Imeelezwa Bungeni kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanafanya adabrakadabra, yaani wimbo wa mazingaombwe (kiini macho) kwa wananchi ili waamini wanayosema wakati si kweli. Wabunge waliochangia wanasema baadhi wa wanaCHADEMA ni madalali wa siasa waliofadhiliwa kuvuruga amani nchini na wanapeana nafasi za viti maalumu kwa ukabila na mahusiano ya damu.