CHADEMA Wamkubali Nape kwa maneno yake

CHADEMA Wamkubali Nape kwa maneno yake

tata mura

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2012
Posts
275
Reaction score
49
Katika hali ya upepo ya kisiasa, Chadema wamekuwa wakihaha kila kukicha pindi Nape anapokuwa anatoa sera za kisiasa juu ya Chama kikuu cha upinzani Tanzania bara (CHADEMA) kwa nukuu mbali mbali; Mfano: Nape hivi karibuni amesema Dr. Slaa ni mwanachama wa CCM, na yeye bila hiyana akajitokeza na kukiri kuwa ni kweli kwa kumiliki kadi ya CCM. Na nyingine nyingi hadi viongozi wa Chadema wakatishia kwenda Mahakamani kitendo ambacho sasa, kesho na keshokutwa hakitawezekana ama kwa uoga au kukosa wataalamu wa kisheria.

Wakimkimbilia Tundu Lissu Jimboni kwake pamemshinda hadi hivi karibuni alikiri kuwa CCM wamemshinda hivyo hawawezi tena, hii ilitokea pale alipo itisha Mkutano na Wananchi wa Jimbo lake bila Maandamano tarehe 08/12/2012 kijijini Mang'onyi. Si hayo tu alikiri mambo mengi na mengine alionekana anawadanganya wananchi na kufikia hali wa kuanza kumuaibisha pale aliposema CCM wameanzisha mradi wa kilimo na umwagiriaji na alishangaa kusikia CCM wanasema wamelima mashamba hekta 20 wakati yeye anajua shamba lililolimwa ni hekta moja mwananchi mmoja akanyosha mkono na kumtuliza kwa kumwambia Mheshimiwa tunaomba ulekebishe kauli yako kwani kwahili unasema uongo, eneo lililo limwa hadi sasa tunapo ongea ni zaidi ya hekta 21 na kudhibitishia hivi nami ni mmoja wapo wa wanakikundi hivyo Mheshimwa tunakukalibisha ujionee ili unapopanga sera zako zinyooke.

Mbali zaidi ni pale Nape alipotangaza kuwa sasa CCM wanawavua Magamba wanachama wao, Chadema wakadakia kwa kusema VUA GAMBA VAA GWANDA. Kwa hali hii inaonyesha wazi Chadema wanaishi kwa mgongo wa CCM hivyo wanatakiwa kujipanga zaidi.

Ukweli unagharimu lakini ili ufanikiwe lazima uufanyie kazi. Kwa asiyeamini awasiliane na wahusika wampe ukweli ulivyo.

Nawasilisha
 
CHADEMA ----- CCM
mbowe alianza na mpaka kieleweke - -- j.k akaja na nginja nginja mpaka 2015

kufufua viwanda vya korosho alianza zitto--- Kinana nae karukia

kushusha cement bei(ilani ya cdm 2010) -- -Kinana kairukia

elimu bure hadi kidato cha 6(ilani cdm 2010) ---ikarukiwa na lowasa&mkutano mkuu ccm 2012

Nape ili aendelee kusikika kwenye media ni lazima attack mwanasiasa,hajadili hoja
 
Punguza hasira si wote wanywapombe kama ulivyo wewe. Pole kama umeguswa
 
Dah kweli umeanzisha thread na imesomwa hongera sana
Halafu waambie akina Nape na Kinana vipi ziara ya Mtwara mbona hata tathmini hakuna
 
Wewe ni kilaza,huyo Nape ni vuvuzela anayetegemea hadi ateuliwe na baba yake mdogo Kikwete hajawahi kuchaguliwa hata lever ya umonta darasani na wananchi,siku zote huteuliwa,kwa hyo hana jipya mana si chaguo la watu,awaache waongee wanasiasa wakongwe waliochaguliwa na watu,yeye Nape ni kula kulala,subirini 2015 muione nguvu ya uma inaposhinda! Viva Chadema
 
Mmm, kama Nape nae ndio anaonekana kuwatetemesha CHADEMA, basi huko magamba kweli wameishiwa, mtu ambaye hajui hata sifa za mwanachama hai wa chama chake zikoje? mtu ambaye aliwahi kusema CHADEMA wanataka kuuza nchi kwa mapampuni ya kibepari while magamba ndio wameshikilia nchi na tayari almost everything kimeisha uzwa kwa baraka zao! halafu eti huyu ndio anaweza kuwatetemesha CHADEMA, ajabu kweli!
 
Wewe ni kilaza,huyo Nape ni vuvuzela anayetegemea hadi ateuliwe na baba yake mdogo Kikwete hajawahi kuchaguliwa hata lever ya umonta darasani na wananchi,siku zote huteuliwa,kwa hyo hana jipya mana si chaguo la watu,awaache waongee wanasiasa wakongwe waliochaguliwa na watu,yeye Nape ni kula kulala,subirini 2015 muione nguvu ya uma inaposhinda! Viva Chadema
hivi Nyerere alikuwa kachaguliwa na nani alipokuwa kiongozi wa Tanzania wakati wa uhuru?

Je! alikuwa ni vuvuzela! hivi mtu kama hakuchaguliwa maana yake hana kakili?wewe ulishawahi kuchaguliwa kipindi na mahali flani?
 
We tata mura ni mzigo kama mizigo mingine tu ya magamba (CCM). Mnatoka na thread za kipuuzi/kijinga mkiamini wa tz wote ni wadanganyika. Wewe na Nape waathirika wa uchakachuaji wa elimu ambayo inatakiwa imuongoze binadam aongee nini, aseme mbele ya watu. Hoja ya kijinga ya umilikaji wa kadi inaonyesha jinsi msivyotambua mipaka ya umilikaji wa kadi za chama cha siasa. Kama alivyofafanua wakili Kimong'oro kadi ya chaam ni mali ya mwanachama hivyo pindi akiacha ana halali ya kuitunza au kuitupa au kuchoma moto. Kinachowanyanyua watu na akili zao kuingia barabarani na hoja yenye ***** inashangaza sana. Waambieni watz mna mpango wa kuwafanyia nini kuondoa umaskini baada ya kusota miaka 51 ya uhuru si vinginevyo. Tambueni kuwa watu sasa wameerevuka na kujua haki zao.
 
Nahisi huyu ni le kibonge anarudi kwa style mpya haya karibu ulingoni, na kwa vile kiboko yako ni Ester wassira naamini utapata tuu jibu nani anategemea mgongo wa mwingine
 
hivi nyerere alikuwa kachaguliwa na nani alipokuwa kiongozi wa tanzania wakati wa uhuru?je! alikuwa ni vuvuzela! hivi mtu kama hakuchaguliwa maana yake hana kakili?wewe ulishawahi kuchaguliwa kipindi na mahali flani?

TANU walimpigia kura kuwa mwenyekiti.. akiwa Makerere alichaguliwa kuwa kiongozi wa wanafunzi.. haya kilaza Nape sasa tumrudie?
 
Kwa nini kila wakati ni mambo ya kinapenpe. Nape ni nani, huyu mtu kaishiwa busara kabisa mdomo wake unanuka matusi tu hata sijui kwa nini unamsifia. Labda na wewe ni mmoja wa aina ya kina Nape. Watanzania tuna matatizo lukuki yaliyosababishwa na viongozi wenye hulka za Kinape, kwa nini tusitumie muda wetu kujadili jinsi ya kupata ufumbuzi? Kwa nini tunakwepa kuongea juu ya ufisadi, kuibwa kwa ndovu, kuficha hela nje ya nchi, kutorosha wanyama wetu, mikataba inayowafaidisha viongozi dhaifu, mauaji ya wananchi wasio na hatia nk. ambavyo ni mali ya watanzania wote, kuliko kujadili upuuzi huu. Unanikera kweli, be mature mentally.
 
tata mura Bibie, matatizo ya watanzania siyo CHADEMA kukiri utoto au ujinga wa mtoto mwenzenu Nape.

Matatizo ya watanzania yanatokana na sera mbovu za CCM, shule kukosa walimu, madawati na maabara, hospitali kukosa wataalam, dawa, maji, umeme na x-ray machines, wizi na ufisadi uliokithiri wa viongozi wa serikali ya CCM, kupanda bei kwa bidhaa zote, wakulima kukopwa mazao yao (korosho-Mtwara), viongozi wa serikali kukosa ubunifu na uongozi bora hivyo kuishia kuning'unika na kulalamika kila kukicha, na mbaya zaidi viongozi wa CCM kushindwa kabisa kutambua matakwa ya watanzania na badala yake kuanza kuwatumia wajinga kama wewe kushinda mitandaoni kutetea uvundo na umaskini wa fikra za CCM!

Nakuhakikishia CCM haitapendwa na wananchi kwa propaganda za kichovu kama hizi, badala yake serikali yake itatue matatizo ya wananchi wake. Na wewe hutaisaidia CCM kwakushinda unaandika huu ujinga wako hapa jamvini! Poleni sana watoto.
 
Last edited by a moderator:
Katika hali ya upepo ya kisiasa, Chadema wamekuwa wakihaha kila kukicha pindi Nape anapokuwa anatoa sera za kisiasa juu ya Chama kikuu cha upinzani Tanzania bara (CHADEMA) kwa nukuu mbali mbali; Mfano: Nape hivi karibuni amesema Dr. Slaa ni mwanachama wa CCM, na yeye bila hiyana akajitokeza na kukiri kuwa ni kweli kwa kumiliki kadi ya CCM. Na nyingine nyingi hadi viongozi wa Chadema wakatishia kwenda Mahakamani kitendo ambacho sasa, kesho na keshokutwa hakitawezekana ama kwa uoga au kukosa wataalamu wa kisheria....

Mawazo kama haya msitegemee ukombozi wa nchi hii utakuwa rahisi. Tena ukute huyu ni msomi ana degree, lakini anaandika kitu cha kijinga kabisa. Tuna safari ndefu sana kufika huko tunakokutaka. Mwenye akili timamu hawezi angashangilia ujinga anaoufanya bwana nape na ccm yake, ila ipo siku haya yote yatakoma.
 
We tata mura ni mzigo kama mizigo mingine tu ya magamba (CCM). Mnatoka na thread za kipuuzi/kijinga mkiamini wa tz wote ni wadanganyika. Wewe na Nape waathirika wa uchakachuaji wa elimu ambayo inatakiwa imuongoze binadam aongee nini, aseme mbele ya watu. Hoja ya kijinga ya umilikaji wa kadi inaonyesha jinsi msivyotambua mipaka ya umilikaji wa kadi za chama cha siasa. Kama alivyofafanua wakili Kimong'oro kadi ya chaam ni mali ya mwanachama hivyo pindi akiacha ana halali ya kuitunza au kuitupa au kuchoma moto. Kinachowanyanyua watu na akili zao kuingia barabarani na hoja yenye ***** inashangaza sana. Waambieni watz mna mpango wa kuwafanyia nini kuondoa umaskini baada ya kusota miaka 51 ya uhuru si vinginevyo. Tambueni kuwa watu sasa wameerevuka na kujua haki zao.




Ni ukweli usiopingika watu wameelimika na wanautambuzi wa uhakika kwa kujua uongo na ukweli. Jaribu kufuatiria na ya Tundu Lissu kama na yeye anasingiziwa. Sema mtu akiwaamsha ili uendelee kuleta upinzani nchini kwa ujuha wenu munaona kuwa yu mjinga.
 
Mawazo kama haya msitegemee ukombozi wa nchi hii utakuwa rahisi. Tena ukute huyu ni msomi ana degree, lakini anaandika kitu cha kijinga kabisa. Tuna safari ndefu sana kufika huko tunakokutaka. Mwenye akili timamu hawezi angashangilia ujinga anaoufanya bwana nape na ccm yake, ila ipo siku haya yote yatakoma.

Siyo kwamba nashangilia bali nawashtua msikalie kujibu hoja za Nape, ila kwa uelewa mdogo wa wafuasi wa Chadema ikiwa mwaona ni ufahari kujibizana. Hivi mtu akipita akakukuta mnapigana na mwenu hali u na akili kamili, akienda zake si atasema nimekutana na wenu wawili wakipigana au atasema nimekutana na mtu mwenye akili timamu akipigana na mwenu? kama anakujua ataenda na kusema hivi fulana kachanganyikiwa lini?. Hivyo kama Nape hafai huku wanajibizana na Dr/Padri. Slaa wote wawili si hawafai? Pole kwa mtazamo hasi
 
hivi nyerere alikuwa kachaguliwa na nani alipokuwa kiongozi wa tanzania wakati wa uhuru?je! alikuwa ni vuvuzela! hivi mtu kama hakuchaguliwa maana yake hana kakili?wewe ulishawahi kuchaguliwa kipindi na mahali flani?

Huwezi linganisha tofali na mlima Kilimanjaro, kwanza uundwaji wake ni katika mazingira tofauti na hivyo vipo tofauti kabisa. Nyerere alichaguliwa na wajumbe wa mkutano wa TANU na baadaye wakakubaliana yeye awe rais wa kwanza wa Tanzania. Nape amehurumiwa na Kikwete (mtu mmoja tu) hana tofauti na microphone ya wauza mitumba wa manzese.
 
Back
Top Bottom