luhala
JF-Expert Member
- Feb 25, 2012
- 412
- 142
Kadiri 2015 inavyosogea CHADEMA inazidi kusakamwa na tuhuma toka kwa wasioitakia heri kwa tuhuma hizi au zile zikiwemo za ukaskazini, migogoro ya ndani na kuhusishwa na ukristo na hivi karibuni wimbi la wanaojitangaza kuwa watagombea urais kwa tiketi ya chama hicho.
Matukio haya; liliwepo lile la waziri kukitabiria "kifo" chama hiki kabla ya uchaguzi ujao yananiaminisha kuwepo mkono wa serikali katika kutengeneza "migogoro" ndani na nje ya chama hiki. Sasa nakumbuka mazungumzo yangu na mmoja wa viongozi wateule wa JK mara baada ya kuapishwa na kuwateua viongozi wake waandamizi ambapo mimi na jamaa yangu mmoja tulikwenda kumpongeza mmoja wa wateule wake hao ambaye tulisoma nae na kufanya nae kazi kwa miaka kadhaa na alibahatika kuteuliwa tena katika nafasi ya uongozi katika serikali ya awamu ya pili ya JK. Baada ya kutafakari sana nimeamua kuyaweka mazungumzo yetu ili ma-great thinkers watafakari na waone kama kuna relation na yanayojitokeza sasa kwa CHADEMA.
Alikuwa jamaa yangu aliyenifahamisha mapema kabisa kwamba rafiki yetu yule alipata uteuzi tena katika awamu hii na kuniasa twende kumpongeza licha ya msimamo wangu wa kuziunga mkono harakati za CHADEMA. Tulikwenda naa kupokelewa kwa bashasha na baada ya mazungumzo marefu yakiwemo ya kumpongeza yeye binafsi kuteuliwa na mgombea urais wao "kushinda" ghaflaalibadilika na kuanza kufoka ifuatavyo:
"Washenzi hawa wametusumbua sana safari hii, wamemsumbua sana mheshimiwa na nasema hu ndiyo mwisho wao. Hatutawapa fursa nyingine tena ya kutusumbua kama walivyofanya safari hii. Kwani wao CHADEMA ni nani haswa, mbona wenzao NCCR tuliwamaliza kianina? Nakwambia 2015 hakutakuwa na CHADEMA wala huyo mnayemwita Dr. Slaa kwani serikali ina mikono mirefu na tumeshajipanga kuhakikisha kunakuwa hakuna usumbufu tena 2015. Nakwambieni huyo Dr. Slaa na hata Mbowe watausikia ugombea urais kwenye bomba tu na tutahakikisha vyombo vyetu vinawavuruga kabisa na huenda hata wasiwepo ifikapo 2015"
Ni baada ya maneno hayo mwenzangu alianzisha topic nyingine iliyotamalaki huku tukigida bia na kutafuna kuku hadi tulipoagana. Toka wakati huo tunawasiliana kwa simu lakini hatuzungumzii siasa.
Kazi kwenu ma-great thinkers kutafakari kama mihemko inayoitwa "migogoro" ndani ya CHADEMA ina uhusiano na remarks za kiongozi huyu mwandamizi.
Matukio haya; liliwepo lile la waziri kukitabiria "kifo" chama hiki kabla ya uchaguzi ujao yananiaminisha kuwepo mkono wa serikali katika kutengeneza "migogoro" ndani na nje ya chama hiki. Sasa nakumbuka mazungumzo yangu na mmoja wa viongozi wateule wa JK mara baada ya kuapishwa na kuwateua viongozi wake waandamizi ambapo mimi na jamaa yangu mmoja tulikwenda kumpongeza mmoja wa wateule wake hao ambaye tulisoma nae na kufanya nae kazi kwa miaka kadhaa na alibahatika kuteuliwa tena katika nafasi ya uongozi katika serikali ya awamu ya pili ya JK. Baada ya kutafakari sana nimeamua kuyaweka mazungumzo yetu ili ma-great thinkers watafakari na waone kama kuna relation na yanayojitokeza sasa kwa CHADEMA.
Alikuwa jamaa yangu aliyenifahamisha mapema kabisa kwamba rafiki yetu yule alipata uteuzi tena katika awamu hii na kuniasa twende kumpongeza licha ya msimamo wangu wa kuziunga mkono harakati za CHADEMA. Tulikwenda naa kupokelewa kwa bashasha na baada ya mazungumzo marefu yakiwemo ya kumpongeza yeye binafsi kuteuliwa na mgombea urais wao "kushinda" ghaflaalibadilika na kuanza kufoka ifuatavyo:
"Washenzi hawa wametusumbua sana safari hii, wamemsumbua sana mheshimiwa na nasema hu ndiyo mwisho wao. Hatutawapa fursa nyingine tena ya kutusumbua kama walivyofanya safari hii. Kwani wao CHADEMA ni nani haswa, mbona wenzao NCCR tuliwamaliza kianina? Nakwambia 2015 hakutakuwa na CHADEMA wala huyo mnayemwita Dr. Slaa kwani serikali ina mikono mirefu na tumeshajipanga kuhakikisha kunakuwa hakuna usumbufu tena 2015. Nakwambieni huyo Dr. Slaa na hata Mbowe watausikia ugombea urais kwenye bomba tu na tutahakikisha vyombo vyetu vinawavuruga kabisa na huenda hata wasiwepo ifikapo 2015"
Ni baada ya maneno hayo mwenzangu alianzisha topic nyingine iliyotamalaki huku tukigida bia na kutafuna kuku hadi tulipoagana. Toka wakati huo tunawasiliana kwa simu lakini hatuzungumzii siasa.
Kazi kwenu ma-great thinkers kutafakari kama mihemko inayoitwa "migogoro" ndani ya CHADEMA ina uhusiano na remarks za kiongozi huyu mwandamizi.