Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Ni vigumu kuangalia picha na kujua nini mkakati wa maandamano ya Chadema. Wanaoandama hawajui lengo kuu la kuandamana kwao, kwa sababu hakuna kauli mbiu. Wakifika uwanjani kuna msururu wa hotuba ambazo hazikuratibiwa.
Kwenye maandamano yao yote, kila raia anaandika chochote popote. Ni haki ya kujieleza kwa kila raia, lakini wanakosa strategic communication. Kuna wakati ujumbe kwenye mabango unakinzana na baadhi ya hotuba.
Sayansi ya public rallies inahitaji ujumbe uratibiwe na waandaaji. Wengine huchapa kabisa mabango na kugawia wananchi. Wananchi wanabakia nayo hata baada ya maandamano.
Mara kadhaa Chadema wameshashauriwa hapa kuboresha kitengo chake cha mawasiliano. Hadi maandamano ya leo inaonekana mbado. Sitaki kuamini kwamba eti Chadema nao hawashauriki kama ccm!
Kwenye maandamano yao yote, kila raia anaandika chochote popote. Ni haki ya kujieleza kwa kila raia, lakini wanakosa strategic communication. Kuna wakati ujumbe kwenye mabango unakinzana na baadhi ya hotuba.
Sayansi ya public rallies inahitaji ujumbe uratibiwe na waandaaji. Wengine huchapa kabisa mabango na kugawia wananchi. Wananchi wanabakia nayo hata baada ya maandamano.
Mara kadhaa Chadema wameshashauriwa hapa kuboresha kitengo chake cha mawasiliano. Hadi maandamano ya leo inaonekana mbado. Sitaki kuamini kwamba eti Chadema nao hawashauriki kama ccm!