HALMASHAURI 70 kati ya 136 nchini, zinakabiliwa na janga la njaa. (Halmashauri zenye njaa ni ailimia ngapi?)
Chiza Alisema tathmini iliyofanywa na serikali kwa kipindi cha Septemba 2012 na Januari 2013, ilibaini kuwa halmashauri 47 katika mikoa 19 zinakabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula. Chiza aliitaja mikoa yenye upungufu mkubwa wa chakula kuwa ni Arusha, Kilimamnjaro, Manyara, Morogoro, Lindi, Tanga, Mtwara, Pwani , Shinyanga, Simiyu, Tabora, Mwanza, Mara, Kagera, Iringa, Mbeya, Rukwa, Dodoma na Singida. (Hivi mikoa ya G5 unaifahamu? je yaweza kuwa na njaa?, Huo ukame ulisemwa bungeni ulitokea lini tanzania na ulielezwa kwa vyombo vipi vya habari, Je Madhara ya kuzuia mipaka kuuza mazao yaliyozalishwa na G5 wameyaongeleaje hiyo serikali yetu makini? )
Katika bajeti yake, wizara imeomba kiasi cha sh 328,134,608,000 kwa ajili ya matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2013/14.Mchanganuo wake sh bilioni 247 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida (Yepi, Chumia tumbo ambayo ni mishahara, posho n.k ) na sh bilioni 81 ni kwa ajili ya shughuli za maendeleo. (Ni asilimia ngapi ya fedha? Serikali makini hujali Matumizi ya kawaida kuliko Maendeleo?)
Chiza alisema katika matumizi ya kawaida sh bilioni 210.1 ni kwa ajili ya matumizi mengine (Yepi? Hata mimi siyajui), sh bilioni 25.6 (mishahara ya wizara) na sh 11.3 (mishahara ya bodi na taasisi).
Alisema kuwa kati ya fedha za bajeti ya maendeleo sh bilioni 23.9 ni fedha za ndani na sh bilioni 57.1 ni za nje.(Serikali makini hutegemea maendeleo kwa fedha za wafadhili?)
Mpaka hapo sina koment soma na chambua mwenyewe