CHADEMA waigawa UKAWA kabla ya UCHAGUZI

CHADEMA waigawa UKAWA kabla ya UCHAGUZI

bmbalamwezi

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2015
Posts
788
Reaction score
195
Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kimeonekana kuigawa UKAWA kutokana na kwamba wao ndio wanajitambulisha kama UKAWA. Kwenye baadhi ya majimbo ambayo CUF au NCCR- Mageuzi wamesimamisha mgombea, wao pia wamesimamisha mgombea wao.

Na siku chache zilizopita NCCR imejitokeza wazi kulalamikia vitendo vya Chadema. Hii ni wazi kwamba upo mgogoro mkubwa ndani ya UKAWA. Sitashangaa huko Masasi Chadema wakisimamisha mgombea wao baada ya kifo cha Dr. Makaidi.

Sasa watu wa jinsi hii wakipewa dola si ndo watachukua raslimali zetu zote?

Kwenu wana jamvi.
 
Pamoja na kuwa ni vigumu kuhusisha kifo cha Makaidi na siasa, lakini uhalisia tutauona kama Chadema hawataweka mgombea wao, maana naona wanataka madaraka kwa udi na uvumba. Hii hatari sana
 
Unafikiri wamehuzunika kwa kifo hicho? Wanashangilia wakijua kuwa wataweka mtu wao maana sera yao ni wao kwanza wengine wataisoma namba ndani ya kijiwe cha Ukawa. Wenyeviti wa vyama hivyo nao wanaangalia maslahi yao tu, ndiyo maana sasa wengi wao wamegeuka kuwa watu wa propaganda za Chadema badala vyama vyao.
 
hawa watu hakika hawastahili kuwa wawakilishi wa serikali yetu kwani mbinu na njia ambazo huwa wanatumia kuingia ikulu ni hatari sana na kama hata wapo tayari kumwaga damu ili waingie ikulu basi ikulu inaingiliwa na majambazi
 
  • Thanks
Reactions: nao
Hakika CHADEMA wanaishi kwa janja janja tuu, na ukweli ni kwamba hakuna muungano wowote ambao miongoni mwa wana hisa wanakuwa wananyonywa, chadema wameshiriki kuua vyama vingine na wanatumia janja janja kuuahadaa umma wa Watanzania.Tutawakataa 25 oct
 
Tulio na upeo tulijua tu,kwamba lazima ukawa igawanyike kabla ya uchaguzi Mkuu kwa kuwa kila mmoja katika ukawa anaangalia maslahi yake,hivyo hilo si jambo la ajabu kwa kuwa kuna vikao vingi vimekuwa vinafanyika chini chini usiku wa manane na baadhi ya viongozi wa vyama kama Nccr, na NLD
 
bmmbalamwezi, mimi siwezi kukubali nchi hii ikatawaliwa na watu wa ukanda mmoja wenye itikadi za kikabila na unafiki wa ukawa
 
naamini post hii kwa sababu ukawa ni vyama vinne lakini alama wanayoitumia sana ni ya chadema ya vidole viwili, ni ishara ya nini kinaendelea na kwa upofu wao hivi vyama vingine vitakufa muda c mrefu
 
Mimi nilijua unauhakika kumbe unadhania tuu? nadhani tiari unapresha wewe kama mm mwongo nenda kapime
 
Umeishia darasa la ngapi mkuu? Maana hata kuandika kwenyewe kumekushinda. Elimu, Elimu, Elimu.
 
Presha anayo mgombea wenu ambaye jana kashindwa kuhutubia na kuwapa vijana wa mtaani kusema kwa niaba yake. Zigo lenu hilo.

Aisee ivi umeshindwa kutambua kwamba itv walitumia ile fursa kuwahoja vijana ili kujua wananini cha kuongea ivi hujiulizi ni chanel gani imewahoji wananchi zaidi ya itv? Panuka kimawazo wewe
 
Ukawa kwa kweli ukifiri hatua chache tu mbele yao unategua kitendawili,ni genge fulani tu hivi,ndo maana waliweza kusema rangi nyekundu ni nyeupe,mtu waliyemtukana mismu kibao,leo malaika wao mhh,ama ndo huku kusema shetan akizeeka anakuwa malaika hahahahha,nipo makini na kura yangu
 
acha ujinga na unafiki .ukawa mbele kwa mbele

Habari za kata ya Msaranga Mjini Moshi. Unaona hao boda boda wanavyokimbilia kusaka hatima ya maisha yao baada ya kupigwa butwaa? Kaangalie hata pale Soweto karibu na Chang'ibay, kwa chalii, mawazo mpaka kule msikitini.
 
Back
Top Bottom