Chadema waboreshe Mabango yao

Mabango haya ndo hasa maneno ya wananchi! CDM mwendo mdundo!! Kawashauri ccm wachonge mabango kisha wagawiwe watu! Let people's heart speaks
 
Ni vigumu kuangalia picha na kujua nini mkakati wa maandamano ya Chadema. Wanaoandama hawajui lengo kuu la kuandamana kwao, kwa sababu hakuna kauli mbiu. Wakifika uwanjani kuna msururu wa hotuba ambazo hazikuratibiwa.

Kwenye maandamano yao yote, kila raia anaandika chochote popote. Ni haki ya kujieleza kwa kila raia, lakini wanakosa strategic communication. Kuna wakati ujumbe kwenye mabango unakinzana na baadhi ya hotuba.

Sayansi ya public rallies inahitaji ujumbe uratibiwe na waandaaji. Wengine huchapa kabisa mabango na kugawia wananchi. Wananchi wanabakia nayo hata baada ya maandamano.

Mara kadhaa Chadema wameshashauriwa hapa kuboresha kitengo chake cha mawasiliano. Hadi maandamano ya leo inaonekana mbado. Sitaki kuamini kwamba eti Chadema nao hawashauriki kama ccm!

Nakubaliana na wewe kuwa ni vizuri ku-harmonize rally messages lakini huwezi kuwazuia wananchi ku-express innermost feelings kuhusu maisha. Nafikiri CDM wanashaurika na wanaweza kujaribu ku-structure shughuli za maandamano zaidi hasa hili la kuwa na kauli mbiu.

Hata hivyo lazima isisitizwe kuwa huwezi kuzuia wananchi kuandika mabango yao. Ni kazi ya wahutubiaji ku-cluster messages za waandamanaji na kuziweka katika muktadha wa kauli mbiu (contextualization); hotuba zao, ambazo mara nyingi huwa ni extemporenious rather than manuscript, zionekane kuakisi feelings za waandamanaji na wananchi kwa ujumla wake.
 
Wakuu, heshima juuuuu kwa wote waliojibu hapa na wale waliopita kimya.

Nimeelimika, ninashukuru sana kunielekeza tena kwa lugha ambayo siyo matusi. Nakubaliana na maelezo yenu, mawazo fikra zangu zilijisokota kidogo. Hutokea, niwieni radhi.

Hata hivyo naamini Chadema wamepata maoni ya wadau kuhusu website, na kwamba bado inawezekana kuhakikisha kuna bango moja lenye kauli mbiu ambalo litakuwa chachu ya mabango ya wananchi. Kitengo cha mawasiliano cha chadema kinahitaji kuboreshwa, sijui tatizo lao ni utaalamu au bajeti wao ndio wanaotakiwa kutathmini na kufanyia kazi
 
Ni mambo mengi yanawumiza wananchi. Hivyo ni vyema waliyoonyesha mabango ya aina mbalimbali kuwakilisha ujumbe wao Nadhani umewafikiwa walengwa. Cheers
 
Nakubaliana na mtoa mada na pia wapinga mada hii. Public rally kama hizi za chadema siyo spontenous kama zile za Tunisia na Egypt, hivyo zinatakiwa zionekane kwamba ziko well and professionally communicated and coordinated. Hili halionekani, kinachoonekana ni Chadema kuambua tu tutaandamana halafu wanaandamana. Bihind it hakuonekani strong information communication and information management unit. Angalia walishindwa hata kulipia live coverage ili kupanua impact ya maandamano yao ya arusha na Mwanza. Wakiendelea na style hii, watakuwa wanatumia nguvu nyingi sana eneo fulani lakini impact yake haimwagiki maeneo mengine ambayo hawana ushawishi. Media is everything, ndiyo maana ccm wali invest sana kwenye media kwa gharama yoyote.

Nakubaliana na wale wanaosema kwamba wananchi wapewe nafasi ya kujieleza wanavyotaka. Lakini sikubaliani kwamba chadema wasiwe na namna wanavyowasilisha na kuhamasisha wananchi kupitia mabango katika haya maandamano. Kama chama wanatakiwa watuoneshe kwamba wanadai nini. Hizi hotuba hazipatikani full katika vyombo vya habari isipokuwa tu kwa wale waliohudhuria mikutano yao. Hivyo hatuwezi kusema eti walieleza malengo yao kwenye hotuba katika mkutano.

Kuna hotuba nzuri sana Dr. Slaa, Mbowe, na Zitto waliwahi kutoa maeneo tofauti wakati wa kampeni. Hatujaona jitihada za kuzirusha zile hotuba kwenye vyombo vya habari ili wananchi wote wapate ujumbe ni nini hasa chadema wanasimamia na waweze kufananisha na mambo yanavyokwenda.

Chadema wameambiwa mara nyingi tangu muda mrefu kwamba waanzishe tv na radio lakini bado wanacheza makida makida tu. Mimi naungana na mtoa mada kwamba in terms of accountability na kutekeleza maoni ya wananchi, Chadema hawana tofauti na CCM.
 
Ujumbe wa mabango ni uwarisia wa maisha ya watu unaowatawala.Kama mtu una shida ukumbuki kama ujavaa vema.kama mtu umelala na njaa mswaki wapiga wanini asubuhi,Bongo ni nini waguswa.Hata kwa kutumia Tashishi,au Tasibia,LENGO UJUMBE UMEFIKA.

Inaonekana unapenda kiswahili sana,lakini inanipa mashaka kama unaweza kukiandika.
 
Nakubaliana na mtoa mada na pia wapinga mada hii. Public rally kama hizi za chadema siyo spontenous kama zile za Tunisia na Egypt, hivyo zinatakiwa zionekane kwamba ziko well and professionally communicated and coordinated. Hili halionekani, kinachoonekana ni Chadema kuambua tu tutaandamana halafu wanaandamana. Bihind it hakuonekani strong information communication and information management unit. Angalia walishindwa hata kulipia live coverage ili kupanua impact ya maandamano yao ya arusha na Mwanza. Wakiendelea na style hii, watakuwa wanatumia nguvu nyingi sana eneo fulani lakini impact yake haimwagiki maeneo mengine ambayo hawana ushawishi. Media is everything, ndiyo maana ccm wali invest sana kwenye media kwa gharama yoyote.

Nakubaliana na wale wanaosema kwamba wananchi wapewe nafasi ya kujieleza wanavyotaka. Lakini sikubaliani kwamba chadema wasiwe na namna wanavyowasilisha na kuhamasisha wananchi kupitia mabango katika haya maandamano. Kama chama wanatakiwa watuoneshe kwamba wanadai nini. Hizi hotuba hazipatikani full katika vyombo vya habari isipokuwa tu kwa wale waliohudhuria mikutano yao. Hivyo hatuwezi kusema eti walieleza malengo yao kwenye hotuba katika mkutano.

Kuna hotuba nzuri sana Dr. Slaa, Mbowe, na Zitto waliwahi kutoa maeneo tofauti wakati wa kampeni. Hatujaona jitihada za kuzirusha zile hotuba kwenye vyombo vya habari ili wananchi wote wapate ujumbe ni nini hasa chadema wanasimamia na waweze kufananisha na mambo yanavyokwenda.

Chadema wameambiwa mara nyingi tangu muda mrefu kwamba waanzishe tv na radio lakini bado wanacheza makida makida tu. Mimi naungana na mtoa mada kwamba in terms of accountability na kutekeleza maoni ya wananchi, Chadema hawana tofauti na CCM.

Kiongozi,

Acha niwe honest kwa kusema wazi kuwa huenda hauko well informed na YANAYOJIRI!

Sielewi unaishi wapi ambapo huwezi ukajua ni kwa sababu zipi maandamano kama ya jana MWANZA, au Arusha yasingeweza kuonyeshwa live!...Unaongelea TV gani hasa?..nadhani unasemea Aljazeera au CNN ndo wangeonyesha live. na sio stations za hapa Bongo!
Napenda ujue kwamba ishu kwa case hii si kushindwa kulipia...big No!..Wamiliki wa stations za TV wamejengewa hofu kubwa japo ni binafsi!..nadhani unaelewa wanachoweza kuzushiwa na serikali wakiwa wakaidi!

Pia juu ya suala la cdm kuwa na various media, mainly TV station, hili kama ungekuwa makini lilishajibiwa na Dr Slaa mara nyingi tu, lakini kwa ufupi ni kwamba linafanyiwa kazi kwenye ngazi mbalimbali za chama, ili lisiwe la kukurupuka!


Pia nakushangaa unaposema ccm wameweka nguvu nyingi kwenye Media....goosh!, hiVi TBC1 ndio media ya ccm?..kama wewe ni mfuatiliaji wa mambo je hukuona wakati wa kampeni TBC1 wakirusha kwa marefu ziara za JK maeneo mbalimbali ikiwa ni mpango-mkakati wa kumfanya aonekane zaidi kwa jamii ya Watanzania kuliko wastani wa wagombea wengine?

Nakufahamisha pia kuwa media ambazo zinamilikiwa na ccm parse hazina uzito wala impact inayotARAjiwa...think of Gazeti la UHURU, redio UHURU FM, WEBSITE,and whatever the sh..it that they are operating..havina mvuto tena mbele ya jamii...labda huko MSANGA na Msoga!

Hizo hotuba nzuri za Mbowe au Dr Slaa ziko prone to the same setback...hata kama una cash ya kumlipa mwenye Media, akiiangalia content ya Hotuba anakukatalia live(kwa hofu ya Wayahudi")!

Kumbuka kwamba kama kungekuwa na TV huru mauaji ya Arusha yangeonyeshwa bila kuwa tampered with, unlike ile counterfeit iliyorushwa na ccm.
So bro usilaumu bila kuweka rationale platform.
 
mabango ni ujumbe wa wananchi kwa serikali.. mi sikubaliani na kukiachia chama kutengeneza hayo mabango kwani sio wote waliokuwepo

kwenye maandamano ni CDM.. inawezekana wafuasi wa nccr, tlp na hata wale wa ccm walioanza kufunguka macho na masikio nao walikuwepo vile vile
 
Gurudumu. OP. Watanzania wanayo mengi kuliko waliyoandaa chadema. Una ushahidi kuwa kuna bango lisilo na ujumbe? Otherwise hayakuwa maandamano ya CCM ya kupongezana kutokana na ujinga wao. Hata kama una issue ya kupeleka kwa wakweo nenda nayo. Just a burning issue.
 
Uhalisia wa mabango (na uzuri/utamu wake) ni mabango yale yanayotoka kwa wananchi wenyewe...ni mioyo halisi inaongea..sio staili za ki-Chama 'kinachotawala' ambapo wahudhuria mikutano huandaliwa, na kufundishwa hadi kushaangilia..kushangilia wanaoneemeka kwa jasho la washangiliaji..na washangiliaji kutohisi hata matatizo waliyonayo wakati wa kushangilia (mfano mikono huchoka haraka kwa njaa)..ni fikra tu

Mwana wa Mtu mimi nakukubali kabisa, JK anatakiwa kupata ile feeling ya Watanzania wenyewe, je wanataka nini na wakati gani, baada ya Uongozi kuitisha maandamano mabango ni kazi ya wananchi kwani hapo ndo wanapoweza kuzungumza(Ndicho kipaaza sauti chao) kwani hawawezi zungumza wote kwenye Mkutano wa kuitimisha lakini kama akiweka kwa maandishi basi tutasoma na wahusika wataelewa. Binafsi nafarijika kwa uhuru huu wakutoa maoni, lakini siyo watanzania wote wanaweza kuwa na Internet hasa ukizingatia Watanzania tumelazimishiwa umasikini ingawa sisi ni tajiri tulipaswa tuheshimike duniani kote kwani tuna kila kitu.
Naipenda nchi yangu Tanzania, nampenda Dr Slaa na wapigania haki wote!
Mungu Ibariki tanzania na watu wake!
 
Kumbe umelitambua hilo, na hata dola uwezo wa kushika hamna

Tumia akili, Nchi yetu ni tajiri, na viongozi hawaongozi kwa fedha zao mifukoni, usiwadanganye wananchi, fikiri mara mbili kabla ya kuweka upuuzi wako humu. CDM wana watu wenye uwezo mkubwa kiuongozi wanahitaji kupewa nafasi.
 
Uzuri wa mabango hayo ni kwamba yameandikwa na wananchi wenyewe bila uratibu wa Chama (nikiwa na maana Chadema). Ndiyo maana yapo hivyo.

Yanatoa ujumbe na maoni toka kwa wananchi moja kwa moja.

Inawezekana baadaye wakaweza kutumia 'material' bora zaidi ili ujumbe usomeke vizuri zaidi, hii ni process.

Muhimu ni kuwa ujumbe umefika kwa wote, ikiwemo Serikali na CCM a.k.a Chama cha Zamani...
 
I take it as a very minor discrepancy!

Mi napenda zaidi kama mabango yatakuwa community-baked/originated, kama ilivyo hapo, maana serikali inapata moja kwa moja kionjo cha mrejesho wa raia kuhusiana na taste ya huduma wanayoipata...hiyo ni live bila chenga!
MABANGO yanayokuwa generated na chama yawepo, well and good, lakini haya ya jamii yanaleta hisia za ukweli zaidi kwa asomaye....my take!

Nakubaliana na wewe PJ...
Serikali inatakiwa kupata ladha halisi ya malalamiko ya mwananchi kutoka kwa mwananchi mwenyewe kwa lugha ya mwananchi mwenyewe.., si yakuandikiwa na mtu mwingine..!
 
Km lengo kuu la maandamano limeshajulikana mabango ni mbwembwe tu....dhana kwamba nyimbo za maombolezo ni alama ya msiba/simanzi haibadilishi maana ya msiba hata km nyimbo hizo zingeacha kupigwa!

Nakuunga mkono. Kule ninakotoka kuna wenzetu wakifiwa huwa wanaweka burudani ya muziki na pombe kwa wale wanaokuja kukesha kwenye msiba kuwapa "company" wafiwa. Lakini hilo haliondoi ukweli kuwa ule unabaki kuwa msiba wenye majonzi kwa ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.
 
Nakuunga mkono. Kule ninakotoka kuna wenzetu wakifiwa huwa wanaweka burudani ya muziki na pombe kwa wale wanaokuja kukesha kwenye msiba kuwapa "company" wafiwa. Lakini hilo haliondoi ukweli kuwa ule unabaki kuwa msiba wenye majonzi kwa ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.

Aisee habari za Kyabakari!

sAKURU-mWITA
sAKURU cHACHA
 
Back
Top Bottom