CHADEMA walisema TRA wanakusanya malimbikizo (Arrears) baada ya miaka minne wameumbuka

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

Katika hotuba yake ya kwanza bungeni ambayo wabunge wa Chadema walisaini posho na kisha kwenda kuingalia kwenye baa Raisi John Magufuli aliahidi kusimamia ukusanyaji wa mapato kupitia TRA ambapo kipindi hicho makusanyo yalikuwa ni wastani wa shilingi za kitanzania bilioni 800 na miezi iliyofuata kweli tukaona ukusanyaji ukiongezeka kufikia wastani wa zaidi ya shilingi Trilioni moja kwa mwezi.

Ajizi nyumba ya njaa,wakaanza kuibuka wapiga ramli wakiongozwa na KUB Mbowe wakisema "TRA inakusanya malimbikizo ya serikali ya awamu ya nne na wakiendelea hivyo itafika siku serikali haitakusanya hata senti kwani biashara zote zitakufa"

Leo zaidi ya miaka minne baadaye tunashuhudia mapato kuimarika kiasi cha kufikia shilingi trilioni 1.9 kwa mwezi Disemba 2019 hii ikiashiria sasa TRA wanakusanya zaidi ya mara mbili kwa mwezi ukilinganisha na miaka minne iliyopita.

Je kuna haja ya kuzingatia maoni ya kambi ya upinzani? Ni kweli kambi ya upinzani inaundwa na watu wenye "akili kubwa"?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakudadavuwa,
Hivi kwa utimamu wako unaamini hizo hadithi za makusanyo hewa ya Jiwe?

Chuo Kikuu wanapewa hela na serikali. Baadaye wanatoa gawio hela hizo hizo walizopewa.

Polisi imekuwa sehemu ya kukusanya hela kibabe. Watu wanaandikwa upuzi wowote ili hela ziende kwa Jiwe.

Vitambulisho hewa vya wajasiriamali wadogo.
 
Hivi kwa utimamu wako unaamini hizo hadithi za makusanyo hewa ya Jiwe?

Chuo Kikuu wanapewa hela na serikali. Baadaye wanatoa gawio hela hizo hizo walizopewa.

Polisi imekuwa sehemu ya kukusanya hela kibabe. Watu wanaandikwa upuzi wowote ili hela ziende kwa Jiwe.

Vitambulisho hewa vya wajasiriamali wadogo.


Hela ya makosa ya barabarani trafiki sidhani kama inaenda TRA, isitoshe kama umeonewa na trafiki unaweza kupinga hiyo faini Mahakamani, Polisi kutoza faini ni kawaida Dunia nzima.
 
Wakudadavuwa,
Hivi kwa utimamu wako unaamini hizo hadithi za makusanyo hewa ya Jiwe?

Chuo Kikuu wanapewa hela na serikali. Baadaye wanatoa gawio hela hizo hizo walizopewa.

Polisi imekuwa sehemu ya kukusanya hela kibabe. Watu wanaandikwa upuzi wowote ili hela ziende kwa Jiwe.

Vitambulisho hewa vya wajasiriamali wadogo.
Kamanda tunaongelea makusanyo ya TRA si gawiwo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakudadavuwa:

nukuu " TRA inakusanya malimbikizo ya serikali ya awamu ya nne, na wakiendelea hivyo hawatakusanya hata senti biashara zitakufa"

sasa jiulize kama kweli una akili timamu, ni biashara ngapi zimekufa toka huu utawala uingie madarakani? watu wangapi wamepoteza ajira zao kwa kupunguzwa makazini? serikali inalazimisha kupokea gawio kutoka kila taasisi hata kama hazina chakutoa, wakasema watawafukuza wakurugenzi wa hizo taasisi wasiotoa gawio kufika ile deadline! hapo ndio utajua, nchi hii bila hao CDM tutatumbukizwa shimoni na CCM, hiyo nukuu hapo juu ni ukweli mtupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakudadavuwa:

nukuu " TRA inakusanya malimbikizo ya serikali ya awamu ya nne, na wakiendelea hivyo hawatakusanya hata senti biashara zitakufa"

sasa jiulize kama kweli una akili timamu, ni biashara ngapi zimekufa toka huu utawala uingie madarakani? watu wangapi wamepoteza ajira zao kwa kupunguzwa makazini? hapo ndio utajua, nchi hii bila hao CDM tutatumbukizwa shimoni na CCM, hiyo nukuu hapo juu ni ukweli mtupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wapinzani wamesaidia sana Watanzania kuujua uongo wa CCM

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakudadavuwa:

nukuu " TRA inakusanya malimbikizo ya serikali ya awamu ya nne, na wakiendelea hivyo hawatakusanya hata senti biashara zitakufa"

sasa jiulize kama kweli una akili timamu, ni biashara ngapi zimekufa toka huu utawala uingie madarakani? watu wangapi wamepoteza ajira zao kwa kupunguzwa makazini? hapo ndio utajua, nchi hii bila hao CDM tutatumbukizwa shimoni na CCM, hiyo nukuu hapo juu ni ukweli mtupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
This is the best comments of a day

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu zangu,

Katika hotuba yake ya kwanza bungeni ambayo wabunge wa Chadema walisaini posho na kisha kwenda kuingalia kwenye baa Raisi John Magufuli aliahidi kusimamia ukusanyaji wa mapato kupitia TRA ambapo kipindi hicho makusanyo yalikuwa ni wastani wa shilingi za kitanzania bilioni 800 na miezi iliyofuata kweli tukaona ukusanyaji ukiongezeka kufikia wastani wa zaidi ya shilingi Trilioni moja kwa mwezi.

Ajizi nyumba ya njaa,wakaanza kuibuka wapiga ramli wakiongozwa na KUB Mbowe wakisema "TRA inakusanya malimbikizo ya serikali ya awamu ya nne na wakiendelea hivyo itafika siku serikali haitakusanya hata senti kwani biashara zote zitakufa"

Leo zaidi ya miaka minne baadaye tunashuhudia mapato kuimarika kiasi cha kufikia shilingi trilioni 1.9 kwa mwezi Disemba 2019 hii ikiashiria sasa TRA wanakusanya zaidi ya mara mbili kwa mwezi ukilinganisha na miaka minne iliyopita.

Je kuna haja ya kuzingatia maoni ya kambi ya upinzani? Ni kweli kambi ya upinzani inaundwa na watu wenye "akili kubwa"?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kinachokusanywa sio clean tax ni mapato yote jumuishi kupitia control namba yaani kuanzia,Ada,kodi,fine za traffic ,fine zote,tozo za utalii,vivuko,visa,hela za halmashauri tozo mbalimbali,nk tofautisha mapato ya serikali na kodi.Ile ya JK ilikuwa ni clean tax kodi tu bila kujumlisha mapato toka sehemu zingine.Kuna tofauti ya kodi na mapato
 
Back
Top Bottom