fullcup
JF-Expert Member
- Jun 21, 2016
- 806
- 2,182
Baada ya tangazo la jana, lililotolewa na Mwenyekiti wa chama taifa viongozi walifanya tathimini. Baada ya mijadala mbalimbali katika vijiwe na mikusanyiko mingine wakaafiki kushiriki uchaguzi.
Baadhi ya viongozi wa matawi ya CHADEMA Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wamekubaliana kushiriki uchaguzi huo.
Wao wanaamini kuwa sababu zilizotolewa wao hawajakumbana nazo hivyo hawaoni sababu ya kutoshiriki.
Matawi hayo ni yale ambayo wagombea wao walipitishwa na hakuna figisu zozote zilizojitokeza. Baadhi ya viongozi wamesema walijiandaa kwa muda mrefu na hawaoni sababu ya kususia na wana uhakika watashinda.
Baadhi ya viongozi wa matawi ya CHADEMA Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wamekubaliana kushiriki uchaguzi huo.
Wao wanaamini kuwa sababu zilizotolewa wao hawajakumbana nazo hivyo hawaoni sababu ya kutoshiriki.
Matawi hayo ni yale ambayo wagombea wao walipitishwa na hakuna figisu zozote zilizojitokeza. Baadhi ya viongozi wamesema walijiandaa kwa muda mrefu na hawaoni sababu ya kususia na wana uhakika watashinda.