaumu CDM lakini tatizo la msingi ni serikali na vyombo vya Dola kukandamiza uhuru wa vyama vya siasa kufanya shughuli zao!
 
Hivi karibuni tumeona kuwa shughuli zote za hiki chama kikubwa cha upinzani zikihamishwa , kutoka mikononi mwa Ofisi zake za kisheria na mikononi mwa Viongozi wake , na kuhamishiwa kwa wale viongozi waliokimbia nchi kwa usalama wao, na pia kuweka makao makuu ya chama mitandaoni

Inashangaza sana kuona wale wazee muhimu na wenye busara wa Chadema, wamekaa kimya huku wakiona Chama kikiyumbayumba.
Mkuu Mkirindi, kumbe na wewe uko kundi langu la wazee wa mwaka 47! Dunia sasa imeshift kutoka physical world kwenda cyber world, hivyo kila kitu sasa ni kimehamia mitandaoni, hivyo Chadema are right, ila wanapaswa kuanzisha its own space. Jana nilitembelea web site ya Chadema, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Official Website nilikuta last update ya habari ilifanywa November 2019! sasa kila kitu ni kwa twitter tuu!. This is wrong!

Kwa vile sasa kila kitu kimehamia mitandaoni, na chadema kinajingamba kwa matumizi ya mitandao, then kitu cha kwanza tulitegemea kuona Chadema inafanya ni kuwa na website live interactive, ukiingia tuu unakuta kila kitu!

P
 
Si ndo mlikuwa mnapenda chadema IFE.
kwani bila chadema nyie hamsikii Raha?
 
Chadema bwana hawapo bungeni lakini bunge halipandi bila stori zao, hawapo serikalini lakini wanawapasua kichwa, wengine wanadai kimekufa lakini wanakiongelea BTW bado Chadema ndio chama atleast cha upinzani kilichowekeza kwenye watu hawa jamaa wana watu
 
Chama kipo vzr,it's better to retreat and have a chance to fight another day,

Nafasi ya kufanya Siasa imebanwa sana hapa Nchini,"intelijensia"ya polisi hii inayoweza kutabili fujo kutokea pale tu Chadema inapoandaa mkutano,lakini haiwezi kuokoa masoko yetu yasiungue kwa moto wa "mchongo",inaleta shida sana.

Watu wanaoweza kuleta mapinduzi kwenye nchi hii,ni daraja la kati,Hawa wapo sekta binafsi,serikalini,na wapo konected sana mtandaoni,hao ndio tunaowalenga,ccm imebaki kama mganga wa kienyeji,na kushika misukule ya watu wasio na ufahamu wa vijijini,kada ile ya chini sana, inayoamini kununua maji "yaliyobarikiwa"pale kwa mwamposa,yanaweza kuwaondolea changamoto za kiuchumi walizonazo.
 
Mkuu Mkirindi , kumbe na wewe uko kundi langu la wazee wa mwaka 47!. Dunia sasa imeshift kutoka physical world kwenda cyber world, hivyo kila kitu sasa ni kimehamia mitandaoni, hivyo Chadema are right, ila wanapaswa kuanzisha its own space. Jana nilitembelea web site ya Chadema, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Official Website nilikuta last update ya habari ilifanywa November 2019!, sasa kila kitu ni kwa twitter tuu!. This is wrong!.
Kwa vile sasa kila kitu kimehamia mitandaoni, na chadema kinajingamba kwa matumizi ya mitandao, then kitu cha kwanza tulitegemea kuona Chadema inafanya ni kuwa na website live interactive, ukiingia tuu unakuta kila kitu!.
P
Waweke muenendo wote wa kesi ya Mbowe mahakamani kwenye website yao.
 
Chama cha kipuuzi sana hiki wanashikiwa akili na Lema na Lissu wanajazana upepo tu huko Space
 
Umeongea kwa usahihi kabisa, kuondoka kwa Dr. Slaa na kushikiriwa bila kosa kwa Mbowe kumeifanya CHADEMA ife. Huu ndio ukweli mchungu. CHADEMA imebaki ya kimtandaoni kwa Lissu , Lema, MMM na Maria Sarungi. Hawa wote wananufaika
 
ACT inakuja kwa kasi na mipango thabiti. Wao wamebaki space za Maria kila siku. Hivi mwananchi wa kawaida wa Tandahimba asiyekuwa na pesa ya kula hayo mambo ya space anayajulia wapi? ACT wao wanaenda vijijini wanaibua changamoto za wananchi na kuzipazia sauti.
 
Mkuu Mkirindi , kumbe na wewe uko kundi langu la wazee wa mwaka 47!. Dunia sasa imeshift kutoka physical world kwenda cyber world, hivyo kila kitu sasa ni kimehamia mitandaoni, hivyo Chadema are right, ila wanapaswa kuanzisha its own space. Jana nilitembelea web site ya Chadema, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Official Website nilikuta last update ya habari ilifanywa November 2019!, sasa kila kitu ni kwa twitter tuu!. This is wrong!.
Kwa vile sasa kila kitu kimehamia mitandaoni, na chadema kinajingamba kwa matumizi ya mitandao, then kitu cha kwanza tulitegemea kuona Chadema inafanya ni kuwa na website live interactive, ukiingia tuu unakuta kila kitu!.
P
Ndugu Pascal, OLD IS GOLD: Chama Binafsi kuhamia Mitandaoni ni katika harakati za kimaendeleo, Ingependeza Chama kihamie huko as Chama na sio individual. Chadema is bigger than the few currently hijacking the party. By the way I have just also visited website yao ni kweli yako iko very OUTDATED, HOW SAD
 
Na hao wote uliowataja ni pro Government iliyomfunga Mbowe, wanautaka Uwenyekiti wa Mbowe ili waue Upinzani rasmi, wameahidiwa power sharing, Mbowe kikwazo kwao!

1643092332415.jpeg
 
Ninapenda kwanza kutoa heshima zangu kwa Mheshimiwa Mbowe, aliyekuwa kizuizini, kwa kuonewa na bila kupewa haki yake kama sheria inavyosema.

Nikirudia mada yangu, hivi karibuni tumeona kuwa shughuli zote za hiki chama kikubwa cha upinzani zikihamishwa, kutoka mikoni mwa Ofisi zake za kisheria na mikononi mwa Viongozi wake, na kuhamishiwa kwa wale viongozi waliokimbia nchi kwa usalama wao, na pia kuweka makao makuu ya chama mitandaoni haswa kwenye kipindi cha MARIA SPACE.

Hili jambo linazungumzwa sana na limewabughudhi sana wengi wetu, kwani Chadema ni mali ya watanzania na kina manufaa kwa waliomo na wasiokuwemo, inaumiza kuona Chama kimetekwa Nyara.

Inashangaza sana kuona wale wazee muhimu na wenye busara wa CHADEMA, wamekaa kimya huku wakiona Chama kikiyumbayumba.
Mpuuzi kweli wewe, halafu unaanza kiunafiki kutaja Mbowe, shetani wewe. Ya Chadema yanakuhusu Nini? Na nyie hamieni Zanzibar, mbona mlihamia Chato?
 
Ndugu Pascal, OLD IS GOLD: Chama Binafsi kuhamia Mitandaoni ni katika harakati za kimaendeleo, Ingependeza Chama kihamie huko as Chama na sio individual. Chadema is bigger than the few currently hijacking the party. By the way I have just also visited website yao ni kweli yako iko very OUTDATED, HOW SAD
Kwenye hili la website, nahisi ni ukata tuu, lakini Chadema ikitangaza inatafuta web admin wa kujitolea, naamini kuna vijana hundreds wenye mapenzi ya dhati na Chadema, watakuwa more than willing kujitolea kui run website ya Chadema free of charge!.
Na hapa sasa ndio unaona pengo la wazi la Chadema kutokuwa na Afisa Habari!.
cc. Tumaini Makene
P
 
Chama cha kipuuzi sana hiki wanashikiwa akili na Lema na Lissu wanajazana upepo tu huko Space
Chadema na Ccm ni kama USSR vs USA enzi hizo. Kama ni ushabiki basi watafananishwa na Simba na Yanga.
 
Back
Top Bottom