CHADEMA Yaanikwa Bungeni Jioni Hii!

CHADEMA Yaanikwa Bungeni Jioni Hii!

Waziri wa Kilimo Mhandisi Chiza ameichambua HOTUBA ya waziri kilimo wa Chadema kuwa haina viwango ilijikita kutoa lawama badala ya majibu muafaka.

Kwa kweli ukifuatilia hotuba ya Waziri Chiza utagundua CCM ipo makini kutatua matatizo ya kilimo wakati CHADEMA wamebaki kupiga kelele kwa kutumia mawaziri vivuli wasio na viwango

we vp kwani serikali iliyomadarakani ni ccm kama wako makini mbona hawatatui changamoto za kilimo ndo maana wapinzani wanalalamika acha ushabiki usio na tija mpaka mchele tunaagiza toka nje wakati ardhi maji nk vipo
 
Hata profesa wao hamna kitu.Mawaziri wao vivuli hawajai hata mkononi. hv kweli wakipewa nchi wataweza kuongoza??
Swali rahisi kabisa! Marekani ina wananchi wangapi? Ina ukubwa gani? Na je ina mawaziri wangapi? Hivi unafikiri Tanzania inahitaji baraza la mawaziri la watu 60 kama la Kikwete? Baraza la Kikwete limejaa watu waliokuwa wanalipwa fadhila tu, hakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kuwa na baraza kubwa kama hili. Hata wewe unalijua hilo. Chadema wakiwa na mawaziri kumi tu wanatosha kabisa. Nchi haiongozwi na mawaziri. Mawazirii ni wasemaji tu wa masuala ya kisiasa. Nchi inaongozwa na watendaji na wataalamu katika sekta mbalimbali kwenye kila wizara. Tunaweza kuwa na mawaziri watano tu, na kazi ikafanyika ya maana kuliko inayofanya na mawaziri 60 wa Kikwete waliopata uwaziri kwa misingi ya kulipana fadhila.
 
Kazi ya Chadema ni kukosoa siyo kupigia makofi serikali ndo maana ya vyama vya ushindani/upinzani duniani kote. Kazi ya Serikali ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa kutumia kodi za watanzania wote , wakiwepo wanachadema, na siyo kwa kutumia mishara yao. kukoselewa siyo kulaumiwa.
Uelewa huu wa maana ya ushindani ndio tatizo letu kubwa kama taifa. Na haswa wanachama na zaidi viongozi wa ccm. Mengi sana yangeepukika kama wengi wangeelewa maana ya upinzani/ushindani na dhana nzima ya Demokrasia. Umbumbumbu tulionao katika swala hili utatutafuna kwa muda mrefu na muda wote ambao CCM itaendelea kuwa madarakani. Kiwango cha elimu nchini kitazidi kushuka, akaunti za Uswiss zitakuwa kubwa na idadi kuongezeka, matibabu yatazidi kuwa duni na nchi kugeuzwa uwanja wa kigaidi kutokana na umaskini.
Mungu iepushe Tanzania na janga hili.
 
Waziri wa Kilimo Mhandisi Chiza ameichambua HOTUBA ya waziri kilimo wa Chadema kuwa haina viwango ilijikita kutoa lawama badala ya majibu muafaka.

Kwa kweli ukifuatilia hotuba ya Waziri Chiza utagundua CCM ipo makini kutatua matatizo ya kilimo wakati CHADEMA wamebaki kupiga kelele kwa kutumia mawaziri vivuli wasio na viwango

Wewe ulitegemea aisifie wakati wakati zakwao zimeshindwa kumtoa mtz kwenye dimbwi laumasikini miaka50?.Ya Cdm iwe namajibugani kwa wtz wakati kodi anakusanya gamba? kwanza namsikitikia Chiza ameshindwa kupigania hata balabala inayopita jimboni kwake mlangoni toka nyakanazi nimashimo yakutisha!
 
Waziri wa Kilimo Mhandisi Chiza ameichambua HOTUBA ya waziri kilimo wa Chadema kuwa haina viwango ilijikita kutoa lawama badala ya majibu muafaka.

Kwa kweli ukifuatilia hotuba ya Waziri Chiza utagundua CCM ipo makini kutatua matatizo ya kilimo wakati CHADEMA wamebaki kupiga kelele kwa kutumia mawaziri vivuli wasio na viwango

Kwa yeyote aliyesikiliza hotuba ya upinzani lazima atakubaliana na Waziri CHIZA
 
Alichofanikiwa jimboni kwake huyo wewe unayemuita mheshimiwa Chiza pamoja nakupewa uwaziri ni kukusanya police wavuta bangi wanyan'ganyi nakubambikia wanavijiji kesi ambavyo police hao niwale wanaotolewa vituo vingine kwa kashifa nakuweka geti balabalani na kukagua baiskeli
 
Waziri wa Kilimo Mhandisi Chiza ameichambua HOTUBA ya waziri kilimo wa Chadema kuwa haina viwango ilijikita kutoa lawama badala ya majibu muafaka.

Kwa kweli ukifuatilia hotuba ya Waziri Chiza utagundua CCM ipo makini kutatua matatizo ya kilimo wakati CHADEMA wamebaki kupiga kelele kwa kutumia mawaziri vivuli wasio na viwango
Matatizo ya kilimo hayatatuliwi kwa hotuba nzuri kijana. Wabunge wengi sana wa CCM wameipinga hiyo budget, mambo mengi yapo kibabaishaji tu humo. Usinogewe na mbwembwe za Waziri, Devil is in the details!!

Yapo matatizo mengi sana ya kilimo nchini kijana. Uliza tunaolima tukueleze, wewe unakaa Lumumba hapo kazi yako kujibu hoja kibabaishaji humu then wasema CCM inadhamira ya kukwamua kilimo bila kujua kinachoendelea. Dhambi sana!


  • Unuingizaj wa Mchele toka Thailand wakati mchele wa wazawa hauna soko ni moja ya mapungufu ya serikali yanayochangiwa na ufisadi.



  • Serikali kupora ardhi na kuwapa wawekezaji wezi ni tatizo jingine.



  • Ukosefu wa dhamira ya dhati kumsaidia mkulima kwa kumpatia pembejeo pmj na elimu ni tatizo jingine.



  • Kilimo cha mikataba wanachoingizwa wakulima wetu na makampun ya kinyonyaji ktk Tumbaku na Pamba ni wizi na unyonyaji unaosimamiwa na serikali kwa manufaa ya wafanyabiashara ila kwa cost ya wakulima. Babu zetu wamegeuzwa manamba kwenye karne hii.



  • Wakulimwa wetu kukopwa mazao yao miaka nenda rudi ni tatizo jingine. Nenda mikoa ya kusin kwenye kwa wakulima wa mkorosho. Nenda Kasulu kwa walima Tumbaku.



  • Ukosefu wa masoko ya uhakika ya mazao yanayozalishwa nchi ni tatizo.

Waziri ilibidi atupe majibu ya kina ya masuala haya. Waziri hayupo Bungeni kufanya Propaganda, hiyo ni kazi ya Nape. Kuna Mbunge mmoja wa Kilwa leo kanifurahisha sana. Kasema huu mzaa unaofanywa na serikali wa kutotatua matatizo ya wananchi sasa hiv itabidi tuufurahie maana serikali inajipalia makaa yenyewe na 2015 njia itakuwa safi sana.

Endeleeni kubisha na kufanya Propaganda badala ya kufanya Kazi. Sasa hiv CDM tunapiga kazi mpaka vijijini kwenda kuwaelimisha wananchi wa vijijin ambao ninyi mnajifanya ndio mtaji wenu. Endeleeni kukataa ushauri ambao kimsingi unawasaidie nyinyi kurudisha mvuto mlioupoteza machon mwa watanzania. Kweli sikio la kufa halisikii dawa. Naishauri mnaubeza tena!!!???

TENA CHONDE KIJANA USISHABIKIE MAMBO USIYOYAJUA UTAISHIA KUPATA LAANA WEWE KWA UJIRA WA ELFU 7000 HIZO UNAZOLIPWA NA CCM.
 
CCM ndo hawana jipya au CDM?

Wewe kwa uelewa wako wa Mulugo nani hapo asiye na jipya katiya aliyeahidi miaka na miaka na anayeomba ridhaa ya kuongoza inchi ili akutoe nawewe kwenye ujinga huo ulionao?
 
Hata profesa wao hamna
kitu.Mawaziri wao vivuli hawajai hata mkononi. hv kweli wakipewa nchi
wataweza kuongoza??

ndio baba we c unajaa mkononi her yako.lakin elewa cku zote mchumia juan ulia kivuln we unachumia kivulin utalia juan
 
Nadhani huyu waziri ni mvivu wa kufikiri kabisa pamoja na wewe uliyeweka uzi huu. Hivi yeye ni nani wa ku-judge hotuba y mwenziye kuwa haina kiwango? ametumia mizania yake binafsi au ya kiutaalam? km ni mizania ya kitaalam mbona hajasema ameipima hotuba ya upinzani kwa vigezo gani hadi kufikia conclusion hiyo? yeye hotuba yake ameipimaje kuona ni bora? Tatizo ni kwamba nchi yetu imezoea kusifiwa hata katika mambo ambayo yako ktk job description! Hivi najaribu kufikiria iwapo km hata waandishi wa vitabu wangekuwa wanasifiana tu nadhani hivi leo hatungekuwa na waandishi wa vitabu hasa vya kitaaluma, make kila kitu wangeona kiko sahihi. Sasa leo waziri anataka kugeuza upinzani uwe wa kusifia hotuba yake badala ya kuikosoa ili iboreke yeye anang'aka kuwa wanapiga kelele! Nashangaa waziri anataka atafuniwe na majibu pia. Yeye akikosolewa hotuba yake so ndiye aende kutafuta suluhisho? Chadema hawako madarakani, yeye waziri ndiye serikali iko madarakani, kwanini asikubali criticism na kisha akaenda kutafuta ufumbuzi wa hizo criticisms badala ya kuzibeza? Nadhani anakosea sana ku-attack watu badala ya hoja.
Waziri wa Kilimo Mhandisi Chiza ameichambua HOTUBA ya waziri kilimo wa Chadema kuwa haina viwango ilijikita kutoa lawama badala ya majibu muafaka.

Kwa kweli ukifuatilia hotuba ya Waziri Chiza utagundua CCM ipo makini kutatua matatizo ya kilimo wakati CHADEMA wamebaki kupiga kelele kwa kutumia mawaziri vivuli wasio na viwango
 
Mwenye macho hambiwi tazama!!Wakati mwingine usikuruke kuposti,tafakari kwanza sio unaandikiwa ujumbe wewe unapost tu!Simliambiwa mchanganye nazenu!
 
Uelewa huu wa maana ya
ushindani ndio tatizo letu kubwa kama taifa. Na haswa wanachama na zaidi
viongozi wa ccm. Mengi sana yangeepukika kama wengi wangeelewa maana ya
upinzani/ushindani na dhana nzima ya Demokrasia. Umbumbumbu tulionao
katika swala hili utatutafuna kwa muda mrefu na muda wote ambao CCM
itaendelea kuwa madarakani. Kiwango cha elimu nchini kitazidi kushuka,
akaunti za Uswiss zitakuwa kubwa na idadi kuongezeka, matibabu yatazidi
kuwa duni na nchi kugeuzwa uwanja wa kigaidi kutokana na umaskini.
Mungu iepushe Tanzania na janga hili.

kh nimeipenda xana. huku jf kuna watoto wa nape ndo maana wanaöongea pumba weng au unacmaj?
 
Back
Top Bottom