Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,438
- 4,463
Taarifa kutoka jukwaa la wahariri ni kwamba wahariri wameitwa Bahari Beach kesho saa 9:00 kuzungumza na uongozi wa Chadema. Hadhari imetolewa. Wahariri wote wapeleke taarifa ili wapewe kadi maalum za kuhudhuria mkutano huo. Ulinzi ni mkali. Yawezekana ndo wakawa wanamtangaza mwanachama mpya.
Chanzo: Katibu Jukwaa la Wahariri, Neville Meena usiku huu
Chanzo: Katibu Jukwaa la Wahariri, Neville Meena usiku huu
Habari za kutwa wakuu, Chadema wanawaalika wahariri na waandishi wa habari katika mkutano muhimu utakaofanyika kesho Jumanne, Bahari Beach Hotel, kuanzia saa 9:00.
Kwa ujumbe huu, tafadhali thibitisha ushiriki wako binafsi, mwandishi wako na mpigapicha kwa Mratibu wa TEF, Prisca Kabendera kupitia namba 0713 488269.
Ni muhimu kuthibitisha kwa kutuma majina kwani kila mmoja atapewa kadi ya mwaliko itakayomruhusu kuingia Ukumbini. Wote mnakaribishwa.