CHADEMA vipi mgombea urais 2015 mbona kama...?

Status
Not open for further replies.
- si ndio sera ya chama chenu matusi, lakini ni mikwara tu ya kuficha umediocre ndio maana hapa hatujali matusi yenu tunawapiga kwa lugha mnayoijua zaidi, majitu mazima na akili timamu mnatetea mediocre eti kwani amegombea mara ngapi so what? Huyo amegombea na kushindwa urais wananchi wamemkataa hana jipya, kwenye udiwani wananchi wamemkataa hana jipya sasa kwa vile nyi eni mediocre mnataka kumpa tena kugombea urais ndio maana mnalia sana,

- well, slaa hafai kabisa hata kuwa katibu wa kata, hafaii kwa sababu kwanza ni muongo na pili hana maadili!!

Le mutuz!!
ni kweli kamanda willy, chama kina matusi hiki!!!!
 
- Well, nimekuwa najiuliza hili swali kwa muda sasa kwamba CHADEMA wanafikiria nini hasa kuhusu mgombea Urais 2015, maana sio siri kwamba kwa sasa hawana, DR. Slaa hawezi tena kugombea na akigombea itakuwa a big insult kwa wengine huko CHADEMA kwa sababu haiwezekani mtu kila akigombea anashindwa halafu mnampa tena huyo huyo, baada kushindwa sana na chaguzi mbali mbali ni clear kwamba hana jipya tena!!

- Mbowe hawezi kugombea tena maana amegombea sana na kushindwa kila wakati, so Zitto ndiye mgombea peke yake ambaye bado kugombea Urais, ni msomi wa kweli, ni mwanasiasa na anawafaa sana CHADEMA, lakini kwa vile huko wenzetu wamezoea kukumbatia mediocre hawamtaki, Walimtegemea sana Waziri wa CCM Sitta, lakini na yeye kawatolea nje sasa swali ni je watampata wapi mgombea credible?

CHADEMA mtafakari hii kuliko kupoteza muda mwingi kushindana na hoja mfu na CCM, ukweli ni kwamba 2015 hamna mgombea credible CCM ina team ya wagombea credible, jipangeni sasa jamani!!

NI USHAURI WA BURE TU JAMANI!!

Wanasiasa wakiwa opposition sio lazima kubadilishana kugombea Kibaki kagombea zaidi ya mara mbili akapata urais kwa mara ya tatu, Abdul Wade wa Senegal kagombea mara tano ya sita akaupata urais, Nicolai Sarkozy wa Ufaransa kabombea mara mbili huko Ufaransa ndio akaupata urais, Richard Nixon wa Marekani aligombea mara mbili ndio akaukwa urais, John Kuffour wa Ghana aligombea mara tatu ya nne akaukwaa urais Ghana, Michael Sata wa Zambia aligombea mara tatu na ya nne akaukwa urais Zambia orodha ni ndefu kwahiyo Bwana Malecela maneno yako ni baseless na useless ambayo hayana mantiki yeyote maana mara nyingi wapinzani waafrika hushindwa sio kwa sera ni sababu ya wizi wa kura toka vyama tawala ukitaka kujua hilo ni kwamba kwanini ni nchi za ulaya na Marekani tu ambazo viongozi walio madarakani hushindwa wakati wamedeliver na viongozi wafrika wa vyama ambao ni wezi, wabadhilifu, wamejaza ndugu zao madarakani na kugeuza nchi miradi yao na familia zao na rafiki zao always wanashinda? jibu ni kuwa hawako ayari kuachia madaraka mfano mzuri CCM haijwahi kushinda Zanzibar toka mfumi wa vyama vingi kuanza kwahiyo acha porojo za siasa za maji taka. Kabla hujauliza safu ya chedema waulize CCM ilikuwaje Kikwete akanunua Urais?
 
bAADA YA KUTUDHALILISHA, HUYU KUBWA JINGA TUNALAZIMIKA KUMUUMBUA. ANASAMBAZA PICHA ZAKE ZA UCHI KWA WADADA MITANDAONI...
 
DR. Slaa hawezi tena kugombea na akigombea itakuwa a big insult kwa wengine huko CHADEMA kwa sababu haiwezekani mtu kila akigombea anashindwa halafu mnampa tena huyo huyo, baada kushindwa sana na chaguzi mbali mbali ni clear kwamba hana jipya tena!!


Mkuu unajua as days goes on unazid kujishushia hadhi hapa JF na katika jamii as well, hebu tuambie Dr ameshagombea mara ngapi ku justify hoja yako Mfu ya kuwa Dr Slaa keshagombea mara Nyingi na Kashindwa, then kama Hoja ni kugombea na Kushindwa, mbona hata Mkwer.e alishindwa 1995 na Ben na Bado akagombea after 10 years???

Mbowe hawezi kugombea tena maana amegombea sana na kushindwa kila wakati,

Na huyu nae ukiulizwa kagombea mara ngapi ku justify kauli ya Kagombea sana utajibuje???

so Zitto ndiye mgombea peke yake ambaye bado kugombea Urais, ni msomi wa kweli, ni mwanasiasa na anawafaa sana CHADEMA

Ni Lini CDM Wamekuajiri kuwa Msemaji wao??? Mbona unajipendekeza hivyo tena kwa Mwanamume mwenzio, , Mtoto wa Kiume kutoka Maneno kama haya Kinywani ni ishara Mbaya sana

My Concern
Kichwa chako kina Reflect kichwa cha Dingiako, Mwl Nyerere hakukosea kabisa Kumuwekea Ngumu Dingi ako na kufuta kabisa ndoto za Dingi ako kujaribu Kunusa Magogoni
Wewe sijui hata huko Nje ulikaa ulikuwa unafanya nn, Huja elimika, una hoja Dhaifu, una Exposure Mfu kabisa.
Unatia Kinyaaa

Ptuuuuuuuuu
 
Kila mara kadri muda unavyoruhusu huwa najaribu kujibu tuhuma mbali mbali dhidi ya Chadema. Mara nyingi kama si mara zote tuhuma hizi zinarushwa na wanajf wenye ID zisizorasmi – unverified users. Hata hivyo, karibuni verified user W J Malelecela ameingia ktk kundi washambuliaji wa viongozi wa Chadema kwanza kwa kwa hoja dhaifu, pili mashambulizi mengine ni binafsi hayahusiani kabisa na masuala yao ya kiuongozi. Ifahamike ukishasema shekhe x au Askofu z ni kichaha, maana yake pia umewadhalilisha pia waumini au wafuasi wa dini hiyo. Vivyo vivyo, matusi yote ya malecela dhidi ya viongozi wetu ( Mbowe na Slaa) ni matusi dhidi ya wanachdema wote nikiwemo mimi kama kiongozi. Kabla sijajibu hoja moja baada ya nyingine soma matusi 2 kati ya nyingi za jana.

1 Unaona si nimesema wanapenda sana kukumbatia mediocre, eti amegombea mara moja tu so what huyu Slaa na Mbowe wote ni mediocre, huyu Mbowe toka mwaka 1990 mpaka leo bado anasoma Degree ya kwanza UK, lakini akiwa bongo hajamaliza, Dr. Slaa ana PhD ya Kanisani lakini anaiba mke wa mwananchi, wote hawafai tena cause wameshagombea Urais na kupigwa chini wakaishia kupata kura zao tu!

- Salaa majuzi kaenda kuongopza kampeni za Udiwani MWanza, kaishia kupigwa chini na wananchi tena kwa kipigo cha mbwa mwizi, then kajaribu Udiwani Viti 27, aibu tena kapigwa chini Viti 22 na CCM, sasa huyu kama sio mediocre ni nini jamani hebu kuweni fair?

- Lema hawezi kugombea Urais, itakuwa maandamano kila siku mpaka biashara zote zitafungwa
kama Arusha, waliobaki Credible ni ( anawataja kadhaa) wote ni wasomi wakubwa lakini kwa vile huko mmezoea mediocre na vilaza hamuwataki, halafu mtautletea tena vilio vyenu vya kuibiwa kura, tafuteni mgombea sasa!!
2 Si ndio sera ya chama chenu matusi, lakini ni mikwara tu ya kuficha umediocre ndio maana hapa hatujali matusi yenu tunawapiga kwa lugha mnayoijua zaidi, majitu mazima na akili timamu mnatetea mediocre eti kwani amegombea mara ngapi so what? Huyo amegombea na kushindwa Urais wananchi wamemkataa hana jipya, kwenye Udiwani wananchi wamemkataa hana jipya sasa kwa vile nyi eni mediocre mnataka kumpa tena kugombea Urais ndio maana mnalia sana,

- Well, Slaa hafai kabisa hata kuwa katibu wa kata, hafaii kwa sababu kwanza ni Muongo na pili hana maadili!!



1. ELIMU YAO.
Malecela ana dai kuwa Mbowe amesoma degree tangu mwaka 1990 hadi sasa. Kwa hiyo, hastahili kuwa kiongozi. Nataka nimfahamishe rafiki yangu kwamba siku hizi dunia imebadilika. Mtu unaweza kubanwa na kazi na ukasoma degree kwa miaka kibao. Ndio maana karibu robo tatu ya graduate wa Tz wanataka open universitiy ambayo inampa mtu uhuru wa kusoma na kusitisha masomo kwa muda. Na hii si jambo la ajabu kwa mtu kama Mbowe ambaye ni kiongozi wa Chama kikubwa kama chetu, anaendesha biashara kubwa nk. Pengine kwa mafanikio aliyoyafikia, Mbowe angekewa ikulu angeshapewa PHD ya Heshima kama JK na kwa vile wenye waogo – watapoteza kazi.
Kuhusu Elimu ya Slaa Malecela hakuna PHD ya kanisani au msikitini. PHD ni PHD tu. Na ujue hii si PHD ya kuzawadiwa kama PHD ya JK.

Hata hivyo, kwa kuwa umeibua hoja ya Elimu ya Mbowe na Slaa, nadhani ni busara nikiuliza kwa heshima na taadhima kama madai yaliyoibuliwa na mwanajf ninayemfahamu vizuri Mwita Maranya kwamba ulizungusha duara elimu ya secondary na bado Mzee kwa vile alikuwa na nafasi kubwa akakupeleka USA. Na Mwita maranya akaendelea kudai kuwa ulienda kusoma vyuo vya kata. Mimi sijui ila nauliza tu.

2 MALECELA ANASEMA MBOWE NA SLAA NI MEDIOCRE. HAWAFAI KUWA VIONGOZI.
Neno hili mediocre maana yake ni average, second rate, ordinary. Kwa lugha nyingine Chadema wote wanaongozwa na viongozi average -wa wastani, ordinary ( wa kawaida) na mbaya sana seconda rate ( daraja la pili) Haya ni matusi makubwa sana kwa watz na wanachadema wote kutoka kwa Mtu anajiita kiongozi wa chama tawala. Ni tusi zaidi kwa wasomi kma akina Dr Kitila, Prof Abdallah Safari, marando nk ambao wanawaon hawa kama viongozi wao.
Hata hivyo, kwa unyenyekevu sana naomba ufafanuzi kwa vile wewe ni high class, si vibaya ukatuambia baadhi ya mafanikio yake ili tuweze kuyalinganisha na mafanikio ya Mbowe na Slaa. Mbowe na Slaa wametuletea Chadema na kuifikisha hapa ilipo kila mtu kwa kipaji chake. Si vibaya tukijua mafanikio yako mheshimiwa sana. Inawezekana baadhi ya mafanikio yako majuu, ni vizuri ukwajulisha wanajf tukulinganishe na hawa second rate.

3. DR SLAA AMEMPOKA MWANANCHI MKE WAKE.
Hili ni suala binafsi mno kiasi kwamba halikupaswa kuletwa hapa JF na mtu mwenye akili timamu. Kuna msemo kwamba ukimkimbiza kichaha aliyekimbia na nguo zako wakati unaoga, wewe unayemkimbiza utaonekana kichaha zaidi kwa kuwa kichaha ana nguo mkononi lakini wewe utakuwa uchi. Mnisamehe kwa leo kama msemo huo utanigeuka. W J. Malecela ana mama mdogo wake anayeitwa Ana killango Malecela. Anna alimkataa mume wake wa kwanza kama Josephine alivyomkataa mume wake wa kwanza. Sasa kwa kadri W J.Malecela anavyomshambulia Dr Slaa anagetendea haki kama pia angehoji mazingira ya Mzee Tingatinga na Anna.
Zaidi ya hayo, nimesoma hapa JF kuwa kuna suala la kutelekeza familia marekani ambalo pia ninaomba ufafanuzi wake kwa unyenyekevu. Kuuliza si ujinga.

4 VIONGOZI HAWA WOTE WAMESHINDWA MARA NYINGI.
Malecela anasema kwa maoni yake, chadema haina mgombea urais na akatushauri tuwachague wengine kwa kuwa Slaa/Mbowe hawachaguliki.wameshindwa mara nyingi.
Mbowe amegombea ubunge mara mbili na kushinda mara zote. Amegombea urais mara moja kupitia chama kisichofahamika na akapata kura za kutosha na kuitangaza chadema nchi nzima kwa mara ya kwanza. Na ile ndo ilikuwa mara ya kwanza chadema kusimamisha mgombea urais. Big achievement.
Dr Slaa vivyo hivyo, amegombea ubunge mara 3 na kushinda. Amegombea urais mara moja na kupata kura mil 2 na ushee. Bahati mbaya hadi leo kura za urais kwa kila jimbo ni siri ya Tume ya Uchaguzi peke yao.
Hata hivyo, mzoefu wa majuu, intellectual who is no mediocre alipotua Dar kutoka kwa obama alishtua ubunge wa Africa Mashariki – akshindwa. Ndani ya mwka moja akajaribu kete yake NEC – akashindwa tena. Kwa bahati mbaya sana mwaka huo huo mtaalam wetu kutoka majuu who is not mediocre – mtu wa higher level hakuweza kumsadia mama mdogo Anna Malecela kushinda uchaguzi, akabwagwa vizuri. Miaka 2 iliyopita intelectul wetu hakuweza kumsaidia baba kushinda kura ya maoni ndani ya ccm.
Kwa hiyo, wakati yeye anadai kwamba Slaa na Mbowe kushindwa mara nyingi ndani ya miaka miwili ndni ya familia yao wameshidwa mara 4. (Intelectual William 2, baba 1 na mama mdogo 1)
Kushindwa mara mbili kwa william ndani ya miaka 2 ni sawa na wastani wa kushindwa mara 10 ndani ya miaka 20. Slaa na Mbowe miaka 20 iliyopita walishindwa mara 1.

5 LEMA NI MAANDAMANO TU.
Kwa kifupi ifahamike kuwa lema haitishi maandamano peke yake. Pale inabidi na kwa makubaliano ya viongozi wote wanaitisha maandamano. Na hilo linatokea kwa kulazimishwa na uziwi wa serikali kutosikia. Hakuna sera ya Chadema kwamba

Kwa kuhitimisha namshauri rafiki yangu aachane mashambulizi binafsi kwa sababu hayana tija. Hii si tabia yangu kuandika mambo binafisi lakini kwa leo mnisamehe mara moja tu. Nilitaka kumwonyesha rafiki yangu umuhimu wa kutofanya hivyo.

Yeye anayeishi ktk nyumba ya glasi asiwarushie mawe wenzake wanaishi ktk nyumba za Glasi.




kila kitu ni
kuandamana tu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom