Yakhe mimi ni mtu wa kwanza kulaani mambo haya ,tena ni nambari one,tokea 2001 ......sasa hii ya Arusha kwangu mimi ni muendelezo tu wa yale ambayo nikiyapinga kwa marefu na mapana ,siejui wakati huo mlikuwa wapi ,maana kama tungelikuwa pamoja wakati huo ,haya ya leo yasingetendeka,lakini mlitutenga na kutona wapemba si watu.
Now police forces kill your brothers and sisters ,poleni sana ,leo hii ndio mnatambua kuwa Serikali ya CCM ni mbaya,leo hii ndio mnatambua kuwa jeshi la polisi halitendi haki ,leo hii ndio mnatambua kuwa jeshi la polisi linauwa raia wasiokuwa na hatia.
Basi wandugu bado huo au hio ni dibaji tu,polisi hao watauwa,watatesa watanajisi na watafanya kila ovu mnalolijua na msilo lijua,kama nasema kama hamkuamua kupambana nao roho kwa roho basi hayo makelele yenu hayatakuwa dawa wala hawatayasikia,endeleeni kuleta matusi hapa labda mnaona hiyo ndio dawa.
WanaJF,
Post ya mwiba inatafsiriwa kama "Crap" na wengi wa wachangiaji, mimi naoana ametumia kejeli kidogo kuwasilisha ujumbe mzito.
Amesema analaani mauaji ya raia wasio na hatia. Hili halina shaka limo kwenye post yake...pia amekwenda mbali kusema wakati 2001 wapemba waliuwawa na hawa hawa Polisi wa serikali inayoilinda CCM na si wananchi. walipofanya mauaji wengi wa watu walifurahia waliona ni sawa tu waliyofanya Polisi wakati huo.
Vyama vyengine vinapoandamana, maoni yanayotolewa humu Jf yanaweza kukufanya ujiulize masuali mengi na usipate jawabu..wengine husema "vunja miguu", "vunja mikono hao", washikishe adabu hao nk.
Waswahili husema "ukimuona mwenzako ananyolewa, wewe tia maji!"
Kwa hiyo, wakati tunauchungu, tunaomboleza vifo vya Watznia wenzetu, pia tutafakari zaidi kuwa ushabiki wa kichama pekee, unatupeleka pabaya, kuna mambo ambayo yanamgusa kila raia, aliye Arusha, aliye Lindi, aliye Tanga, aliye Mbeya, aliye Pemba na kwa hivyo, linapotokea kama hili la Arusha inapasa tushikamane na kudai haki zetu.
kama nimemfahamu vyema Mwiba ni kuwa kama jamii ya Tz ingesimama kidete kutetea, kuunga mkono na kutetea haki za Raia waliouwawa Pemba 2001 leo Polisi na serikali ya CCM isingekuwa na jeuri hii waliyoifanya Arusha.
Badala ya kutupiana matusi, tuutafakari ujumbe wa Mwiba na tuufanyie kazi.
Tushikamane! na Haki ya Raia inapokanyangwa sote, tuhisi kuwa tumeonewa na tudai haki hiyo.
Na CCM na serikali yake haitaishia hapo,itaendeleza kumpiga nyundo kila ambaye anatishia maslahi yao.
kauli za NCCR, CUF nk ni mwanzo mzuri, vyama vinaanza kuona ukweli na taasisi nyengine za kiraia pia. sasa isiwe kwa hili tu.